Friday 27 February 2009

Almunia wa Arsenal

Juzi golikipa namba wani wa Arsenal aligeuka kichekesho ktk vyombo vya habari Uingereza baada ya kuibuka njiani akitembeza* mbwa mitaani.

Wenyeji wanasema kuwa aina ya mbwa aliyekuwa nae kipa huyo huwa ni kwa ajili ya kina mama (wanawake). Kwa utamaduni wa wenyeji, wanaume hawatembei na mbwa wa aina hiyo. Vyombo vya habari (TV, radio na magazeti) vilimchora sana.



*Zingatia:
Ni kawaida kwa watu (Uingereza) kuwapeleka mbwa matembezini karibu kila siku. Mbwa wa Uingereza hutunzwa vizuri na pia wanawekewa bima endapo wapata matatizo.
Kuwa na mbwa kunaweza kuwa ni gharama sana kwa mtu wa kipato cha kawaida na hairuhusiwi kumuacha nyumbani bila uangalizi wowote. Rafiki yangu mmoja alikuwa akisafiri toka Reading hadi Bracknell (mwendo wa dk 20, A329-Motorway) kumpeleka mbwa kwa dada yake (amwangalizie) wakati anapoenda kazini halafu anampitia mbwa jioni baada ya kazi!
Halafu kwa bahati mbaya au nzuri mbwa hawa huishi ndani ya nyumba mchana na usiku, sio nje kama tulivyozoea Afrika.
Kuna matukio kadhaa yaliyokwisha ripotiwa ambapo mbwa wameua watoto wachanga, na wakati mwingine watu wazima nao wamechanwa sura zao na mbwa!

No comments: