Saturday 30 August 2008

John McCain tries youth and gender route!!

My views:
Knowing Obama's youthfullness would go against him McCain tried to neutralise it by picking Ms Palin (even younger than Obama) in order to pull some voters off Obama.

Also following Hillary's defeat to Obama, McCain hopes to gain 'some' women votes through Ms Palin as altenative to Hillary for voters who want women in top office.

So Ms Palin is there to win votes destined to 'young' Obama and 'a woman' Hillary (as she qualifies in both attributes - not only is she (Ms Palin) a woman but also she is younger).
-mosonga2002@yahoo.com

..............................

Republican John McCain made a surprise choice of Alaska Gov. Sarah Palin as his running mate on Friday, (August 29 11:02) at DAYTON, Ohio - adding a political unknown to the presidential ticket who could help him appeal to women voters.

Palin, 44, a self-described "hockey mom," is a conservative first-term governor of Alaska with strong anti-abortion views, a record of reform and fiscal conservatism and an outsider's perspective on Washington.

"She's exactly who I need. She's exactly who this country needs to help me fight the same old Washington politics of me first and country second,"
McCain told a roaring crowd of 15,000 supporters in Dayton, Ohio.

Palin was chosen over more experienced and better known contenders as the Arizona senator grabbed the spotlight from Democratic rival Barack Obama one day after Obama accepted his party's presidential nomination before 75,000 flag-waving supporters at Denver's football stadium.

"The mission is clear. The next 67 days, I'm going to take our campaign to every part of our country and our message of reform to every voter of every background in every political party or no party at all," said Palin, joined on stage by her husband and family. She has five children ranging in age from 18 years to 5 months.

McCain and Palin will face Obama and his No. 2, Joe Biden, in the November 4 presidential election, with polls showing them running neck-and-neck.

The pick followed days of speculation about McCain's choice, with most of the better-known contenders like former Massachusetts Gov. Mitt Romney and Minnesota Gov. Tim Pawlenty eliminated over the last 24 hours.

'18 MILLION CRACKS'

Palin, former mayor of the town of Wasilla, is virtually unknown and untested nationally. That could hurt McCain's argument that Obama, 47, a first-term senator from Illinois, is too inexperienced to handle the White House.

Her selection was welcomed by social conservatives who sometimes have appeared reluctant backers of McCain. An opponent of abortion, Palin had her fifth child in April despite a pre-natal diagnosis of Down syndrome.

She could also help McCain appeal to disaffected supporters of Democrat Hillary Clinton, who lost a bruising primary to Obama. Palin noted the achievements of Clinton and Democrat Geraldine Ferraro, who in 1984 became the first woman vice presidential nominee of a major party.

"Hillary left 18 million cracks in the highest, hardest glass ceiling in America," she said, referring to the 18 million votes Clinton received in the primaries. "But it turns out the women of America aren't finished yet, and we can shatter that glass ceiling once and for all."

Palin would be the first woman U.S. vice president, adding another historic element to a presidential race that has been filled with firsts. Obama, 47, is the first black nominee of a major U.S. political party.

Palin made her mark as a reformer in a state hit by corruption scandals and could help McCain reinforce his own reform message, but the Alaska legislature has thrown a shadow over her reputation by launching an abuse of power probe.

Palin is accused of firing a highly regarded state public safety commissioner. The official charged he was released for resisting pressure from the governor's office to dismiss Palin's ex-brother-in-law, a state trooper who was involved in a contentious divorce and custody battle with her sister.

Elected in 2006, Palin is Alaska's first woman governor. She is also an avid sportswoman who would bring youth and vitality to the ticket. McCain turns 72 on Friday and would be the oldest person to take office for a first term in the White House if elected.

CAMPAIGNS CLASH

The two campaigns initially squabbled over who had more experience -- the young first-term senator from Illinois or the young first-term governor from Alaska.

"Today, John McCain put the former mayor of a town of 9,000 with zero foreign policy experience a heartbeat away from the presidency," said Obama campaign spokesman Bill Burton, adding that she would work to overturn abortion rights and continue Republican economic policies.

"It is pretty audacious for the Obama campaign to say that Governor Palin is not qualified to be vice president. She has a record of accomplishment that Senator Obama simply cannot match," McCain spokeswoman Jill Hazelbaker responded.

Obama, who called Palin to congratulate her, distanced himself from his campaign's statement, describing Palin's selection as "one more hit against the glass ceiling" and complimenting her as a compelling person.

"Obviously a terrific story, personal story. I'm sure that she will help make the case for the Republicans. Unfortunately, the case is more of the same. Ultimately, John McCain is at the top of the ticket," Obama said as he campaigned at a biodiesel plant in Monaca, Pennsylvania.

Palin and Democratic vice presidential pick Sen. Joe Biden of Delaware share at least one thing in common -- both have sons who are in the military and are being deployed to Iraq later this year.

The choice of a vice president rarely has a major impact on a presidential race. Palin will meet Biden, chairman of the Senate Foreign Relations Committee, in a debate in October.

McCain and Republicans open their national convention on Monday.

-source: UK news, yahoo website.

Friday 29 August 2008

Happy Birthday Michael Jackson, McCain

Michael Joseph Jackson, 50 today, (born August 29, 1958) is an American musician and entertainer. The seventh child of the Jackson family, he debuted on the professional music scene at the age of 11 as a member of The Jackson 5 and began a solo career in 1971 while still a member of the group. Referred to as the "King of Pop" in subsequent years, five of his solo studio albums have become some of the world's best-selling records: Off the Wall (1979), Thriller (1982), Bad (1987), Dangerous (1991) and HIStory (1995)
...........................................

John Sidney McCain III, 62 today, (born August 29, 1936) is the senior United States Senator from Arizona and presumptive presidential nominee of the Republican Party in the 2008 presidential election.
..........................................
(source: wikipedia, free encyclopedia)

UEFA Champions League Draw, at Monaco (yesterday)

Today is: Friday, 29/08/2008

MANCHESTER UNITED Vs. ...
17 Sept - Villarreal (H)
30 Sept - Aalborg (A)
21 Oct - Celtic (H)
5 Nov - Celtic (A)
25 Nov - Villarreal (A)
10 Dec - Aalborg (H)
.............................................

Group A
Chelsea, Roma, Bordeaux, Cluj

Group B
Inter Milan, Werder Bremen, Panathinaikos, Anorthosis

Group C
Barcelona, Sporting Lisbon, Basel, Shakhtar

Group D
Liverpool, PSV, Marseille, Atletico Madrid

Group E
Manchester United, Villarreal, Celtic, Aalborg


Group F
Lyon, Bayern, Steaua Bucharest, Fiorentina

Group G
Arsenal, Porto, Fenerbahce, Dynamo Kyiv

Group H
Real Madrid, Juventus, Zenit St. Petersburg, Bate

(source: www.manutd.com)
............................

Thursday 28 August 2008

Man Utd off to Monaco

Reds off to MonacoSir Alex has taken a 19-man squad to Monaco for Friday night’s Super Cup clash with Zenit St Petersburg.

The Reds left Manchester Airport on Thursday morning at 09:00 BST and will train at Stade Louis II later in the day. Kick-off on Friday night is at 19:45 BST.

Ryan Giggs, Michael Carrick and Ben Foster missed out on the trip, as did Fabio and Rafael da Silva.

Cristiano Ronaldo has travelled with the team, although he’s still recovering from injury and won’t feature in Sir Alex’s playing plans.


United squad: Kuszczak, Van der Sar; Brown, Evra, Ferdinand, Neville, O’Shea, Vidic; Anderson, Fletcher, Gibson, Hargreaves, Nani, Park, Possebon, Scholes; Campbell, Rooney, Tevez
-source: www.manutd.com
....................................

Tuesday 26 August 2008

Kinyesi cha ng'ombe

Sio rahisi kufikiria kuwa Ulaya unaweza kupuliziwa na harufu kali za kinyesi cha mifugo. Juzi juzi nikiwa njiani eneo la Shiplake, Oxon (Uingereza) nilipigwa na harufu kali sana ya kinyesi cha ng'ombe huku gesi ya amonia ikitumbuiza kwa mbali. Nilipopiga jicho niliona mifugo aina ya ng'ombe wa kisasa wakiwa wanachunga nje (kwa vile huu ni wakati wa summer).

Leo tena bila kutegemea maeneo ya Yateley, Hants nimesikia jogoo wakiwika zaidi ya mara mbili, nilihisi niko kijijini kwetu TZ!!

Kumbe maisha ni yaleyale tu si Ulaya si TZ, wazungu wanatuzidi kidogo tu hasa kwa jinsi wanavyotumia rasilimali zao kwa manufaa ya wananchi na Taifa kwa ujumla. Watanzania tungelikuwa mbali na sisi kama tusingelikuwa wadokozi wa 'vijisenti' hapa na pale!

Tuesday 19 August 2008

Man Utd: 2008/09 Season

PREMIER LEAGUE (start of the season):
17 Aug Barclays Premier League Newcastle H 16:00 D 1-1 Fletcher
25 Aug Barclays Premier League Portsmouth A 20:00 W 1-0 Fletcher
29 Aug UEFA Super Cup Zenit St Petersburg N 19:45 L 1-2 Vidic
30 Aug Barclays Premier League Fulham (Postponed, new date TBC) H 15:00
........................................
GOALS!
Darren Fletcher: Prem: (1+1)

Friday 15 August 2008

Manchester United Squad numbers

Squad numbers registeredUnited's squad numbers for the 2008/09 campaign have been registered with the Premier League and there are some notable inclusions, especially for the younger members of the Reds' playing staff.

1.Van der Sar, 2.Neville, 3.Evra, 4.Hargreaves, 5.Ferdinand, 6.Brown, 7.Ronaldo,
8.Anderson, 9.Saha, 10.Rooney, 11.Giggs, 12.Foster, 13.Park, 15.Vidic, 16.Carrick,
17.Nani, 18.Scholes, 19.Welbeck, 20.Fabio, 21.Rafael, 22.O'Shea, 23.Evans,
24.Fletcher, 26.Manucho, 27.Silvestre, 28.Gibson, 29.Kuszczak, 31.Campbell,
32.Tevez, 33.Hewson, 34.Possebon, 35.Cleverley, 36.Gray, 37.Cathcart, 38.Zieler,
39.Chester, 40.Amos, 41.Macheda

(source: manutd.com)
.............................................

Wednesday 13 August 2008

BBC kurusha ligi ya Uingereza TZ

Nchini Tanzania, BBC Ulimwengu wa Soka inapatikana mjini Zanzibar katika 94.1 FM na Pemba katika 93.5 FM.

Vilevile unaweza kupata matangazo haya kupitia radio washirika:

Radio Free Africa mjini Dar Es Salaam katika 98.6FM, Mwanza katika 89.8FM, Shinyanga katika 88.2FM, Kagera katika 94.1FM, Arusha katika 89.0FM, Mbeya katika 88.8FM, Dodoma katika 89.0FM, Rukwa katika 89.1FM, Ruvuma katika 89.6FM, Mtwara na Lindi katika 89.0FM, Singida katika 88.3FM, Iringa katika 93.5FM, Tanga katika 99.3FM, Tabora katika 90.0FM, Kigoma katika 90.0FM, Morogoro katika 93.8FM, Kilimanjaro katika 88.2FM, Mara katika 93.5FM na katika 1377 AM/MW kwenye maeneo yote Tanzania.

Pia kupitia Radio One mjini Dar Es Salaam katika 89.5 FM, Arusha katika 95.3 FM, Dodoma katika 100.8 FM, Mwanza katika 102.5 FM, Moshi katika 1323 AM na katika 1440AM kwenye maeneo mengine yote.

Radio 5 mjini Arusha katika 105.7 FM, na Sky FM katika 101.4 mjini Dar es Salaam.

BBC Ulimwengu wa Soka pia inapatikana kote Afrika Mashariki na Kati kwenye masafa Mafupi katika 11705 kHz, na vilevile kwenye tovuti:
http://www.bbcswahili.com/

-(kutoka blog ya beda msimbe, 13/08/2008)
.......................................................
Nasaha za mtu mzima:

'i have been around long enough to understand things (and deal with them as the happen)'
-sven goran erickson, man city manager on his future at city.
april, 2008

Tuesday 12 August 2008

NASAHA ZA MAISHA!
.....................................
'nabii hathaminiwi nyumbani kwao'
......................................
......................................
'it is very difficult to talk about sex but very easier to do it'
-bbcone, 6 o'clock news 11/10/2006
......................................
......................................

Friday 8 August 2008

Olympic games opens in China

A huge fireworks display has signalled the start of the opening ceremony of the Beijing Olympic Games.
Opening ceremony started at 13:00BST, 08/08/2008.
..............................................................

Thursday 7 August 2008

Man Utd's new Brazilian boys!!

The new boys from Brazil. They are twins!!

Fabio da Silva
Born: 9 July 1990, Rio de Janeiro
Age: 18
Former club: Fluminense
Position: Left back / left midfield

Rafael da Silva
Born: 9 July 1990, Rio de Janeiro
Age: 18
Former club: Fluminense
Position: Right back / right midfield

(source: manchester united official website)
.....................................................

Friday 1 August 2008

Kifo cha Mhe Chacha Wangwe (MB)

Tarime wazuia maziko ya Wangwe

MWENYEKITI wa CHADEMA, Bw. Freeman Mbowe, amenusurika kauawa kwa mapanga na mishale, baada ya kuwasili katika kijiji cha Kemakorere, kuhudhuria maziko ya aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wake na Mbunge wa Tarime, marehemu Chacha Wangwe.

Sakata hilo lilianza kujitokeza jana saa nane mchana baada ya Bw. Mbowe kuwasili kijijini hapo akifuatana na viongozi wengine wa vyama vya siasa, Profesa Ibrahim Lipumba (CUF), Bw. Augustino Mrema (TLP), Bw. Joseph Mbatia (NCCR-Mageuzi) na Bw. Bob Makani Mwenyekiti mstaafu wa CHADEMA.

Baada ya kuwasili kwa viongozi hao, kundi kubwa la watu hasa vijana walianza kumzonga Bw. Mbowe kwa kumwonesha mabango mbalimbali kuhusu kifo cha Bw. Wangwe wakisema hakitokani na mapenzi ya Mungu bali ameuawa.

Baadhi ya mabango hayo yalisomeka ifuatavyo: 'Tarime bila Wangwe hakuna amani'; 'Hii ni ajali au risasi?'; 'Viongozi bora hufa kwa ajali na risasi, viongozi wasio waadilifu hufa kwa BP'na 'Hadi kieleweke CCM hawana chao, tutakufa tukiilalamikia Nyamongo'.

Mengine yalisema: 'CCM chunguza Richmond na vijisenti, hatutampata kama Wangwe';'Tutakumbuka msimamo, utetezi, ujasiri na hoja zako' na 'Nyota ya Tarime imezimika meseji sent.'

Kutokana na hali hiyo, watu wa usalama wakiongozwa na askari Polisi wa kawaida na wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) waliwazuia wananchi hao kumzonga kiongozi huyo, lakini hawakufanikiwa kirahisi na hivyo kumlazimisha kuingia uani ambako shughuli za maandalizi ya maziko hayo zilikuwa zikifanyika.

Hatua hiyo ilibadilisha kabisa mazingira ya msiba huo, ambao ulihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, wabunge na wanasiasa, vingozi wawakilishi kutoka Kenya na maelfu ya wananchi.

Hali hiyo ya kutisha ya baadhi ya wananchi kubeba mapanga, mikuki, sime na fimbo huku baadhi yao wakiwa wameziweka hadharani na wengine katika makoti na kujificha migombani, ilimfanya kiongozi wa ukoo huo, Profesa Samwel Wangwe, kuwaeleza baadhi ya viongozi msimamo wa ukoo kabla ya kutangazwa hadharani.

Baada ya maelezo hayo ambayo yalimhusisha pia Mkuu wa Mkoa, Luteni Kanali mstaafu Issa Machibya, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mara, Bw. Liberatus Barlow, Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, Bw. Zitto Kabwe na viongozi wengine wa ukoo, iliwabidi kuingia ndani kwa dakika 10 kufanya mjadala wa kuzika au la.

Baada ya muda huo, viongozi hao walitoka nje na Profesa Wangwe kupanda jukwaani na kutoa matangazo ambayo muda wote yalikuwa hayasikiki kutokana na kelele za waombolezaji, wakidai hawamtaki Mbowe bali wanataka Mbunge wao.

Hata hivyo, Bw. Kabwe alionekana kuwavuta wananchi hao kwa kusema maneno ya kumpamba marehemu, kuwa alikuwa kiongozi aliyependa kutetea wanyonge, hasa wapiga kura wake, hivyo kulazimika kunyamaza na kusikiliza kilichokuwa kikielezwa na msemaji huyo wa familia.

Katika kauli hiyo ya ukoo, Profesa Wangwe alisema:
"Sisi kama ukoo baada ya kupokea mwili wa marehemu na kuufikisha hapa, maneno mengi yamesemwa na ili kuondoa maneno hayo, tumeona ni vizuri tukachunguza mwili wa marehemu kwa kutumia mtaalamu wetu ambaye atawasili wakati wowote kuanzia sasa ... naomba sasa tuwe watulivu wakati tukisubiri hatua hiyo na mwili leo hauzikwi,” alisema Profesa Wangwe na kushangiliwa.

Kauli hiyo pamoja ya kuonesha imani kwa wananchi, lakini bado wangine walianza kutoa maneno yaliyolenga kwa Mbowe kuwa "tunataka Mbunge wetu si Mbowe," hali hiyo ilimfanya Mkuu wa Mkoa kusimama na kuomba amani.

Hata hivyo, kauli hizo hazikueleweka kwa wananchi hao hasa vijana, hivyo kumlazimu Mkuu wa Mkoa kuita polisi na kumsindikiza Bw. Mbowe katika gari lake, ambapo pamoja na ulinzi huo mkali, bado wananchi hao walimfuata hadi alipoingia ndani ya gari na kusindikizwa kwa ulinzi mkali kuelekea Tarime na hatimaye Musoma.

Pamoja na Bw. Mbowe, viongozi wengine waliohudhuria msiba huo wakiwamo wa Kenya, kila mmoja aliondoka kivyake wakihaha kutafuta magari ya kuwavusha ili kuepuka kipigo hicho kilichokuwa kikitangazwa na wananchi.

Kiongozi wa wabunge 20 waliotumwa kuwakilisha Bunge, Bw. William Shelukindo, akielezea hali hiyo alisema katika historia hajawahi kuona kitendo kama hicho lakini ilionesha jinsi wananchi hao walivyompenda Mbunge wao.

“Imesikitisha kweli imenifanya kutosoma salamu za Spika wa Bunge hata kutoa ubani wa Bunge tumekimbia kuepuka kufa pale...sasa vitu hivi vitaandaliwa utaratibu wake, lakini nawaomba wananchi watulie wamzike mbunge wao,” alisema Bw. Shelukindo.

Kwa upande wake, Waziri aliyewakilisha Serikali Bw. Steven Wassira, alisema kitendo hicho kimewasikitisha, lakini alisema hakuna njia ya kupata ukweli wa kifo cha Mbunge huyo hivyo ni vema familia kama ilivyoamua, kufanya uchunguzi huo upya katika kujiridhisha.

Bw. Wassira aliwataka wananchi wa jamii ya Tarime kuamini kuwa Bw. Wangwe amekufa na hakuna siasa kwenye jambo hilo.

"Sisi hatukuja hapa kufanya siasa , Rais (Jakaya Kikwete) alipoenda kutoa heshima hakuwa anafanya siasa, tumekuja kushirikiana na familia kufanikisha mazishi," alisisitiza Bw. Bw. Wassira na kuongeza;

"Sisi hatuna mgogoro, kama serikali tunakubaliana nao (wanafamilia) na tunaafiki uamuzi huo kwa heshima ya marehemu na familia." Bw. Wassira alisema tukio hilo ni kubwa na ni la majonzi na yanakuwa makubwa zaidi kutokana na kifo chake kuwa cha ghafla.

Alisema kabla ya kifo chake alizungumza na Bw. Wangwe Bungeni jioni akiwa mzima lakini walivyopata taarifa za kifo chake ilishangaza sana. Alisema baada ya kupata taarifa za kifo chake alikuwa wa kwanza kumjulisha kaka yake Profesa Wangwe.

Aliwataka wananchi wa Tarime kuwa wavumilivu kwani tukio hilo sio la kwanza kuwatokea na kutolea mfano kifo cha Baba wa Taifa, Marehemu Julius Nyerere.


Awali, baada ya Profesa Wangwe kutoa kauli hiyo, Bw. Kabwe alisema watahakikisha uchunguzi unafanyika na kutangaza hadharani matokeo yake na kusema tayari Polisi wamemkamata mmoja wa abiria waliokuwa wakisafiri na Mbunge huyo siku ya ajali.

"Kama kila kitu kitakwenda sawa tunatarajia kesho (leo) uchunguzi utakuwa umekamilika," alisisitiza. Alipoulizwa kama vurugu zilizojitokeza jana hazitaweza kujirudia leo Profesa Wangwe alijibu: "Mimi na wewe hatukujua kama haya (vurugu) yatatokea siwezi kusema kesho itakuwaje."

Shughuli za ujenzi wa kaburi hadi hatua hiyo inafikiwa, zilikuwa zimekamilika.

(source:majira, Imetolewa mara ya mwisho: 01.08.2008 0112 EAT.
George John, Tarime na Reuben Kagaruki, Dar)

..........................................................................

Biography: David Miliband

......................................................................
David has been MP for South Shields since June 2001. His wife Louise plays the violin for the London Symphony Orchestra, and they divide their time between London and South Shields. David is married with two children.

David was born in London and went to primary school near Leeds where he also attended Benton Park Secondary School for a year. However the bulk of his secondary education was at Haverstock Comprehensive School in London.

He studied Politics, Philosophy and Economics at Corpus Christi College, Oxford. In 1988/9 he won a Kennedy Scholarship to study for a Masters' Degree at the Massachusetts Institute of Technology in the United States.

David's first job was in the voluntary sector, working for the National Council for Voluntary Organisations. He was then Research Fellow at the Institute for Public Policy Research, and from 1992-94 Secretary of the Commission on Social Justice, set up by the then Leader of the Labour Party, John Smith, to work out new approaches to welfare policy.

From 1994 to 1997 David worked as Head of Policy for Tony Blair, working on the policies that would help Labour into government. He was then Head of the Prime Minister's Policy Unit in Downing Street during Labour's first term in office from 1997 to 2001. He helped found the Centre for European Reform, and has edited two books, Reinventing the Left, and Paying for Inequality.

David is a member of the Whiteleas and Cleadon Social Clubs, as well as President of South Shields Football Club - The Mariners.

(source: www.davidmiliband.info)
.......................................................................

Msiba: Kifo cha Mhe Chacha Wangwe (MB)

Familia yagoma kumzika Wangwe
Maziko ya aliyekuwa Mbunge wa Tarime (CHADEMA), Bw. Chacha Wangwe, yameahirishwa baada ya kutokea mtafaruku kufuatia wazee na ndugu wa marehemu kutaka uchunguzi ufanyike baada ya kudai ndugu yao alipigwa risasi mdomoni iliyojitokeza kisogoni.

Kufuatia kuahirishwa kwa maziko hayo, mtafaruku mkubwa uliibuka baada ya kundi la vijana wa kijiji hicho waliokuwa na mabango yenye ujumbe mbalimbali, kuanza kurusha mawe hovyo na kusababisha wageni wakiwemo viongozi mbalimbali waliofika kwenye maziko hayo kukimbia.

Wazee wa kijiji cha Kemakorere waligoma mwili wa marehemu kuzikwa hadi hapo uchunguzi wa kina utakapofanywa upya na daktari kutoka Dar es Salaam na wao kuridhika na ripoti yake.

Kwa mujibu wa ratiba, maziko yalipangwa kufanyika jana saa 7.15 hadi saa 8 mchana lakini kuanzia asubuhi majira ya saa 3:00, ukoo wa Wangwe ulifanya mkutano chini ya mwenyekiti wake, Profesa Samwel Wangwe na kuazimia kuahirisha maziko hadi uchunguzi wa daktari kutoka Dar es Salaam utakapofanywa upya.

Habari zilisema mara baada ya mwili wa marehemu kufikishwa kijijini kwake Kemakorere, wanandugu na wazee waliutoa kwenye jeneza na kuuangalia ambapo baadhi ya wajumbe wa kikao hicho waligundua kwamba alipigwa risasi mdomoni iliyotokea kisogoni.

Baada ya kugundua hilo, wajumbe hao waliwaeleza waandishi wa habari kuhusu suala hilo, huku wakisisitiza maziko hayo yaahirishwe hadi uchunguzi wa kifo utakapofanywa tena.

Profesa Wangwe, ambaye ni kaka wa marehemu alisema baada ya ukoo kujadili kwa kina wameona kuwa kuna utata katika kifo hicho na kwamba hawataweza kuzika kama ilivyopangwa.

Alisema wameiomba serikali kuwa na subira hadi baada ya kuletwa daktari mwingine wa kufanya uchunguzi kwa madai kuwa hawana imani na uchunguzi uliofanywa awali.

Hata hivyo, ilipotimia saa 5 asubuhi, Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Bw. Stanley Kolimba, ambaye alikuwa msimamizi wa mazishi hayo, aliiagiza kamati ya maandalizi ya madiwani kwenda kuutoa mwili wa marehemu Wangwe ili kuanza kwa ibada ambayo ingefanywa na Mchungaji wa Kanisa la Wasabato, Muso Stephen wa mtaa wa Nyabasi, lakini wana ndugu walikataa.

Viongozi wengi mashuhuri wa vyama na serikali na maelfu ya wananchi waliwasili kuhudhuria mazishi hayo.

Baadhi ya viongozi hao wakiwemo Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Salehe Ramadhan Feruzi, Mwenyekiti wa CHADEMA, Bw. Freeman Mbowe, Katibu Mkuu Dk. Wilbroad Slaa, Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, Bw. Zitto Kabwe, Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mara, Bw. Makongoro Nyerere, Mjumbe wa NEC, Christopher Gachuma, walilazimika kutimuka mbio baada ya tangazo la kuahirisha mazishi, kufuatia vijana kuanza kurusha mawe hovyo hali iliyoleta mtafaruku mkubwa.

Vijana hao walianza kukimbia huku wamebea mabango ambayo mengine yalikuwa yakiwa na ujumbe usemao, ‘bila Wangwe hakuna haki Tarime,` `viongozi mashuhuri kwa nini hufa kwa ajali na BP,` `tungeukagua mwili tungeridhika,` `Wangwe umekufa kweli kwa ajali au kwa risasi au kwa ushirikina,`.

Aidha, ndugu wa marehemu walilitaka Jeshi la Polisi kumweka chini ya ulinzi Deus Mallya, aliyekuwa ndani ya gari la marehemu wakati wa ajali iliyotokea Wilaya ya Kongwa, Dodoma, ili ahojiwe vizuri na kumtaja aliyempiga risasi Wangwe na siyo taarifa za kwamba marehemu alikufa kwa ajali.

Na katika hatua nyingine, Mwenyekiti wa CHADEMA, Bw. Freeman Mbowe, jana alinusurika kuuawa kwa mapanga baada ya kuwasili katika kijiji cha Kemakorere kuhudhuria mazishi ya marehemu Wangwe.

Hali hiyo ilianza kujitokeza saa 8:00 mchana baada ya Bw. Mbowe kuwasili kijijini hapo akiwa ameongozana na baadhi ya viongozi wengine wa vyama vya siasa, Profesa Ibrahim Lipumba (CUF), Bw. Augustine Mrema (TLP), Bw. Joseph Mbatia (NCCR-Mageuzi) na Bw. Bob Makani kiongozi mstaafu wa CHADEMA.

Baada ya kuwasili kwa viongozi hao, kundi kubwa la watu hasa vijana, walianza kumzonga Bw. Mbowe kwa kumuonyesha mabango mbalimbali ya kuonyesha kifo cha Wangwe si cha mapenzi ya Mwenyezi Mungu bali ameuawa.

Kufuatia hali hiyo, maofisa wa Usalama wa Taifa wakiongozwa na askari polisi wa kawaida na wale wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), waliwazuia wananchi hao kumzonga kiongozi huyo, lakini haikuwa kazi rahisi na hivyo kulazimika kumwingiza uani ambako shughuli za maandalizi ya mazishi hayo zilikuwa zikifanyika.

Hali hiyo ilifanya kubadilisha kabisa mazingira ya msiba huo, ambao ulihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, wabunge na wanasiasa, viongozi wa wawakilishi kutoka nchini Kenya na maelfu ya wananchi.

Mazingira hayo ya kutisha huku wananchi hao wakiwa wamebeba mapanga, mikuki, sime na fimbo wengine wakiwa wameziweka hadharani na wengine wamezificha katika makoti na kujificha migombani, ilimfanya kiongozi wa ukoo huo, Profesa Samwel Wangwe, kuwaeleza baadhi ya viongozi msimamo wa ukoo kabla ya kutangazwa hadharani.

Baada ya maelezo hayo ambayo yalimhusisha pia Mkuu wa Mkoa, Luteni Kanali Mstaafu Issa Machibya, Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Riberatus Barlrow, Naibu Katibu Mkuu CHADEMA, Bw. Kabwe Zitto na viongozi wengine wa ukoo iliwabidi kuingia ndani kwa dakika 10 kufanya mjadala wa kuzika ama la.

Baada ya dakika hizo, viongozi hao walitoka nje ambapo Profesa Wangwe alipanda jukwaani na kuanza kutoa matangazo ambayo muda wote yalikuwa hayasikiki kutokana na kelele za waombolezaji wakidai hawamtaki Mbowe bali wanataka Mbunge wao.

Hata hivyo, Bw. Kabwe, alionekana kuwakonga wananchi hao kwa kusema maneno ya kumpamba marehemu kuwa ni kiongozi aliyependa kutetea wanyonge hasa wapiga kura wake hivyo kulazimika kunyamaza na kusikiliza kilichokuwa kikielezwa na msemaji huyo wa familia.

``Sisi kama ukoo baada ya kupokea mwili wa marehemu na kuufikisha hapa maneno mengi yamesemwa na ili kuondoa maneno hayo tumeona ni vizuri tukachunguza mwili wa marehemu kwa kutumia mtaalam wetu ambaye atawasili wakati wowote kuanzia sasa naomba sasa tuwe watulivu wakati tukisubiri hatua hiyo na mwili leo hauzikwi,`` alisema Profesa Wangwe huku akishangiliwa.

Kauli hiyo pamoja na kuonyesha imani kwa wananchi, lakini wengine walianza kutoa maneno yaliyomlenga Mbowe kuwa wanataka Mbunge wao sio Mbowe.

Hali hiyo ilimfanya Mkuu wa Mkoa wa Mara, kusimama na kuomba amani.

Hata hivyo, kauli hizo hazikueleweka kwa wananchi hao hasa vijana, hivyo kumlazimu mkuu huyo kuita polisi na kuanza kumsindikiza Mbowe katika gari lake ambapo pamoja na ulinzi huo mkali, lakini bado wananchi hao walimfuata hadi alipoingia ndani ya gari na kusindikizwa kwa ulinzi mkali kuelekea Tarime kisha Musoma.

Pamoja na Mbowe na viongozi wengine waliohudhuria msibani hapo wakiwemo hao wa Kenya, kila mmoja aliondoka kivyake na kuanza kuhaha kutafuta magari ya kuwavusha kuepuka kipigo hicho kilichokuwa kikitangazwa na wananchi.

Kiongozi wa wabunge 20 waliotumwa kuwakilisha Bunge, Bw. William Shelukindo, akielezea hali hiyo alisema katika historia hajawahi kuona kitendo kama hicho lakini imeonyesha jinsi wananchi hao walivyompenda Mbunge wao.

``Imesikitisha kweli imenifanya kutosoma salamu za Spika wa Bunge hata kutoa ubani wa Bunge tumekimbia kuepuka kufa pale...sasa vitu hivi vitaandaliwa utaratibu wake lakini nawaomba wananchi watulie wamzike mbunge wao,`` alisema Shelukindo.

Kwa upande wake waziri aliyewakilisha serikali, Bw. Steven Wassira alisema kitendo hicho kimewasikitisha lakini alisema hakuna njia ya kupata ukweli wa kifo cha mbunge huyo ni vema familia kama ilivyoamua kufanya uchunguzi huo upya katika kujiridhisha.

Awali baada ya Profesa Wangwe kutoa kauli hiyo Bw. Kabwe alisema uchunguzi watahakikisha unafanyika na kutangaza hadharani matokeo yake na kusema tayari polisi wamemkamata mmoja wa abiria aliyekuwa akisafiri na mbunge huyo siku ya ajali.

Shughuli za ujenzi wa kaburi hadi hatua hiyo inafikiwa ilikuwa imekamilika na hadi jioni hii hakuna taarifa zaidi zilizotolewa kuwa mwili wa marehemu huyo utazikwa lini.

(SOURCE: 2008-08-01 11:15:21
Na George John, PST Tarime, Nipashe)

...........................................................................