Monday 30 June 2008

Kituo cha Polisi Kati ( ni tafsiri sahihi?)

Mara nyingi vyombo vingi vya habari hutangaza tafsiri ya maneno 'Central Police Station' kama kituo cha Polisi cha 'Kati'.

Mimi huwa nafikiri kuwa tafsiri sahihi ni kituo 'Kikuu' cha Polisi.

Mfano:
Kamati Kuu ya CCM huwa ni 'CCM's Central Committee'
Benki Kuu ni 'Central Bank', n.k.

Inakuwaje kiitwe kituo cha kati? Au ndio tafsiri sahihi? Ningependa kuelemishwa kuhusu hiyo tafsiri, maana inawezekana mimi ndie nimepitiwa kidogo!

..........................................................
KWA MFANO TAZAMA HII HABARI:

Mintanga akamatwa na polisi
(Source: Nipashe, 2008-07-07 09:03:21. By Somoe Ng'itu)
Jeshi la Polisi nchini linamshikilia Rais wa Shirikisho la Ngumi za Ridhaa Tanzania (BFT), Shaaban Mintanga kutokana na kudaiwa kuhusika na sakata la mabondia wa hapa nchini kukamatwa Mauritius kwa tuhuma za kukutwa na madawa ya kulevya.

Mintanga, ambaye awali alikuwa Rais wa Chama cha Ngumi mkoa wa Dar es Salaam (DABA) anashikiliwa katika kituo cha Polisi Kati.
.....................................

Euro2008: España Campeones!!!

It was 22 days of action and entertainment from Saturday (first game KO 17:00 BST) June 07 to Sunday (last game KO 19:45 BST) June 29, and finally, Spain are the new Europen Champions after a 1-0 victory over Germany yesterday in Vienna, Austria.

How they (Spain) made it:
GROUP D
Tue 10/06/2008 KO 17:00 BST Spain 4 v. Russia 1
sat 14/06/2008 KO 17:00 BST Sweden 1 v. Spain 2
Wed 18/06/2008 KO 19:45 BST Greece 1 v. Spain 2

QUARTER FINAL
Sun 22/06/2008 KO 19:45 BST Spain 0 (AET) 4 (pens.) v. Italy 0 (AET) 2 (pens.)

SEMI FINAL
Thu 26/06/2008 KO 19:45BST Russia 0 v. Spain 3

FINAL
Sunday 29/06/2008 KO 19:45 BST Germany 0 v. Spain 1

SPAIN CHAMPIONS EURO-2008 co-hosted by Austria and Switzerland.
..............................................................

Ripoti ya EPA

(Na Mwandishi Wetu, 29.06.2008 0033 EAT. (Majira))
Ripoti ya ufisadi EPA yavuja
*Yadai Utawala wa Mkapa ulishindwa kuuzuia
*Kampuni zenye fedha zao zatinga mahakamani

SERIKALI ya Awamu ya Tatu chini ya Rais Mstaafu, Bw. Benjamin Mkapa, ilishtukia harufu ya ufisadi kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), iliyokuwa kwenye Benki Kuu ya Tanzania (BoT) tangu mwaka 1997 lakini ikashindwa kuizuia.
Makosa hayo ya utawala wa Mkapa ndiyo yaliyoendelea kuruhusu mwanya wa ufisadi kwenye akaunti hiyo hadi Januari, mwaka juzi ulipoingia utawala wa Rais Jakaya Kikwete. Hayo yamo kwenye ripoti ya ukaguzi iliyofanywa na kampuni ya Ernst & Young ambayo gazeti hili limenasa nakala yake.
Katika kipindi cha wiki kadhaa, ripoti hiyo iliyokuwa siri kubwa, imekuwa ikisambazwa kwa kasi miongoni mwa watu mbalimbali baada ya kuvuja kutoka serikalini. Ripoti hiyo ndiyo iliyosababisha Rais Kikwete kumfuta kazi aliyekuwa Gavana wa Benki hiyo, marehemu Dkt. Daud Balali na kuingia Profesa Benno Ndulu.
Utata wa malipo ya EPA Ripoti hiyo inaanika kuwa tangu mwaka 1997 Serikali ya Mkapa ilianza kubaini utata katika uendeshaji wa akaunti ya EPA na kuanza kuihoji BoT ikitaka maelezo ya kina kuhusu akaunti hiyo.
"Tume ya Ukaguzi imebaini kuwa kupitia barua ya aliyekuwa Katibu Mkuu wa Hazina (Raphael Mollel) ya Oktoba 17, 1997, Wizara ya Fedha ilianza kuwa na shaka kuhusu uendeshaji wa akaunti ya EPA," inasema ripoti ya Ernst & Young na kukariri sehemu ya barua hiyo ya Mollel kwenda BoT iliyoandikwa:
"Hazina ingefurahi kama ingeweza kupata hesabu halisi ya fedha zilizoko kwenye akaunti ya EPA, ili iweze kuweka sera nzuri zaidi katika matumizi ya fedha hizo."Kama unavyojua Hazina imekuwa ikipata tetesi zinazotofautiana kuhusu hali halisi ya akaunti hiyo. Wakati fulani iliashiriwa kwamba hakuna pesa yoyote kwenye akaunti hiyo na kuwa madeni yangepaswa kulipwa kupitia raslimali za nchi."Uchunguzi huo hata hivyo umebaini kuwa pamoja na barua hiyo, uongozi wa BoT haukuwa tayari kutoa ushirikiano huo, jambo ambalo sasa linazidi kuiongezea nguvu dhana, kwamba ufisadi kwenye akaunti hiyo ulianza kufanyika siku nyingi.
Baada ya miaka mingi ya ukimya, hatimaye katika barua yake ya Julai 2005, kwenda kwa Katibu Mkuu wa Hazina, Bw. Gray Mgonja, Gavana wa Benki Kuu wakati huo, Dkt. Ballali, aliashiria kuwa isingekuwa rahisi wao kutoa hesabu halisi ya fedha zilizokuwa kwenye akaunti ya EPA. Akataja tatizo la mfumo wa kompyuta."Ifahamike kuwa ni vigumu kwa sasa kutoa hesabu halisi za akaunti ya EPA, kwa sababu malipo yote yanafanyika kadri maombi (ya wadai) yanavyokuja na hakuna muda maalumu. Hata hivyo pindi matatizo ya kiufundi katika mfumo wetu wa kompyuta yatakapokuwa tayari, tutakuwa katika nafasi nzuri ya kutoa mchanganuo," ilisema barua hiyo. Tofauti na maelezo hayo ya Dkt. Ballali, hesabu za wadai zilizo sahihi na zilizokuwa na utata zilikwishawekwa bayana kupitia ripoti ya Lazard iliyokamilika mwaka 2004 na zaidi, wakati BoT wakisingizia mtandao wa kompyuta kuwa mbovu, mtandao huo huo ndio mwezi mmoja uliofuata, uliotumiwa na watendaji wa Benki hiyo kuidhinisha malipo kwa kampuni 22.
Uchunguzi unaonesha kuwa wakati Dkt. Ballali akiieleza Serikali kuwa kulikuwa na tatizo la kompyuta, lakini malipo yakaendelea kupitia orodha zilizokuwa kwenye mtandao huo, hadi mauti yanamfika jijini Washington, Marekani, hivi karibuni. Hakuwahi pia kuipa Serikali taarifa rasmi kuhusu EPA kama alivyoahidi na kama ilivyoombwa tangu mwaka 1997 na Serikali nayo ilionekana ghafla kuondoa wasiwasi wake juu ya akaunti hiyo."Timu ya ukaguzi haikupata ushahidi wowote kuwa mchanganuo huo uliwahi kuwasilishwa kwenye Wizara ya Fedha," inakariri Ernst & Young katika ukurasa wa 19 wa ripoti yake. Mchanganuo mgumu?Wakati viongozi BoT wakishindwa tangu mwaka 1997 kuonesha mchanganuo wa fedha za EPA, uchunguzi wa kikaguzi umedhihirisha kuwa katika akaunti ya fedha hizo namba 9991 509 101 ambayo awali ilikuwa NBC kabla ya kuhamishiwa kwenye akaunti namba 9924 191 011 iliyokuwa BoT, ushahidi kadhaa uliopatikana umehitimisha kuwa mfumo wa kompyuta ya akaunti hiyo haukuwa na hitilafu yoyote na ulikuwa ukiendelea kutumika. Kwa mfano, hadi mwaka 2004 takwimu halisi kuhusu akaunti ya EPA zilikuwa hivi:
Madeni yaliyohakikiwa na kulipwa dola milioni 228,
madeni ambayo wadai waliruhusu yafutwe (ikiwa sehemu ya msaada) dola milioni 216. Jumla ndogo dola milioni 444.
Hesabu zaidi za akaunti hiyo zinaonesha kuwa sehemu kubwa ya deni hilo iliyosalia ilikuwa haijalipwa kwa sababu mbalimbali kama ifuatavyo:
Madeni yaliyokuwa na utata/kesi dola milioni 25, wadeni waliokataa masharti (ya mkusanya madeni) dola milioni 14,
deni lisilokidhi viwango (cha mkusanya madeni) dola milioni tatu, wadai ambao hawakujitokeza kabisa dola milioni 48, deni ambalo ilishindikana kuhakikiwa, dola milioni 143, jumla ndogo dola milioni 233 na jumla ya deni lote (lililolipwa na lililobaki na utata) dola milioni 677. Kwa mujibu wa mapendekezo ya Mkaguzi wa Kimataifa M/S Lazard aliyefadhiliwa na Benki ya Dunia, BoT ilishauriwa kutolipa deni lililosalia lenye utata la dola milioni 233, kutokana na utata ulioanishwa hapo juu na ushauri huo ulikuja kutiliwa nguvu baadaye na ripoti nyingine ya wakaguzi wa PriceWaterhouseCoopers ya Ufaransa. Lakini mwaka mmoja baadaye, BoT hiyo hiyo ikaibuka, katika mazingira tata na kuanza kuwalipa waliojiita mawakala wa kampuni hizo za nje. Kipindi chote hicho Serikali iliyokuwa imekwishaona utata na iliyokuwa ikinyimwa ripoti za akaunti hiyo, haikuonekana kuwa na wasiwasi tena."Ripoti (ya wakaguzi kutoka M/S Lazard) ilihitimisha kuwa sehemu kubwa ya madeni yalishapitwa na wakati na ikaishauri Wizara ya Fedha kutoyalipa," inasema ripoti ya Ernst&Young, Wizi wa kisomi Huku zikitumia mihuri ya mawakili wenye majina na maelezo hewa, nyingi kati ya kampuni 22 zilizopitishiwa malipo kutoka akaunti ya EPA, sasa imebainika kuwa zilighushi nyaraka mbalimbali. Ernst & Young wanaonesha kuwa kati ya sh. 133,015,186,220 zilizochotwa kutoka EPA, nyaraka zilizowasilishwa na zile kampuni 22 zinazotuhumiwa kuchota sh. 90,359,078,804, 13 zilibainika kuwa za kughushi. Ripoti ikaeleza zaidi kuwa kiasi kilichosalia cha sh. 42,656,107,416.61 haikuweza kubainika mara moja usahihi au ubatili wake, kwa sababu mbalimbali ikiwamo kukosekana nyaraka zozote au sehemu ya fedha hizo kuwa na kesi mahakamani. Serikali kizimbani Hivi sasa pamoja na kuwapo kesi za awali, imebainika kuwa baadhi ya kampuni ambazo majina yao yalitumika katika ulaghai wa fedha za EPA ikidaiwa kuwa yalitoa ruhusa madeni yalipwe kwa niaba yao, yamekana kufanya hivyo na baadhi pamoja na mambo mengine, yakilalamikia uzembe wa Serikali ya Tanzania kupitia BoT kwa kuwalipa watu ambao wao kamwe hawakuwa na mikataba nao. Majira Jumapili ilijaribu kuwasiliana na baadhi ya kampuni zilizoingizwa katika utapeli wa EPA kwa fedha zao kulipwa mawakala hewa, karibu zote ziliamua kutolizungumzia suala hilo, huenda zikisubiri hatua za kisheria.Watendaji wa kampuni za Mirrlees Blackstone ambayo kuanzia mwaka 2002/03 ilibadili jina na kuitwa Man B & W Diesel Limited, Metsopaper na Iveco ambazo ni miongoni mwa wahanga wa majina na mihuri yao kughushiwa, hawakupenda kulizungumzia sana suala hilo kwenye vyombo vya habari walipotakiwa na gazeti hili kulizungumzia. Sakata la EPA kwa kifupi Kati ya mwaka 1970 na 1980, Serikali ya Tanzania ilipokea huduma mbalimbali kutoka kampuni na taasisi za nje, lakini kushuka kwa thamani ya shilingi kulikochangiwa na vita ya Kagera kunaifanya Serikali ishindwe kulipa madeni hayo kutokana na ukosefu wa fedha za kigeni.Kati ya mwaka 1985 na 1995, Benki ya Dunia iliona haja ya kuisaidia Tanzania kulipa madeni hayo kupitia mikakati mbalimbali ukiwamo wa kuyanunua (Debt Buy Back).
Mwaka 1985 Akaunti ya EPA ilihamishwa kutoka NBC kwenda BoT.Mwaka 1994, ili kuhakiki wadai halisi, Tanzania ilitangaza kwenye vyombo vya habari vya kimataifa wenye madai wajitokeze. Kampuni chache sana zikaitikia mwito huo.

Saturday 28 June 2008

Kamba au usanii?

Jana mwanahabari mmoja (political editor) wa bbc bwana Nick Robinson aliniacha hoi!

Alikuwa akielezea kwenye tv kuhusu kupanda bei ya mafuta (fuel). Akaenda kituo cha mafuta, akachukua pampu na kuingiza katika tenki la gari yake huku akiendelea kulonga juu ya kupaa bei za mafuta kila kukicha!

Baada ya dakika moja hivi alirudisha pampu na kufunga kifuniko cha tanki.

Lakini cha ajabu muda wote huo jamaa akilonga maneno lukuki mita ya mafuta ilikuwa inaonyesha mafuta yanaingia ni lita 0.000 na bei ya mafuta yanayoingia 0.000, kilichokuwepo pale ni bei inaoonyesha kuwa lita moja ni kiasi fulani.

Kumbe alienda pale kuzuga tu!! Jamaa angesimama tu aseme maneno badala ya kuzuga kituoni kama vile anajaza mafuta kumbe anawakinga wenzake ambao walikuwa na shida ya kweli kujaza mafuta kwa pampu hiyo aliyoing'anga'ania muda wote huo.

Acha hizo Nick!! 'You have Been Framed'
.............................

What a concert for 'Madiba'!

I wish Sarafina and her friends were at Hyde Park yesterday to witness what they had been waiting for many years. In the film 'Sarafina', Leleth Khumalo plays a starring role as Sarafina in the struggle to free Nelson Mandela and for the South Afican freedom. Ms Leleth Kumalo played 'Nelson Mandela' in the concert in that famous film titled 'Sarafina'.

Well, the Hyde Park in London was full to capacity. Music stars and other respected public figures from all over the world, including PM Gordon Brown, were present at the Nelson Mandela's birthday concert.

The perfomance was terrific. Amy Winehouse was fabulous with her hit 'Rehab' and she later came back to lead the song 'Free Nelson Mandela', originally sang in 1988 at Wembley Stadium for Mandela's 70th birthday while he was still in jail. In his brief speech yesterday, Mandela confirmed that he and his colleagues, far away in the prison, heard the voices from London! He was actually thanking Londoners for that.

Mandela said that after 90 years now it is time for the 'new hands to lift the burden' and he finished by saying 'it is in your hands, Thank You!'

It is also worth mentioning other hits which shook the crowd with jubilation. 'Gimme Hope Jo'anna' by Eddy Grant was very much entertaining. Sipho (hard-stick) Mabuse entertained the crowd with the song 'Jive Soweto'. His famous saxaphone was an attraction of its own, and he was supported by the choir from Soweto! Mmmh! His stage show girls were fantastic.

Jamelia, Leona Lewis, Simple Minds and Will Smith, just to mention few, added colour in the concert last evening.

I think that this was a chance for Nelson Mandela to say goodbye to the world in public. He wishes to spend his time in private - writing autobiography and sharing time with close family members and friends after a hectic public schedule after he was released from jail on 11 February 1990.
...............................................................

Friday 27 June 2008

June 27, 2008: It's Mandela & Brown's Day

1. Nelson Mandela's fund-raising concert at Hyde Park in London is taking place later today.
Funds realised will go to his charity 46664 (HIV, Aids Campaign).
It is part of his 90th birthday celebrations culminating on the actual 'big day' on July 20.
...................................................................

2. Today is Gordon Brown's Anniversary.
One year as the Leader of the Labour Party and as the British PM after taking over from his predecessor Tony Blair exactly one year ago.

Gordon Brown has had a very hard time during his first year in office, especially, because of his indecision on whether to call the General Elections last October. He let the rumours go on for too long, only to announce late that elections were not going to take place! For sure, the 'indecision' did a great deal of harm to his reputation for the first time since he took helm.

On other hand, issues like the closure of over 2,000 Post Offices in the country and the abolition of the 10p tax band (and to introduce one flat band of 20p) did not do him any favours!

However, his last performance in the PMQs on wednesday was fantastic! He warned the leader of the opposition David Cameron, 'You can get by without substance some of the time, but you cannot get by without substance all of the time'. Some political commentators say that David Cameron does not have specific policies.
................................................................

3. USA: (source: www.cdc.gov) National HIV Testing Day, June 27, 2008
June 27 is National HIV Testing Day, which focuses on the importance of knowing one's current human immunodeficiency virus (HIV) infection status.

In 2003, approximately 25% of the estimated 1 million persons in the United States infected with HIV were unaware of their infection.

CDC* encourages learning one's HIV status through HIV testing and has recommended that voluntary HIV testing be offered routinely in health-care settings to all persons aged 13-64 years. Persons at higher risk for HIV should get tested more frequently (e.g., men who have sex with men should get tested at least annually).

To address the disproportionately high rate of HIV infection among blacks, CDC has increased HIV testing opportunities in 23 geographic areas with the largest number of HIV cases, so that more blacks can know their HIV status.

Persons who learn that they are infected with HIV at an earlier stage of infection can survive longer by receiving appropriate care and can prevent transmitting HIV to others. Additional information is available at http://www.hivtest.org

CDC* - Centers for Disease Control and Prevention
..........................................................

Thursday 26 June 2008

Ghorofa lililoporomoka Dar: Nini kinafanyika?

Hivi karibuni nilipata habari za kuporomoka kwa jengo refu la ghorofa 10 huko Dar (barabara ya Kisutu/Zanaki). Baada ya jengo kuanguka wananchi wanajiuliza na kushindwa kujua lawama zimwendee nani.

Nitajaribu kufafanua juu ya kazi iliyopo ktk miradi mikubwa inayofanana na huu wa Jengo lililoanguka Kisutu, Dar, pamoja na wahusika ktk nafasi zao (nani ni nani ktk miradi kama hii).

Lengo langu sio kumnyooshea kidole yeyote aliyehusika ktk ujenzi wenyewe.

Wahusika wakuu ni kama ifuatavyo:
1. Mwenye jengo (client)
2. Msanifu/wasanifu wa jengo (designers -architect as head of the team)
3. Makandarasi (contractors -engineers)
4. Makandarasi wadogo (sub-contractors -engineers, materials suppliers etc.)
5. Mamlaka (wapitisha michoro na kutoa kibali)
6. Wananchi (Public as eventual users or neighbours)

Kazi ya mwenye jengo ni kutoa kazi (yeye ndiye mwenye mradi na anaulipia). Anamtafuta mtaalamu ili amfanyie kazi ili atimize ndoto yake.

Mtaalamu ambaye anachukua jukumu la kutimiza ndoto ya mwenye jengo ni masanifu majengo (architect). Msanifu majengo anafanya kazi ya uchambuzi wa mahitaji wa mwenye mradi (client's requirements) kwa kuzingatia uwezo wa kifedha wa client.

Client anaweza kumpa architect mahitaji ya mradi wake (Client's Requirements) au architect anaweza kumwandalia mteja wake mahitaji hayo.

Baada ya utafiti (analysis) msanifu majengo anamwendea mwenye mradi (client) na kumwonyesha mapendekezo (sketchy propasals) pamoja na makisio ya gharama ya mradi (cost estimates). Mwenye mradi akiyakubali mapendekezo, msanifu anaandaa michoro yote.

Michoro husika ni ya kisanifu (architectural) na ya kihandisi (engineering drawings). Kazi hii inafanywa na timu ya wataalamu ktk fani ya majengo/ujenzi chini ya uangalizi wa msanifu majengo.

Kwa ufupi:
Architect ni mshauri wa mradi na anakuwa kiungo kati ya mwenye mradi (client) na wajenzi/makandarasi.

Architect anaandaa:
1. Brief (habari kuhusu mradi -site location, analysis (incl. soil investigation)),
2. Michoro (architect and engineer/working drawings),
3. Schedules,
4. Specifications of materials and workmanship,
5. Cost estimates (Bill of Quantities),
6. Contract document.

Baada ya hapo kinachofuata ni mchakato wa kutangaza tenda (tendering). Makampuni yanayopenda kujenga mradi husika yanatuma maombi kwa kufuata utaratibu uliotangazwa na mwenye mradi. Baada ya hapo uchambuzi unafuatia kwa kuchagua kampuni itakayojenga mradi (pamoja na wakandarasi wadogo kama watahitajika kulingana na ukubwa wa mradi).

Kinachofuatia ni kutoa/kukabidhi mradi kwa mkandarasi aliyeshinda tenda (contract offer)

Hatua ya mwisho ni mradi kuanza (ujenzi).

Kazi inapoanza architect anakuwa ni mkaguzi wa maendeleo ya mradi. Wakandarasi kazi yao ni kutumia michoro na vipimo (and specifications) viliyotayarishwa na architect ili kujenga jengo kama ilivyoonyeshwa ktk makubaliano (contract). Zaidi ya hapo kila asubuhi au kila wiki kunakuwa na mkutano ktk 'site' (site meeting) ili kujadili maendeleo ya Ujenzi wa mradi au matatizo yaliyojitokeza na kuyatafutia ufumbuzi. Mawasiliano yote kati ya wahusika yakuwa ktk maandishi (kwa kumbukumbu).

Kuhusu Jengo lililoanguka Kisutu, Dar
Tume iliyoundwa, kwa msaada wa wataalamu (wasanifu majengo, wahandisi, surveyors etc.), watachunguza hatua zote hapo juu na kuona kila mhusika kwa nafasi yake alitimiza wajibu wake ipasavyo.

Tume itachunguza michoro ya ujenzi na kulinganisha na ubora wa kazi yenyewe ya ujenzi kama ilifuata specifications zilizotolewa na wataalamu. (Kuanzia msingi wa jengo; type of foundation and contruction methodoly, kuta au structural members, cement-sand-aggregates ratios, etc.)

Tume itaangalia kumbukumbu za mawasiliano (nyaraka) kati ya wahusika kwenye ujenzi wa mradi.

Itachunguza kama wahusika ngazi zote wana elimu na uzoefu unaostahili ktk ujenzi wa mradi huo wa jengo (eneo la Kisutu, la ghorofa kumi)

Pia itachunguza kama mamlaka husika zilipitia michoro na kutoa kibali cha kazi kwa uwazi na haki.

Kwa maoni yangu, hayo ni baadhi ya mambo ambayo tume ya uchunguzi iliyoundwa na mkuu wa mkoa wa Dar itayapitia ktk kazi yake ya kutafuta chanzo na undani wa tatizo au matatizo yaliyosababisha tukio la kuanguka kwa jengo hilo la ghorofa kumi, mali ya Kampuni ya McSon Investment Ltd.
..................

Mhe AC: Tunakukumbuka

Leo umetimia mwaka mmoja kamili tangu Mbunge wa CCM (Vijana) Mhe Amina Chifupa Mpaka-njia afariki dunia ktk hospitali ya JWTZ Lugalo.

Nimeikumbuka siku hii kwa sababu ya kile alichokiamini na kukipigania Mhe Amina enzi za uhai wake.

Aliweka mbele maslahi ya Taifa na kupigania haki za wananchi hasa kina mama na vijana. Alikuwa mbele ktk kuhamasisha michezo nchini na aliwahi kusafiri nje ya nchi akiwa na timu ya Taifa (Stars) ktk mchezo dhidi ya timu ya taifa ya Msumbiji.

Pia alikuwa na njozi za kuanzisha na kusimamia mashindano ya vijana wa chini ya umri wa miaka 17 nchini kote. Bahati nzuri mwaka huu michuano hiyo imefanyika chini ya udhamini wa kampuni ya vinywaji baridi -coca-cola. Ingawa mashindano haya yamefanyika baada ya Mhe Amina Chifupa kututoka, jambo la msingi ni kuwa atakumbukwa kwa kuwa miongoni mwa waasisi wa mawazo ya michezo hii.

Ninapendekeza kuwa michuano hii kuanzia mwakani iitwe 'Mashindano ya Kombe la Amina Chifupa' kwa heshima yake ktk kuwawakilisha na kuwapigania vijana wa rika zote.
....................................................................

Biography (Amina Chifupa (MP))

Born: May 20, 1981.

Education:
Primary School in Mwanza.
Secondary school: Kisutu Secondary School in Dar es Salaam in 1994.
(completed O`Level education in 1998)
High School: Tambaza Secondary School and Makongo Secondary School (completed Form Six in 2001)

Employment:
-Member of Parliament (CCM, Vijana)
-Radio Clouds FM, Dar es Salaam-based as a broadcaster.
(She held the post until she ventured into politics in 2005 through the CCM youth wing)

Higher education:
Enrolled as student at the Open University of Tanzania for a Bachelor`s degree in Political Science.

(SOURCE: Guardian, 2007-06-28 09:07:35. By Guardian Reporter)
..............................................

Tuesday 24 June 2008

Kuanguka kwa jengo Kisutu: Jicho langu

Baada ya jengo kuanguka wananchi wanajiuliza na kushindwa kujua lawama zimwendee nani.

Nitajaribu kufafanua juu ya kazi iliyopo ktk miradi mikubwa inayofanana na huu wa Jengo lililoanguka Kisutu, Dar, pamoja na wahusika ktk nafasi zao (nani ni nani ktk miradi kama hii).

Lengo langu sio kumnyooshea kidole yeyote aliyehusika ktk ujenzi wenyewe.

Wahusika wakuu ni kama ifuatavyo:
1. Mwenye jengo (client)
2. Msanifu/wasanifu wa jengo (designers -architect as head of the team)
3. Makandarasi (contractors -engineers)
4. Makandarasi wadogo (sub-contractors -engineers, materials suppliers etc.)
5. Mamlaka (wapitisha michoro na kutoa kibali)
6. Wananchi (Public as eventual users or neighbours)

Kazi ya mwenye jengo ni kutoa kazi (yeye ndiye mwenye mradi na anaulipia). Anamtafuta mtaalamu ili amfanyie kazi ili atimize ndoto yake kwa kumpa mahitaji yake mtaalamu au mtaalamu anamuandalia mahitaji client.

Mtaalamu ambaye anachukua jukumu la kutimiza ndoto ya mwenye jengo ni masanifu majengo (architect). Msanifu majengo anafanya uchambuzi wa mahitaji wa mwenye mradi (client) kwa kuzingatia uwezo wa kifedha wa client. Baada ya utafiti (analysis) msanifu majengo anamwendea mwenye mradi (client) na kumwonyesha mapendekezo (propasal) na makisio ya gharama (approximate estimats). Mwenye mradi akiyakubali mapendekezo, msanifu anaandaa michoro yote. Michoro husika ni ya kisanifu (architectural) na ya kihandisi (engineering drawings).

Kwa ufupi:
Architect ni mshauri wa mradi na anakuwa kiungo kati ya mwenye mradi (client) na wajenzi/makandarasi.

Architect anaandaa:
1. Brief (habari kuhusu mradi -site location, analysis (incl. soil investigation)
2. Michoro (architect and engineer/working drawings)
3. Schedules
4. Specifications of materials and workmanship
5. Cost estimates (Bill of Quantities)
6. Contract document

Baada ya hapo kinachofuata ni mchakato wa kutangaza tenda (tendering). Uchambuzi unafuatia kwa kuchagua kampuni itakayojenga mradi, na wakandarasi wadogo kama watahitajika kulingana na ukubwa wa mradi.

Kinachofuatia ni kutoa/kukabidhi mradi kwa mkandarasi aliyefuzu tenda (contract offer)

Hatua ya mwisho ni mradi kuanza (ujenzi).

Architect anakuwa ni mkaguzi wa maendeleo ya mradi. wakandarasi wao kazi yao ni kutumia michoro na vipimo (and specifications) viliyotayarishwa na architect ili kujenga jengo kama ilivyokusudiwa na mwenye mradi.

Jengo lililoanguka Dar
Tume iliyoundwa kwa msaada wa wataalamu (wasanifu majengo na wahandisi as expert witnesses) watachunguza hatua zote hapo juu na kuona kila mhusika kwa nafasi yake alitimiza wajibu wake ipasavyo.

Tume itachunguza michoro ya ujenzi na kulinganisha na ubora wa kazi yenyewe ya ujenzi kama ilifuata specifications zilizotolewa na wataalamu. (Kuanzia msingi wa jengo -aina na ujenzi wake, kuta, structural members, cement, sand, aggregates ratio etc.)

Itachunguza kama wahusika ngazi zote wana elimu na uzoefu unaostahili ktk ujenzi wa mradi huo (eneo la Kisutu, la ghorofa kumi, mali ya Kampuni ya McSon Investment Ltd)

Mamlaka husika kama zilipitia michoro na kutoa kibali cha kazi kwa uwazi na haki.

Kwa maoni yangu binafsi hayo ni baadhi ya mambo ambayo tume ya uchunguzi iliyoundwa na mkuu wa mkoa wa Dar itayapitia ktk kazi yake ya kutafuta chanzo na undani wa tatizo au matatizo yaliyosababisha tukio la kuanguka kwa jengo hilo la ghorofa kumi, mali ya Kampuni ya McSon Investment Ltd.
..................


(SOURCE: Alasiri, 2008-06-23 17:44:47. Na Sharon Sauwa, Jijini)
Juzi, mishale ya saa 4:00 na saa 5:00, jengo hilo la ghorofa kumi, mali ya Kampuni ya McSon Investment Ltd ambalo likuwa likijengwa na mkandarasi wa Kampuni ya N.K Decorators lilianguka na kuzua kizaazaa cha aina yake.

Katika tukio hilo, watu walioshuhudia walisema kuwa dalili za jengo hilo kutaka kuanguka, zilionekana tangu mapema na watu walipewa taarifa za kutoka.

Baada ya kuanguka, kazi ya ukoaji ilifanywa kwa kukishiriana na Jeshi la Wananchi wa Tanzania, Zimamoto na mgambo wa Jiji la Dar es Salaam.

Tayari Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Abbas Kandoro ameshaunda timu ya kuchunguza tukio hilo, ambayo imepewa wiki mbili kukamilisha kazi yake.
........................................................

TZ: Mbunge afafanua 'madudu' ya EPA

Asante Mhe. Slaa kwa kutufafanulia, hata mie nilikuwa sifahamu haya mambo kwa undani!
......................................................
....................................................
Slaa amjibu Mkulo
(SOURCE: Nipashe, 2008-06-24 12:23:01. Na Mwandishi Wetu, Dodoma)
Mbunge wa Karatu (CHADEMA), Dk. Wilbroad Slaa, amemjibu Waziri wa Fedha, Bw. Mustapha Mkulo, kuwa amepotosha umma na kwamba kambi ya upinzani imeshtushwa na kauli aliyoitoa kuwa fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) si za serikali bali za wafanyabiashara.

Dk. Slaa ambaye ni Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani kuhusu makadirio ya matumizi ya fedha za ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, alisema bungeni jana kuwa kauli hiyo ni ya kupotosha.

Taarifa hiyo ni ya kupotosha. Kambi ya Upinzani imefanya utafiti wa kina na kugundua kuwa fedha hizo kimsingi zinatokana na programu inayoitwa ``Debt Buy Back Program``.

EPA imefanyiwa kazi sana na Timu ya Lazard na baadaye ukaguzi wa PricewaterhouseCoopers (France) tarehe 25 November, 2004,`` alisema.

Aliongeza, hata hivyo, kwamba ukaguzi uliofanywa na Deloitte and Touche 2006 na baadaye kuthibitishwa na Ernst and Young, 2007 ulithibitisha kuwa kampuni 22 zilifanya biashara na makampuni yanayodhaniwa kuwa ni ``hewa``.

Alisema hivyo wafanyibiashara hao, wala ``principles`` wao kutoka nchi za nje hawakuweka fedha zozote BoT kwa lengo kutumiza masharti ya Debt Buy Back Program kama alivyotaka kueleza Waziri wa Fedha.

Alisema kwa msingi huo, fedha zilizoibwa ni za serikali na kwamba kwa taarifa aliyonayo, Ripoti ya Ukaguzi wa EPA katika kifungu cha 3.20, 3.23, na 3.24, kinatamka wazi uwepo wa ``fraudulent supporting documents submitted in to support claims`` (nyaraka za kughushi ili kuhalalisha malipo).

Alisema ufisadi uliotumika ni pamoja na kutumia hati za kughushi katika kutoa fedha kutoka BoT, malipo ya viwango visivyo sahihi au kutumia viwango visivyo sahihi vya kubadilisha fedha (incorrect amounts and incorrect exchange rate).

Alisema ukaguzi ulionyesha kuwa kati ya Sh. bilioni 133, malipo ya zaidi ya sh. bilioni 90.3 yalifanyika kwa kutumia hati za kughushi (invalid and fraudulent supporting documents) na kwamba nyaraka hizo zimeonyeshwa katika kiambatanisho C, zikionyesha pia majina ya makampuni husika.

Dk. Slaa alisema katika kifungu cha 3.25, ukaguzi huo ulishauri kuwa kwa malipo ya zaidi ya Sh. bilioni 42.6, uchunguzi wa kina unahitaji kufanyika.

Alisema taarifa hiyo haikutolewa wazi kwa Bunge wala kwa Watanzania ambao ndio wenye mali hiyo na serikali ni mdhamini kwa niaba yao tu.

``Ufisadi unaotisha zaidi ni ule uliofanyika kupitia Kampuni ya Kagoda Agriculture Ltd iliyosajiliwa nchini, chini ya Sheria ya Makampuni, Sura ya 212, tarehe 29 Septemba, 2005 na kupata hati namba 54040.

Wakurugenzi waliosajiliwa wa Kagoda ni watu wawili wenye anuani za Kipawa Industrial area, Plot no 87 Temeke Dar es Salaam, na P.O. Box 80154 Dar es Salaam, kinyume na utaratibu wa kusajili makampuni kwa wakawala wa serikali, BRELLA, ambao unahitaji wakurugenzi wa makampuni kujisajili kwa kuonyesha anuani ya mahali anapoishi na siyo Sanduku la Posta,`` alisema.

Aliongeza kuwa kwenye fomu za usajili, ambapo John Kyomuhendo amejionyesha kuwa ``Promoter`` hawakuonyesha kama ni wakurugenzi mahali pengine kwenye kampuni nyingine yeyote.

``Cha kushangaza ni kuwa kampuni hiyo ambayo wakurugenzi wake dhahiri wanaonekana wapya kabisa katika uwanja wa biashara, ndani ya wiki nane tu walikuwa wamekwisha kuchotewa zaidi ya Dola za Marekani milioni 30.8, yaani zaidi ya sh. bilioni 40 kwa kinachoelezwa na ukaguzi wa EPA kuwa hati bandia ambazo dalili za wazi ni kuwa hati hizo karibu zote zimesainiwa na watu wasiohusika,`` alisema.

Alisema baadhi ya makampuni yaliyodhaniwa kufanya biashara na Kagoda au hayako kabisa au yamekwisha kubadilisha majina yao (Kif.3.27).

Alisema makampuni hayo yako Marekani, Japan, Ujerumani, Italia, Ufaransa mengine hata anuani zake hazikujulikana kabisa. Alisisitiza kwamba katika hali kama hii, inayoonyesha wazi kuwa kulikuwa na kugushi.

``Waziri Mkulo alipokuwa akijibu alitetea kuwa fedha za EPA si za Serikali. Kinachotisha zaidi, Mhe. Spika, hata Kampuni ya Ukaguzi ya Deloitte kwa barua yao kwa Gavana wa Benki Kuu ya tarehe 6, Septemba 2006 na kwa Wakurugenzi wote wa BoT ya Oktoba 10, 2006 walipomjulisha Gavana, pamoja na wajumbe wote wa Bodi ni pamoja na Katibu Mkuu wa Hazina Bw. Gray Mgonja, kuwa kuna utata kuhusu Kampuni ya Kagoda,`` alisema.

Alifafanua utata huo kwamba japo kampuni hiyo ilisajiliwa Septemba 29, 2005, Septemba 10 2005 ilikuwa tayari na mkataba wa kiasi cha fedha za Japan 956,110.986 na Kampuni ya Nishizawa Ltd na mkataba mwingine wa Dola za Marekani 9,057,463.90 wa Septemba 12, 2005 na Kampuni ya Textima Ltd.

``Mikataba hii yote inatamka kuwa `Kampuni hii imesajiliwa Tanzania kwa mujibu wa Sheria,` jambo ambalo dhahiri ni udanganyifu na ni uvunjifu wa Sheria,`` alisema.

Aliongeza kuwa Kampuni ya Deloitte ilionyesha katika barua walizomwandikia Gavana na wajumbe wa Bodi zikiwa na dosari kadhaa, moja ikiwa mikataba hiyo na maneno na mfumo unaofanana, jambo linaloashiria kuna kughushi, kwani makampuni kwa kawaida yanapenda kuwa na vipengele visivyofanana.

Alisema kwamba kati ya hati zote hizo, hakuna hata moja iliyowekwa kwenye barua halisi (letterhead) za Kampuni zao, na kwamba mikataba yote ilisainiwa ukurasa wa mwisho tu, tofauti na kawaida ya kusaini mikataba.

Alisema makampuni 12 katika sakata hilo yalikuwa na mhuri (seal) unaofanana na ule wa Kampuni ya Kagoda.

``Mambo haya yote yalipaswa kutoa ishara kwa Benki Kuu kuwa mikataba yote imeghushiwa lakini wala siyo Benki Kuu wala Wakurugenzi walioshituka na kuchukua hatua pamoja na barua hiyo ya Deloitte,`` alisema.

``Mheshimiwa Spika, fedha hizi zililipwa kupitia Benki zetu wenyewe, yaani Benki ya Kitanzania ambayo ni CRDB.

Hii ni Benki ambayo ilipaswa kuonyesha uzalendo kwani pamoja na ukweli kuwa benki za kigeni kama vile Kenya Commercial Bank na Barclays Bank walikataa kulipa fedha hizo baada ya kuona kuwa zina harufu ya kifisadi na hata ikafikia mahali wakafunga Account za mteja mmojawapo baada ya kutilia shaka malipo hayo na kuwaandikia BoT pamoja na kuwarudishia hundi zao.``
..............................................................

Monday 23 June 2008

Mbunge wa Tanzania ya leo!

Nilikuwa sielewi kuwa kazi ya mbunge TZ ni kutekeleza ahadi alizotoa ktk kampeni kwa kutumia hela toka mfukoni mwake? Kwa mtaji huu ili mtu awe mbunge anatakiwa kuwanazo!! Nayaunga mkono mawazo ya Rostam (MB) kuwa kuchangia maendeleo jimboni sio lazima uwe mbunge!
.................................

.................................
(Kutoka majira, 23.06.2008 1244 EAT)
VYAMA vya CHADEMA na CCM katika wilaya ya Igunga mkoani hapa, vimesema havitamruhusu Mbunge wa Jimbo la Igunga, Bw. Rostam Aziz, kuacha kugombea ubunge mwaka 2010.

Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti mjini Igunga juzi, kutokana na kauli ya Bw. Rostam ya kutogombea tena ubunge mwaka 2010, viongozi wa vyama hivyo walisema bado wanahitaji huduma yake.

Walisema Mbunge huyo amewafanyia mengi jimboni na kwamba mwaka 2010 ni mapema kuacha kugombea, kwa kuwa kuna mambo ambayo ameahidi kuyatekeleza, hivyo kuhitaji muda zaidi.

Katibu wa CHADEMA wa Wilaya, Bw. Moka Changarawe, alisema mbunge huyo amewasaidia kwa mambo mengi, yakiwamo ya kuwajengea mabwawa na huduma mbalimbali za maendeleo tena bila kujali itikadi za vyama.

"Mbunge huyu kuna ahadi ameanza kuzitekeleza, hivyo haitakuwa vema aachie ngazi huku akiwa katikati ya kuzikamilisha, sisi tutampa muda mwingine amalizie, lakini si sasa," alisema na kuongeza kuwa hata wanachama wa CHADEMA Igunga wana imani naye.

Naye Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Igunga, Bw. Felix Mkunde, alisema kauli ya Bw. Rostam, waliipokea kwa hisia tofauti na kwamba wataijadili ili wahakikishe anabadili msimamo wake kwa kuwa bado wanamhitaji.

"Hayo ni mawazo yake binafsi, hatuwezi kumlazimisha kubadili msimamo, lakini bila shaka ni mwelewa na ataelewa ni nini tunachokizungumza sisi na kwa nini tunahitaji bado mchango wake jimboni," alisema Bw. Mkunde.

Aliungwa mkono na Katibu wa CCM wa Wilaya hiyo, Bibi Evelyne Jordan, ambaye alisema Halmashauri ya Wilaya ya CCM kwa kauli moja ilishasema kuwa haitambui wazo hilo la Mbunge Rostam na bado inamhitaji.

Hata hivyo, Bw. Rostam alipoulizwa, alisema ni kweli huo kwa sasa ndio msimamo wake na si lazima awahudumie wananchi wa Igunga akiwa bungeni, kwani anaweza kutoa mchango wake akiwa nje ya Bunge.

"Kama mwana Igunga, nitaendelea kuwatumikia wananchi hata nikiwa nje ya Bunge," alisema.

Kuhusiana na hilo, Bibi Jordan alisema akiwa bungeni na nje ya Bunge ni tofauti, na ndiyo sababu wafanyabiashara na vijana wa wilaya ya Igunga wameshasema hawatakubali kumpoteza na wanamtaka aendelee kuwawakilisha bungeni.

Bw. Rostam aliingia bungeni mwaka 1994 baada ya kifo cha aliyekuwa mbunge wa Igunga, marehemu Charles Kabeho na katika uchaguzi wa 1995 na 2000 alipita bila kupingwa.
................................

Saturday 21 June 2008

June 21: Summer solstice came and went

Yes that longest day is about to end in few hours time ushering in the start of the summer 'proper'!

Day lengths starts to shorten as from today. Days will become shorter and shorter till winter (shortest day time!)

Bye-bye!

Bill Gates: Helping the needy

(with the help of extracts from daily expess, june 21, 2008 pg 41-42)
Bill Gates, (52) and his wife Melinda, (43) launched their charity in 2000 known as Bill and Melinda Gates Foundation.

Ever since, and even before that, they have donated over £3.5bn. supporting work in more than 100 countries.

'With success I have been given great wealth, with great wealth comes great responsibility to give back to society, to see that those resources are put to work in the best possible way to help those in need', says Bill Gates.

At one time Bill Gates refused to fly first-class because he didn't think it was worth the money.

Reginald Mengi: An example to follow

(form: ippholdings website)
From a very humble beginning in the eighties as a small scale ball-point pen assembler in a living room, IPP has grown into a major diversified company. Today, the group comprises four core divisions;
Media
Beverages
Household and Beauty care
Minerals Prospecting and Mining

Talk about our success, future plans!

Lately the debate has turned to be of one man -Cristiano Ronaldo- whether he stays or not, instead of Manchester United's success over the last two seasons!

If the club is not careful it would find itself drugged into the debate and forget to prepare for the next season's competitions.

The issue is to strengthen the squad and preparing the team for next season! It is not about Ronaldo's latest single of 'Madrid!'; which is on top of the chart!!

Nobody is arguing that Ronaldo isn't great at the moment but we should also remember that the team is not only about Ronaldo. There is a squad of 30 plus United players. Those players should as well be remembered for their massive contribution. So if one player (Ronaldo) wants to leave - let him go!

Manchester United will always move forward. Winning titles is their motto!

Ushamba, fasheni na msimamo!

Si kipindi kirefu kilichopita mtu akionekana na mfuko wa plastic uliotumika anaonekana mshamba. Siku hizi wataalamu wanasisitiza kutumia mifuko ya plastic (rambo) mara kwa mara ili kutunza mazingira.
Nani angetembea barabarani na viroba (mifuko ya gunia), mtaa mzima wangemzungumza kuwa mtu wa kuja. Lakini hivi sasa ndio imerudi iko ktk fasheni - eti wanaiita 'bio-degradable'! Si ndio ileile tuliyokuwa tunachekwa nayo lakini?

Je ungeshona nguo kwa sindano ya mkono hiyo nguo ungeivalia wapi? Lakini unaonaje siku hizi si makoti yanatoka kwa staili ya ushonaji wa mkono!! Au ukivalia nguo ndani nje, inakuwaje. Siku hizi zinashonwa ndani nje na inakubalika!

Vipo vitu vingi vizuri ambavyo watu wanaacha kufanya eti kwa sababu ni vya ki-shamba.
Muda si muda unakuta ndio vipo ktk chati. Lakini vinakuwa ktk chati kwa sababu fulani (mtu maarufu) kaonekana navyo.

Ni kwanini mtu aache kufanya mambo yale aliyozoea kufanya au yale yanayomfaa ktk maisha ya kila siku kisa ataonekana mshamba? Lakini mtu kama Beckam au Naomi Campell akiyafanya yaleyale 'ya kishamba' - inaonekana ni fasheni!

Cha msingi ni kuwa na msimamo na utaratibu wako kimaisha na pia kujali utamaduni wako kiustaarabu!

Friday 20 June 2008

June 21: Summer solstice

Summer solstice - the longest day of the year, when the Sun is at its most northern point in the sky.

Please Sir Alex, can you sign Schweinsteiger!

I watched Bastian Schweinsteiger of Germany as he played against Portugal yesterday with great interest.
I was very much pleased with his ability on the pitch! He has got energy, skills, speed, awareness/movement off-ball and is also a good finisher.
I recommend his name to the Manchester United manager, Sir Alex Ferguson, I hope he would suit us!
.........................................
Biography:
(From Wikipedia, the free encyclopedia)
Bastian Schweinsteiger (born August 1, 1984 in Kolbermoor, Bavaria, Germany) is a professional footballer from Germany who plays as a midfielder for Bayern Munich.
Personal information:

Date of birth: August 1, 1984 (1984-08-01) (age 23)
Place of birth: Kolbermoor, West Germany
Height: 1.81 m (5 ft 11+1⁄2 in)
Playing position: Midfielder
Current club: Bayern Munich
........................................

Thursday 19 June 2008

'Wakurya': awaonavyo Jenerali

Nimepitia haraka haraka makala ya 'Rai ya Jenerali Ulimwengu' ktk gazeti la Raia Mwema wiki hii Juni 18-24, nikaona habari kuhusiana na wakurya. Alichokisema Jenerali ni kweli.
Ila ni lazima niseme kuwa mara nyingi kusema ukweli kunatuacha ktk mazingira magumu ya kuchukiwa ktk jamii.
Wapo watu ktk jamii wenye kupenda sifa, kazi yao ni kurembaremba maneno kwa kuyafanya matamu (bila kuelezea hali halisi ilivyo) ili wasionekane wabaya.
Unapokuwa mpenda 'haki na ukweli' si ajabu kuona unachukiwa na wapenda njia za mkato; lakini ipo siku moja jamii itaelewa na kuthamini mchango wako, kwani penye ukweli uongo hujitenga!
............................
............................
(nukuu kutoka Raia Mwema 18-24 June, 2008)
'Ni muhimu, basi, kuwathamini wale wachache wanaodiriki kutoa maoni yao, wawe ndani ya utawala au nje, kwa sababu hawa ni watu adimu katika jamii yetu. Zamani kidogo niliwahi kuandika kwamba sote tunahitaji kuwa "Wakurya" kwa kiasi fulani, kwa maana ya kuambizana ukweli hata kama haupendezi. Hadi sasa "Wakurya" tulio nao bado hawatoshi. Tuwathamini hao wachache waliopo ...'

Tuesday 17 June 2008

Tanesco: New Applications (Charges)

(source: www.tanesco.com)
Application Fees.........................Tshs
All new applications.......................5,000/-

New service lines charges......................Tshs
Underground service lines.........................Actual Cost +10%

Overhead service lines-Single Phase:
DI with Conventional Meter.........................140,000/-
DI with LUKU Meter– single phase....................200,000/-
TIConventionalmeter.................................140,000/-
TI with LUKU Meter..................................200,000/-
---------------------------------------------------------------------

Overhead service lines-Three Phase:
TI Conventional meter, (16mm² cable).................280,000/-
TI LUKU meter, (16mm² cable).........................450,000/-
TI Conventional meter, (36mm² cable).................350,000/-
TI LUKU meter, (36mm²cable)..........................550,000/-

Monday 16 June 2008

June 16, 1976: Soweto massacre!!!

(from: wikipedia)
The Soweto uprising or Soweto riots were a series of clashes in Soweto, South Africa on June 16, 1976 between black youths and the South African authorities. The riots grew out of protests against the policies of the National Party government and its apartheid regime.

On the morning of June 16, 1976, thousands of black students walked from their schools to Orlando Stadium for a rally to protest against having to learn through Afrikaans in school. Many students who later participated in the protest arrived at school that morning without prior knowledge of the protest, yet agreed to become involved. The protest was intended to be peaceful and had been carefully planned by the Soweto Students’ Representative Council’s (SSRC) Action Committee, with support from the wider Black Consciousness Movement. Teachers in Soweto also supported the march after the Action Committee emphasized good discipline and peaceful action.

Tsietsi Mashininini led students from Morris Isaacson High School to join up with others who walked from Naledi High School. The students began the march only to find out that police had barricaded the road along their intended route. The leader of the action committee asked the crowd not to provoke the police and the march continued on another route, eventually ending up near Orlando High School. The crowd of between 3,000 and 10,000 students made their way towards the area of the school. Students sang and wove placards with slogans such as, "Down with Afrikaans", "Viva Azania" and "If we must do Afrikaans, Vorster must do Zulu".

The rioting continued and 23 people, including two white people, died on the first day in Soweto. Among them was Dr Melville Edelstein who had devoted his life to social welfare among blacks. He was stoned to death by the mob and left with a sign around his neck proclaiming 'Beware Afrikaaners'.

The violence escalated as the students panicked; bottle stores and beerhalls were targeted as many believed that alcohol was used by the government to control black people. The violence abated by nightfall. Police vans and armored vehicles patrolled the streets throughout the night.

Emergency clinics were swamped with injured and bloody children. It is not known how many injured children sustained bullet wounds because doctors refused to collect such details for fear that police would target the families of such children. In many cases bullet wounds were indicated on hospital records as abscesses.

Emotions ran high after the massacre on June 16. Hostility between students and the police was intense, with officers shooting at random and more people joining the protesters. The township youth had been frustrated and angry for a long time and the riots became the opportunity to bring to light their grievances.

The 1,500 heavily armed police officers deployed to Soweto on June 17 carried weapons including automatic rifles, stun guns, and carbines. They drove around in armoured vehicles with helicopters monitoring the area from the sky. The South African Army was also order on standby as a tactical measure to show military force. Crowd control methods used by South African police at the time included mainly dispersement techniques, and many of the officers shot indiscriminately, killing many people.

The accounts of how many people died vary from 200 to 600, with Reuters news agency currently reporting there were "more than 500" fatalities in the 1976 riots. The original government figure claimed only 23 students were killed. The number of wounded was estimated to be over a thousand men, children, and women.

Soweto is an urban area in the City of Johannesburg, in Gauteng, South Africa. Its name is an English syllabic abbreviation, short for South Western Townships.

June 16 is now celebrated in South Africa as Youth Day.

Man Utd: Prem L/ge 2008/09 -III

April 2009
04 Apr Barclays Premier League Aston Villa H 15:00
11 Apr Barclays Premier League Sunderland A 15:00
18 Apr Barclays Premier League Wigan A 15:00
25 Apr Barclays Premier League Tottenham H 15:00
May 2009
02 May Barclays Premier League Middlsbro A 15:00
09 May Barclays Premier League Man City H 15:00
16 May Barclays Premier League Arsenal H 15:00
24 May Barclays Premier League Hull City A 15:00

Please note: These fixtures will change. They do not take into account games which will be shown live on UK television, nor changes that will be made due to the club's participation in the UEFA Super Cup in Monaco on 29 August and the FIFA Club World Cup in Tokyo in December. Fans are strongly advised not to make travel or accommodation arrangements until final fixture dates are known.

Man Utd Prem L/ge 2008/09 -II

November 2008
01 Nov Barclays Premier League Hull City H 15:00
08 Nov Barclays Premier League Arsenal A 15:00
15 Nov Barclays Premier League Stoke City H 15:00
22 Nov Barclays Premier League Aston Villa A 15:00
29 Nov Barclays Premier League Man City A 15:00
December 2008
06 Dec Barclays Premier League Sunderland H 15:00
13 Dec Barclays Premier League Tottenham A 15:00
20 Dec Barclays Premier League Wigan H 15:00
26 Dec Barclays Premier League Stoke City A 15:00
28 Dec Barclays Premier League Middlsbro H 15:00
January 2009
10 Jan Barclays Premier League Chelsea H 15:00
17 Jan Barclays Premier League Bolton A 15:00
27 Jan Barclays Premier League West Brom A 19:45
31 Jan Barclays Premier League Everton H 15:00
February 2009
07 Feb Barclays Premier League West Ham A 15:00
21 Feb Barclays Premier League Blackburn H 15:00
28 Feb Barclays Premier League Portsmouth H 15:00
March 2009
04 Mar Barclays Premier League Newcastle A 19:45
14 Mar Barclays Premier League Liverpool H 15:00
21 Mar Barclays Premier League Fulham A 15:00

Please note: These fixtures will change. They do not take into account games which will be shown live on UK television, nor changes that will be made due to the club's participation in the UEFA Super Cup in Monaco on 29 August and the FIFA Club World Cup in Tokyo in December. Fans are strongly advised not to make travel or accommodation arrangements until final fixture dates are known.

Man Utd: Premier League 2008/09 -I

August 2008
16 Aug Barclays Premier League Newcastle H 15:00
23 Aug Barclays Premier League Portsmouth A 15:00
29 Aug UEFA Super Cup Zenit St Petersburg N 19:45
30 Aug Barclays Premier League Fulham H 15:00
September 2008
13 Sep Barclays Premier League Liverpool A 15:00
20 Sep Barclays Premier League Chelsea A 15:00
27 Sep Barclays Premier League Bolton H 15:00
October 2008
04 Oct Barclays Premier League Blackburn A 15:00
18 Oct Barclays Premier League West Brom H 15:00
25 Oct Barclays Premier League Everton A 15:00
28 Oct Barclays Premier League West Ham H 20:00

Please note: These fixtures will change. They do not take into account games which will be shown live on UK television, nor changes that will be made due to the club's participation in the UEFA Super Cup in Monaco on 29 August and the FIFA Club World Cup in Tokyo in December. Fans are strongly advised not to make travel or accommodation arrangements until final fixture dates are known.

Man Utd: Pre-season Fixtures

(from: www.manutd.com, 16/06/2008)
July 2008
12 Jul Aberdeen A 15:00
19 Jul Kaizer Chiefs N 15:30
22 Jul Orlando Pirates N 20:10
26 Jul Kaizer Chiefs or Orlando Pirates N 15:30
August 2008
02 Aug RCD Espanyol H 15:00
04 Aug Peterborough A 19:45
06 Aug Juventus H 20:00
...................
10 Aug Community Shield Portsmouth N 15:00

Saturday 14 June 2008

Bajeti 2008/09: Kipaumbele

(kutoka Nipashe 13/06/2008)
Maeneo sita ambayo yamepewa vipaumbele katika bajeti hiyo kuwa ni:
1. miundombinu ya barabara Sh. bilioni 973.3,
2. afya Sh. bilioni 803.8,
3. kilimo Sh. bilioni 460,
4. maji Sh. bilioni 230.6 na
5. nishati Sh. bilioni 383.1.
6. ???

Bajeti 2008/09: 'wananchi waisifia'

(SOURCE: Nipashe, 2008-06-14 10:11:12)
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Kilimo, Sokine (SUA), Dk. Damiani Gabagambi:
``Nilitarajia kwenye bajeti serikali izungumzie suala la kupunguza matumizi yasiyo ya lazima (mfano magari ya kifahari -mashangingi) lakini sijaona kitu, wasipobana matumizi hakuna kitakachofanyika. Fedha watakusanya na zitaishia kwenye matumizi yasiyoeleweka na ambayo hayamsaidii mtanzania,`` alisema.

Dk. Gabagambi alisema hakuna sababu kwa viongozi wa serikali kununuliwa magari ya kifahari ya aina hiyo. Landrover inaweza kuwa gari mwafaka kwa kiongozi wa nchi inayoendelea kama Tanzania.

Dk. Semboja Haji Khatib, mchumi kitaaluma, aliisifu bajeti hiyo kwamba haina makali sana kwa wananchi.
Hata hivyo, alisema:
1. bajeti hiyo inaandamwa na changamoto nyingi, kubwa ikiwa ni kupanda kwa bei ya mafuta duniani pamoja chakula na mfumuko wa bei.

2. suala la chakula linapaswa kuchukuliwa kama changamoto badala ya tatizo kwa vile Tanzania ikijipanga vyema ina uwezo wa kuzalisha chakula cha kutosha hadi kuuza nje, hususan mchele katika eneo la Afrika Mashariki.

Naye Dk. Damian Gabagambi, alisema:
1. hii ni bajeti ya kibiashara ambayo haionekani kuleta mapinduzi ya kilimo nchini.
Kiwango cha asilimia 6 kilichopangwa kwa ajili ya kilimo ni kidogo kwani nchi za Afrika ziliwahi kukutana Maputo, nchini Msumbiji, na kukubaliana kwamba bajeti ya kilimo inatakiwa kufika asilimia 10.

2. sio vizuri serikali kuwazuia wakulima wanaopata soko la mazao yao nje.

3. ndege ya kisasa inayotumiwa na rais, aina ya Gulfstream 550, iuzwe kwani gharama zake za uendeshaji ni mzigo kwa uchumi wa Tanzania.
Ndege hiyo iliyonunuliwa kwa Sh. bilioni 40 kutoka kampuni moja nchini Marekani, inatumia mafuta ya mabilioni inaporuka.
``Hakuna sehemu hapa Afrika ambapo unaweza kuifanyia matengenezo ile ndege, hivyo hata matengenezo kidogo lazima iende Marekani, iruke isiruke lazima ikafanyiwe matengenezo,``
Ingawa ndege hiyo muda mwingi haitumiki lakini lazima ifanyiwe matengenezo kila mwisho wa mwezi, hali inayolitia hasara kubwa taifa. Hata Rais Kikwete amekuwa akiitumia ndege hiyo mara chache kutokana na kutambua gharama kubwa za uendeshaji wa ndege hiyo. Licha ya ndege hiyo kununuliwa kwa gharama kubwa haiwezi kutua katika viwanja vingi vya ndege havya hapa nchini.

Mtaalamu wa Uchumi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Godius Kahyarara, ameitaka serikali kuhamasisha matumizi ya nishati mbadala kwa matumizi mbalimbali kupunguza matumizi ya mafuta, ili iweze kufanikiwa kupunguza mfumuko wa bei nchini.
Alisema njia itakayosaidia kupunguza mfumuko wa bei, ni matumizi makubwa ya nishati mbadala kama gesi ya majumbani na katika vyombo vya usafiri hasa magari ya serikali.

``Gesi tunayo ya Songosongo, lakini bila kuhamasisha matumizi yake, bei ya mafuta katika soko la dunia na hapa nchini itapandisha bei ya bidhaa nyingine, jambo ambalo litakwamisha jitihada za kupunguza mfumuko wa bei,`` alisema.

Kuhusu sekta ya miundombinu na kilimo ambazo kwa ujumla zimetengewa asilimia 19 ya bajeti yote, alisema sekta hizo zinapaswa kutengewa bajeti kubwa zaidi.
``Miundombinu isiangalie ujenzi wa barabara pekee, maana tuna-overload barabara zetu, tuangalie reli na ndege, lakini kwa kujua mchango wa kilimo chetu ambacho ni uti wa mgongo wa taifa katika kukuza uchumi``

Aidha, alisema sekta ya elimu inapaswa kwenda sambamba na ukuaji wa uchumi.
``Tujue namna elimu itakavyosaidia kupunguza uhaba wa wataalam ili kukuza uchumi wetu, tuiboreshe kwa lengo la kushindana katika ushindani wa soko la ajira ndani na nje ya nchi,``

Hata hivyo, alisema bajeti ya mwaka huu ni nzuri na kwamba imeangalia vitu muhimu na kumlinda mwananchi wa kawaida.

Mwenyekiti wa chama cha Sauti ya Umma (SAU), Bw. Paul Kyara, alisema bajeti hiyo ina mapungufu katika maeneo kadhaa, na kutoa mfano kuwa haijatoa kipaumbele kwa sekta ya kilimo iliyotengewa asilimia sita ya bajeti yote.
``Kilimo pamoja na kuwaajiri watu zaidi ya asilimia 80, kuchangia zaidi ya asilimia 40 ya pato la taifa, na asilimia 30 ya mapato ya fedha za kigeni, inawezekana vipi kikatengewa asilimia 6.8, tu, ``

Wakati huohuo, ubalozi wa Marekani nchini, umeipongeza bajeti ya Tanzania na kueleza kuwa inamuelekeo mzuri kwa Watanzania kujikwamua na umaskini.

Taarifa iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari na ubalozi huo, ilieleza kuwa Watu wa Marekani wamepongeza bajeti hiyo pia kwamba si tegemezi kama ilivyokuwa bajeti zilizopita. Pongezi nyingi zimeelekezwa kwa Rais Jakaya Kikwete na Waziri wa Fedha kwa kutoa bajeti yenye muelekeo mzuri hasa katika sekta ya elimu, kwani itaboresha elimu nchini.

Mwaka mmoja: Mama Jojia tunakukumbuka

Leo ni mwaka mmoja tangu mama Jojia aage dunia. Hiki kimekuwa kipindi kigumu kwa shemeji yetu Jojia pamoja na ndugu zake.

Lakini tunapenda kumhakikishia Jojia kwamba tuko pamoja nae ktk kumkumbuka na kumuenzi mama yetu mpendwa!

Familia yangu inaungana na shemeji Jojia (pamoja na familia yake yote na ukoo wote) ktk kumkumbuka mama leo.

Mwenyezi Mungu awape faraja wanandugu na jamaa wote.

Kaa macho, kuna NOTI bandia za 10,000/=

(SOURCE: Nipashe, 14/06/2008)
Mkazi wa Kasulu mjini Emmanuel Ndonya amenusurika kutiwa mbaroni na polisi baada ya kupatikana na noti mbili bandia zenye thamani ya Sh.20,000.

Aliiingia nazo katika benki ya NMB Kasulu kwa nia ya kuzihifadhi lakini alishtukiwa na alipobaini kuwa amenaswa alikimbia na kuziacha fedha hizo.

Noti hizo ni zenye namba AU 0326348 na AS 3067372

Friday 13 June 2008

Sura ya Bajeti 2008/09

Mapato Shilingi Milioni
A. Mapato ya Ndani 4,728,595
(i) Mapato ya Kodi (TRA) 4,497,070
(ii) Mapato yasiyo ya Kodi 231,525
B. Mikopo na Misaada ya Nje Ikijumuisha MDRI*/MCA(T)** 2,429,535
C. Mauzo ya Hisa za Serikali 58,000
JUMLA YA MAPATO YOTE 7,216,130

Matumizi
D. Matumizi ya Kawaida 4,726,650
(i) Deni la Taifa 648,284
(ii) Wizara 2,478,099
(iii) Mikoa 85,743
(iv) Halmashauri 908,756
(v) Matumizi Maalum 364,391
(vi) Marekebisho ya Mishahara ya Serikali 241,377
E. Matumizi ya Maendeleo 2,489,480
(a) Fedha za Ndani 938,380
(b) Fedha za Nje 1,551,100
JUMLA YA MATUMIZI YOTE 7,216,130
..............................

*MRDI -the Multilateral Debt Relief Initiative
The 6th review (of the United Republic of Tanzania with IMF), under the 3-year Arrangement under the Poverty Reduction and Growth Facility and Request for a 3 year Policy Support Instrument.

**MCA(T) -Millennium Challenge Account—Tanzania
Each country with a signed Compact establishes a government entity responsible for implementing the projects within the Compact and for overseeing its Millennium Challenge Account (MCA). These organizations are called MCA Entities.

In overseeing its MCA and implementing the Compact projects, the Entity:
-Serves as the central point of contact for MCC, other donors, contractors, consultants and the country's citizens;
-Establishes financial and reporting systems and manages procurements;
-Drafts and executes, with MCC's assistance, work plans for Compact programs;
-Creates a web site for posting project status, news and procurements; and
-Develops a unique logo to identify projects as both MCA and as a grant from the American people.

Bajeti 2008: Vinywaji bei juu TZ

(SOURCE: Nipashe, 2008-06-13 09:32:43. Na Boniface Luhanga)
Serikali imefanya marekebisho ya viwango vya ushuru kwa bidhaa mbalimbali kwa ama kuvipandisha, kuvishusha au kusamehe kwa mwaka ujao wa fedha wa 2008/09.

Hata hivyo, ushuru wa mafuta ya petroli, haukuguswa na viwango hivyo vipya vitaanza kutumika Julai Mosi, mwaka huu.

Hatua hiyo ilitangazwa jana mjini hapa na Waziri wa Fedha na Uchumi, Bw. Mustapha Mkulo, wakati akiwasilisha bungeni makadirio ya mapato na matumizi ya serikali kwa mwaka wa fedha wa 2008/09 utakaoanza rasmi Julai Mosi.

Bidhaa zilizofanyiwa marekebisho ya ushuru kwa asilimia 12, viwango vya sasa na vya zamani kuwa ni vinywaji baridi kutoka Sh. 48 hadi Sh. 54 kwa lita, bia zinazotengenezwa na nafaka ya hapa nchini ambayo haijaoteshwa, kutoka Sh. 173 hadi Sh. 194 kwa lita.

Bia nyingine zote kutoka Sh. 294 hadi 329 kwa lita huku ushuru wa mvinyo unaotengenezwa kwa zabibu inayozalishwa nje ya nchi kwa kiwango cha asilimia 25, ukipanda kutoka Sh. 940 hai Sh. 1,053 kwa lita.

Viwango vya ushuru wa bidhaa kwenye sigara vimebadilishwa ambapo zile zisizo na kichungi na zinazotengenezwa kutokana na tumbaku inayozalishwa nchini kwa kiwango cha angalau asilimia 75, kutoka Sh. 4,775 hadi Sh. 5,348 kwa sigara 1,000.

Sigara zenye kichungi zinazotengenezwa kwa tumbaku inayozalishwa nchini kwa kiwango cha angalau asilimia 75, zitapanda kutoka Sh. 11,266 hadi Sh. 12,618 kwa sigara 1,000.
Sigara nyingine zenye sifa tofauti na (a) na (b), pia zimerekebishwa ushuru kutoka Sh. 20,460 hadi Sh. 22,615 kwa sigara 1,000.

Tumbaku ambayo iko tayari kutengenezwa sigara (cut filler) inapanda kutoka Sh. 10,333 hadi Sh. 11,573.

Ushuru wa `cigar`, unabaki asilimia 30.

Ushuru wa bidhaa katika huduma za simu za mkononi unapanda kutoka asilimia saba ya gharama ya matumizi ya huduma, hadi asilimia 10 ya gharama hiyo. Sababu kubwa ya rekebisho hilo katika bidhaa ya huduma za simu ni kwenda sanjari na mfumuko wa bei (adjustment for inflation).

Serikali imepunguza kiwango cha ushuru wa bidhaa kwenye mafuta mazito ya HFO, kutoka Sh. 117 hadi Sh. 97 kwa lita, lengo likiwa ni kupunguza gharama ya uzalishaji viwandani na kuongeza uwezo wa ushindani wa bidhaa katika soko.

Mfumo wa kutoza ushuru wa bidhaa kwenye magari pia umerekebishwa kutoka ule wa sasa wa asilimia 10 kwa magari yenye ukubwa wa injini cc 2000 na kuwa na viwango viwili vya asilimia tano na 10 kama ifuatavyo:
Magari yenye ujazo wa injini isiyozidi CC 1,000 lakini hauzidi cc 2000 kiwango cha ushuru kitakuwa asilimia tano ya thamani ya gari, wakati magari yenye ujazo wa injini unozidi cc 2,000, kiwango cha ushuru kitakuwa asilimia 10 ya thamani ya gari.

Kuhusu sheria zinazosimamia kodi za magari, viwango vya ada zake vimepunguzwa ambapo kwa magari yenye ujazo wa injini usiozidi cc 500 kutoka Sh. 50,000 hadi Sh. 30,000.

Kwa magari yenye ujazo wa injini unaozidi cc 500 lakini hauzidi cc 2500, kutoka Sh. 80,000 hadi Sh. 50,000 ambapo magari yenye ujazo wa injini usiozidi cc 1500 lakini hauzidi cc 2500 kutoka Sh. 150,000 hadi Sh. 120,000.

Magari yenye ujazo wa injini usiozidi cc 2500 lakini hauzidi cc 5000 kutoka Sh. 330,000 hadi Sh. 140,000 wakati yale yenye ujazo wa injini usiozidi cc 5000 kutoka Sh. 175,000 hadi Sh. 150,000.

Serikali imesamehe ada ya mwaka ya leseni za magari kwa matrekta ya kilimo lakini imeongeza ada ya usajili wa magari kutoka Sh. 27,000 kwa pikipiki na Sh. 20,000 kwa gari na kwamba ada hii inalipwa mara moja tu na mwenye gari.

Hatua zote hizo kwa pamoja, zitapunguza mapato ya serikali kwa takriban Sh. milioni 2,380.

Serikali imesamehe ushuru wa forodha kwenye majembe ya mkono pamoja na pembejeo nyingine zote za kilimo zinazoingizwa kutoka nje.

Vile vile, serikali imesamehe ushuru wa forodha kwenye mali ghafi na vifaa vinavyoagizwa na kampuni ya TANELEC kwa ajili ya kutengeneza mashine za kuongeza na kupunguza nguvu ya umeme.

Ushuru wa forodha kwenye shayiri pia umeondolewa lakini kwa ile itakayoagizwa na kampuni za bia za hapa nchini kwa kiwango isichozidi tani 20,000 hadi mwisho wa Desemba, mwakani.

Ushuru wa forodha kwenye mashine za jamii ya kompyuta zinazotambulika chini ya HSCODE 8443.31.00 na 844.32.00 kwa kuwa kompyuta kwa sasa hazitozwi ushuru wa forodha.

Ushuru wa forodha kwenye madini ya Sodium Sulphate, kutoka asilimia 25 hadi asilimia 10 ili kupunguza gharama za uzalishaji viwandani.

Serikali imeondoa ushuru wa forodha kwa magari yaliyotengenezwa maalum kwa ajili ya ukusanyaji takataka yatakayonunuliwa na serikali za mitaa au mawakala waliodhinishwa na serikali za mitaa.

Mafuta ghafi ya kula, pia yameondolewa ushuru wa forodha wa asilimia 10.

Mafuta yaliyosafishwa kidogo (semi-processed), yataendelea kutozwa ushuru wa asilimia 10 ambapo hatua hiyo itaviweka viwanda vya mafuta hapa nchini katika nafasi nzuri ya kiushindani na vile vya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Hatua hizo kwenye ushuru wa forodha kwa pamoja, zitapunguza mapato ya serikali kwa takriban Sh. Milioni 762.

Katika mwaka wa fedha wa 2008/09, serikali imepanga kupata mapato ya jumla ya Sh. trilioni 7.216 ambapo kati ya kiasi hicho, mapato ya ndani ni Sh. trilioni 4.729.

Mapato kutoka kwa wahisani ni Sh. trilioni 2.249 wakati Sh. Bilioni 58.000, serikali inatarajia kutokana na uuzaji wa hisa zake asilimia 21 katika benki ya National Microfinance (NMB).

Katika mwaka wa fedha wa 2008/09, serikali imepanga kutumia Sh. trilioni 7.216 ambapo matumizi ya kawaida yatakuwa Sh. trilioni 4.727 ambayo alisema ni chini ya mapato ya ndani ya Sh. trilioni 4.729.

Matumizi ya maendeleo yamepangwa kuwa Sh. trilioni 2.489 ambapo katika matumizi hayo kiasi cha, Sh. bilioni 1,551.100, kitatokana na fedha za wahisani kupitia miradi pamoja na basketi.

Kiasi kilichobaki cha Sh. bilioni 938.380, kitatokana na mchango wa wahisani kupitia misaada ya bajeti, mapato yatokanayo na mauzo ya hisa za serikali pamoja na ziada itakayotokana na mapato ya ndani.

Maeneo sita ambayo yamepewa vipaumbele katika bajeti hiyo kuwa ni miundombinu ya barabara Sh. bilioni 973.3, afya Sh. bilioni 803.8, kilimo Sh. bilioni 460, maji Sh. bilioni 230.6 na nishati Sh. bilioni 383.1.

Sekta hizo sita za miundombinu ya uchumi na huduma za jamii, zimetengewa takriban asilimia 64 ya bajeti yote ya mwaka 2008/09.

Thursday 12 June 2008

Bei ya vyakula juu!

Bajeti 2008/09: Mambo Magumu!
(SOURCE: Alasiri, 2008-06-11 18:01:14 Na Sharon Sauwa)
Wakati Waziri wa Fedha na Mambo ya Uchumi, Mhe. Mustafa Mkulo akitarajiwa kuwasilisha bajeti ya mwaka 2008/09 katika mkutano wa 12 wa Bunge kesho (alhamis), bei ya vitu imepanda maradufu kulinganisha na kipato na hivyo kuwafanya wananchi wengi kuwa na maisha magumu zaidi.

Mwandishi amebaini kuwa mbali na pesa nyingi wanazolipa wakazi wa Jijini kutokana na kupanda kwa gharama za usafiri, pia vyakula, huduma za matibabu, umeme na hata vifaa vya ujenzi vimepanda mno kwa namna inayofanya maisha yawe magumu zaidi.

Bei za vyakula na bidhaa/huduma mbalimbali kulingana na uchunguzi wa gazeti 'Alasiri':
Nauli ya daladala hutozwa kati ya Sh. 250 hadi Sh. 1,000 kulingana na eneo na umbali wa safari yenyewe, katika baadhi ya maeneo mengi Jijini.
unga wa mahindi huuzwa kati ya Sh. 700 hadi 800 kwa ujazo wa kilo moja.
Mchele huuzwa kati ya Sh. 900 hadi Sh. 1,300,
maharage Sh. 1,200 hadi Sh. 1,500
mkaa kipimo kimoja kikiwa kati ya Sh. 700, 1,000 na hadi Sh. 1,200 kwa maeneo kama ya Kimara Bonyokwa.
vitunguu na nyanya ambavyo vyote, huuzwa kwa wastani wa Sh. 100 kwa kimoja, au Sh. 400 kwa fungu lenye nyanya tatu hadi nne au vitunguu vya idadi hiyo
bamia fungu likiuzwa kati ya Sh. 100 na 300.
nyama ya kawaida imekuwa kimbilio la wengi kwa sasa, kutokana na ukweli kuwa yenyewe imeendelea kuuzwa kwa wastani wa Sh. 2,800 hadi 3,500, kulingana na eneo.
Sukari nayo huuzwa kwa Sh. 1,000 hadi Sh. 1,200 kwa kilo,
mafuta ya kula huuzwa Sh. 150 kwa kipimo kidogo kabisa kwenye maeneo kama ya Tandale na Buguruni huku fungu la bamia ni sh 100.
dagaa wanaopendwa zaidi toka Kigoma huuzwa kwa kati ya Sh. 7000 hadi sh 9,000,
nanasi Sh.1,000 na 1,500,
embe dodo sh. 500 hadi 700 na
machungwa Sh.100 hadi 150.

maji yanayouzwa kwenye madumu katika maeneo yenye shida ya maji huuzwa kwa kati ya Sh. 300 hadi Sh. 500 kwa dumu moja la lita 20.
mafuta ambayo hutajwa kuwa ni sababu kubwa zaidi ya kupanda kwa maisha imeendelea kupanda siku hadi siku ambapo sasa, katika baadhi ya vituo vya mafuta, dizeli huuzwa kwa Sh. 1,950 kwa lita, Petroli Sh. 1850 na mafuta ya taa Sh. 1,300.

Bei ya samaki imekuwa haishikiki, ingawa hushuka kidogo pale wanapovuliwa kwa wingi wakati bahari inapotulia na giza kutawala usiku.

Tuesday 10 June 2008

Wanawake, ngono na kondomu!

Njia rahisi ni kwa mwanamke kujinunulia kondomu anazoona zinafaa (ki-ubora) na za kutosha (ki-idadi) ili zitumike pale anapojihusisha na tendo la ngono.
Pia, kwa kusema ukweli, mwanamke mwenyewe anao uwezo kabisa kuhakikisha kuwa kondomu inavaliwa na inatumika kama ataamua kufuatilia kabla ya tendo lenyewe maana mwanamke ndie kama kondakta wa 'bus'; abiria lazima alipe nauli kabla ya safari!!
-mosonga2002@yahoo.com
...................

(SOURCE: Nipashe, 2008-06-10 10:57:51 Na Kibuka Prudence, PST, Kagera)
Meneja wa Shirika la PSI mkoani Kagera Bw. Clement Mbogo, amesema wanawake wana uwezo wa kuhamasisha matumizi ya kondomu na amewashauri kujali maisha yao kwa kuacha kudharau umuhimu wa kutumia kondomu katika kupiga vita maambukuzo ya Ukimwi.

Alisema nafasi ya mwanamke katika kumshawishi mwanaume kutumia kondomu ndiyo njia pekee ya kupunguza kuenea kwa maambukizo ya virusi vya Ukimwi na magonjwa mengine yanayotokana na zinaa.

Alibainisha kuwa kumekuwepo na ushirikiano mdogo kutoka kwa mwanamke mara anapokuwa katika mazingira ya kukutana kimwili na mwanamme, hali ambayo inamfanya mwanamume kujiamulia kwa lo lote atakalo.

Alisema wanaume wengi wamekuwa wakitumia udhaifu wa wanawake wakati wanapokuwa sehemu za faragha na kuamua kutotumia kondomu huku wakiwalaghai wenzao wao kuwa wamezitumia wakati wanapokuwa katika mahusiano ya kimapenzi.

Hivyo, aliwataka wanawake kote nchini kutoona aibu wakati wanapokuwa na wapenzi wao wajitambue kuwa nao wanahaki ya kutoa ushauri wa matumizi ya kondomu ili kuokoa maisha yao na kuyaokoa maisha ya wenza wao.

Daladala wapandisha nauli kinyemela Dar!

Natoa rai kwa vyombo husika (viongozi SUMATRA) vifuatilie na kutafuta ufumbuzi kwa masilahi ya wananchi! Hii ni kero!

.................
(kutoka: Nipashe, 10/06/2008. Na Godfrey Monyo & Romana Mallya)
Uchunguzi umebaini kuwa, pesa zilizoongezwa katika nauli za sasa kwa baadhi ya daladala ni kati ya Sh. 50 hadi Sh. 200 wakati katika baadhi ya barabara kulikuwa na upungufu mkubwa wa magari ya abiria ikiwa ni matokea ya magari hayo kufanya kazi.

Baadhi ya daladala zinazofanya safari zake kati ya Mbagala rangi tatu na Mwenge zilipandisha nauli hadi kufika Sh. 600 wakati awali ilikuwa Sh. 350.

Aidha, magari yanayofanya safari zake kati ya Gongolamboto na Posta yalipandisha nauli hadi kufikia Sh. 500 badala ya Sh. 350.

Monday 9 June 2008

Kandanda TZ!

Matokeo ya mechi za kimataifa nchini yanazidi kukatisha tamaa. Toka ngazi za vilabu hadi timu za Taifa tumekuwa hatufanyi vizuri kwa kipindi kirefu sasa.

Tatizo ni nini hasa.
Wataalamu tunawaleta sana tena kwa gharama kubwa, lakini bado tu. Tumejenga uwanja wa kisasa lakini bado.
Labda tatizo ni upeo wa uelewa wa wachezaji kimichezo na kisaikolojia - kwa maana kwamba wanahitaji kutoka nje (hasa nchi za ulaya) ili wachanganyike na wenzetu ili waweze kujifunza zaidi. Pia walimu wazalendo wawe wanapata kozi nje (ulaya).

Kwa hiyo serikali kupitia wizara ya michezo na utamaduni na shirikisho la kandanda waandae fungu maalumu la kuinua kandanda nchini kwa kuwatoa nje wachezaji na makocha ili waone na kujifunza zaidi.

Saturday 7 June 2008

June 07

Fungua njia mtoto kaanza tambaa!
-King Kiki Mpango Mwanza

'Willkommen' Euro 2008!

Euro 2008 starts later today in Switzerland and Austria, as co-hosts.

Normally I support England, but this time they did not qualify for the finals.

France is my second choice, because of Manchester United's Patrice Evra, Sylivestre and Saha connections.

Van der Sar's Holland will be my alternative choice!

So I won't get any disappointment as it is not so often that two good teams lose their games at same stage unless they meet each other at knockout stage, and if they meet football will be the winner!!

Best wishes to all football fans.

Friday 6 June 2008

Is that jingle Sikinde's?

Music from Africa is rarely (if any) heard in radios or tv in UK.

But I am very much interested to know if the piece of instrumental music, or a jingle, heard in the bbc one's tv program -homes under the hammer- is from the song performed by our very own Mlimani Park orchestra (Sikinde). The jingle seems to be taken from the song 'mimi kazi yangu taxi driver' released in the early 1980s -RTD production. The saxaphones and trumpets in the jingle reminds me of the legend King Enock's time at Mlimani Park!

I would be happy to get the truth or info on that potential good news!

Thank You!!

Love, Perfomance and Life!

Last season in different occassions I heard from Alan Shearer and Tony Adams that there were players who need to be loved in order to get out the best from them.

Shearer, the former Southampton, Blackburn and Newcastle star, was talking in the famous BBC One/Two matchday highlights program -Match of the Day; where he is the regular pundit.

In the show Shearer mentioned that Jermain Jenas was not performing well at Newcastle because he was not loved. At the moment Jenas is doing well at Tottenham Hotspars because he is loved (he needs to be loved).

Also Jenas' teammate, Dimitar Berbatov, was another player whose performance needs to be boosted by love. When Berbatov is loved, he plays very well according to Shearer.

Tony Adams, assistant manager at Portsmouth FC, (once on tv -skysports(?)) said that Glen Johnson who plays at Portsmouth is doing well at the moment because he needed to loved -something which he lacked at Chesea!

These comments might be true or might not, but in my own view I think it is true that 'love' is an important component in everyday life (not only in sports as Shearer and Adams have pointed out).

Human beings naturally do react positively to love being shown to them by others.

That is why I said this yesterday; give love as much as you would like to be loved!

Thursday 5 June 2008

Love and wisdom

Think love,
Think yourself,
Think about others

Wednesday 4 June 2008

Congratulations to Barrack!

Senator Barrack Obama has secured enough votes (delegates) be the Democratic Party nominee for the US Presidential Elections later this year!
To be fair, I must admit that I didn't expect him to beat Senator Hillary Clinton; so he has proved me wrong!
However, I would like to congratulate him for the achievements against his fellow Party member (it is the victory within the party).
Also I wish him success and victory in the forthcoming election campaigns!
In fact, his policies are good and they were a secret weapon for his victory.
Now I hope that Sen. Clinton will be his running mate and eventual Vice President of the United States.

Tuesday 3 June 2008

Ronny's doing a Gabbi!

The Portuguese national team and Manchester United's star, Cristiano Ronado is reminding me on what happened with Gabriel Heinze in the summer of last year.

Heinze, who was one of the most respected defenders at United, for his own reason(s) wanted to be sold away to Liverpool but Man utd were unwilling to sell. Then after continuous calls/requests from Heinze and his agent United reluctantly agreed to sell but not to rival Liverpool. So United cashed in from Real Madrid instead and off he went!

What Ronaldo is trying to do here is just to follow Gabbi's footstep so that he can be allowed to leave. But I think circumstances are different between the two. Ronaldo has 4 years on his contract and his age is only 23 while Gabbi had 2 years left with the age of 26 or 27!

Because Ronaldo and Heinze are close friends, I am tempted to think that the latter has got some influence on the former's current open move!

nice words ...

'there is a fine line between
success and failure (winning and losing)'

Vipimo viwe sawa kisheria!

Wembe huu unaotumika kukimbizana na wauza bangi au wapika gongo utumike pia kuwashughulikia na kuwafikisha ktk mkondo wa sheria wezi wa mabilioni ya fedha za umma (mafisadi) ambao wanahusishwa na kashfa mbalimbali nchini!
Vyombo vya dola visiwe na mstari wa mbele tu kuwashughulikia hawa wananchi ambao wanasumbuliwa na umasikini, ambapo hela ambazo zingesaidia kuwanasua watanzania ili wasiuze bangi au gongo zimechukuliwa na wachache. Huyu mwananchi kama angekuwa na hela ya mkopo toka serikalini angefanya jambo la maana, lakini hela zenyewe serikalini zinaliwa na wachache (wenye uchu wa madaraka na utajiri); maskini wa watu anabaki njaa tupu na kuanza kuhangaika na maisha!
Nashangaa kweli!!
...........
...........

Mkazi wa Kisarawe akukutwa na bangi kilo saba!
(SOURCE: Alasiri, 2008-06-03 16:06:38. Na Sharon Sauwa)
Mkazi wa Kisarawe mkoani Pwani, William P.,38, anashikiliwa na Polisi kwa tuhuma za kukutwa na bangi kilo saba.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Kikosi cha Kuzuia Madawa ya Kulevya Nchini, Godfrey Nzowa, mtuhumiwa alikamatwa kutokana na taarifa kutoka kwa wasamaria wema. Alikamatwa wakati akiziuza kwa wateja wake.

Atafikishwa mahakamani, wakati wowote upelelezi ukikamilika.

Monday 2 June 2008

Flashback: Back to June 2007

Usinichekeshe
Friend: Before my uncle became rich, he had nothing in his purse!
Bogi: My uncle didn't have even a purse!!!
(Courtesy: James Tumusiime, Bogi Benda)

Posted by MOSONGA at 10:25 0 comments
.........................

Thursday, 14 June 2007
Poleni Brother George na Shemeji Georgia
Nimepokea habari za msiba wa mama yetu mpendwa kwa masikitiko makubwa. Kwa kweli mama ameacha pengo lisilozibika.
Poleni sana Nyakaho, Adam & family, Maula, Nuru na ukoo mzima, ndugu na marafiki.
Mimi pamoja na familia yangu tuko pamoja nayi ktk kipindi hiki cha majonzi. Na nawaombea faraja na moyo wa ustahimilivu katika kipindi hiki kigumu.
Mungu Awabariki sana.
Amen.

Posted by MOSONGA at 18:40 0 comments
............................

...nyumba jirani ...
Jaji mmoja mwandamizi amenusurika mvua (jela) baada ya kutuhumiwa kwa kosa la kum-flash mwana mama mmoja Oktoba 2006. Hakimu amesema kuwa mlalamikaji hakutoa ushahidi wa kutosha kutia hatiani mlalamikiwa.
Jaji mtuhumiwa huyo mkazi wa west London maeneo ya Wimbloden alituhumiwa kuwa ktk kipindi hicho Oktoba mara 2 alimvulia nguo za ndani dada huyo ndani ya treni. Ilibidi jaji atoe ushahidi kwa kutumia nguo yake ya ndani aina ya ck na kuonyesha ni jinsi gani ilivyo vigumu kumfunulia mtu maungo yake ya siri, tena ndani ya treni iliyojaa watu. Kwa hiyo huyo jaji alidai kuwa mlalamikaji alikosea kumtambua mtuhumiwa halisi (mistaken identity).
Baada ya hukumu Jaji na mkewe walifurahi na kusema sasa ataendelea na kazi yake kama kawaida maana jina lake limesafishwa.

Posted by MOSONGA at 18:31 0 comments
................................
Wednesday, 13 June 2007
Nukuu Za Mwalimu J K Nyerere
'Hakuna umaskini mbaya kama umaskini wa mawazo, ni umaskini mbaya sana'
Mwalimu J. K. Nyerere, 01/5/1995.

'Njia ya kwenda jehanam imejaa tele nia njema'
Mwalimu Nyerere, 1994

'Mtu mwenye akili akikuambia neno la kipumbavu -ukalikubali, anakudharau!'
Mwalimu Nyerere 01/5/1995

Posted by MOSONGA at 11:01 0 comments
...........................
Tuesday, 12 June 2007
Jicho kwa Nyumba Jirani!
UK wana mpango wa kuanzisha 'compulsory volunteering' kwa vijana. Watu wanasema hii ni 'morden version' ya JKT tuliyokuwa nayo kwetu!
Kwa sasa wanao utaratibu wa Community Service Voluteering (CSV) ambao unafanya kazi.


There is a call to scrap Tests for all children at 7, 11 & 14.
The General Teaching Council (UK) study say that exams are failing to improve standards and put children off school. Also teachers are being forced to 'drill' children to pass tests (for the sake of schools' good positions on the league tables) rather than giving a broader education.
According to the study, exams leave pupils in a state of panic.


UK wameandaa utaratibu wa madaktari (GPs) kupewa nafasi ktk maduka makubwa ili watu waweze kuwaona madaktari bila kukatiza ratiba zao za kila siku! Kwa maana hiyo mtu akienda shopping anamwona daktari dukani huku shopping ikiendelea. Watu wako 'busy' kiasi cha kusahau au kuchoka kwenda hospitalini!


England goes smokefree on July, 01, 2007. It will be against the law to smoke in virtually all enclosed public places and work places. If someone does smoke in public he/she could be fined or end up in court.

Posted by MOSONGA at 18:25 0 comments
Let's Share This
Diane Abbott, MP, has urged black Labour Party members to vote Jon Cruddas for the Deputy Labour Party Leadership post.
She said that he (Jon) will help ordinary black people and he's the change the Party needs. Other areas he will help include immigration and equal rights in employment especially on minimum wages and agency staffs to get equal treatment as permanent ones.

Posted by MOSONGA at 14:55 0 comments
'Nukuu'
'Mimi sina kigugumizi katika kutoa uamuzi wa haki kwa sababu si wakala wa mtu yeyote. Serikali lazima isimame upande wa wanyonge, ikisimama upande mwingine wanyonge hao hawana pa kukimbilia'.
-Rais Jakaya Kikwete, 23/11/2006.

'Kasi ya serikali kushughulikia kero za wanachi ikiwemo rushwa ni ndogo ikilinganishwa na maneno yanayotolewa na viongozi wa serikali'
-Sheikh Suleiman Gologosi, Mkurugenzi, Idara ya Dini Bakwata, 05/12/2006.

'Siri ya Ndoa ... imarisha upendo, utulivu, kuheshimiana (achana na tamaa za kimwili)'.
-Flora Wingia, Maisha Ndivyo Yalivyo, 17/9/2006.

'Defeat at Southend (1-0, Carling Cup) was a timely reminder of the importance of hardwork'.
-Sir Alex Ferguson, Manager Manchester United, 10/11/2006.

'Tensions between migrants and local residents of flashpoints include noise from migrants, accommodation, parking, street drinking, and driving standards'.
-Spending Watchdog (UK), 31/01/2007.

'Politicians are masters at promising and not delivering'.
-Wooly word, Daily Star, 11/6/2007

'You have to fight a lot in life but you come out of it stronger and better'.
-Justine Henin, French Open Champion (Women), 11/6/2007

'Something that doesn't kill you makes you stronger'
-Jordan, Crystal Palace FC Chairman 2004/05 (?)

Posted by MOSONGA at 14:37 0 comments
Monday, 11 June 2007
Mko wapi?
Tafadhali tuwasiliane popote mlipo, mie hapa ndio maskani.

1. Bosco Kitura - Mazengo na Masange/Luwa JKT
2. Marwa Kenani - MUSS
3. Zephania Mongo (Mosonga) - MUSS
4. Ernest Makale

And who else ... yes, you who reads this!!!!!!!

Posted by MOSONGA at 12:29 0 comments
Let's share this ...
How to take care of your few coins ...
1. budget properly
2. stick to budget
3. don't spend more than you earn
4. stop unnecessary purchase (careless spending)

Posted by MOSONGA at 12:25 0 comments
Happy Birthday/Anniversary
Jengo jipya la Bunge la Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dodoma linatimiza mwaka mmoja hapo kesho 12/6/2007 tangu lilipofunguliwa rasmi mwaka uliopita na Rais Kikwete.

Posted by MOSONGA at 12:22 0 comments
Napendekeza ...
Mabango/vibao, ukubwa wa maandishi, rangi za kuonyesha majina na anuani za shule za msingi na sekondari za serikali Tanzania ziwe na mfumo mmoja (format/standard).

Posted by MOSONGA at 12:20 0 comments
I didn't know this, did you?
1. Everyday we take 21,600 breaths!

2. Eye tests are recommended every 2 years!

3. A human being have 2 sq.m. of skin (area) and that it weighs a total of 5kg!!

4. We shed 19kg. of skin in our life time!

5. Tony Blair's father was a Conservative (Torry) member who, at one time, wanted to contest for a Parliamentary seat through Torry ticket!!

Posted by MOSONGA at 10:49 0 comments
Thursday, 7 June 2007
Wise words
'The secret to happyness is accepting some miserable times are inevitable'
June 2007

Posted by MOSONGA at 18:51 0 comments
Tuesday, 29 May 2007
Wisemen and Wisdom
'You are not defeated on anything until you've given up; and that the worst sin is despair!'
Mwalimu J.K. Nyerere.

'Politics may be the art of the possible, but at least in life give the impossible a go'.
Tony Blair, PM (UK), 10/5/2007

Posted by MOSONGA at 11:41 0 comments
...............................................
...............................................

Shirikisho A/Mashariki: ulikuwa ni utabiri au ukweli?

Tarehe 04/12/2006 niliwahi kuisema Kenya juu ya maendeleo yao kidemokrasia kwamba ni kikwazo tosha kutoruhusiwa kuwa mwanachama wa shirikisho (wakati nikijenga hoja kuwa huu sio wakati muafaka kuanzisha shirikisho la Afrika Mashariki).

Na kweli wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka jana (2007) maoni yangu yalipata nguvu zaidi, maana wakenya wenyewe walithibitisha dukuduku langu la wakati huo lilikuwa na ukweli! Ziliibuka vurugu na mapigano ambayo yaligeuka kuwa mauaji ya raia mithili ya vita vya wenyewe kwa wenyewe tulivyosikia au kuona ktk vyombo vya habari huko Somalia, Burundi na Rwanda!

Nilisema hivi: "Kenya demokrasia ni finyu sana na juzijuzi wameshindwa kutuletea wabunge 9 tu wa bunge la A. Mashariki na hadi sasa kesi iko mahakamani. Sasa wana ubavu wa kutoa wabunge wa bunge hilo la shirikisho? Tumeona hawana ubavu huo!! Uongozi wao si wa uwazi, tumeona mawaziri/manaibu waziri wanaachia ngazi" -04/12/2006

Na kweli Kenya hamna ubavu huo wa kutuchagulia wabunge au mnasemaje?

Shirikisho A/Mashariki: Nionavyo IV

Tarehe 11/12/2006 nilihitimisha maoni yangu kwa kubashiri kuwa watanzania walio wengi hawalitaki shirikisho na kweli ndivyo ilivyotokea kuwa. Nikagusia matatizo ya Muungano wetu Bara na Zanzibar; na sasa imebainika ni kweli una mapungufu -angalia maendeleo ya mwafaka ...(soma zaidi hapo chini)!
.............
.............

(at 05:41AM Monday on December 11, 2006):
Wachangiaji wamekuwa wakitoa mapendekezo yao juu ya nini kifanyike. Ukipitia michango kadhaa utapata mapendekezo ya wachangiaji, tena wamependekeza mengi sana. Baadhi ya michango au mapendekezo ni kama ifuatavyo:
1. Jumuiya ya Afrika mashariki iendelezwe na kusaidiwa kikamilifu na nchi wanachama. Mchangiaji mmoja alisema yale mashirika ya jumuiya yarudi, bandari, reli, ndege n.k.
2. Fursa za SADC na COMESA zitumiwe kikamilifu.
3. Kero za muungano wa Tanzani Bara na Zanzibar zitafutiwe ufumbuzi haraka na kwa uwazi. Wazanzibari hawawezi kukubali kuingizwa katika muungano mwingine wakati huu tulio nao hawaufurahii hasa kutokana na mpasuko uliopo pamoja na kero zingine zilizopo ktk muungano wetu.

Tunaweza kuwa competitive ndani ya jumuiya yetu, au ktk SADC/COMESA. Pamoja na hayo, nchi zote za jumuiya ya Afrika Mashariki ziko ktk SADC/COMESA, je hilo shirikisho lina nini kipya?
Mwisho, sio kweli kwamba wakubwa wameshakubali au kupitisha shirikisho. Wananchi ndio tutakaoamua.
Nina imani kubwa watanzania walio wengi watakataa uundwaji wa shirikisho.
Jumuiya-YES, shirikisho-NO.

Shirikisho A/Mashariki: Nionavyo III

Wakati nikitoa maoni yangu kipindi hicho, niliweza kuungwa mkono na watanzania wenzangu ktk nyakati tofauti. Kwa mfano ....
.....................
.....................
(at 06:25AM Tuesday on December 05, 2006, Dr.Khamis said):
Naunga mkono maneno ya Edison na wengineo wanaopinga “FEDERATION”. Sasa hivi kwenye Jumuiya YA Afrika ya Mashariki tuna,Tanzania,Kenya,Uganda,Rwanda na Burundi.
1. Tuwe na ushirikiano kwenye uchumi kama ule wa zamani, Bandari,Reli na Ndege.
2. Tushirikiane kuunda tena East African Airways na tuone kwamba tunafanikiwa sio kama sasa hivi kila nchi ina kampuni yake ya ndege.
3. Tujenge reli mpya na tuziimarishe reli za zamani ili usafiri wa mizigo na abiria uwe wa nafuu.Tukifanya hivi tutapunguza ajali za barabarani.

Nchi ambayo ni ya “amani” katika nchi hizi tano ni Tanzania pekee na kidogo Kenya. Historia ya Uganda ni vita, ya Rwanda ni vita na Burundi ni vita tu. Mpaka dakika hii hakuna Amani Rwanda,Burundi wala Uganda.
Hakuna “democracy” huko Uganda, Burundi wala Rwanda. Wengine wanataka kuwa Rais wa Maisha na kubadilisha katiba zao.
Federation itataka iwe na aina moja ya fedha(Monetary System) kama vile tunavyoona Euro currency katika EU –countries. Fedha ya Tanzania ni dhaifu sana.
Federation itataka iwe na jeshi moja,Bunge moja, serikali moja, rais mmoja tu.

Watanzania bado hatuko tayari na FEDERATION bali tuko tayari na muundo wa ushirikiano kama ule wa zamani wa JUMUAI YA AFRIKA YA MASHARIKI. Ni jukumu la serikali ya Tanzania kuwandaa watanzania kwa Federation. Mapaka muda huu Serikali ya Tanzania haijafanya matayarisho yoyote ya kuwaandaa wananchi wake katika hatua kubwa sana hii ya Federation.

Shirikisho A/Mashariki: Nionavyo II

Nilichosema na mwanachi mmoja kanisaidia kwa kufafanua kuhusu kauli yangu!
................
...............
(at 03:04AM Tuesday on December 12, 2006):
Kitu ambacho mwanakijiji na wengine wanaounga mkono shirikisho wanashindwa kuweka wazi ni kuwa hilo shirikisho lina kitu gani kipya?
Tunayo jumuia ya Afrika Mashariki;
Tuna SADC na COMESA
Huko nyuma ilikuwepo PAFMECSA.
So come out and tell us what difference or addition (if any) will this federation bring to the majority of Tanzanians.
It is clear that we Tanzanians are not ready so why should we rush? I understand there are some Tanzanians abroad who have somehow achieved something and would like to take advantage of the federation system. These are people whom I call greedy and self-centered*. They don't think about the majority of youth in our country who can not compete! We need time to prepare our selves as a NATION, not as individuals who are not even living in the country!
.................

*(at 12:54AM Wednesday on December 13, 2006, Dr.Khamis said):
We “Tanzanians living abroad are not GREEDY AND SELF-CENTERED “.Some of us have given you examples like that of EU just to show how a federation works and how to come around various obstacles. EU for example has one monetary system with EURO as the currency. But not all EU countries have EURO as a day-to-day currency in their monetary system. We are living aboard as well as in Tanzania since we donate money in the form of US$ to our relatives living in Tanzania in this way are helping Tanzania economically.
We are not poor (Thanks GOD) like our brothers and sisters living in Tanzania and have accumulated experience(s) that is highly required in the country.
My advice to you all Tanzanians DON’T JOIN THE FEDERATION UNTIL YOU KNOW WHAT YOU WANT TO ACHIEVE IN THAT FEDERATION.

WHY DO WE WANT A POLITICAL FEDERATION? WHAT ARE THE ADVANTAGES AND DISADVANTAGES OF THIS FEDERATION?
CAN WE SERVIVE AS A NATION OUTSIDE THIS FEDERATION?

Shirikisho A/Mashariki: Nionavyo I

Serikali yetu ilipounda tume ya kukusanya maoni kuhusu mpango wa kuharakisha uanzishwaji wa Shirikisho la Afrika Mashariki, sikubaki nyuma ktk kuchangia maoni yangu. Mimi nilikuwa mmoja wa wananchi waliopinga uanzishwaji wa Shirikisho hilo.
Nilipata fursa kutoa maoni yangu ktk majukwaa mbalimbali.
Baadhi ya maoni niliyoyatoa ni kama ifuatavyo (yako ktk sehemu nne, na niliyatoa kupitia m/kijiji blog):

..............................
..............................

(at 10:34AM Monday on December 04, 2006, edison said):
Naunga mkono dhana ya ushirikiano kibiashara na kiuchumi kama ilivyo sasa na huko nyuma.
Hakuna haja kwa wakati huu kuanzisha shirikisho la kisiasa (rais mmoja na bunge moja).
Kwa kifupi siungi mkono "federation".
Kwanza sijui kuna vigezo gani vimewekwa na wahusika (au viongozi wa A. Mashariki) kwa kila nchi mwanachama wa Jumuiya, ili kujiunga na 'shirikisho!!!".
Haiwezekani eti kwa sababu za kijiografia tu ziwe kigezo cha kila nchi kujiunga.
Mimi nina vigezo vyangu binafsi, labda leo niongelee hivi vitatu kwa pamoja:
Utulivu, Amani na Demokrasia
Nchi pekee inayoweza ku'tick' all the boxes ni TZ tu.
Kenya demokrasia ni finyu sana na juzijuzi wameshindwa kutuletea wabunge 9 tu wa bunge la A. Mashariki na hadi sasa kesi iko mahakamani. Sasa wana ubavu wa kutoa wabunge wa bunge hilo la shirikisho? Tumeona hawana ubavu huo!! Uongozi wao si wa uwazi, tumeona mawaziri/manaibu waziri wanaachia ngazi. Hizo si dalili njema! Sera zao za ARDHI na Tanzania sio haziendani kabisa. WaTZ hatutaweza ku-access ARDHI yao kama watakavyoweza ku-access ARDHI yetu TZ!!!
VERDICT: Kenya haiwezi kujiunga ktk shirikisho.
Uganda: MUSEVENI AMEBADILI KATIBA YA NCHI ILI ATAWALE KWA VIPINDI KADRI ANAVYOJISIKIA (maisha?). Huu si mfano mzuri wa kukumbatia. Uganda kuna vita vya siku nyingi na Lord's Resistance Army na hatujui mustakabali wake! Hili tulifumbie macho na kumkaribisha Konyi na LRA ktk shirikisho, tutambebea mbeleko gani? Mgogoro Uganda na DRC umeishia wapi?
VERDICT: Uganda haistahili kujiunga.
Rwanda: Rekodi ya nchi hii kidemokrasia sio nzuri pia. Sina hakika Kagame ni mwanademokrasia halisi au ni mtu anayetabilika. Wamekuwa ktk vita kwa muda mrefu na tuhitaji muda kuona amani ya kweli ipo Rwanda.
VERDICT: TUNAHITAJI MUDA KUONA MAENDELEO YA AMANI NA DEMOKRASIA YA KWELI. It's a NO, for now!
Burundi: Ndio juzi juzi tu wametia saini makubaliano ya amani na PELIPEHUTU. Tunahitaji muda wa kutosha ku-assess maendeleo ya amani, usalama wa raia na ya demokrasia, pamoja na utekelezaji wa makubaliano yao. Pia tutahitaji ushahidi wa kututhibitishia kuwa silaha zote za kijeshi/kivita zimekabidhiwa kwa vyombo halali vya dola. Wapigaji wote wa msituni wakabidhi miundombinu ya kijeshi/kivita yote waliyo nayo ktk vyombo vya dola ili tuwe na imani juu ya usalama wa raia kwa sasa na siku zijazo na kudhibiti vitendo vya unyang'anyi, ujambazi wa silaha na ujangiri katika eneo la Jumuiya.
VERDICT: NI MAPEMA MNO kuiamini Burundi kama nchi iliyo na amani na demokrasia ya kweli. Hatujui kama hii amani ya sasa ni sawa 'volcano' hai, iliyolala au iliyokufa! I am afraid, it's a NO to Burundi.
Hizi ndio sababu zangu za kulikataa SHIRIKISHO kwa nguvu zangu zote. Ninazo sababu nyingi ila hizi ni za msingi kwangu. Athari zake (shikisho)zinaweza zisitupate sisi, ila vizazi vijavyo vinaweza kutulilia kama hatujali maslahi ya utaifa kwanza!!
NB:
Tusidanganyike kwa kiini macho cha Ajira, kwa hata kwa mazingira ya sasa (bila shikirikisho) ajira ni ngumu na sisi ndio nchi kubwa, mipaka ikiwa wazi wageni wataingia kwetu na kuua kabisa hii ajira iliyopo. Sera ya elimu na ardhi ya TZ ni nzuri kuliko nchi jirani, i.e. zinawajali wanyonge. Rwanda na Burundi kuna 'population density' kubwa sana, kwa hiyo watamiminikia TZ.
Shikisho litawanufaisha zaidi Kenya, Uganda, Burundi na Rwanda, kuliko waTZ tutakavyofaidika nalo. Tuta-loose wala hatuta-benefit a lot!
WAPO WACHACHE KTK TANZANIA WATAKAONUFAIKA SANA NA MUUNDO WA SHIRIKISHO. ILA WATANZANIA WALIO WENGI WATAPATA SHIDA SANA! Sasa lipi bora, wachache wapete na tuwaache wengi ktk shida?
Tusione haya wala aibu kusema 'NO' kwa muungano wa shirikisho! Muundo wa sasa WA JUMUIYA unatosha hasa ktk masuala ya kibiashara na kiuchumi!
Asante sana.

Cristiano Ronaldo v. Man United

Cristiano ronaldo is a great player as he has proved that over time by winning several trophies and honours since he joined Manchester United from Sporting Lisbon.

But unfortunately, since the end of the season, I think he has been given wrong advice from those close to him (like professional advisors or even family members and friends). His comments are not consistent, always giving contradictory remarks about himself on his future football career with Man United!

It would be wise now to focus or concentrate with his national team duty as the Euro 2008 finals are only five days away! Also, if he is a true professional, should remember that he has got a contract to honour at Manchester United.

On the other hand if he feels he can no longer pursue his career at Old Trafford, thats is well and good. I think the club will bless your wish. There is no reason to block his move.

Manchester United is the greatest football club in the world, and without question it will always move forward with or without Cristiano Ronaldo.

Remember, there are still plenty of talented players around who can wear no.7 jersey and perform wonders. It is time now to give them a chance and I am sure they won't let Man United down. The club is always bigger than any individual(s) at the club!!

Bendera ya Taifa letu

Haya hapo chini ni maoni yangu mahala fulani kuhusu tafsiri ya rangi za bendera yetu ya Taifa hasa rangi 'nyeusi'.
Nikiangalia mfano wa wenzetu wa Afrika Kusini*, wao wamebainisha kabisa rangi; -nyeusi na nyeupe- kwa maana kuwa wapo weusi na wasiokuwa weusi ambao wanawakilishwa na rangi nyeupe*!

Ktk maoni yangu haya sina maana ya kuwabagua weupe ila ningependa kujua kama tafsiri ya rangi 'nyeusi' ktk bendera yetu inawawakilisha pia wenzetu wasiokuwa weusi. Ningependa nao wajisikie/waone kuwa wanawakilishwa ktk alama muhimu ya Taifa letu.

Wangwana, kama nimetoka nje ya mstari napenda kuomba radhi 'in advance', lakini nadhani sio vibaya/mwiko kuuliza -eti jamani!
Kuuliza si ujinga!
...........................
...........................
(Na Mosonga. Tarehe October 30, 2007 9:00 PM)
Jamani naomba tuandae mjadala wenye Kichwa cha habari:
Bendera yetu ya Taifa inakidhi matakwa ktk mazingira ya sasa?
Wakati wa kupigania uhuru, kujikomboa na kupata uhuru Tanganyika na mapinduzi ya Zanzibar, rangi za bendera yetu zilikuwa na tafsiri yake ktk mazingira ya wakati huo. Lakini sasa mazingira yamebadilika.
Rangi hizo ni:
Kijani- uoto wa asili
Njano-madini na utajiri
nyeusi-wananchi (kwa maana ni weusi??)
bluu-maji bahari, maziwa na mito

Swali langu liko ktk rangi nyeusi ktk mazingira ya leo inawakilisha nini?
Je ni wakati muafaka kubadili au kuongeza rangi ktk bendera ya taifa ili iwakilishe watanzania wa asili (race) tofauti na weusi??
Naomba nieleweke kuwa sina ugomvi na huyu miss TZ ila (je) bendera yetu inamjumuisha au inambagua? au tuna-assume au kufumba macho na kudhani iko sawa!!
..............................
..............................
*Sahihisho:
Serikali ya A. kusini inasema kuwa rangi ktk bendera yao ya Taifa hazina tafsiri yoyote (www.info.gov.za/aboutgovt/symbols/flag.htm).
"The national flag was designed by a former South African State Herald, Mr Fred Brownell, and was first used on 27 April 1994. The design and colours are a synopsis of principal elements of the country's flag history. Individual colours, or colour combinations represent different meanings for different people and therefore no universal symbolism should be attached to any of the colours."