Saturday 28 February 2009

Raha ya Wembley

Kesho ni siku ya fainali ya Kombe la Ligi wenyewe wanaita Carling Cup - kwa sababu za udhamini. Fainali hiyo ni kati ya timu za Manchester United na Tottenham Hotspur (Spurs), itachezwa ktk uwanja wa kisasa kabisa wa Wembley uliopo ktk halmashauri ya mji wa Brent -kaskazini mwa jiji la London.

Kutokana na ratiba ya mechi hiyo, inaonekana United ndio watakuwa wenyeji na hivyo kuwa na haki ya kuvaa jezi zao za nyumbani (ingawa hata Spurs nao watavaa jezi zao nyeupe kwa vile hazifanani na za Manchester United).

Kutokana na United kuwa wenyeji, nategemea washabiki wake wataingia uwanjani kupitia mageti ya mashariki (mageti A, B, P na N) na pia kupitia mageti K na L nyuma ya goli la kusini mashariki. Kwa maana hiyo mashabiki wa Spurs watatumia mageti D, E, F na G kama wageni (away fans) na upande wa nyuma ya goli la kaskazini magharibi. Upande wa away team (timu ya genini) huangaliana na ngazi za kuingilia (ramps) za Pedestrian Way unapotokea stesheni ya Wembley Park.

Bendera za timu ya Manchester United, Chama cha soka -FA, na ya Tottenham Hotspur zinaning'inizwa kwenye paa la timu ya nyumbani kwa juu!

Nje ya uwanja mashabiki hupata nafasi ya kununua vitu (merchandise) vya timu zao mfano jezi, skafu, bendera n.k. bila kusahau 'matchday program' ambayo huuzwa Paundi 5 hadi 10 kwa kutegemea uzito wa mechi.

Mageti ya kuingia uwanjani hufunguliwa mapema siku za mechi -kama saa nne hivi kabla ya mechi - kwa hiyo kesho mageti yataanza kuwa wazi kuazia saa tano za asubuhi. kwa vile mechi inatarajiwa kuanza saa tisa alasiri za Uingereza.

Kwa wale wenye tiketi halali huingia kupitia vilango vidogo (turnstiles) ambapo tiketu zao huchambuliwa (scan) kuona kama ni za halali. Tiketi bandia hukataliwa na chombo cha ku-scan na hivyo mhusika huzuiliwa kuingia. Ukishaingia tu baada ya turnstile, kuna ukaguzi wa vitu ulivyo navyo kwa sababu za kiusalama na kama una chupa za glasi au makopo (cans) vitu hivyo huzuiliwa -huwezi kuingia navyo. Na kama una chupa za plastiki za maji au vinywaji, zinafunguliwa na vifuniko vinachukuliwa na walizi unapita na chupa yako bila mfuniko. (unajua chupa yenye mfuniko inaweza kutumika ktk fujo na ikawa silaha kumrushia mtu na kumjeruhi, ndio maana hazikubaliki kuwa na mifuniko au zile za glasi na makopo).

Ukishapita sehemu ya ukaguzi (nyuma ya turnstiles), unaelekea kwenye korido pana sana ambalo huzunguka uwanja mzima.

Upande mmoja wa korido kuna vyumba/vibanda vya biashara (migahawa, baa, vinywaji na huduma ya kwanza) na upande wa pili kuna vyoo, vyumba vya stoo na ofisi ndogondogo za walizi na biashara). Vyoo vimepakana na majukwaa ya kukaa watazamaji. Kila block moja uwanjani ina vyoo vya jinsia moja.

Katikati ya korido hilo pana kuna vimeza vidogo kwa ajili ya kuweka viungo vya vyakula mfano sukari, chumvi, pilipili, maziwa, kahawa n.k. ambavyo vinakuwa ktk vimifuko vidogovidogo vya karatasi -ni ruksa kujichukulia kadri upendavyo!

Baada ya vyoo, kuna lango jingine linaitwa Block. Napo kuna wasaidizi wa kuhakikisha mtazamaji anafika ktk siti yake. Panahitaji wasaidizi kutokana na mfumo wa uwanja. Imeshatokea mara nyingi mtu anafika uwanjani kushabikia timu moja na anatumia geti sahihi, lakini anaingia Block tofauti na hivyo kukosa siti na kama ana jezi ya timu pinzani, anaweza kupata wakati mgumu anapotangatanga maeneo ya wapinzani wake!

Kama mtu una mpango wa kukaa na mwenzako ktk siti zinazofuatana hakikikisha umekata tiketi yenye geti moja mfano gate F, Block moja (mfano Block 110) na Row moja Mfano Row 29 na siti zinazofuatana mfano seat no. 22 na 23. Unaweza kupata geti moja, block moja, na siti moja ila Row tofauti kwa hiyo hamtakaa pamoja! Au mnaweza kupata geti moja (mfano Geti F) ila Blocks tofauti bila kujua - (mfano Blocks 110 na 112), na mkapata Row na siti sawa kabisa -hamtakaa pamoja! Iko hivi: mmoja atapata tiketi hii - Gate F Block 110 Row 34 Seat 17 na mwingine hii - Gate F Block 112 Row 34 seat 18 (Hapo hamuonani ndugu!). Kwa hiyo ni muhimu kuwa makini wakati wa 'booking' au unaponunua tiketi ya watu wawili au ya kundi la watu wanaofahamiana. Ebu fikiria mke au mme wako mkapotezana siti, itakuwaje!

Sababu kubwa ya kuingia mapema uwanjani ni kwa ajili ya biashara inayoendeshwa na wenye uwanja (Wembley). Maana watazamaji wakiingia mapema watanunua vyakula, vinywaji, program za mechi n.k. na hivyo kuingiza fedha zaidi kwa wenye uwanja mbali na kiingilio ulicholipa. Pia wakati wa mapumziko watazamaji hupata fursa ya mwisho kununua wakitakacho uwanjani maana baada ya mapumziko huduma hizo hufungwa. (Ila kwa mechi zilizoandaliwa na UEFA, ni marufuku pombe kuuzwa. Mfano wakati wa mechi za Euro, Champions League au UEFA Cup final, pombe hairuhusiwi. Ila kwa kesho pombe ni ruksa kwa vile waandaaji ni FA ya Uingereza). Ni marufuku kuvuta sigara maeneo yote ya ndani ya Uwanja, na ukishaingia ndani ya geti hakuna kutoka mpaka kipenga cha mwisho au labda ukitoka hakuna kuingia tena ndani.

Hiyo ndio Wembley, na kwa vyovyote vile mechi ya kesho itakuwa ya kukata na shoka!

Saint David's Day

Saint David's Day (Welsh: Dydd Gŵyl Dewi) is the feast day of Saint David, the patron saint of Wales, and falls on 1 March each year. The date of March 1st was chosen in remembrance of the death of Saint David on that day in 589, and has been celebrated by followers since then. The date was declared a national day of celebration within Wales in the 18th century.

In 2006 Saint David's Day was officially celebrated on 28 February by Roman Catholics and on 2 March by the Anglican Church in Wales, because 1 March 2006 was Ash Wednesday, which is a day of penitence on which feast days are not celebrated.

A poll conducted for Saint David's Day in 2006 found that 87% of the Welsh wanted it to be a bank holiday, with 65% prepared to sacrifice a different bank holiday to ensure this. A petition in 2007 to make St. David's Day a bank holiday was rejected by the then British Prime Minister Tony Blair.


(From Wikipedia, the free encyclopedia)

'Ghost highstreets'

Inahofiwa kuwa maeneo ya mijini (highstreets) Uingereza inaweza kugeuka 'mahame' endapo hali mbaya ya uchumi itaendelea kama ilivyo sasa.

Wakuu wa halmashauri za miji za Uingereza wanasema hali sio nzuri kwa wenye maduka kwa vile biashara imedumaa kabisa siku hizi. Watu hawanunui bidhaa madukani na hivyo kuzorotesha mapato ya kibiashara na pia serikalini kupitia kodi za mauzo.

Tayari maduka makubwa kadhaa yameshafunga biashara zao (mfano Woolworths, Adams, Zavvi n.k.) na wale wanaoendelea na biashara wanaendesha zoezi la kupunguza gharama za uendeshaji kwa kupunguza wafanyakazi pamoja na kufunga baadhi ya matawi ya biashara ambayo hayana faida.

Nafasi za kazi majeshini

Nyumbani kwetu Tanzania ni vigumu wananchi kujua nafasi za kazi ktk majeshi yetu zinapotokea (Jeshi la Wananchi (JWTZ), Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Polisi, Magereza n.k.)

Inatakiwa nafasi ziwe zinatangazwa hadharani kupitia vyombo vyote vya habari (magazetini, tv, na internet kupitia tovuti za serikali) ili wananchi wote wenye sifa wapate nafasi sawa ktk usaili na hatimaye ajira majeshini.

Entertainment: Awards Diary 2009

February:
BAFTA (British Academy of Film and Television Arts)
Brit Awards (The Brits) -2nd weekend of Feb?
Oscars
RTS (Royal Television Society) -Last wednesday of Feb?

Friday 27 February 2009

Feliz Cumpleaños* to you my wife!

With each passing year, you become more beautiful and young. Because the heart that loves is always young.

It's so nice to share special moments with you, not only as my wife but also my best friend.

I wish you a year filled with love and joy.

Happy Birthday.

From your loving husband, M.R. (Baba Tezzi)
February 27, 2009.





*Feliz Cumpleaños (Spanish) means Happy Birthday.

Swali

Nimekuwa najiuliza mara kwa mara swali hili.

Ktk miaka ya 1950 hadi 1960 wanafunzi kutoka barani Afrika walioenda ng'ambo kusoma walipokutana nje ya masomo walikuwa wanajadili mambo ya ukombozi wa bara letu la Afrika. Viongozi kama Mwalimu JK Nyerere, Kwame Nkrumah, Patrice Lumumba, Robert Mugabe n.k. walidhamiria kupigania uhuru mara waliporudi nyumbani kwao. Na kweli miaka ya 1960 ilikuwa ni ya vuguvugu la ukombozi wa Afrika.

Miaka mingi imepita baada ya nchi za kiafrika kujipatia uhuru wao na bado kuna wanafunzi kutoka Afrika wanaendelea kwenda ng'ambo tena kwa kiwango kikubwa kuliko enzi zile za Mwalimu.

Je wanafunzi walioko ng'ambo kwa sasa wana ajenda angalao moja inayowaunganisha kuhusu bara la Afrika? Suala kubwa sasa Afrika linalotawala anga ni umaskini (uchumi), mazingira, magonjwa na utandawazi. Je kwa staili ya kina Mwalimu waafrika waliopata nafasi kufika nje ya nchi na kujionea maendeleo kwingineko duniani wanalo jukwaa la kuratibu uzoefu wao na kujipanga namna ya kusaidia nyumbani Afrika.

Kina Mwalimu, Lumumba, Kenyatta, Sekou Toure kama wangekuwepo tungewaonyesha nini kulinganisha na juhudi zao?

Wito wangu ni kuwa walioko nje waungane na kuwa kitu kimoja, kuwa na sauti moja, kuandaa ajenda ya pamoja ili kuibadilisha Afrika. Vizazi vijavyo vitashukuru endapo uzoefu uliopatikana ng'ambo utairudishwa nyumbani ili kusaidia kuleta mabadiliko ya kiuchumi na kijamii.

Wale wenye taaluma zao (mfano waliosoma uchumi, biashara, sayansi, uhandisi, udaktari n.k.) onyesheni cheche zenu kwa maendeleo ya Taifa mojamoja na bara zima kwa ujumla! Wimbi la mchango wenu litaonekana ikiwa kutakuwa na jukwaa la pamoja ktk kutoa sauti au nasaha zenu kwa manufaa ya nchi zenu na Afrika. Au mnasemaje?

Mzee mzima kwenda na maji?

Siasa za Uingereza zinazidi kuingia ktk hatua nyingine. Kuna dalili kubwa kuwa Waziri Mkuu Gordon Brown anaelekea kupigwa mweleka na David Cameron wa chama cha Conservatives ktk uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwakani katikati.

Kwa kweli mambo hayakumwendea vema bwana Brown wa Labour tangu achukue madaraka. Hii inaonekana kuwa ni laana inamrudia kwa vile alihusika kwa namna moja au nyingine kumwondoa Tony Blair ktk 'mapinduzi baridi' ndani ya chama cha Labour.

Tayari kuna tetesi kuwa wabunge wa Labour wanajiandaa kuondoka 'benchi' upande wa serikali bungeni na kuhamia benchi la upinzani kwa vile chama chao kinaelekea kung'olewa madarakani. Wabunge wa chama tawala hukaa upande wa kushoto na wa upizani hugawana jukwaa la upande wa kulia (kuna vyama vingi vya upinzani mfano Consevertives, Lib.Dem, DUP, SNP-Scotland, PC-Wales, Respect n.k.).

Tetesi nyingine ni kuwa wabunge wale wakubwa (seniors) wanajiandaa kuwania kinyang'anyiro cha uongozi wa chama mara baada ya bwana Brown kung'oka (hii ni baada ya uchaguzi mkuu ambao Labour hawana matumaini ya kushinda na kurudi madarakani tena kama chama tawala bali wanatengemea kurudi kama chama cha upinzani ktk uchaguzi huo wa mwakani).

Ktk wingu hilo hilo kuna wabunge wa Labour ambao wameshaotea kuwa watapoteza ubunge wao na baadhi yao wameshatangaza kutowania tena ubunge. Mbunge aliyetajwa kukimbia 'aibu' hiyo ni Bwana Salter wa Reading Magharibi aliyetangaza kung'atuka kutoka siasa za Westminster mwakani. Mwenzake kutoka Labour -Reading Mashariki alidondoka ktk uchaguzi uliopita!

Dalili kubwa za Labour kubwagwa zilianzia ktk chaguzi za Udiwani mwaka jana ambapo mabaraza mengi ya udiwani yaliyokuwa chini ya Labour yalienda mikononi mwa Connservatives au Lib. Dems. Hiyo ilikuwa 'trela', picha kamili ni mwakani ambapo mzee mzima Brown na chama chake cha Labour wanatarajiwa kunyolewa bila maji!

Siwaombei Labour mabaya, bali hali halisi inaonyesha kuwa wataadhibiwa na wananchi ktk uchaguzi mkuu mwakani.

Almunia wa Arsenal

Juzi golikipa namba wani wa Arsenal aligeuka kichekesho ktk vyombo vya habari Uingereza baada ya kuibuka njiani akitembeza* mbwa mitaani.

Wenyeji wanasema kuwa aina ya mbwa aliyekuwa nae kipa huyo huwa ni kwa ajili ya kina mama (wanawake). Kwa utamaduni wa wenyeji, wanaume hawatembei na mbwa wa aina hiyo. Vyombo vya habari (TV, radio na magazeti) vilimchora sana.



*Zingatia:
Ni kawaida kwa watu (Uingereza) kuwapeleka mbwa matembezini karibu kila siku. Mbwa wa Uingereza hutunzwa vizuri na pia wanawekewa bima endapo wapata matatizo.
Kuwa na mbwa kunaweza kuwa ni gharama sana kwa mtu wa kipato cha kawaida na hairuhusiwi kumuacha nyumbani bila uangalizi wowote. Rafiki yangu mmoja alikuwa akisafiri toka Reading hadi Bracknell (mwendo wa dk 20, A329-Motorway) kumpeleka mbwa kwa dada yake (amwangalizie) wakati anapoenda kazini halafu anampitia mbwa jioni baada ya kazi!
Halafu kwa bahati mbaya au nzuri mbwa hawa huishi ndani ya nyumba mchana na usiku, sio nje kama tulivyozoea Afrika.
Kuna matukio kadhaa yaliyokwisha ripotiwa ambapo mbwa wameua watoto wachanga, na wakati mwingine watu wazima nao wamechanwa sura zao na mbwa!

Mkuu Nicky! Karibu sana

Mkuu nashukuru sana kwa salaam zako na nakukaribisha -tupige simu maana network zote zinapatikana juu ya kijiwe cha Ussongo!

Wednesday 25 February 2009

WoW

...................................
'life is what happens to you while you are busy making other plans'
-john lennon's quote used by 'breakfast', bbc-one tv, 20/11/2008)
.....................................

EWW

Miaka ya 1970-80 nchi yetu ilifanikiwa sana ktk kampeni ya kupambana na adui ujinga (kutojua kusoma na kuandika). Kutokana na mafanikio hayo Tanzania ilikuwa ya kwanza ktk bara la Afrika kwa kuwa na asilimia 90 ya watu wanaojua kusoma na kuandika.

Miaka ya 1990 rekodi yetu imeshuka sana hadi kufikia kwenye asilimia 60. Sina uhakika kipindi hiki tunachoanza karne mpya ya 21 kiwango hicho kiko ktk hali gani.

Mwalimu J.K. Nyerere alisema 'jifunze kusoma, wakati ni huu!'

Wakati ambapo serikali inatilia mkazo uanzishwaji na uimarishwaji wa elimu ya shule za msingi, sekondari na vyuo, Elimu ya Watu Wazima (EWW) nayo ipewe kipaumbele stahili ili isizimike kienyeji kwani wapo wanaoihitaji na serikali isiwanyime haki yao!

Tuesday 24 February 2009

WoW

'not all the facts are true'
-nov.2008

'Georgina' - Marijani Rajabu

Pata Miziki ya Dansi (Tanzania) ya kina Marijani Rajabu, Hemedi Maneti n.k.

Ingia link hii

http://home.arcor.de/tizedboy/

Ebu jikumbushe wimbo huu:
GEORGINA - Safari Trippers (Marijani)

[Wote]
Ooo Georginaaaa....

Siku uliyoondoka, uliniacha nalia na machozi.

Umekwenda kuishi mbali nami, Georgina wa mamaaaa.

Sipati usingizi, nikikumbuka tulivyoishi mimi nawe Georginaaaaa.

Ooo Georgina.

(repeat Wote)


(Chorus)
[Wote]:
Umeondoka Georgina, umeniachia masikitiko

Georgina, Georgina oooo (repeat)

[Marijani]
Nauliza Georgina oooo
Ni lini utarudi? oooooo
Uniondoe wasiwasi oooooooo

Georgina wa mama aaa
Georgina Georgina oooo

(Repeat Chorus)

source: Michuzi Blog. Tuesday, February 24, 2009

Umaskini wa Nishati

Pamoja na kwamba nchi kama Uingereza imeendelea na iko ktk dunia ya kwanza wapo wanachi wa nchi hiyo ambao wanaishi ktk aina 'mpya' ya umaskini.

Wananchi walio ktk tabaka la kati na chini kiuchumi wako njia panda kiuchumi kutokana na ugumu wa maisha na hasahasa kutokana na bei za kulipia bili mbalimbali kupaa hewani!

Kipato wananchopata hakitoshi kukidhi mahitaji yao ya kawaida ya kila siku. Mshahara ukipatikana bili ya kwanza kabisa kulipwa ni deni la nyumba (mortgage) au pango (house rent). Malipo ya bili hii ndiyo makubwa kuliko yote! Baada ya hapo bili ya umeme, gesi na maji hufuata (maana bila kupasha nyumba joto mtu unaweza kukauka kwa baridi ktk kipindi hiki cha baridi (winter). Baadae bili ya chakula!

Lakini kutokana na makali ya maisha mtu anaweza akaamua kutolipia bili ya umeme/gesi ili anunue chakula kwa ajili ya familia. Hali hii inajulikana kama umasikini wa nishati - kwa kimombo wanaita 'fuel poverty' - kwa maana watu hujiuliza 'should we EAT or HEAT?

Monday 23 February 2009

Words of Wisdom (WoW)

'I don't know the key to success but the key to failure is trying to please everybody'
-changamotoyetu.blogspot.com, 15/11/2008

Premiership Grounds (A-Z): 2008/09

Anfield - Liverpool 40,000+ (Merseyside)
Brittania Stadium - Stoke City
City of Manchester Stadium - Manchester City
Craven Cottage - Fulham FC (London
Emirates - Arsenal 60,000+

Ewood Park - Blackburn Rovers
Fratton Park - Portsmouth (South)
Goodison Park - Everton (Liverpool, Merseyside)
JJB Stadium - Wigan Athletics
Kingston Communications (KC) Stadium - Hull City

Old Trafford - Manchester United 76,000+
Reebok Stadium - Bolton (Greater Manchester)
Riverside - Middlesborough (North east)
Stadium of Light - Sunderland (North East)
Stamford Bridge - Chelsea 40,000+ (London)

St James' Park - Newcastle United (North East)
The Hawthorns - West Bromwich Albion (Birmingham)
Upton Park - West Ham United (London)
Villa Park - Aston Villa (Birmingham)
White Hart Lane - Tottenham Hotspur (London)

Benki Kuu: Hivi ni kweli?

.
.
Hivi ni kweli na inawezekana .....

.... mtu mmoja (Amatus Liyumba) apitishe ujenzi wa mabilioni ya hela pale Benki Kuu na pakajengeka kwa miaka 6 bila wakubwa wa Benki Kuu na wa nchi kuhusishwa?

... ghorofa 2 zijengwe pale mahali nyeti vile bila idhini au baraka za ikulu?


Tusidanganyane!
.
.

Inter v. Manchester United, Tue Feb.24

Travelling squad;

Goalkeepers:
Van der Sar, Foster, Kuszczak.

Defenders:
Ferdinand, Evra, O'Shea, Evans, Fabio, Eckersley.

Midfielders:
Giggs, Park, Carrick, Nani, Scholes, Possebon, Gibson, Fletcher, Ronaldo.

Forwards:
Rooney, Berbatov, Tevez, Welbeck.


source: www.manutd.com

Friday 20 February 2009

Nyumba 75,000 kutwaliwa na mabenki!

Nimeona habari leo kuwa waingereza wengi mwaka huu wanaelekea kupoteza nyumba zao kutokana na kukabiliwa na ukata (ukapa?) na hivyo kushindwa kulipa madeni yao ya kila mwezi. Waingereza walio wengi hukopa hela kutoka taasisi za fedha (benki) kwa ajili ya kununua nyumba za kuishi na baadae hukatwa kila mwezi kulingana na ukubwa wa deni.

Ugumu wa maisha umepelekea wengi wao kutolipa deni kwa miezi mitatu mfululizo iliyopita. Hicho ni kiashirio kwa mabenki kuchukua hatua zaidi ili kurejesha fedha zao, na inahofiwa kuwa nyumba 75,000 ziko mbioni kutwaliwa na kunadiwa na mabenki kwa ajili ya kugomboa deni lao. Maisha ya watu hao yanategemewa kuwa magumu hasa baada ya kupoteza makazi yao. Hilo ni ongezeko la asilimia 60 ukilinganisha na takwimu za mwaka jana ktk kipindi kama hiki. Habari hii ni kwa mujibu wa kipindi cha 'breakfast', bbcone-tv 20/02/2009.

Thursday 19 February 2009

1/7 ni 'wakuja'

Takwimu zilizotolewa juzi uingereza zinasema kuwa kuna wafanyakazi wapatao milioni 4 kutoka nje ya uingereza ambao wanafanya kazi ktk nchi hiyo. Hii ni sawa mfanyakazi mmoja kati ya saba, ya wanaofanya kazi, anatoka nje ya uingereza.

Tayari malalamiko yametanda ktk baadhi ya vyombo vya habari kutaka mipaka idhibitiwe na kutoruhusu watu kuingia nchini kwao na kuchukua kazi ambazo zingefanywa na raia wa nchi.

Hii yote imeletwa na matatizo ya uchumi yaliyoikumba dunia hivi sasa -kwa sababu wafanyakazi hao walikuwapo tangu zamani ila wamekumbukwa baada ya watu (wazawa) kupoteza kazi zao hivi karibuni.

Kusema kweli siku hizi kuna watu wengi sana wanazunguka mijini na mitaani (hasa ktk high streets) hawana pa kwenda wala cha kufanya. Na siku hizi huwezi kutofautisha siku za weekend, siku-kuu na siku za kawaida maana uwingi wa watu siku za kawaida za juma umeongezeka.

Bahati njema ni kwamba raia wa hapa kama hawana kibarua huwa wanadai malipo (benefits) kutoka serikalini, kwa hiyo anayeumia kwa sasa ni serikali yao na ndio maana inahaha kutafuta nafasi za kazi kwa raia ili isiendelee kuwalipa 'benefits'.

Kwa 'wakuja' kama hawana job wanaipa 'fresh' maana hawana haki kupata 'benefits' pamoja na kwamba wanalipa kodi na bima ya taifa (n.i.) kama kawaida.

Tuesday 17 February 2009

Tujihadhari na Nyama nyekundu

Utafiti umeonyesha kuwa nyama ya ng'ombe, kondoo, nguruwe n.k. husababisha magaonjwa ya saratani ya; matiti, ... (prostate) na tumbo. Pia nyama hizo ambazo hujulikana kama red meat zikiwa na mafutamafuta husababisha magonjwa ya moyo na kiharusi. Tunapotumia nyama ni vizuri kuondoa tabaka la mafuta ili kujiepusha na madhara hayo kiafya.

Sio vibaya kula nyama, ila tunachoshauriwa ni kuwa isiwe kila siku na kila mlo (kula nyama mara 2 kwa wiki sio vibaya).

Wataalamu wa afya na vyakula wanatushauri kutumia nyama za kuku na samaki kwa wingi huku tukipunguza matumizi ya nyama nyekundu.

Pia tunashauriwa kutumia matunda na mboga za majani ili kujikinga na saratani na magonjwa ya moyo.


Habari hii ni kwa mujibu wa gazeti la daily-express la J'nne Februari 17, 2009 ukurasa wa 7.

TZ: Upinzani wa kisiasa uwe 24/7

Huwa naona viongozi wetu wa upinzani nchini wakati mwingine wanajisahau na kuwa wananchi wa kawaida tu. Ninamaanisha kuwa hawana kitu au sera mbadala ili kupambanisha na serikali ya CCM ktk maisha ya kila siku.

Mfano kila mwisho wa mwezi Rais wa Jamhuri ya Muungano hutoa hotuba kwa wananchi. Viongozi wa vyama vya upinzani hugeuka wananchi vijiweni kuijadili na wakati mwingine kuipiga 'madongo', wakati hawana kitu mbadala kuonyesha kuwa wao wangefanyaje au wangetoa ujumbe gani tofauti kwa wananchi ktk hali kama ile. Kwa uelewa wangu ningetegemea viongozi wakuu wa vyama vikubwa vya upinzani nao wangetoa salaam zao za kila mwezi na za kufunga mwaka ili wananchi, ambao ni wapiga kura, waone kitu ambacho wanaweza kukipata ikiwa watachagua upinzani.

Viongozi wa upinzani kuweni macho kila wakati kuwapa wananchi kitu ambacho wangekipata endapo wangewachagueni mwaka 2005 au kuwaonyesha wananchi uwezo wenu ikiwa watawachagua mwaka 2010.

Kila hatua ambayo CCM inaipiga navyi pigeni sambamba au zaidi. Pekueni ahadi zote za muda mrefu ambazo CCM imezitoa lakini haijatekeleza au imetekeleza kwa rasha rasha. Mfano wananchi tuliahidiwa maji safi na salama yatapatikana umbali wa mita 400 kwa kila mtanzania ifikapo 1992. Lakini leo hii hata wale waishio mjini maji ni ya shida achilia mbali wa vijijini.

Je wapinzani mna cha kuwahakikishia wananchi endapo watakupigieni kura? Mnasemanje kuhusu hilo la maji. Vipi kuhusu umeme, barabara, uchangiaji elimu toka shule ya msingi hadi elimu ya juu, makazi bora kwa wananchi, matibabu n.k. Wekeni pamoja sera zenu na zijulikane kwa wananchi wakati wote, hakuna haja kusubiri wakati wa uchaguzi. Ziwekeni wazi sera wa kupitia vipeperushi (kwa ajili ya kuwasambazia wananchi), wekeni matangazo ktk vyombo vya habari, internet (mambo ya utandawazi) n.k.

Ni muhimu wapiga kura waelewe ni kitu gani CUF, CHADEMA, TLP, NCCR-Mageuzi n.k. wanaamini na wanasimamia (what is your selling point). Je mnauzika? Wateja watapenda bidhaa zenu (sera)? Mfano mteja akitaka kununua kitu au bidhaa fulani anajua duka au mahala pa kununua. Kwa maana hiyo hiyo ninaamini kuwa wapiga kura wangependa kujua kuwa endapo watahitaji mabadiliko kwa namna moja au nyingine ni chama kipi kiko tayari kuleta tofauti au mabadiliko wanayoyategemea. Kila siku kwenu iwe ni ya mapambano dhidi ya CCM. Wakati mwingine mnajisahau na mnakuwa wana-CCM bila kujijua!!

Pia nawashauri muandae orodha ya wagombea udiwani na ubunge ktk kata na majimbo ambayo yako mikononi mwa CCM ili wanolewe mapema na kuwa tayari kwa wakati wowote (kwa maana chaguzi ndogo huwa hazujulikani ziko lini). Orodha hii iwe kwa ajili ya matumizi ndani ya Chama sio kwa ajili ya Tume ya Uchaguzi. Chadema watakumbuka kilichowapata ktk uchaguzi mdogo kule Mbeya Vijijini hivi karibuni. Sababu yake ni ndogo tu, maandalizi ya zimamoto. Ndio maana nasema vyama vya upinzani jiandaeni sasa kwa kuteua orodha 'ghafi' ya wanaoweza kugombea endapo itatokea uchaguzi mdogo. Hili linawezekana endapo mtawashirikisha wanachama wenu. Mnaelewa ni majimbo gani yako kwa CCM kwa hiyo andaeni orodha ya wagombea (ndani ya chama) ktk majimbo hayo na kata zote kisha muyapitie na kuchuja halafu mnatunza hiyo orodha. Pia mtawapa mafunzo wahusika (candidates) mapema ili nao wawe tayari.

Anzeni sasa, msingoje 2010 MTACHELEWA!

NB: Sikumaanisha muanze kampeni za uchaguzi.

Monday 16 February 2009

Ushauri: Mliodhalilishwa mna haki kudai fidia

Pamoja na serikali kumvua madaraka aliyekuwa Mkuu wa Wilaya fulani (kule Kagera) kwa sababu za kuamrisha walimu wachapwe viboko na polisi, bado mimi naamini kuwa hiyo hatua haitoshi.

Ushauri wangu kwa walimu waliodhalilishwa na Mkuu wa Wilaya:

1. Wafungue kesi ya madai dhidi ya serikali kudai fidia ya fedha kutokana na udhalilishwaji hadharani uliofanywa na serikali. (walimu hao hawana hata kazi ya kutafuta ushahidi, kesi yao iko wazi). Hapa serikali ina kesi ya kujibu na inatakiwa kulipa fidia kwa kiwango abacho mahakama itaona kinafaa.
Pia asasi za kutetea haki za binadamu nchini ziwasaidie hao walimu ili kesi yao iandikishwe mahakamani -na walimu wapate haki yao. Hili litakuwa funzo kwa serikali na wawakilishi wake ili wakati wote wazingatie miiko, maadili ya kazi na kuheshimu katiba ya Jamhuri ya Muungano.

2. Walimu wahamishwe vituo vyao vya kazi kwenda vituo watakavyopenda wenyewe kwenda kufanyakazi.

Sasa ni mwendo wa kugombea 'vibarua'!

Hali mbaya ya kiuchumi inayoikabili dunia nzima kwa sasa, imeingia nchini Uingereza kwa kishindo. Waajiri wanapunguza wafanyakazi au kufunga kabisa shughuli zao na hivyo watu wasio na ajira wamekaribia milioni 3 kwa mujibu wa tarakimu za wiki iliyopita kutoka ofisi ya mtakwimu wa serikali.

Hali hii pia inapelekea misuguano ya kitabaka hasa baina ya wazawa na wahamiaji walioko hapa kutafuta maisha.

Magazeti ya leo yametoa kilio kikubwa kuwa wahamiaji kutoka nchi za Ulaya mashariki wanaua soko la ajira kwa wazawa kwa vile wahamiaji hao wanakubali kupokea ujira mdogo sana (chini ya theluthi ya kima cha chini). Imeripotiwa na magazeti hayo kuwa wahamiaji hao hupokea kiasi cha Paundi 2 za Uingereza kwa saa wakati kima cha chini ni Paundi 5 za Uingereza. Endapo hawa wahamiaji wataendelea kufanya kazi kwa ujira huo, ina maana kuwa waajiri wengi watawatumia ili kuokoa hala. Kwa hiyo waingereza wanataka wahamiaji hao waondolewe ili kazi hizo ziende kwa wazawa na kwa malipo halali.

Kwa maoni yangu, naona dalili za 'kiubaguzi' zinarejea taratibu kwa kisingizio cha uhaba wa ajira. Wazawa wanaibana serikali yao ili kazi zisiende kwa wahamiaji, lakini kwa kichinichini wale wabaguzi wanatumia mwanya huo kufikisha ujumbe na kutimiza ndoto zao. Maana kila wazawa wanapoongelea mambo haya ya ajira, wanaunganisha kuwa waondolewe wahamiaji.

Hii ni patashika, mwisho wake hakuna ajuae ...!

Why use Metric system?

Two days ago, presenters of talksport radio (10:00-12:00) Mike Parry and Nigel Pearson (in for Andy Townsend) critised BBCSports TV for using kilogrammes for weights of rugby players instead of the british units i.e. stones, pounds (lb.), and ounce (oz.)

according to Parry, BBC defended itself by saying that it used kgs. because of its viewers abroad. But Parry argues that the 'Beeb' should care more for its domestic viewers because are the ones who pays for TV lincensing fee.

Empirial system is still in use in UK till now, and if you are in this country you should be able to convert their units into the metric ones! For example in football, commentators refer to players' heights in foot and inches (instead of metres and cm!) and yards instead of metres. In shops you see/read weights in pounds, volumes in pints (if you are lucky, kgs. or litres can be included in brackets). In roads and motorways distance and speed is shown in miles e.g. 50m. ahead this means 'miles' not 'metres'.

The easier way to avoid confusion, is to employ your basic maths knowledge instantly in order to get the exact picture or feeling of what is meant by these empirial units because not all of us are familiar with them!

Stroke

When STROKE strikes, act F.A.S.T.

FACE -has their face fallen one side? Can they smile?
Arms -can they raise both arms and keep them there?
Speech -is their speech slurred?
Time -time to call 999 if you see any single one of these signs.
(for Tanzania: send the patient to hospital immediately)

source: an advert by NHS, www.nhs.uk/act fast

Saturday 14 February 2009

From her ... (censored!)

The heart chooses someone,
whose togetherness shall mean
the world, and
I am glad that for me
you are that special someone,
..... .... ...........
......... ...... .........
and without whom,
life would seem incomplete.
.......... ..... ........
.... ..... ................
............... .... ....
I know that you shall be my love
... .... ... ......

Happy Valentine's Day

xxx

Friday 13 February 2009

To My Special One!

You are
My Love Forever

the closer we come,
the more
I realise how
lucky I am
to have you in
my life!

Happy Valentine's Day

Polisi wanapopelelezana wenyewe!

Kikosi cha Polisi cha Thames Valley kimetangaza kuwatafuta raia wema wa Uingereza (wa kujitolea)watakaopenda kujiandikisha ili wawe wapelelezi wa polisi kwa ajili ya kuwachunguza polisi! Imeeleweka hiyo?

Hii ni staili ya wale watu wanaoitwa huku kama 'mystery shoppers'. Watu hawa huingia dukani au ofisini na kujifanya wateja lakini lengo lao kuu ni kuchunguza kama wahudumu husika wanawajali wateja na kuzingatia miiko ya kazi. Watu hawa huripoti kwa wakubwa wa maduka au ofisi husika. Lengo la kuwatumia 'mystery shoppers' ni kuboresha huduma kwa wateja na kulinda heshima ya wenye duka au ofisi hasa ktk kipindi hiki cha dunia ya ushindani.

Kwa hiyo hao raia wakijitokeza wataandikishwa kibarua (cha kujitolea) na polisi kwa siri. Kazi yao ni kujifanya kama wamepatwa na matatizo fulani (victims) mfano kubakwa, kuibiwa au tatizo lolote. Kisha wanaripoti polisi. Hapo ndipo kazi yao itaanzia, kazi yao hasa itakuwa kutathmini jisi polisi walivyoshughulikia tatizo lao na kisha kuripoti kwa siri kwa wakubwa wa polisi. Ni kama kuwachunguza utendaji wa polisi kimtego!

Kazi kwao hao mapolisi watakaochemsha au kuzembea kazini, Big Brother Huyo kaingia! Kaeni chonjo, hii ni saa mbaya!

Je huko kwetu TZ uwajibikaji uko ktk kiwango gani. Wenzetu wanatafuta namna ya kusafisha jeshi ni vizuri na sisi tujiangalia nafasi yetu.

Mwaka Arch-Consult website

Taaaatatrataaaa.......

Mwaka Arch Consult Ltd have a brand new website.

You can now get them online without a hussle of travelling to see them at their Mikocheni offices.

Please visit them (while sitting on your chair) at http://www.mwakaconsult.com

Or you can contact them by e-mail via: mwaka@mwakaconsult.com

Mwaka Consult Welcomes you all!

... thank you dad!

My daughter has just told me that last evening she had a beautiful birthday party at home.

She celebrated with a number of her frieds and enjoyed the food, drinks and bites. it was a simple party but the one to remember!

Friends and neighbours who joined her include Gire, Saumu, Rehema, Janeth, Rigo, Samuel, Abilai, Hamza, John and Njaka.

Thursday 12 February 2009

siku njema mwanangu

tezzi,
siku ya leo iwe ya furaha na upendo kwako.
wazazi wako tunakutakia heri maishani mwako na mungu akubariki.
h/birthday mwanangu eeee!

dondoo: kiharusi (stroke)

nimesikia redioni tangazo likielezea mambo muhimu ya kujali ili kugundua dalili za stroke (kiharusi).

kwa kifupi wanasema FAST.

F- Face. uso umeshuka upande mmoja?
A- Arms. inawezekana kunyoosha mikono na kuganda hapohapo? (mbawa za ndege)?
S- Speech. kuongea polepole?
T- Time. ni muda wa kupiga simu 999 kuomba msaada wa huduma ya kwanza haraka. (kwa Tanzania, mpeleke mgonjwa hospitali mara moja endapo dalili hizo zitajionyesha kwa mgonjwa).

Kugundua dalili mapema kunaweza kumsaidia mgonjwa kuepuka ulemavu wa maisha au kuokoa maisha yake!

... hata hivyo ameonyesha uungwana!

hivi karibuni niliandika kuwa mheshimiwa waziri mkuu wetu alikosea mara 2.

pamoja na makosa hayo aliyoyafanya bado anastahili pongezi kwa kuonyesha ukomavu wa kiuongozi pale alipoomba msamaha hadharani (ndani ya bunge). ni ustaarabu unaostahili kuigwa. nategemea yaliyotokea yatakuwa funzo na hayatatokea tena huko mbeleni.

nakupa 5 mhe mizengo p. k. pinda!

panya mjini reading!

halmashauri ya mji wa reading (borough council) hivi karibuni imetaja maeneo yenye panya kwa mujibu wa gazeti la evening post la reading toleo la jumanne 10/02/09.
maeneo hayo ni
oxford road, church road (caversham), wokingham road, friar street (katikati ya mji) n.k.
inaonekana panya hao wanakaribishwa na mabaki ya vyakula maana maeneo husika yana migahawa mingi pamoja na takeaways nyingi!

Tuesday 10 February 2009

Kwanini maisha ni magumu 'Yu Kei'*

Msukosuko wa uchumi ulioanzia kule Marekani umeitikisha uingereza ktk msingi wake wa kiuchumi na matokeo yake yanaonekana dhahiri mitaani na ktk nyumba za watu. Kwa hili wala halihitaji mtaalamu aliyebobea kutoka Chuo Kikuu kulielezea.

Chanzo kikubwa kabisa ni mabenki kutoa mikopo kwa watu wasio na sifa au kampuni zisizo na sifa za kukopeshwa. Kundi hili la watu au makampuni ni kubwa sana na nadhani ndio maana mabenki yalimezea mate uwingi wao na kuona kuwa watapata faida kubwa kwa kukopesha hela. Si unajua biashara ni matangazo na matangazo ni watu/wateja!!! Kwa maana hii mabenki yaliikubali 'risk' ya kuwakopesha watu hawa hela kwa mategemeo kupata faida mbeleni.

Kilichofuata ni mabenki kuwatafuta watu na kuwashawishi kuchukua mikopo kadri wawezavyo kwa masharti nafuu. Watu na makampuni yakakubali na kuchangamkia hizo pesa. Kukopa harusi kulipa matanga. Tukumbuke hii mikopo ilitakiwa ilipwe kidogo kidogo na kwa riba. Wateja walikuwa wepesi kupokea mikopo lakini kulipa wakawa na kigugumizi. Wateja walipozoea utamu wa hela, wakawa wanabadili benki. Wakichota toka Benki A, wanatumia wakiishiwa wanaenda benki B, baadae C, E, D n.k. Lakini cha ajabu ni kwamba hawa wateja walikuwa wanasahau wajibu wao wa kurejesha kidogo kidogo kila mwezi! Baada ya miaka kadhaa (mitano au zaidi)mabenki yakawa yametoa hela nyingi ambazo ziko mikononi mwa wateja, kwa upande mwingine wateja wakawa hawarudishi.

Mabenki yakashtuka. Kazi ya kufuatilia wateja ikaanza. Wateja hawana hela - wameshakula au kutumia na wengi wao hawarudishi (wameishia mitini?). Mabenki nayo yanatakiwa kurudisha hela maana na wao walikopa kwingineko. Ndio ikaanza vuta nikuvute hadi siri ikafichuka na kubatizwa jina 'credit crunch'. Huo ndio mchezo ulioanzisha 'Credit Crunch', kwa maelezo mepesi. Ikumbukwe kuwa wengi wa waliokopeshwa hawakuwa na sifa za kukopeshwa ila mabenki yalilegeza masharti ili kupanua uigo wa soko. Matokeo yake wema (au uongozi mbaya) umeziponza benki. Na benki nazo sasa zinadaiwa na wadeni wao. Mabenki mara nyingi hukopeshana wenyewe kwa wenyewe au hukopa kutoka mifuko mbalimbali ya akiba mfano mifuko ya pensheni. Na bahati mbaya sasa hela za pensheni za wastaafu ndio zimefyekwa na mabenki na hivyo 'credit crunch' imewakumba hata ambao hawakuwemo (wastaafu)!

Sasa baada ya mabenki kushtuka na kusitisha mikopo kwa wateja wake nini kimefuata?

Waingereza huwa wanaishi kwa mikopo. Karibu kila kitu cha mwingereza amekopa na kulipa taratibu. Wanatumia kadi za benki (credit card au debit card). Kuanzia nyumba wanazoishi, samani (fanicha), magari, simu za mikononi, safari (holiday), nguo na chakula wao hulipa kwa kadi. Na huo ni mkopo. Benki zinapositisha kuingiza hela ktk kadi hizo ina maana mteja hawezi kutumia kadi kwa kuchanja popote. Hii ina maana atakosa hata kununua mkate na sukari.

Hicho ndicho kitu kinachowaumiza waingereza kwa sasa. Hela haikai maana ikipita benki tu inakatwa kulipia madeni ya nyuma. Kwa hiyo mwisho wa mwezi ukifika mshahara hawauoni na wala hawaugusi. Wanachoambulia ni 'bank statement' inayoontesha hela iliyoigia mwisho wa juma au mwezi na kukatwa na wadeni (mabenki).

Makampuni nayo hayapati mikopo maana hayaaminiki. Kwa hiyo makampuni yanaishia kupunguza wafanyakazi au kufunga biashara maana hakuna mikopo ya kuendesha shughuli zao na wala hakuna wateja. Tayari makampuni kadhaa yamefunga biashara zao hapa Reading, kwa mfano: adams, marksandspencer (simplyfood outlets -caversham), woolworths na baa (pubs) nyingi tu. Kusema kweli hali ni ngumu kwa waajiri na waajiriwa. Mwajiri akibanwa mbavu anapunguzia maumivu yake kwa wafanyakazi.

Nani alitegemea kuwa bidhaa za madukani zitadoda Uingereza. Maana hapa kila msimu una fasheni yake na kuna misimu minne kwa mwaka kwa hiyo wafanyabiashara hutegemea kubadili bidhaa kila msimu mpya unapoanza. Kilichotokea sasa ni kuwa watu wameanza kutumia vya zamani, hawanunui vipya! Kama ni nguo zinavaliwa za misimu iliyopita, kiasi kwamba huduma ya mitumba nayo imeathirika. Watu hawatoi nguo au viatu vyao vilivyotumika kwa mashirika ya misaada kwa nchi zinazoendelea kwa vile hawawezi kumudu gharama za kununua nguo mpya. Huko Tanzania tusijeshangaa bei za mitumba kupaa, chanzo chake kiko huku -watu hawatoi nguo zao zilizotumika tena. Hela inaelekezwa ktk kununua mahitaji muhimu tu mfano chakula, kulipia bili za umeme na gesi. Watu wanaanza kutembea kwa miguu badala ya kutumia gari au kuchangia magari kuepuka gharama za mafuta. Kila mtu anaangalia kitu ambacho anaweza kujinyima ili mradi kuokoa matumumizi yasiyo ya lazima. Karibu familia zote za Uingereza zimeathirika na hali ya uchumi kuyumba.

Kibaya zaidi ni pale wazawa wanapotumia uzawa wao kuishinikiza serikali yao itoe ajira kwa wazawa tu na sio wageni toka nje ya Uingereza. Bahati nzuri serikali imekataa wazo hilo. Imetangaza kuwa kazi zitatolewa kwa ushindani endapo mwingereza atakuwa na sifa basi atapewa kipaumbele, lakini sio kwamba mwingereza apewe kazi kwa vile amezaliwa Uingereza. Sifa kwanza, uzawa baadae. Hata hivyo dalili hizi za uzawa si njema hasa kwa raia watokao nje ya nchi za jumuia ya Ulaya. Tayari sheria kadhaa zimetungwa hapa Uingereza kuwatenga watokao nje ya eneo la EU, waafrika tukiwemo. Huo nao ni uzawa tu! Pia ninaelewa kuwa kwa sasa hivi nafasi nyingi za kazi na mafunzo ya kazi huwaendea wazawa na wa-EU.

Hali inaweza kurejea kawaida au machungu haya yanaweza kupungua pale mabenki yatakapochukua hatua madhubuti kama vile kufuta madeni ya wateja wao sugu na pia kurudisha imani (confidence) kwa wateja wao (watu, makampuni madogo -small/medium scale enterprises, makampuni makubwa n.k.). Zoezi hili si la usiku mmoj, litachukua muda mrefu. Tayari serikali mbalimbali duniani zimeamua kuyakwamua mabenki yao ili yarejeshe imani kwa wateja wao na kuanza kukopesha tena. Ndio maana siku hizi tunasikia maneno kama vile 'stimulus packages', 'responsible lending' n.k. yakitumiwa na wakubwa ktk serikali (wanasiasa) na taasisi za kimataifa. Haya ni maandalizi ya kusawazisha mambo na ni jukumu la serikali (zote) kusaidia mabenki ili yaondokane na matatizo yaliyoyakumba ili yawe huwe huru tena kufanya kazi zake za kibenki kama kawaida. Kama zoezi hilo litafaulu, ni dhahiri pia ajira zitashamiri tena, kazi mpya zitachomoza na waliojiajiri watapata ahueni kwa kupata huduma za kibenki ambazo kwa sasa zimesitishwa. Hatimaye watu wataendesha maisha yao kwa uhakika na furaha. Hayo ndiyo mategemeo na matumaini ya wengi.



*nimeandika makala hii kwa uelewa wangu wa kawaida. mimi sio mchumi.

Man Utd: Uefa Champ/League Squad

Reds name Euro squad
Sir Alex Ferguson will have 30 players to select from when United return to the Champions League this month.

The club has registered 25 names on the main list, known as "List A" in the competition rules, and an additional five players born on or after 1 January 1987 on "List B".

The absence of Owen Hargreaves through injury and Manucho on loan to Hull City has freed up two spaces on "List A" - these have been filled with Federico Macheda (squad no. 41) and Davide Petrucci (43) from United's reserve-team ranks.

New signing Zoran Tosic is not registered, however, as he is ineligible. The Serbian played - and scored - for Partizan Belgrade in their third qualifying round defeat by Fenerbahce.

United's "List A" squad for the Champions League last 16 is as follows:

Goal Keepers:
1. Van der Sar, 12. Foster, 29. Kuszczak

Defenders:
2. Neville, 3. Evra, 5. Ferdinand, 6. Brown, 15. Vidic, 20. Fabio, 21. Rafael, 22. O'Shea

Midfielders:
8. Anderson, 11. Giggs, 13. Park, 16. Carrick, 17. Nani, 18. Scholes, 24. Fletcher, 34. Possebon, 43. Petrucci

Forwards:
7. Ronaldo, 9. Berbatov, 10. Rooney, 32. Tevez, 41. Macheda

"List B":
GK: Ben Amos,
Def: Richard Eckersley, Jonny Evans,
Mid: Darron Gibson and
Fwd: Danny Welbeck.

source: www.manutd.com, 09/02/2009

Monday 9 February 2009

I got it right!

Reds bag Barclays awards
Sir Alex Ferguson and Nemanja Vidic have been named Barclays Manager and Player of the Month respectively for January.

The Reds picked up maximum points from five Premier League matches in January without conceding a single goal, and duly moved top of the league with a game in hand on rivals Liverpool and Chelsea.

Sir Alex's men showed an ability to put teams to the sword, beating Chelsea 3-0 and West Brom 5-0, whilst also displaying the grit and determination to grind out 1-0 wins against Wigan, Bolton and Everton.

Vidic, who lost out to Dimitar Berbatov in ManUtd.com's monthly player award, was an integral part of those wins and indeed United's recent record run of clean sheets.

It's the first time Vidic has won the Barclays award. The Serbian produced a string of impressive displays in defence but also contributed at the other end of the pitch, scoring against Chelsea and West Brom.

Sir Alex, however, is no stranger to the accolade. This is his 22nd Manager of the Month trophy. (source: www.manutd.com, 07/02/2009)

..............................................
What I predicted ...

Friday, 6 February 2009
Manager of the Month (January 2009)
My manager of the month in the Premier League is Sir Alex Ferguson ...
Posted by MOSONGA RAPHAEL at 15:46

Player of the Month
Nemanja Vidic of Manchester United is my favourite player of the Month of the Premier League for January.
Posted by MOSONGA RAPHAEL at 15:45

Thursday, 29 January 2009 January awards are ours
This month's manager and player of the month should be coming from Manchester United.
We came back from on fourth place and we kept winning every game until now and our players have been brilliant!
I hope Sir Alex deserves to be manager of the month and Ryan Giggs or Dimitar Berbatov should be player of the month (in Premier League).
Posted by MOSONGA RAPHAEL at 13:14
(source: mosonga.blogspot.com 29/01/2009 and 06/02/2009)
...................................................

Friday 6 February 2009

Man Utd Fixtures: February 2009

February 2009
08 Feb Barclays Premier League West Ham A 16:00 W 1-0 Giggs
15 Feb FA Cup Derby County A 16:30 W 4-1 Nani, Gibson, Ronaldo, Welbeck
18 Feb Barclays Premier League Fulham H 20:00 W 3-0 Scholes, Berbatov, Rooney
21 Feb Barclays Premier League Blackburn H 17:30 W 2-1 Rooney, Ronaldo
24 Feb UEFA Champions League Inter Milan A 19:45 D 0-0

source: www.manutd.com

February Fixtures, 2009

February 2009
08 Feb Barclays Premier League West Ham A 16:00 W Giggs
15 Feb FA Cup Derby County A 16:30 W 4-1 Nani, Gibson, Ronaldo, Welbeck
18 Feb Barclays Premier League Fulham H 20:00 W 3-0 Scholes, Berbatov, Rooney
21 Feb Barclays Premier League Blackburn H 17:30 W 2-1 Rooney, Ronaldo
24 Feb UEFA Champions League Inter Milan A 19:45 D 0-0

source: www.manutd.com

February 06, 1958 (03:04pm GMT)

The darkest day: Feb 6th 1958
February 6th will forever be circled on the calendars of everyone connected with Manchester United.

On that day in 1958, the darkest day in United's history, 23 people - including eight players and three members of the club's staff - suffered fatal injuries in the Munich air crash.

Flying back from a European Cup tie against Red Star Belgrade, the team plane stopped in Germany to refuel. The first two attempts to take off from Munich airport were aborted; following a third attempt, the plane crashed.

source: www.manutd.com

Manager of the Month (January 2009)

My manager of the month in the Premier League is Sir Alex Ferguson.
His team has won all the matches of January and has made a record (number of clean sheets).

Player of the Month

Nemanja Vidic of Manchester United is my favourite player of the Month of the Premier League for January.

Hello! Classmates, Teachers & Seniors

PART ONE: WANAFUNZI WENZANGU:

A:
Baranga S/Msingi, Musoma (V): Darasa la I, II-VII
Iselamagazi S/Msingi, Nindo, Shinyanga (V): Darasa la I (part of).
Mapinduzi S/Msingi, Mugumu, Serengeti: darasa la II (part of).
Mkondo wangu: Darasa la I-VIIB.
Anuani ya shule: POBox ... Musoma, Tanzania.

01. Marwa Richard Nyamonge -mkondo B Tambaza Sec, Mazengo H/Sch.
02. Juma Marwa Chogoro -mkondo A Azania Sec, Usagara H/Sch., IFM, TZ Posts
03. Ms Naomi Matutu Baruro -B; Bwiru Girls, Rugambwa H/Sch., Marangu TC, Igunga Sec
04. Ms Mbusiro Michael Kehengu -B
05. Ms Rhobi Chacha Mosenye(?) -B
06. Chacha Nyamonge -Std VIA akahamia Sisimba S/M Mbeya, CBE Dar, Police Dar
07. Ms Severina Joram Nkenge -Std VIIA
08. Ms Nyamahemba Washiki -B
09. Ms Wesiko Marwa (monita std I-III) -B
10. Mwita Gati -B
11. Ogunya Mkama Ogunya -B
13. Ms Bhoke Magabe -B
14. Mtatiro Marwa Tienyi -B
15. Ms Bhoke Nyakorema -B
16. Ms Rhobi Msoba -B
17. Chacha Nyamaranya -A
18. Ms Nyawasha Machela -A
19. Ms Elizabeth Wanda -A
20. Marwa Gati -A
21. Ms Bhoke Sarya Mrisya -A
22. Charles Messanga -A
23. Mwita Magabe -A
24. Ms Bhoke Magweiga Kisyeri -B
25. Charles Kisyeri*-A
26. Chacha Mwita -A
27. Chacha Mwita -B
28. Mwita Mashauri -B
29. Chacha Mashauri -A
30. Mwita Marwa Kisyeri -B
31. Mwema Mnanka Samo -Std IVB akahamia Kongoto
32. Musoma Wanda* - Std VIIA
33. Ms Wegesa Wambura Nyakubhilela* -A
34. Ms Ghati Magweiga Kisyeri* -A
35. Ms Scholastica William -B
36. Laurent John-B
37. Buhuru (Uhuru) Samson -B
38. Ms Kichele Gati -A
39. Ms Kichele Magige Bwana -A
40. Ms Bhoke Kiginga -A (Bibi Afya)
41. Ryobha Chacha
42. Juma Mgusuhi (Kamba) -A
43. Nkombe Maswi Ketenta -B
44. Ms Mkami Maswi Ketenta -B
45. Ketango Washiki -A
46. Charles Fanuel Namba -B hadi std IV walipohama
47. Ms Robi Marwa Mwita 'Nyamaghuli' Drs I-IIIB -Dada
48. Ms Ghati Nyisane 'Seleghai' Drs IA -cousin
49. Mwita Makori -A
50. Kimwama -B, up to IIIB?
51. Mwita Marwa -B
52. Ms Gati Mnanka (d/o Robi Kisima) -B
53. Alan Christopher -(classmate) (Iselamagazi P/Sch., Shinyanga Rural)
54. Marco Francis -(classmate) (Iselamagazi P/Sch)



B:
Musoma Secondary School. Musoma. Kidato cha: I-IV
Mkondo wangu: Kidato cha IB, IIB, (IIIA, IVA -Additional Maths)
Bweni langu: Amri Abeid, first cubicle (LHS) after Common Room
Anuani ya shule: POBox 54 Musoma

01. Haruna Mohamed 'Voice' -Shaaban Robert from Kamunyonge -Musoma, UDSM
02. Deogratius Mwema Thomas
03. Nyanda Gapale
04. Raphael Jowel - , from Lamadi
05. Venance Ndunga 'Power' - Boss wa 'bwalo', from Magu, Sokoine University
06. Paul Mshimo -Tosamaganga H/Sch., BoT
07. Paul Kamalamo - ,UDSM
08. Leonard William Fweja -Amri Abeid, Tosamaganga, Sokoine Uni, Reading Uni UK
09. Marco Waryoba -Mkwawa Uni
10. Ponsian Constantine -S/Robert
11. Emmanuel Ernest (baba...shibhe!)-S/Robert, Mbeya Tech. College
12. Muungano James 'Bom-Bom' -S/Robert (midfielder wa shule -football)
13. Sophareth Magessa Kataso (Master of Ilele -'irrelevant') -Makongoro
14. Niva Michael -Lumumba
15. Maulid Gakole -Amri Abeid
16. Robinson Magambo -A.A
17. Patroba Materere -S/Robert
18. Kasambalala Evarist* -Lumumba
19. Kizito Nkwabi- Lumumba
20. Alfred Andrew Auma -Mkwawa
21. Yusto Sylivester 'VC' -CBE DSM,
22. Mayunga Ng'home -Amri abeid
23. Kicheche (kamnyama) - A/Abeid
24. (Super Short) Nyasanda -
25. (?) Bondo -
26. Marwa Kenani - Amri Abeid
27. Msafiri (Traveller) Mchemba-A.A
28. Chongo Cosmas -
29. Bartazar Chilato -Amri Abeid
30. Aruni Kitomwa (Form IB)-A.A
31. Zakayo Richard* -Makongoro
32. Makubi Mabusi -A.A; I,IIB; III,IVB Arts
33. Daniel Matiko Werema Mwita -Mkwawa. From Nyamelambala, Tarime
34. Josiah Zephania -Mkwawa. From Bungulele, Tarime
35. Chacha Magita -A.A From Tarime
36. Chacha Makubo - From Magoto, Tarime
37. Juma Simango -A.A From Ngoreme, Serengeti
38. Mapinduzi Wambura -Mkwawa from Nyamatare, Musoma
39. Mtete Bega -
40. Maira Maira -(only Form IB)
41. Kisika Mugire - (only Form IB)
42. Bernard Malebo (Mugendi) - , UDSM, Poverty Africa Mbeya
43. Deogratious Malamsha -A
44. Basole Thomas - C Pure Science
45. Vedastus Ambrose - went for CBA Kibaha High School
46. Charles .... - C Pure Science, Land Surveying Ardhi Institute
47. Lumanija -


C:
Mazengo High School, Dodoma. Kidato cha V-VI
Comb. yangu: PGM
Mkondo wangu: G3
Bweni langu: Mwongozo,
Chumba changu: No.9 Down (Form V) & Room No.14 Down (Form Six)
Anuani ya shule: POBox 47 Dodoma

01. Maulid Gakore, PGM- Mwongozo, G2 'Ndagada' (dorm. mate, also from Musoma Sec)
02. Bosco Kitura, PGM-Azimio
03. Alphonce Kiheri, PGM-Muungano G2 UDSM, NSSF, BoT
4. Shadrak Metili -PGM, G2 UDSM, NSSF
05. Manyama -PCB Mwongozo
06. Bilauri -PGM, G3
07. Emmanuel Mabirika -PGM, G3
08. Mwakyembe -PGM, G3
09. Deosdadit Hokororo -PGM, G3
10. Arnold Masaro -PGM, G3
11. B Chagula -PGM, (President, students' govt)
12. John Danda -PGM, G3. British Council
13. Wilfred Mmari -PGM, stream G2 (room-mate no.09Down, no.14Down), UDSM
14. Siston Makafu -PGM, G3
15. Samson Sesani -PCB
16. Michael Ndaskoi -PGM G3
17. Fikeni Yona -PGM G2 (roommate No.09D, No.14D)
18. Ruta -PCB
19. Ali Jonas?? - PGM G3
20. Charles ... -PGM, G3 (from Mby)
21. Rozam ... -PGM, G3 (from Mwakaleli, Tukuyu)
22. Adrian Mwanuke* -PGM, G3 UDSM, BoT
23. Baldwin Chilumba -EGM from Chidya Sec.
24. Daniel Lohay -EGM from Mbulu (Iraq(??))
25. Mchomvu -EGM
26. Roman - PGM, G2; Sectretary Students' Govt, UDSM (Law)


KURUTA (SERVICEMEN/WOMEN) WENZANGU

D:
MASANGE & LUWA JKT
Kombania yangu: C-Coy (Masange, Tabora) & B-Coy (Luwa, S'wanga).
Anuani ya kikosi: POBox 14 Tabora.
Anuani ya kikosi: POBox ... S'wanga, Rukwa.

01. Alphonce Kiheri B/C Coy- Masange/Luwa
02. Robinson Magambo HQ/B Coy-Masange/Luwa, Musoma Sec
03. Jumanne Kasanda -Masange/Luwa
04. Ms Happyness Temu a/A Coy- Masange/Luwa
05. Ms Isabela Akaro B Coy- Masange
06. Ms Audrey Komeka B Coy- Luwa
07. Bosco Kitura Masange na Luwa
08. Ms Elizabeth Fanuel Namba -Masange
09. Kipii -Masange/Luwa
10. Ms Devotha John -Masange/Luwa HQ Coy, UDSM
11. Yudas Msangi -Masange


E:
Architecture, Ardhi Institute/UCLAS
Kozi yangu: Architecture
Anuani ya Chuo: POBox 35176 DSM

Huruma Nkone
Gozbert Kakiziba
Eliah Mpembeni
Emmanuel Ngadu
Emmanuel Naikara
Benjamin Maula
Ms Yvonne Ketang'enyi Matinyi
George Raiton
Ms Veronica Peter Otaru
Ms Scolastica Mandwa
Robert Chuwa
Raphael Mbabu
Ray Sitti
Mathew Mwakagamba
Shempemba
Ms Joyce Romwald
Maro
Ernest W M Makale
Hamis (Patrick) Madaki -'Kirumba'
Goodluck Malle
Ms Amina Abdalla
Joseph Ringo
Rajabu Mazola
Mgeni
Vasco Bokella
Edwin Sannda
Fadhili Msemo
Emmanuel Nyengo
Idd Ally
Aidan
Ms Nneka Minja
John Makoye
Ally Simbano
Ms Levina Alexander (Boojo!! Waitu!)


......................................................



PART TWO: WALIMU WANGU

A:
Baranga S/Msingi, Darasa la I-VII.

Fanuel Namba (FN) -English (Mwalimu Mkuu wa kwanza hadi 1980)
Makaranga Kubwela (MK) -Kiswahili
Nyafungo Kubwela (NK) -Sayansi Kimu (dada wa Makaranga, baadae mrs CW)
Amas Joseph (AJ) -English, Sayansi (Mwalimu Mkuu 1980-86)
Chacha 'Mbegete' Jasson (CJ) -Siasa, Michezo, Kiswahili
Chilemeji Wilson Mabuba (CW) -Kiswahili, Hisabati, English
Telesphory Paschal (TP) -English
Flora Matutu (FM); Mrs Amas Joseph -English
Leonidas Lwehumbiza (LL) -Sayansi
Robert Makuna (RM) -Jiografia
Obedi Mangunu (OM)-Kiswahili
Mwita Nyamhanga Obonyo (MN)-Sayansi Kimu, Jografia
Tui Nyamhanga Obonyo* (TN)-Kiswahili, Siasa
Mwita Magweiga Kisyeri (MM) -Hisabati
Daudi Sira 'Philipo Daniel' (DS) -English, Siasa
Marwa Nyansembe (MN)-Hisabati, Kiswahili, Jiografia
Mzee John (father of Laurent John) -Dini
Sisikwa Sisikwa (brother of Buhuru Sisikwa)-Dini
Mzee Majinge -Iselamagazi, Nindo


B:
Musoma Sec. School (MUSS), Kidato cha I-IV

1.English
-Mganga
-Bulongo
-Mwombeki
-Matutu (Literature, 'Sons and Daughters' by Camara)

2.Physics
-Ms Rwango
-Johnson

3.Biology
-Mrs Mwita
-Mathias

4.Chemistry
-Fundisha AN
-Laban

5.Agriculture
-Wambura
-Seleli
-Swai
-Mmari

6.Geography
-Mrs Wambura
-Kagosi
-Rugaimkamu (Regional Geography Form IV)
-Jamhuri

7.Kiswahili
-Malima (Mzei)
-Kisaka

8.Additiona Mathematics
-Msagasa
-Nyonda, from Usagara High School

9.Basic Mathematics
-Lugai*
-(Bondowe)

10.Siasa
-Maningu

11.History (I&II)
-Malima
-Mganga

Headmaster: Nashon Otieno Otuolo
Second Master: Kaishozi
Librarian: Otieno


C:
Mazengo High School (Dodoma), PGM, Kidato cha V-VI
1.Physics:
-Abraham Nyanda
-Mrs Kafumu

2.Geography:
-Sanga

3.Advanced Mathematics:
-Ms O'Connel (from Boston, US)
-Mwinuke (also academic master)

Headmaster (Mazengo): Sylivester Mkoba*


D:
Maafande wangu JKT, (Masange na Luwa)
Lt.Col Lorry -CO, Masange
Ssgt Mluya -Sirmajor wa Kombania C-Coy
Sgt Kazoba -C-Coy Masange, Catch phrase: 'Kuruta umeona picha yangu kwenye stempu?'
Cpl Kashandago C-Coy (mjongomeaji!!)
Cpl Kimaro
Lt Majani -OC, A-Coy Masange

Lt Nyenyema* -QM, Luwa
WWII Salum, Luwa
Ssgt Lucas Chacha, Luwa (Mzee Wangu)
SSgt Dawson, Luwa
Sgt Edward, Luwa
Cpl Mrope, Luwa
Cpl Ndunguru, Luwa
Cpl Misigaro, Luwa


E:
Ardhi Institute/UCLAS

Lazaro Peter C1 III, C6 III; C9.1 I
A Mosha C1 I, II; C6 I; C9.1 I, II; C15 IV
Gillya C2 I, II, III; C9.1 V
Simon Mhando C3 I; C4 III
Nderimo C4 I, II
Cyriacus Lwamayanga C5.1 I, II, III; C5.2 II(part); C9.1 I; C13 IV; Field training I-III
Kyomi* C5.2 II(part)
Z Moshi C5.2 III, IV; C10
Lekule C6 II, C9.1 V, C11 IV
Mkonny C7 III, C9.1 III
K A W Byabato C5.3 I, II; C15 I
Mattesso C8 II, III(part of), IV; C9.1 II
Mandwa (of URP Dept) C8 III(part of)
L B Bulamile C7 II, IV; C9.1 III
Kajuna* C9.1 I, C9.2 I
L Mosha C9.1 IV, C10
Liberatus Mrema C9.1 II, IV; C14 IV
Adrian C5.2 II
Tirio Manga C1 I; C9.1 I
Ms Eliofoo C12 III
Mwakipesile C1 IV
...(part time lecturer) C7 V
...(part time lecturer) C12 IV
...(part time lecturer, from UDSM) C4 IV
...(part time lecturer, from Min. of Lands HQ) C8 III(part of)
Kai.?. C12 II

Course Codes, unofficial:
C1. Theory of Architectural Design (Principles of Design)
C2. History of Architecture
C3. (Engineering) Mathematics
C4. Theory of Structures
C5.1 Building Materials
C5.2 Building Construction
C5.3 Building Services
C6. Environmental Science
C7. Professional Practice
C8. Settlement Planning
C9.1 Design studio
C9.2 Design Art and Presention Technique
C10. Dissertation/Thesis
C11. Urban Planning
C12. Building Economics
C13. Architectural Conservation
C14. Landscape Architecture
C15. Interior Design
C16. Workshop
.................................................

*passed away, according to the information I have.

Waziri Mkuu alikosea mara 2

Sakata la mauaji ya maalbino, waziri mkuu Mhe Kayanza Mizengo Peter Pinda alikosea.
1. Kutamka kuwa wauaji wa maalbino nao wauwawe. Matamshi yake yalikiuka katiba ya Jamhuri ya Muungano ambayo yeye ameapa kuilinda.
2. Aliomba msamaha kwa masharti, kwa kutumia neno 'kama'.
'Kama' kuna mtu nimemkosea naomba msamaha. Alitakiwa aombe msamaha wa jumla kwani alikosea kwa asilimia 100.

Chama Cha Mapinduzi

Hongera kwa CCM kutimiza miaka 32 hapo jana.

Endelezeni yale mazuri yaliyoanzishwa na waasisi wa Chama na kamwe msijisahau au kulewa madaraka ya muda mrefu! Namsiwadharau wananchi, hasa wa kipato cha kawaida maana hao ndio waajiri wenu!

Danganya Toto!!

Makampuni ya kusambaza Umeme na Gesi UK yametangaza eti yanashusha bei ya bidhaa zao kuanzia mwezi ujao mwishoni ili kuwapunguzia mzigo watumiaji.
Hii ni danganya toto kwa vile wanajua wameshapata faida tayari. Imekuwa kawaida kwa haya makampuni kupandisha bei mwezi wa 9 au wa 10 (kipindi cha baridi kinapoanza) na kupunguza gharama za malipo mwezi wa 3 au wa 4 kwa vile msimu wa joto unakaribia kuanza.
Kwa hiyo hilo punguzo ni kiini macho tu. Kama kweli hayo makampuni yanajali basi yapunguze bei zake kuanzia Octoba na sio April!
Matumizi makubwa ya umeme na gesi huwa yako ktk kipindi cha msimu wa baridi (hasa Desemba hadi Machi) kwa hiyo wateja wa umeme wangeshukuru kupata punguzo kipindi hiki na sio kuwapunguzia bei pale ambapo hawahitaji kutumia umeme zaidi!
Haya watapunguza kwa sasa, lakini ikifika Septemba/Oktoba utawasikia -gharama za uendeshaji zimeongezeka na bei ya umeme na gesi imepanda kwa hiyo 'tunaongeza bei'!!!

Wiki ya Barafu UK

Wiki hii tangu jumatatu 02/02/2009 kumekuwa na baridi kali na kuanguka barafu kiasi cha kusababisha hali ya usafiri kuwa ya shida na pia shule kufungwa.
Barabara kubwa zilikuwa zinamwagiwa chumvi ili barafu iyeyuke na barabara kupitika ila kwa zile barabara za ndani zilikuwa ni kero tupu!