Friday 30 November 2007

'Skendoz'

Wakati wenzetu nchi zilizoendelea kama Uingereza na Marekani, viongozi wao wakuu au wagombea uongozi hukumbwa na kashfa za kutumia madawa ya kulevya na uvutaji bangi wakati wa ujana wao, sisi wabongo (waafrika) kashfa yetu kubwa inaweza kuwa wanawake au ukware!
Ni wasichana wangapi mtu amepitia? Ni wanawake wangapi umezaa nao watoto? Ni watoto wangapi umezaa nje ya ndoa? Au umeshatelekeza wanao, mkeo/wakeo?
Haya ni baadhi ya maswali ambayo yakijibiwa yanaweza kuibua kashfa na hata kumnyima mtu kura huko mbeleni.

Kwa upande wangu mie naomba kufanya 'dili' na 'totoz' wangu huko nyuma; chondechonde msiniangushe jamani. Hatukuachana kwa ubaya wowote eti??!! Na kwa bahati nzuri hakuna ka-mzigo nilikowaachia, au sio! Tubaki marafiki wa kawaida tu na tusaidiane kila mmoja anapokuwa mhitaji, kwani wote ni binadamu na makosa hayana mwenyewe!
Je kura yenu nimeipata au nimeikosa?

Yanga: Majina yaliyoenda CAF

Majina Yanga yatumwa CAF
Fomu za usajili wa wachezaji watakaochezea Yanga katika mashindano ya Kombe la Shirikisho mwakani jana zilitumwa katika Shirikisho la soka barani Afrika (CAF) kwa ajili ya kupata leseni.

Orodha hiyo ina majina ya wachezaji 27 na hivyo Yanga imebakisha nafasi tatu za usajili endapo itataka kuongeza hapo baadaye itakapokuwa imesonga mbele.

Wachezaji wa Yanga waliosajiliwa katika mashindano hayo ya kimataifa ni:

Ivo Mapunda, Benjamin Haule, Jackson Chove,
Amir Maftah,
Said Maulid,
Mrisho Ngassa,
Fred Mbuna,
Shadrack Nsajigwa,
Abuu Ntiro,
Abuu Ramadhani.

Credo Mwaipopo,
Gaudence Mwaikimba,
Waziri Mahadhi,
Nadir Haroub `Canavaro,
Vicent Barnabas,
Athumani Iddi,
Laurent Kabanda,
Aime Lukungu,
Samuel Ngassa,
Jerry Tegete.

Yanga itaiwakilisha nchi kwenye mashindano hayo kutokana na kufanikiwa kumaliza ligi ikiwa imeshika nafasi ya pili huku bingwa ambaye ni Simba itashiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa wa Afrika na Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati.

* SOURCE: Nipashe, 30 Nov 2007
By Somoe Ng'itu

SPUTANZA: Chama cha wanasoka wa zamani

Wakongwe wa Yanga kuiongoza SPUTANZA

29 Nov 2007
By Badru Kimwaga, Jijini

Wachezaji watatu wa zamani wa timu ya Yanga, Ramadhani Kampira, Sekilojo Chambua na Mohammed Husseni `Mmachinga` wameteuliwa kukiongoza Chama cha Wachezaji wa Soka wa Tanzania, SPUTANZA, ambapo moja ya majukumu waliyopewa ni kuhakikisha wanawaandikisha wanachama wapya na kuunganisha nguvu za wachezaji wote wa mkoa huo.

Uteuzi wa viongozi hao wapya wa chama hicho waliteuliwa hivi karibuni baada ya kufanyika kikao cha uongozi wa taifa wa SPUTANZA uliokutana jijini na tayari wameshapelekewa barua za kufahamishwa juu ya uteuzi huo.

Mmoja wa viongozi hao aliyechaguliwa kuwa Mwenyekiti, Ramadhan Kampira amesema yeye na wenzake waliletewa barua iliyotiwa saini ya Mwenyekiti, Venance Mwamoto kuwa watakiongoza chama cha mkoa wa Dar es Salaam ili kuhakikisha chama kinakuwa na nguvu na kuwaunganisha wachezaji wote wa zamani na wale wa sasa wanaoendelea kucheza mpira.

Kampira amesema mbali na jukumu la kusaka kwa kuhamasisha wachezaji wote kujiunga na chama cha mkoa pamoja na kile cha taifa, pia watakuwa na kazi ya kuwaunganisha wachezaji hao hususani wale wa zamani ambao wamesahauliwa na taifa licha ya michango yao mpaka leo kuwepo katika kumbukumbu za Tanzania.

Kampira aliwashukuru wale wote waliofanikisha kuteuliwa kwao na kuahidi kutekeleza kwa hali na mali majukumu yote waliyopewa huku akisisitiza kitu cha msingi ni kupewa ushirikiano wa kutosha.

* SOURCE: Alasiri

Thursday 29 November 2007

Man Utd 2 Sporting Lisbon 1

Last Tuesday, Manchester United made it 5 wins out of 5 games, claiming the top spot in the group.
Line-Up:
Kuszacz, O'shea, Ferdinand, Vidic, Evra, Carrick, Ronaldo, Anderson, Fletcher, Nani, Saha.
Subs used:
Giggs for Nani 46'
Teves for Saha 46'
Hargreaves for Fletcher
Match Goals (2):
Teves, Ronaldo

Remaining Matches:
December 2007
03 Dec Barclays Premier League United Vs Fulham 20:00 H
08 Dec Barclays Premier League United Vs Derby County 15:00 H
12 Dec UEFA Champions League United Vs Roma 19:45 A
16 Dec Barclays Premier League United Vs Liverpool 13:30 A
23 Dec Barclays Premier League United Vs Everton 12:00 H
26 Dec Barclays Premier League United Vs Sunderland 15:00 A
29 Dec Barclays Premier League United Vs West Ham 15:00 A

January 2008
01 Jan Barclays Premier League United Vs Birmingham 15:00 H
12 Jan Barclays Premier League United Vs Newcastle 17:15 H
19 Jan Barclays Premier League United Vs Reading 15:00 A
30 Jan Barclays Premier League United Vs Portsmouth 20:00 H

February 2008
02 Feb Barclays Premier League United Vs Tottenham 15:00 A
10 Feb Barclays Premier League United Vs Man City 12:00 H
23 Feb Barclays Premier League United Vs Newcastle 15:00 A

March 2008
01 Mar Barclays Premier League United Vs Fulham 15:00 A
08 Mar Barclays Premier League United Vs Bolton 15:00 H
15 Mar Barclays Premier League United Vs Derby County 15:00 A
22 Mar Barclays Premier League United Vs Liverpool 12:00 H
29 Mar Barclays Premier League United Vs Aston Villa 15:00 H

April 2008
05 Apr Barclays Premier League United Vs Middlsbro 15:00 A
12 Apr Barclays Premier League United Vs Arsenal 15:00 H
19 Apr Barclays Premier League United Vs Blackburn 15:00 A
26 Apr Barclays Premier League United Vs Chelsea 15:00 A

May 2008
03 May Barclays Premier League United Vs West Ham 15:00 H
11 May Barclays Premier League United Vs Wigan 15:00 A

GOALS!!!!!!
Saha-Prem:1+1=2
Scholes-Prem:1+ =1
Nani-Prem:1+1 Champ Lg: =2
Vidic-Prem:1+1 =2
Ronaldo-Prem:1+2+1+2 Champ Lg:1+2+1+1 =11
Tevez-Prem:1+1+2 Cham Lg:1+1 =6
Rooney-Prem:1+2+1 Champ Lg:1+1+1 =7
Giggs-Pre:1+ Champ Lge: =1
Ferdinand:Prem:1+ Champ Lg:1+ =2
Gerard Pique- Prem: Champ Lg:1 =1

Tuesday 27 November 2007

Bogi

Ken: Sorry, did you say you come from Hawaii or Havaii?
Patel: Havaii.
Ken: Thanks.
Patel: You are Velcome!

Sophi: I wonder why you men keep on looking on that girl?
Bogi: Why, she has got a nice figure and face!
Sophi: But take away figure and face what have you got?
Bogi: You!
(note:sophi is bogi's wife)

Esther: why has it taken you too long to give a shilling to that begger?
Sophi: it took me even longer to get it from Bogi!!!
(esther is bogi's sister, sophi is bogi's wife)

mechanic: (after repairing bogi's car) the cost is 1,000/=
bogi: why 1,000/= while you have only touched a wire?
mechanic: o.k. 100/= for touching a wire and 900/= for knowing which wire to touch!

partly from bogi-benda cartoons(by james tumusiime).

Newton's Law of Gravitation

Newton's Law of Gravitation
Newton's Universal Law of Gravitation states that;
'any two objects exert a gravitational force of attraction on each other. The direction of the force is along the line joing the objects.
The magnitude of the force is proportional to the product of the gravitational masses of the objects, and inversely proportional to the square of the distance between them'.

The constant of proportionality G is known as the universal gravitational constant. It is termed a "universal constant" because it is thought to be the same at all places and all times, and thus universally characterizes the intrinsic strength of the gravitational force.


where,
m1 exerts a force on m2 .
m2 exerts a force on m1 .
The magnitude of the gravitational force is:
F12 = G. (22)


G is Newton's constant:
G = 6.67 x 10- 11 N m 2 /kg 2.
The constant of proportionality G is known as the universal gravitational constant. It is termed a "universal constant" because it is thought to be the same at all places and all times, and thus universally characterizes the intrinsic strength of the gravitational force.
The Center of Mass for a Binary System

where R is the total separation between the centers of the two objects. The center of mass is familiar to anyone who has ever played on a see-saw. The fulcrum point at which the see-saw will exactly balance two people sitting on either end is the center of mass for the two persons sitting on the see-saw.
Here is a Center of Mass Calculator that will help you make and visualize calculations concerning the center of mass.

Partly from: www.glenbrook.kl2.il.us

My Physics memory put to test!

This is what I still remember (about laws of motion etc.) ....

Newton's Laws of Motion: (Form Two)
Law 1:
'Everybody continues in motion in a straight line unless it is compeeled by an external force'

Law 2:
'The rate of change of momentum is directly proportiona to the force applied and takes place in the direction of force'
F=Ma (M=mass, a=acceleration

Law 3:
'To every action there is an equal and opposite reaction'.
or
'Actions and reactions are equal and opposite'.
(Check in A.F. Abbott)


Newton's Law of Universal Gravitation (Form Five):
'The force of attracion between two bodies (masses) is proportional to the product of their masses and inversely proportional to the square of their distance apart'.
i.e. F = GMm/r/r

This is also called the 'inverse-square law'
(Check Nelkon & Parker)

Next time I will be Challenging my memories on other areas in Phyics or any other subject.

Living

'As humans, we continually put limits on ourselves for no reason at all!

What's worse is putting limits on God who can do all things.

WHEN YOU'RE BUSY JUDGING PEOPLE, YOU HAVE NO TIME TO LOVE THEM'.

From: Michuzi (Nicki)

Zone 6: AFRICA*

51 teams involved, 12 groups
5 slots
+1 South Africa qualifies directly as the host; so Africa to have 6 teams!

Group 1
1. Cameroon
2. Cape Verde Islands
3. Tanzania
4. Mauritius

Group 2
1. Guinea
2. Zimbabwe
3. Namibia
4. Kenya

Group 3
1. Angola
2. Benin
3. Uganda
4. Niger

Goup 4
1. Nigeria
2. South Africa
3. Equatorial Guinea
4. Sierra Leone

Group 5
1. Ghana
2. Libya
3. Gabon
4. Lesotho

Group 6
1. Senegal
2. Algeria
3. Liberia
4. Gambia

Group 7
1. Ivory Coast (Cote d'ivoire)
2. Mozambique
3. Botswana
4. Madagascar

Group 8
1. Morocco
2. Ethiopia
3. Rwanda
4. Mauritania

Group 9
1. Tunisia
2. Burkina Fasso
3. Burundi
4. Seychelles

Group 10
1. Mali
2. Congo
3. Sudan
4. Chad

Group 11
1. Togo
2. Zambia
3. Swaziland
4. Eritrea

Group 12
1. Egypt
2. DR Congo
3. Malawi
4. Djibout

*These groups in the Africa zone will also be used to determine the qualifiers for Africa Cup of Nations Finals in 2010 (to be held in Angola?)

ZONE 5: EUROPE

53 teams for 13 slots,
9 groups - winners qualify directly to the finals.
8 best runners-up to be paired for a play-off for the remainig 4 slots.

GROUP 1
1. Portugal
2. Sweden
3. Denmark
4. Hungary
5. Albania
6. Malta

GROUP 2
1. Greece
2. Israel
3. Switzerland
4. Moldova
5. Latvia
6. Luxembourg

GROUP 3
1. Czech Republic
2. Poland
3. N. Ireland
4. Slovakia
5. Slovenia
6. San Marino

GROUP 4
1. Germany
2. Russia
3. Finland
4. Wales
5. Azerbaijan
6. Liestain(spelling?)

GROUP 5
1. Spain
2. Turkey
3. Belgium
4. Bosnia-Herzegovina
5. Armenia
6. Estonia

GROUP 6
1. Croatia
2. England
3. Ukraine
4. Belarus
5. Kazakhstan
6. Andorra

GROUP 7
1. France
2. Romania
3. Serbia
4. Lithuania
5. Austria
6. Faroe Islands

GROUP 8
1. Italy
2. Bulgaria
3. Republic of Ireland
4. Cyprus
5. Georgia
6. Montenegro

GROUP 9
1. Netherlands (Holland)
2. Scotland
3. Norway
4. Macedonia
5. Iceland

ZONE 3&4 (CONCACAF & SOUTH AMERICA ZONES)

3. CONCACAF (NORTH, CENTRAL AMERICA & CARRIBEAN ZONE)
35 Teams for 3.5 slots. 3 teams qualify for World Cup while the 4th has to win a play-off match against a team from South America Zone.

Group A
1. (winner of: Dominica v. Berbados) v. USA =.. winner takes the position 1
2. (winner: Turks... v. St Lucia) v. Guatemala =... winner takes position 2
3. (winner: Bermuda v. Cayman islands) v. Trinidad&Tobago =... winner pos 3
4. (winner: Aruba v. antigua&Babuda) v. Cuba =... winner takes position 4

Group 2
1. (Belize v. St Kitt&Nevis) v. Mexico =... winner takes position 1
2. (Bahama v. British Virgin Islands) v. Jamaica =... winner pos 2
3. (Dominican Rep. v. Puerto Rico) v. Honduras =...
4. Canada v. St Vincent Grenadine =...

Group 3
1. (US Virgin Islands v. Grenada) v. Costa Rica =...
2. (Suriname v. Montserrat) v. Guyana =...
3. (Elsalvador v. Anguilla) v. Panama =...
4. (Nicaragua v. Netherlands Antilles) v. Haiti =...


4 SOUTH AMERICA ZONE
10 TEAMS involved in a single group for 4.5 slots.
4 teams to qualify automatically for the finals in South Africa 2010. The 5th team to play a qualifying match against the 4th team from the North/Central America &Carribean Zone (Zone 3)
The matches in this group are already underway.

World Cup 2010: Asia, Oceania (Zone 1&2)

Zone 1: ASIA
Total 41 teams. 4 places available and the 5th team plays a play-off match with a winner in the Zone 2 (Oceania Zone).

Group 1:
1. Australia
2. China
3. Iraq
4. Qatar

Group 2
1. Japan
2. Bahrain
3. Oman
4. Thailand

Group 3
1. Korea Rep. (South Korea)
2. Korea DPR (North Korea)
3. Jordan
4. Tukmestan

Group 4
1. Saudi Arabia
2. Uzebikistan
3. Lebanon
4. Singapore

Group 5
1. Iran
2. Kuwait
3. UAE (United Arab Emirates)
4. Syria


OCEANIA* (Zone 2):
10 teams, (0.5 slots) the winner of the zone qualifying matches to play a play-off match with the 5th team in tha Asia Zone for the World Cup place in 2010.

*Games already underway

Monday 26 November 2007

Ke Nako! Celebrating African Humanity

FIFA's World Cup Qualifying Draw:
Official opening by the South African President His Excellency Thabo Mbeki,
Sunday 25 November 2007.

Ajali ya MUSS: Leo ni miaka 21

Mnamo tarehe 26/11/1986, miaka 21 iliyopita Shule ya Sekondari Musoma (MUSS) ilipata pigo kubwa ktk historia yake chini ya Mkuu wa Shule Nashon Otieno.

Gari la shule ambalo wanafunzi walilibatiza jina la FOKKER (Isuzu Tipper tani 7) likiwa njiani toka Shule ya Ualimu Bweri, Manispaa ya Musoma, ilipata ajali ktk kona jirani na machinjioni. Katika ajali hiyo wanafunzi kadhaa walipoteza maisha yao (ingawa sikumbuki idadi yao kwa uhakika ila ni kati ya 8 na 10 hivi!).

Timu ya mpira wa miguu ya Shule ilialikwa kucheza mechi ya kirafiki na wenzao wa Chuo cha Bweri.
Katika msafara huo wa Bweri nami ilikuwa niwemo. Mimi pamoja na rafiki yangu Amon Herman Kafugugu tulikuwepo na tulipania kupanda FOKKA la shule ili kwenda kushuhudia mpambano. Lakini kutokana na wingi wa wanafunzi ndani ya gari (washangiliaji na wachezaji)nafasi haikuwa inatosha kwa wote waliokuwepo kuondoka kwa FOKKA. Ilibidi mwalimu wa michezo Ndugu Maningu apunguze idadi. Mimi na Kafugugu ni miongoni mwa waliopunguzwa na hivyo hatukuondoka. Wapo walioenda kwa miguu maana pale na Bweri sio mbali na wakati wa kurudi walidandia gari.

Jioni ile wakati wa kurejea shuleni ktk kona, huenda kutokana na mwendo wa kasi FOKKA ilipiduka na kuua hapo hapo. Habari za ajali zilipofika shuleni, wanafunzi karibia wote tulikimbia kuelekea eneo la ajali. Tulipofika pale tulianza kutoa msaada pale tulipoweza na kusimamisha baadhi ya magari ili kutoa msaada wa usafiri hadi hospitali ya mkoa. Kwa kweli barabara ilifungika kwa muda ktk kipindi chote cha kuhudumia majeruhi na kuwanasua majeruhi na waliopoteza maisha, maana wengine walikuwa wamebanwa na vyuma vya gari!

Mwanafunzi mwingine aliuwawa ktk ajali ya pili (ajali ndani ya ajali). Lori moja likitokea Bweri, wakati giza lilishaanza, lilipita katikati ya wanafunzi waliokuwa wamezunguka eneo la ajali bila tahadhali wala kupunguza mwendo; na lilitokomea bila kusimama. Rafiki yangu Kafugugu nae alinusurika ajali ya pili ingawa alikanyagwa mguu (foot) ambao aliuuguza (jeraha) kwa zaidi ya mwezi hospitalini!

Ukumbi wa MUBIG ulitumika katika kutoa salaam za mwisho kwa marehemu.

Ingawa majina yao yamenitoka lakini bado nawakumbuka wanafunzi wenzangu waliopoteza maisha yao ktk umri mdogo. Natoa pole kwa wote walioguswa ktk ajali na misiba hasa ndugu na marafiki wa marehemu.

Bolton 1 Man Utd 0

Manchester United suffered the second defeat in the premiership at Bolton on Saturday.

Man Utd:
Van dar Sar, Brown, Ferdinand, Pique, Evra, Hargreaves, Nani, Carrick, Saha, Teves, Giggs.

Subs: Anderson for Pique

Saturday 24 November 2007

Punctuation makes a difference!

woman without her man is a savage!

woman, without her man, is a savage!

woman without her, man is a savage!

Fine Lines ...!

There is a fine line between:-
-SUCCESS and FAILURE!
-being RICH and being POOR!

Friday 23 November 2007

Fuel scarcity on way!!

Oil crisis looming, warns TPDC

The Tanzania Petroleum Development Corporation has warned that the country was without strategic oil reserves and the national economy was in for a crisis.

According to the TPDC, the lack of oil stocks makes the production sector and the entire economy the country prone to a crisis in the event of man-made or natural calamities like tsunami.

The public corporation`s board chairman, Robert Mboma, said in Dar es Salaam yesterday that at least half of the nation`s imported oil needs should have been reserved for use during hard times.

He said before the 1999 liberalisation of oil importation the corporation used to keep some oil and other petroleum products in a reserve meant for use during emergencies.

`We (TPDC) have enough experience of almost 23 years and have the ability to supply oil on behalf of the Government and to keep oil reserves while also raising profit for the Government,` noted Mboma.

Energy and Minerals minister Nazir Karamagi said that the idea to establish the reserve after the liberalisation of the oil sector came about through a 2006 Government announcement that directed that a national Strategic Petroleum Reserves be established.

He said the decision to establish the SPR, which was presented in the National Assembly in July 18, 2006, was meant to ensure that the country faced no fuel shortages even during hard times.

Having no reserve oil stocks for emergency purposes when the petroleum supply chain was disrupted was a scenario that dictated some serious thoughts, he added.

He called for an establishment and management of the facility, saying oil was very important to the country`s security as well as economic, social and, political development.

The Chairman of the Parliamentary Committee on Investment and Trade in the House recently, William Shellukindo, while presenting a 2006 report in the House recently, said there was a need for the Government to support TPDC financially so that it could establish a National Strategic Petroleum Reserve.

* SOURCE: Guardian, 23 Nov 2007
By Gadiosa Lamtey

(The remarks were made during the opening of the sidelines of an oil stakeholders` workshop on the TPDC`s role in Dar es Salaam on 22/11/2007. The workshop served as a platform for stakeholders to air their views on the current arrangement under which TPDC is the sole importer of petroleum and other oil products. Stakeholders, including private oil dealers, were expected to learn guidelines from the corporation on ways to effectively participate in the oil business).

By Mosonga

England will bounce back stronger!

I watched the match against Croatia and I think it was not England's day because everything weren't going England's way.
Sometimes to win you need a little bit of luck! Throughout 90+ minutes England weren't lucky at all!
Croatia made only two attempts in the first half and it happened they were on target and hence their goals.
Nothing was wrong with England or Steven McClaren - they were just unlucky!
Even in the first game in Zagreb it was bad luck, the same with Macedonia 0-0 draw!
However, I am optimistic that England will come back next year fresh and with vigour, hopefully they might be the World Cup Champions in 2010.
Because they are capable of that and have quality as well!

Thursday 22 November 2007

Happy Marriage

Tips of a happy marriage:
1. Love
2. respect to each other
3. give each other space
4. understand the differences
5. discipline
6. hardwork
7. looking in the same direction
8. share common values
9. commitment (to each other?)
10. be religious (worship)
11. being loyal to each other
12. Fidelity

Wednesday 21 November 2007

Ndoa

Huu ni wakati wa kutunza familia zetu, tuheshimiane, tuvumiliane, tusameheane. Na zaidi ya yote, tuachane na tamaa za mwili zisizo na tija.
-na Anti Flora, 18/11/2007

Tuesday 20 November 2007

Her Majesty's Diamond Anniversary

Her Majesty The Queen, today, celebrates her 60th (diamond) anniversary of her marriage to His Royal Highness Prince Philip. This is a long and happy marriage; the first in the history of the mornachy.

I wish them all the best and a happy marriage all time! God Bless the Queen!
-By Mosonga

Ukatili wa Wanaume kwa Wanawake! (Parts I&II)

PART I
Ukatili majumbani: Jinamizi linalowatafuna wanawake kimyakimya

Ukatili wa majumbani unaendelea kumkandamiza mwanamke wa Kitanzania na yule wa Afrika kutokana na mila potofu, tamaduni au desturi zilizopitwa na wakati kuendelezwa na baadhi ya makabila.

"Mtoto wangu niliyezaa na aliyekuwa mume wangu wa kwanza anashikiliwa na aliyekuwa mume wangu wa pili mpaka pale familia yangu itakapomlipa ng’ombe wanane aliotoa kama mahari wakati nikiolewa”.

Haya ni maneno ya Bi. Ester Masiaga, binti mdogo mwenye umri wa miaka 20 ambaye katika umri wake huo, amekwishaolewa mara mbili na kuachika.

Kwa sasa angelikuwa na watoto wawili, lakini kwa bahati mbaya mimba aliyobeba akiwa kwa mume wake wa pili, iliharibika kutokana na kipigo kikali alichopata toka kwa aliyekuwa mume wake wa pili.

Akizungumza kwa huzuni kubwa na machozi yakimtoka, Bi. Ester anasema anakumbuka kuwa akiwa na umri wa miaka 16 baba yake mzazi alimchukua toka mikononi mwa mama yake mkoani Mwanza na kwenda kumuozesha kwa mwanaume mmoja, aliyemtaja kwa jina moja la Emmanuel katika kijiji cha Mwananchi.

Anasema mwanaume huyo alikuwa ni mtu mzima kushinda yeye ila hakumbuki alikuwa na miaka mingapi, ila kwa kumwangalia katika sura yake alijua ni mtu mzima.

`` Sikuwahi kwenda shule kwa kuwa wazazi wangu hawakunisomesha,`` anaongea binti huyo mwenye rangi ya chungwa, mrefu na anayeonyesha kukata tamaa ya maisha.

Anasema kuwa kutokana na kuwa na umri mdogo kazi nyingine za nyumbani zilimpa shida kuzifanya na hiyo ilisababisha kupigwa kila siku na mumewe huyo, hadi aliporudishwa kijijini kwao akiwa na mimba ya miezi sita.

Anaongeza kuwa shangazi yake alichukua jukumu la kumtunza hadi alipojifungua mtoto wake wa kwanza.
Anasema mtoto wake huyo alipofikisha miaka miwili alitafutiwa mwanamume mwingine na kuozeshwa huko Musoma, mkoani Mara.

Anasema kuwa kama ilivyokuwa kwa mume wake wa kwanza kuwa na umri mkubwa, vivyo ndivyo ilivyokuwa kwa mume wake wa pili anayemtaja kwa jina la Chacha Range.

“Mateso yalikuwa ni kila siku, lakini haya yalizidi maana hata mwanangu niliyekwenda naye huko alikuwa akiteswa na wakati mwingine alilazwa katika majani yenye umande asubuhi,” anasema Bi. Ester huku machozi yakimtoka.

Anasema manyanyaso hayo yalizidi na siku moja asubuhi, alikutana na mwanawe huyo akiwa amelazwa katika majani na alipohoji kulikoni, hapo ndipo amani ikatoweka ndani ya nyumba.

Anasema mumewe alimjia juu na kuanza kumwangushia kipigo kikali, na kumtaka kuondoka ndani ya nyumba hiyo haraka iwezekanavyo.

* SOURCE: Nipashe, By Usu-Emma Sindila, 20 Nov 2007.


PART II
Unamfukuza mkeo wa ndoa, unalundika vimada ndani!
Vurugu ndani ya familia zetu wakati mwingine ni za kujitakia. Yapo matatizo ambayo yangeweza kutatuliwa mapema ili hali ya amani na utulivu nyumbani irejee, lakini kwa kuyapuuza, yakazua matatizo mengine makubwa zaidi.

Niliwahi kuchambua kituko kimoja ambapo baba mwenye ndoa yake aliamua pia kumuweka kinyumba shemeji yake(mdogo wa mkewe), kisha hausigeli ndani ya nyumba yake.

Shemeji pamoja na hausigeli baada ya kutambulishwa rasmi kwa bi-mkubwa walijengewa nyumba zao jirani na bi-mkubwa huyo. Bila shaka vurugu zile ulizisoma.

Leo sikiliza vurugu zinazokaribia kufanana na hizo ujionee namna nyumba zetu zinavyobomoka kutokana na sababu mbalimbali, moja ikiwa na kutoridhika na kile ulichokitafuta mwenyewe kwa utashi wako.

Yupo baba mmoja mwenye kazi nzuri tu inayomuingizia kipato. Anaye mkewe wa ndoa ambaye wamebahatika kuzaa watoto watatu.

Wamejenga nyumba yao nzuri kubwa ya kifahari na kwa ujumla maisha yao yalikuwa mazuri.

Miaka miwili hivi iliyopita, baba huyu akaletewa nyumbani mtoto ambaye alimzaa nje ya ndoa.

Inasemekana mtoto huyo aliletwa na mama yake mzazi baada ya baba kukwepa malezi. Mama kumfikisha tu kwa babake akatimua zake. Bi-mkubwa ilibidi akae kimya, hali iliyoashiria kumkubali mtoto yule. Hakuona sababu ya kulumbana na mumewe.

Baba huyu anaye dada yake ambaye inavyoonekana alikuwa haelewani na wifi yake(mke wa kaka yake). Mara kwa mara walikuwa wakizozana kwa masuala yasiyoeleweka.

Wakati kutokuelewana huko kukiendelea, baba mwenye nyumba akawa naye hawaelewani na mkewe. Kila siku mzozo wakati mwingine bila sababu.

Ikafikia wakati mume huyu akawa anamwambia mkewe iko siku nitamchinja kwa kisu. Mama akadhani ni utani, hawezi. Kwani kwa kisa gani kikubwa hata kufikia uamuzi huo.

Kama utani, mume huyu akamwambia bi-mkubwa nikirudi nyumbani leo nisikukute, la, nitakuchinja kweli. Akaondoka zake.

Bi-mkubwa akadhani ni masihara, aliporejea akashangaa kumkuta. Alichofanya mzee aliingia jikoni kuchukua kisu. Mama kuona vile akamnyakua mwanaye mdogo wa miaka mitatu hivi na kukimbia naye.

Akapeleka malalamiko yake kwa ndugu zake, mshenga wa ndoa na hata kufikisha mahakamani akiomba talaka na mgawanyo wa mali walizochuma na mumewe.

Siku ile bi-mkubwa alipotimka nyumbani, jioni yule wifi yake akamleta mwanamke ambaye alikuwa hawara wa kaka yake ili azibe nafasi iliyoachwa.

Kaka yake kuona vile akafurahi na moja kwa moja akamkabidhi bed-room aliyokuwa akilala na bi-mkubwa. Hata dada yake alishangilia kwani hakumpenda katu bi-mkubwa kama hawara huyu.

Haukupita muda, yupo mwanamke mwingine ambaye alikuwa amewekwa kinyumba na baba huyu na tayari alikuwa amezaa mtoto.

Nyumba aliyokuwa amepangishwa kodi ikawa imeisha. Na aliposikia kuwa bi-mkubwa ameondoka, naye mbio na mwanae wakatinga kwa mzee.

Kufika pale baba akawa anashangaa lakini ikatumika busara ambapo yule hawara wa kwanza alipewa chumba kingine na yule aliyekuja na mtoto akaruhusiwa kulala chumbani alikokuwa akilala bi-mkubwa kabla ya kutimua.

Sasa katika nyumba ile kukawa na wanawake wawili walioziba pengo la bi-mkubwa baada ya kuondoka.

Katika kushughulikia mzozo baina yake na mumewe, bi-mkubwa akaamuriwa na vyombo vya usuluhishi kwamba arejee kwa mumewe wakati shauri lile likipatia ufumbuzi.

Bi-mkubwa alikubali kurudi katika mji wake. Hata hivyo, kutokana na vitisho vya awali vya mumewe kwamba angemchinja, hakuthubutu kulala katika chumba chake na mumewe bali alilala chumba kingine.

Chumba kikubwa aliendelea kuishi yule bibie aliyekuja na mtoto mchanga. Bi-mkubwa kwa sasa ametulia akisubiri maamuzi ya kudai talaka. Lakini hawa vimada wawili, ni purukshani tupu.

Inapotokea bwana mzee anataka kumtoa outing mmoja wao, inabidi afanye mahesabu makubwa. Anafanya kama mwizi yaani atampa kideti huyu akidhani mwenzake hatajua.

Lakini kwa jinsi wanawake hawa wawili walivyojiwekea mtandao wa kumfuatilia mwanaume huyu, mwenyewe anawavulia kofia.

Anaweza kumwambia mmoja amfuate mahali fulani wakati fulani.

Huku akiamini kuwa inakuwa ni siri. Lakini anapokuwa akijiburudisha, ghafla anatokea mwenzake, anavuta kiti na kutaka ahudumiwe sawia.

Bwana hana la kufanya, kwani wote ni wanawake zake, hivyo anatulia kama zumbukuku.

Si unajua mtu aliyetekwa nyara anavyokuwa mjinga. Anapelekeshwa tu hajui hili wala lile.

Yote haya ni ya kujitakia. Bwana huyu hivi ana raha gani katika maisha haya ya kuzungukwa na wanawake wasio na tija kwake?

Wao nyumbani ni kula kulala na kumtafuta leo anakunywa baa gani. Hivi baba huyu biashara ziyeyuke, arudi pale nyumbani watakuwa wanatizamana vipi?
Binafsi, matatizo mengine wanadamu tunajitakia.

Mke mkubwa alikuwa nyota ya bahati kwa baba yule. Alikuwa mtulivu na mvumilivu. Ona pale alipoletewa mtoto wa nje kwa mara ya kwanza, alitulia, hakuona sababu ya kuzua rabsha kwani alitambua Maisha Ndivyo Yalivyo na hata kama angebisha, mtoto kashazaliwa na ameletwa kwa baba yake, kumbe angefanya nini zaidi? Namsifu mama huyu kwa hili, ni mvumilivu na aliyekomaa.

Huyu ndiye aliyekuwa mke anayeweza kubeba mambo. Hofu yake kubwa ni ile hatua ya mumewe kumtishia kumchinja, vinginevyo asingeondoka nyumbani kwake. Alipenda mji wake, alipenda familia yake, hata majirani wameeleza hayo.

Sasa baba huyu hana amani. Kila kukicha wanawake hawa wanamvizia yuko wapi. Je, ana raha gani huyu? Baba ni kiongozi wa nyumba, kiongozi wa familia, anapoyumbishwa na tamaa za nje ya ndoa, familia nayo ni kama vile imetoweka.

Watoto kamwe hawawezi kuishi katika misingi ya maadili mema, tulivu na endelevu.
Huu ni wakati wa kutunza familia zetu, tuheshimiane, tuvumiliane, tusameheane. Na zaidi ya yote, tuachane na tamaa za mwili zisizo na tija.

Wasalaam

SOURCE: Nipashe
Na Anti Flora Wingia, 2007-11-18
Email:
fwingia@yahoo.com

Monday 19 November 2007

Malikia atimiza 60 ktk ndoa

Malikia wa Uingereza kesho anatimiza miaka 60 ya ndoa tangu alipooana na Prince Philip mwaka 1947. Wakati huo malikia alikuwa binti mfalme na alikuwa na umri wa miaka 21!

Saturday 17 November 2007

Nguo za watoto rangi gani?

Kuna mazoea kwa wazazi wengi kuchagulia watoto rangi za nguo za kuvaa kulingana na jinsia zao. Mfano imezoeleka kuwa nguo za rangi bluu ni kwa mtoto wa kiume na pinki kwa wa kike.
Hivi karibuni wataalam kadhaa walikuwa na mjadala kuhusu hilo, ktk kipindi cha luninga 'the one show' (the 'beeb'). Wote walisema kuwa hakuna sababu yoyote ya maana zaidi ya mazoea na mtu anaweza kuvaa rangi yoyote bila kujali jinsia yake, watoto kadhalika!
Inaonekana hiki ni kitu cha kuiga tu, na inawezekana kuwa vipo vitu vingi tunaiga bila kujua vina uhalali au umuhimu gani kwetu na kimaisha kwa ujumla.

Friday 16 November 2007

Utapeli wa mchana kweupee!

Ndugu zanguni tujihadhali na watu kama hawa.Wanatumia njia ya e-mail kutaka kufanikisha kiu yao!!
HUU NI UTAPELI.
KAENI CHONJO, UKITELEZA TU UMELIWA!!
Soma hapa chini upate undani!
Na Mosonga


Date: Fri, 16 Nov 2007 01:14:18 -0800 (GMT-08:00)
From: robertfore@earthlink.net Add to Address Book Add Mobile Alert
Yahoo! DomainKeys has confirmed that this message was sent by earthlink.net. Learn more
Subject: NOTIFICATION OF BEQUEST

NOTIFICATION OF BEQUEST .
I am Dr. Robert Fore,Managing Partner,with Robert Fore
& Associates Law firm, London Branch.Admitted, 1974.
Education: LL.B 1973 Bristol University Practice
Areas: Corporate; Commercial; Oil & Gas,International
Trade; Banking, inheritance law, e.t.c

On behalf of the Trustees and Executor of the Estate
of Late George Brumley, I wish to notify you that late
George Brumley made you one of the beneficiaries of
his estate. He left the sum of Five Million One
Hundred Thousand Dollars (USD$5,100.000.00 )to you.
This may sound strange and unbelievable to you, but it
is real and true.

Late Mr. Brumley and all his family were among the
victims that died a charter plane crash on Mount
Kenya. The flight crashed into the snow-capped,
16,355-foot Lenana Peak on Mount Kenya destroying the
entire plane and killing all passengers on board.Late
George Brumley died on the month of July 2003 at the
age of 68. You can see details of his death in the CNN
link below:

http://www.cnn.com/2003/WORLD/africa/07/20/kenya.crash/index.html

He was a widely travelled man and devoted most of his
time and wealth to charity and humanitarian work. His
great philantropist work is well known and recorded
all over the world. He must have been in contact with
you in the past or you were nominated to him in his
vision to expand his Charity work. Simply put, he was
a very dedicated sufis and Christian who loved to give
out. His great philanthropy earned him numerous awards
during his life time. In dedicating this funds to you
and other beneficiaries, he instructed that you are to
use part of the funds to promote his legacy through
activities that aim to help the old, poor, needy and
disabled in the society. Late Brumleys' legacy is the
love of charity.

Please If I reach you as I am hopeful, endeavor to get
back to me as soon as possible so we can start
processing the release of the funds to you. You are to
reply me immediately providing the following
information:

1.Your Full names.
2.Valid Contact address.
3.Contact Telephone and fax numbers.

Regards,

Dr. Robert Fore
14 York Road,Ilford Essex,
IG1 3AD London, England.

PS : For the purpose of confidentiality please contact
me through my personal email:robertfore_567@hotmail.com

Thursday 15 November 2007

Muhidin Issa Michuzi: Bongo Celebrity?

Juzi, nilikuwa naongea na marafiki hapa Boston. Tukawa tunajadili habari za Tanzania kama serikali kuongeza mishahara ya wafanyakazi na madhara yake. Watu wameachishwa kazi shauri ya waajiri kushindwa kulipa mishahara mikubwa. Tuliongea kuhusu wasichana wanaopata mimba shuleni Bongo na kasi ya UKIMWI. Tuliongea kuhusu kuingiza magari Bongo na barabara zilivyojaa magari mpaka yanashindwa kutembea.

Ajabu tulijadili kwa kirefu zaidi kaka Michuzi na blogu yake maarufu ambayo karibu kila MTanzania nje ya nchi ana habari nayo. Tulisema amekuwa kama Oprah hapa Marekani, mtu ambaye watu wanamwamini na wanamtegemea kwa mambo kadhaa. Kuna watu ambao hawana raha mpaka wameona blogu ya Michuzi kama vile watu hawaoni raha mpaka wameona show ya Oprah.

Watu wakitaka habari za Bongo hawaendi kwanza ippmedia.com au site ya Daily News wanakimbilia blogu ya Michuzi. Na sasa kwa vile watu wengi wanasoma blogu ya Michuzi basi watu wanataka habari zao zionekane pale maana wanajua wengi wataziona.

Michuzi akibandika kitu watu wanakimbilia kwenye blogu yake kutoa maoni yao maana wanajua wengi watasoma. Kama kuna msiba watu wanatoa habari pale, pia kama kuna haja ya mchango watu wanatoa habari pale. Juzi tuliona habari ya mtoto mdogo aliyehitaji msaada wa kutengeneza uso. Watu walitoa pesa na ushauri mara moja. Pia Michuzi kaanzisha lugha ya 'Michuzi talk' yaani kuandika kiingereza kwa kiswahili. Wabongo wanaipenda kweli.

Na Michuzi akitoa maoni yake watu wanaona kama ndo sheria. "Michuzi kasema!" Lakini hasa navyoona waBongo wa nje ya nchi wanampenda kwa sababu anatoa picha za nyumbani na kufanya watu wajisikie hawako mbali na nchi yao.

Tulibishana kuhusu habari ya kuwa eti anatoza watu kubandika habari zao kwenye blogu. Ilibidi nimpigie Michuzi kumwuliza. Alisema hiyo habari si kweli. Hatozi hata senti tano kubandika kitu kwenye blogu yake. Alisema wakati mwingine anaweza kupewa kitu kama shukurani lakini hatozi.

Kwa kifupi uhusiano wangu na Michuzi ulianza zamani hata kabla hajawa mpiga picha wa Daily News. Alikuwa ni kijana tu mwenye kamera aliyekuwa anapiga picha za watu wakiwa disko. Msemo wake ulikuwa, " Natafuta michuzi!" Ndo kapewa jina la Michuzi. Tukamshauri awe mpiga picha wa kujitegemea Daily News, yaani freelance. Akawa analeta picha nzuri kuliko hata wapiga picha walioajiriwa pale.

Nakumbuka alivyoajiriwa Daily News mwanzoni wahariri waligoma kumwita Michuzi, wakasema atumie jina la Muhidini Issa. Lakini kila mtu alikuwa anamwita Michuzi na watu wa nje wakawa wanamwita Michuzi, mwisho walikubali aitwe Michuzi. Kwanza ilikuwa kwenye brackets, 'Michuzi'. Mwisho waliachia vizuizi na Michuzi ndo ilikuwa jina lake.

Michuzi ana moyo ya kazi anayofanya. Na kwa wasiojua Michuzi ni mwigizaji mzuri sana.


Kutoka: blog ya Chemi

Bkr zajengwa upya!

Hii habari ni kuhusu 'virginity repair'.

Kutokana na maadili ya ki-afrika ni vigumu kuiandika waziwazi hapa na kwa undani.

Ila kwa kifupi wapo wateja wa umri wa 'teens' na early 20s wa kike wanafanya 'procedure' hii Uingereza. Gharama zake ni Paundi 4,000/=, na hufanyika siku chache kabla ya mhusika kufunga ndoa na mume mtarajiwa. Zoezi hili humpumbaza 'mume' (pamoja na mashemeji/wakwe) siku ya kwanza ktk ndoa na hivyo kuwa na hisia kuwa ameoa mwanamke bikira.

Wasemaji kutoka wizara ya afya wanasema kuwa lengo lao ni kuhakikisha wanashughulika na kutoa huduma kwa ajili ya 'both physical and psychological health' ya wananchi wao.
Wengi wa wanaofika ktk hospitali kupata huduma hii ni kutoka 'ethnic minority' hasa wenye asili ya Asia wanaoishi Uingereza kwa sababu za imani zao kijamii, ambapo ni kashfa binti akipoteza bikira kabla ya kuolewa!

Huduma hii imekuwa ikitolewa kwa miaka 18 sasa. Nchi Asia, nyingine sheria haziruhusu!

Kwa nini madeni tusiyoyaweza?

Nimesoma hukumu kuhusiana na madai dhidi ya naibu waziri Mheshimiwa Fulani nimeshangaa.
Kwanza najiuliza ni kwa nini amejiingiza ktk deni kubwa kiasi hiki na wala (kwa maoni yangu) hakuwa na shida kubwa kimaisha, kama vile ugonjwa au dharura yoyote, ambayo imemlazimisha kuingia deni hilo!
Kusema ukweli, yeye kama waziri na ana uwezo kuendesha maisha yake ya kawaida bila kujiingiza ktk mkopo wa mamilioni ya hela!

Mimi binafsi naona hili liwe fundisho kwetu sote hasa watu wa kipato cha kawaida. Ni vizuri tukumbuke kutumia kwa uwiano na kiasi tunachopata au kuingiza.
Tujizuie na kujiingiza ktk bili za juu kuliko uwezo wetu au bila kuwa na mikakati ya kurejesha fedha za wale wanaotukopesha.

Unaona hata hela ya ada ya mwanae (Mheshimiwa ...) inadaiwa kuwa ni zaidi ya sh. 10,000,000/=.

'... pia anadai Sh.10,300,000 kama malipo ya gari pamoja na ada ya shule ya mtoto wa ....'
-Gazeti Nipashe, 15/11/2007.

'He further observed that the complainant had managed to get 500,000/-, being part of the alleged 10,300,000/- initial payment for the purchase of a new vehicle and school fees for defendant’s daughter'
-The Guardian, Thu 15 Nov. 2007.

Mi naona kiwango hiki ni kikubwa, hata kuliko kumsomesha mtoto Chuo Kikuu na kuhitimu shahada (kwa muda wa miaka mitatu).

Kwa wale tusio na uwezo mkubwa kifedha, tutumie shule na huduma za serikali ili kuepukana na kupatwa na hali kama hii!

Ni kweli kuwa wakati mwingine kutafuta msaada wa aina ya mkopo hakuepukiki, lakini pale pasipo na ulazima tujiepushe mzigo mzito wa madeni. Tukope kwa kadri ya uwezo wetu.

Kumbuka kukopa harusi kulipa matanga!!!

Na Mosonga

Wednesday 14 November 2007

Vijana Chipukizi ...!

Nakumbuka zile nyimbo nilizoimba enzi za udogo wangu Shule ya Msingi na nilipokuwa ktk Jeshi la Kujenga Taifa kwa mujibu wa Sheria (baada ya kidato cha Sita)!

Shule ya Msingi Baranga mwaka 1978/79 kulikuwa na gwaride la vijana wadogo toka shule mbalimbali Baranga, Kongoto, Nyambili, Sirori Simba, Wegero n.k.
Mwalimu Mgongo toka Kongoto ndie aliyeendesha mafunzo. Mara ya kwanza yalianzia Baranga halafu tukaenda Kongoto.

Wimbo maarufu sana ninaoukumbuka ni huu:
'Vijana chipukizi, kutembea kwao kuringa kwao ni sawa-sawa ...' (mara 2)
Chorus:
'Kutembea kwao'
(kiitikio) 'Ni sawa-sawa'
'Kuringa kwao'
(kiitikio) 'Ni sawa-sawa'
'vijana chipukizi, kutembea kwao kuringa kwao ni sawa-sawa' (mara 2)

Darasani Napo tuliimba nyimbo:
Mwalimu Telesphory Paschal alikuwa anatuimbisha sana. Baadhi ya nyimbo hizo;
'row row your boat; row row your boat!' (mara 2)
'gently down the stream' (mara 2)
'merrily merrily merrily life is bad a dream!' (mara 2)

'home again, (home again)
'when shall I see my home again,
when shall I see my brothers and sisters?
Never forget my home'

'jembe ni kitu bora kwa watu wote,
jembe ni kitu bora kwa wakulima, ...'

mchaka-mchaka;
'kambonaa kakimbia azimio (azimio la arusha)'

'banda wa malawi (banda wa malawi),
katuvalia ngozi ya simba, hatujali eee hatujali.
banda wa malawi (banda wa malawi),
katuvalia ngozi ya chui, hatujali ee hatujali!'

Sijui mwanangu ataimba nyimbo kama hizi shuleni au zilishapitwa na wakati!

Tuesday 13 November 2007

Kunradhi, Mheshimiwa Malecela!

Nimesoma juzi ktk gazeti Nipashe ushauri wa Mheshimiwa John Cygwiyemis Malecela kwa CCM, kuwa ibadili utaratibu wake wa kutafuta viongozi/wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa. Mhe Malecela alisema kuwa alishawahi kuongea na makamu mwenyekiti/rais wa ANC cha Afrika Kusini Ndugu Jacob Zuma juu ya utaratibu wanaoutumia na kuuona ni mzuri kuliko wa CCM. Pia Mhe Malecela amesema kuwa zipo nchi nyingi kusini mwa Afrika mfano Msumbiji (FRELIMO?) ambazo taratibu zao kutafuta viongozi zinafaa kuigwa na hazina malalamiko kutoka kwa wagombea hasa wanaoshindwa ktk chaguzi ndani ya chama.
Mawazo na ushauri huu wa Mheshimiwa Malecela aliyoyatoa huko nyumbani kwake Mvumi Mission, ktk sherehe ya kumpongeza kung'atuka umakamu m/kiti, ni mazuri na hayapaswi kufumbiwa macho na kuyazibia masikio. Yanafaa kuigwa na CCM na hata vyama vya upinzani kwani lengo ni maelewano ndani ya vyama na ushindani sawia.

Pamoja na kuridhishwa na mchango huu wa mawazo ya Mheshimiwa Malecela, bado mimi nina swali la nyongeza nalielekeza kwake.

Mhe Malecela amekuwa makamu wa mwenyekiti CCM Taifa kwa miaka 15, amekuwa ndani ya chama tangu enzi za TANU na sasa ni mjumbe wa kudumu kamati kuu ya CCM.
Hivi kweli Mheshimiwa ulishindwa kuyapeleka mapendekezo/mawazo yako ktk vikao halali vya CCM ili viyafanyie kazi?
Ni kwanini unayasema haya baada ya wewe kung'atuka na uko nje?
Kama ulijua haya mapungufu ulitumiaje nafasi yako kama makamu wa mwenyekiti wa chama (tena ngazi ya Taifa) kuyatafutia ufumbuzi.
Ulikuwa na nafasi ya kuonana na kuongea na wenyeviti wote wa CCM enzi za uongozi wako: wahesimiwa Rais wastaafu Ali Hassan Mwinyi, Benjamin W Mkapa na mhe Rais wa sasa Jakaya Kikwete, na makatibu wakuu wao Ndugu Gama, Philip Mangula na wa sasa Yusuf Makamba.
Ulikuwa na uwezo kabisa kusaidia kivitendo, je ulifanya hivyo?
Kama ulishindwa wewe, Makamu Mwenyekiti, mtu wa ngazi za juu kabisa kicheo - unamwambia nani aifanye hiyo kazi?

Monday 12 November 2007

Nguvu za Kiume

Jamani, jamani, jamani, kuna jirani yangu kafa hivi majuzi. Alikuwa ni baba wa makamu, mmarekani mweusi. Alikuwa mcheshi na ilikuwa kila tukionana lazima tusalimiane. Mara ananinunulia kahawa halafu tunakaa namsimulia kuhusu Afrika. Yule baba, alionekana mzima na mwenye afya fiti kabisa. Nilibakia kushangaa kusikia kafa na si kwa ajali. Mke wake alifariki mwaka juzi, lakini miezi ya karibuni alikuwa anaonekana mwenye furaha kwa vile alipata mpenzi, dada mwenye miaka 25 hivi.

Story niliyoskia ni hivi:
Kumbe jamaa alikuwa na matatizo ya moyo. Alifia kitandani akiwa kwenye shughuli ya kufanya tendo la ndoa na mpenzi wake. Tena wanasema alifariki mara alipofikia kilele cha tendo. Navyosikia ilikuwa ni ‘massive heart attack’. Kama ni massive bila shaka na utamu wa shughuli hakujua kuwa yuko hatarini.

Nasikia huyo mpenzi wake alipiga sana makelele majirani walipigia simu polisi 911 kwa vile walidhania wameingiliwa na majambazi. Wanasema baba wa watu kamwangukia yule dada na kafa macho wazi.Lakini bado nilikuwa nashangaa maana kama nilivyosema awali, jamaa alionekana kuwa na afya. Kumbe jamaa alikuwa mtumizi wa Viagra, yaani vile vidonge vya kuongeza uume, na kumpa mwanaume uweza wa kufanya tendo la ndoa.

Ndugu zake wanalalamika kweli, maana hakuzipata kwa prescription ya daktari, alizaiagiza kwenye mtandao (internet). Kwa kumwangalia alivyofiti nisingefikiria kuwa ana matatizo ya nguvu za kiume.

Kumbe mtazame mtu, matatizo yake anayajua mwenyewe na daktari wake.

Nikawa najiuliza kama jamaa alijua ana matatizo ya moyo, kwa nini alitumia Viagra. Maana hata tangaza kwenye TV na magazeti wanaonyo kuwa kabla ya kutumia. Halafu pia wanaonya kuwa mwanaume anaweza kupofuka kama anatumia. Lakini wanaume bado wanazitumia!

Na siku hizi dawa za kuongeza nguvu za kiume ziko nyingi kuna Ciallis, Levitra, Yohimbine na mengine. Hizo dawa zina side effects kama kuumwa kichwa, kuharisha, pua kuziba, macho mekundu, tumbo kuumwa na mengine mengi. Pamoja na side effects bado zina soko kubwa. Na zikipigwa marufuku nina amini kuwa watu watatajirika kwa kuzifanyia magendo.

Kwa kweli wanaume wako tayari kufa kama wakishindwa kufanya tendo la ndoa. Nashindwa kuelewa sababu. Yaani tendo la ndoa ni tamu kiasi hicho au wanahofia kuwa kwa vile hawa-‘function’ tena ndo basi si wanaume? Mtu anakuwa tayari kuhatarisha maisha yake kwa ajili ya kufanya tendo la ndoa.

Mwanaume anaambiwa anaweza kupofuka akitumia hiyo dawa lakini bado yuko tayari kuchukua risk. Halafu mwanaume akiitwa ‘hanithi’ yuko tayari kupigana au kuua. Sijui bila kusimamisha anajiona si mtu tena…sielewi kabisa! Nikawa najadiili na marafiki zangu juzi na tulikubaliana kuwa wanaume wako tayari kuchukua ‘risks’ kuliko wanawake.

Yaani mwanaume anaweza kufanya tendo la ndoa hata akijua kuwa kuna hatari ya mwenzake kuwa na ugonjwa wa zinaa na ataambukizwa. Bongo, walikuwa wanasema eti, ‘Ajali Kazini’! Hiyo ajali inaweza kukuua! Sijui hiyo ume ikisimama ndo basi tena, akili zote zinahamia hapo.

Nauliza tena, tendo la ndoa ni tamu kiasi kwamba mko tayari kuhatarisha maisha yenu?

Kukosa nguvu za kiume zi mwisho wa dunia jamani. Bado tunawahitaji!Lakini nikirudi kwa marehemu jirani yangu, uwongo mbaya, alikuwa anatabasamu ndani ya jeneza lake!

NB:
Nyie wanaume mnaotaka kutumia hizo dawa kawaone daktari wenu kabla ya kuanza kuzitumia.


Kutoka: Chemi Che-Mponda Blog

rushwa ya ngono

Yapo makundi matatu ya ngono:
Ngono-hiarishwa, Ngono Hiyarishwa-Haramu na Ngono Haramu

Ngono-'Hiyari'shwa
Aina ya kwanza ya ngono hiarishwa ni ile ambayo ime'hiyari'shwa kidini, kimila au kisheria na wajamianaji wahusika wote wawili wanakubaliana.

Ngono 'Hiyari'shwa-Haramu
Aina ya kwanza ya ngono `'hiyari'shwa haramu` ni ile ambayo mjamiiaji mmoja (hasa wa kiume) anahiyarisha na mwingine (hasa wa kike) anakataa na kushurutishwa.

Ngono ya namna hii inatokea wakati wazazi wakitaka binti aolewe hata kama ni kinyume cha mapenzi ya huyo binti, kwa sababu mila inaruhusu na pia kuna manufaa wanayoyataka.
Aina hii ya ngono inamaanisha kwamba wazazi wanamshurutisha binti kwa sababu mila inaruhusu na kwa sababu wana manufaa ya kiuchumi.
Hii ina madhara ya kimaumbile na kihisia kwa binti anayehusika, na inapingana na mitazamo ya kisasa, haki za binaadamu na pengine sheria zinazopitishwa, hasa kwa sababu inawahusu mabinti ambao wanapaswa wawe masomoni badala ya kuozwa.
Ngono ya aina hii itaendelea kuleta utata, kwa sababu imo ukingoni mwa ngono 'hiyari'shwa na ngono haramu, kwa sababu kwa upande mmoja ime'hiyari'shwa na mila (kusudi kumnufaisha mzazi) lakini ni haramu kwa yule mshurutishwa kwa sababu anachukuliwa mateka.
Aina ya pili ya Ngono-'Hiyarishwa'-Haramu ni ngono ya shinikizo ambapo mjamiiaji mmoja (hasa wa kiume) anamshinikiza mjamiaji mwingine (hasa wa kike), kwa manufaa ya kuridhisha hisia na hamu zake huku yule mshurutishwa anaye'hiyari'sha ngono hiyo naye ana manufaa ya kibiashara.
Hii ndiyo inayoitwa -ngono ya rushwa-, kwa sababu kama ni kazi haajiriwi kazi hiyo kwa sababu ametimiza masharti ya ajira hiyo, lakini kwa sababu njia ya mkato imetumika.

Ngono-Haramu:
Ngono haramu ni ile ambayo mshurutishwa hahiari, wala haikubaliki kijamii, kibinafsi kisheria, kitamaduni wala kidini. Hii hupewa majina kama vile kubaka, kunajisi, na kadhalika.

By Anti Flora Wingia, 11 Nov 2007
Email: fwingia@yahoo.com

* SOURCE: Nipashe

Man Utd 2 Blackburn Rovers 0

Manchester United beat Blackburn Rovers 2-0 yesterday to go top of the Premier League table, with both goals coming in a space of two minutes by Cristiano Ronaldo.
Now Arsenal have to beat Reading today by a margin of 2 goals to regain top spot!

Man United line-up v. Blackburn Rovers:

Van der Sar

Brown
Ferdinand
Vidic
Evra

Hargreaves
Ronaldo
Anderson
Giggs

Saha
Tevez

Substitutes:
Carrick for Hargreaves
Nani for Saha

MAN UNITED (EVERY GOAL)!
Saha-Prem:1+1=2
Scholes-Prem:1+ =1
Nani-Prem:1+1 Cham Lg: =2
Vidic-Prem:1+1 =2
Ronaldo-Prem:1+2+1+2 Champ Lg:1+2+1 =10
Tevez-Prem:1+1+2 Cham Lg:1 =5
Rooney-Prem:1+2+1 Champ Lg:1+1+1 =7
Giggs-Pre:1+ Champ Lge: =1
Ferdinand:Prem:1+ Champ Lg:1+ =2
Gerard Pique- Prem: Champ Lg:1 =1

Saturday 10 November 2007

Ajali ya FOKKA la MUSS Novemba 1986!

Miaka 21 iliyopita Shule ya Sekondari Musoma (MUSS) maarufu kama Alliance ilipata pigo kubwa ktk historia yake chini ya Mkuu wa Shule Nashon 'Otuolo' Otieno.

Gari la shule ambalo wanafunzi walilibatiza jina la FOKKER (Isuzu Tipper tani 7) likiwa njiani toka Shule ya Ualimu Bweri, Manispaa ya Musoma, ilipata ajali ktk kona jirani na machinjioni. Katika ajali hiyo wanafunzi kadhaa walipoteza maisha yao (ingawa sikumbuki idadi yao kwa uhakika ila ni kati ya 8 na 10 hivi!) mojawapo ni classmate wangu Ezekiel, wa kidato cha tatu na Ali Mussa wa kidato cha nne.

Tarehe 26/11/1986 ilikuwa siku ya majonzi makubwa kutokana na mkasa huo. Timu ya mpira wa miguu ya Shule ilialikwa kucheza mechi ya kirafiki na wenzao wa Chuo cha Bweri. Katika msafara huo wa Bweri nami ilikuwa niwemo. Mimi pamoja na rafiki yangu Amon Herman Kafugugu wa kidato cha IV (arts) tulikuwepo na tulipania kupanda FOKKA la shule ili kwenda kushuhudia mpambano kama waandishi wa habari. Mimi nilikuwa naandika habari za kidato changu hasa ktk Ligi za madarasa na yeye hivyo hivyo kwa upande wake. Lakini siku hiyo tulitaka kwenda kwa ku-cover habari ya pamoja.

Lakini kutokana na wingi wa wanafunzi ndani ya gari (washangiliaji na wachezaji)
nafasi haikuwa inatosha kwa wote waliokuwepo kuondoka kwa FOKKA. Ilibidi mwalimu wa michezo Ndugu Maningu apunguze idadi. Mimi na Kafugugu ni miongoni mwa waliopunguzwa na hivyo hatukuondoka. Wapo walioenda kwa miguu maana pale na Bweri sio mbali na wakati wa kurudi walidandia gari.

Jioni ile wakati wa kurejea shuleni ktk kona, huenda kutokana na mwendo wa kasi FOKKA ilipiduka na kuua hapo hapo. Habari za ajali zilipofika shuleni, wanafunzi karibia wote tulikimbia kuelekea eneo la ajali. Tulipofika pale tulianza kutoa msaada pale tulipoweza na kusimamisha baadhi ya magari ili kutoa msaada wa usafiri hadi hospitali ya mkoa. Kwa kweli barabara ilifungika kwa muda ktk kipindi chote cha kuhudumia majeruhi na kuwanasua majeruhi na waliopoteza maisha, maana wengine walikuwa wamebanwa na vyuma vya gari!

Mwanafunzi mwingine aliuwawa ktk ajali ya pili (ajali ndani ya ajali). Lori moja likitokea Bweri, wakati giza lilishaanza, lilipita katikati ya wanafunzi waliokuwa wamezunguka eneo la ajali bila tahadhali wala kupunguza mwendo; na lilitokomea bila kusimama. Rafiki yangu Kafugugu nae alinusurika ajali ya pili ingawa alikanyagwa mguu (foot) ambao aliuuguza (jeraha) kwa zaidi ya mwezi hospitalini!

Ukumbi wa MUBIG ulitumika katika kutoa salaam za mwisho kwa marehemu.

Mwanakwaya wa Shule na class-mate wangu (mkondo tofauti) Raphael Jowel alitunga nyimbo mbili ktk kuomboleza vifo vya wenzetu. Kwa bahati mbaya nimeshasahau baadhi ya mistari ktk wimbo mmoja lakini nakumbuka maneno machache sana ...

'(Ilikuwa) Ilikuwa tarehe ishirini na sita mwezi wa Novemba, themanini na sita,
....
Chorus:
(watu wengi walisikitikaaaaa jamaniiii, kusikia FOKKA imepindukaaa ...)
.....'

Ingawa majina yao yamenitoka lakini bado nawakumbuka wanafunzi wenzangu waliopoteza maisha yao ktk umri mdogo sana. Natoa pole kwa wote walioguswa ktk ajali na misiba hasa ndugu na marafiki wa marehemu.

The Cabinet, The United Rep of Tanzania

President and Commander -in- Chief of the Armed Forces of the United Republic of Tanzania
H.E Jakaya Mrisho Kikwete

Vice - President
H.E Dr. Ali Mohamed Shein

President of Zanzibar
H.E Amani Abeid Amani Karume

Prime Minister of the United Republic of Tanzania
Rt.Hon. Edward Ngoyai Lowassa

Ministers of State in the President's Office

Public Service Management
Hon. Hawa Abdulrahman Ghasia

Good Governance
Hon. Philip Sang’ka Marmo

Political Affairs and Civil Societies Relations
Hon. Kingunge Ngombale Mwiru

Ministers of State in the Vice President's Office

Union Affairs
Hon. Dr. Hussein Ali Mwinyi

Environment
Hon. Prof. Mark James Mwandosya

Ministers of State in the Prime Minister's Office
Regional Administration and Local Government
Hon. Mizengo Kayanza Peter Pinda

Parliamentary Affairs
Hon. Dr. Batilda Salha Burian

Minister for Foreign Affairs and International Co-operation
Hon. Bernard Kamillius Membe

Minister for East African Co-operation
Hon. Dr. Ibrahim Said Msabaha

Minister for Finance
Hon. Zakia Hamdani Meghji

Minister for Planning, Economy and Empowerment
Hon. Dr. Juma Alifa Ngasongwa

Minister for Industry, Trade and Marketing
Hon. Basil Pesambili Mramba

Minister for Agriculture, Food Security and Co-operatives
Hon. Stephen Masatu Wassira

Minister for Natural Resources and Tourism
Hon. Prof. Jumanne Abdallah Maghembe

Minister for Water
Hon. Dr. Shukuru Jumanne Kawambwa

Minister for Energy and Minerals
Hon. Nazir Mustafa Karamagi

Minister for Infrastructure Development
Hon. Andrew John Chenge

Minister for Health and Social Welfare
Hon. Prof. David Homeli Mwakyusa

Minister for Education and Vocational Training
Hon. Margareth Simwanza Sitta

Minister for Higher Education, Science and Technology
Hon. Prof. Peter Mahmoud Msolla

Minister for Labour, Employment and Youth Development
Hon. Capt. John Zefania Chiligati

Minister for Lands, Housing and Human Settlements Development
Ho. John Pombe Joseph Magufuli

Minister for Information, Culture, and Sports
Hon. Muhammed Seif Khatib

Minister for Defence and National Service
Hon. Prof. Juma Athumani Kapuya

Minister for Public Safety and Security
Hon. Harith Bakari Mwapachu .

Minister for Home Affairs
Hon. Joseph James Mungai

Minister for Justice and Constitutional Affairs
Hon. Dr. Mary Michael Nagu

Minister for Community Development, Gender and Children
Hon. Sofia Mnyambi Simba

Minister for Livestock Development
Hon. Anthony Mwandu Diallo


DEPUTY MINISTERS AND THEIR RESPECTIVE MINISTRIES

Prime Minister’s Office

Disaster and HIV/AIDS
Hon. Dr. Luka Jelas Siyame

Regional Administration and Local Government
Hon. Celina Ompeshi Kombani

Foreign Affairs and International Co-operation
Hon. Seif Ali Iddi
Hon . Dr. Cyril August Chami

East African Co-operation
Hon. Dr. Diodorus Buberwa Kamala

Finance
Hon. Abdisalaam Issa Khatib


Hon. Mustafa Haidi Mkulo

Planning, Economy and Empowerment
Hon. Gaudence Kayombo

Industry, Trade and Marketing
Hon. Hezekiah Ndahani Chibulunje

Agriculture, Food Security and Co-operatives
Hon. Christopher Kajoro Chizza
Dr. David Mathayo David

Energy and Minerals
Hon. William Ngeleje

Infrastructure Development
Hon. Dr. Maua Abeid Daftari
Hon. Dr. Milton Makongoro Mahanga

Health and Social Welfare
Hon. Dr. Aisha Omar Kigoda

Education and Vocational Training
Hon. Mwantumu Bakari Mahiza
Hon. Ludovick John Mwananzila

Higher Education, Science and Technology
Hon. Gaudensia Mugosi Kabaka

Labour, Employment, and Youth Development
Hon . Jeremia Solomon Sumari
Hon. Dr. Emmanuel John Nchimbi

Lands, Housing and Human Settlements Development
Hon.Rita Louise Mlaki

Community Development, Gender and Children
- VACANT AFTER THE DEATH OF SALOME MBATIA, MP SPECIAL SEATS

Public Safety and Security
Hon. Mohamed Aboud

Home Affairs
Hon. Lawrence Kego Masha

Livestock Development
Hon. Dr. Charles Ogessa Mlingwa

Natural Resources and Tourism
Hon. Zabein Muhaji Mhita

Information, Culture and Sports
Hon. Daniel Nicodem Nsanzungwako
Hon. Joel Nkaya Bendera

Justice and Constitutional Affairs
Hon. Mathias Meinrad Chikawe

Defence and National Service
Hon. Omar Yussuf Mzee

Thursday 8 November 2007

Man United 4 Dynamo Kiev 0

Manchester United yesterday defeated Dynamo Kiev 4-0 in a group F UEFA Champions League encounter to go through to knockout stage (last 16) scheduled for late February 2008.
Young United trio - Gerard Pique, Danny Simpson and late on Jonny Evans - helped United to keep clean sheet, with four goals coming from Pique 31min., Carlos Tevez 37', Wayne Rooney 76' and on fire Cristiano Ronaldo on 88th minute.
Mancchester United now tops Group F table with maximum points (12) with two games remaining.
Final two games for United are in November 27 (Tuesday) against Sporting Lisbon at Old Trafford and an away tie against Roma on Wednesday, 12th December, 2007. Both games kicks of at 19:45 GMT.

Man United Line-Up against Dynamo Kiev:

Van der sar,

Simpson,
Pique,
Vidic,
Evra,

Carrick,
Ronaldo,
Fletcher,
Nani,

Tevez,
Rooney

Substitutes:
Kuszacz for Van der sar 45',
J Evans for Pique,
Saha for Tevez.

Tuesday 6 November 2007

CCM Taifa: Ni KKM*

Mkutano Mkuu wa CCM wa Nane umemchagua kwa kishindo Mwenyekiti wa chama hicho, Rais Jakaya Kikwete na Makamu wake wawili kutoka Tanzania bara na visiwani.

Matokeo:
Mwenyekiti Taifa, Rais Kikwete aliibuka kwa
kura za NDIYO: 1,887 (99.73%) kati ya kura 1,892 zilizopigwa.
Kura za HAPANA: 5
Hakuna kura hata moja iliyoharibika.

Makamu Mwenyekiti Tanzania Visiwani, Rais Amani Abeid Karume,
kura za NDIYO 1,886 (99.68%)
kura za HAPANA 1

Kwa upande wa Makamu Mwenyekiti Tanzania Bara, Bw. Pius Msekwa
kura za NDIYO 1,879 (99.78%)
kura za HAPANA 5

* KKM ni kifupi cha Kikwete, Karume na Msekwa

Katibu Mkuu CCM ni Lt. Kanali mstaafu Yusuf Makamba

Na Mosonga

Matokeo: Waliogombea NEC-CCM, 2007

Leo napitia orodha ya walioomba ujumbe wa Halmashauri Kuu Ya CCM Taifa ili kuona kama wamefanikiwa. Orodha ya wagombea ilitolewa 03/8/2007. Tayari Mkutano Mkuu wa kawaida wa CCM umeshafanyika na orodha ya washindi imepatikana!
Na Mosonga

03 Aug 2007
Chama Cha Mapinduzi (CCM), jana kilitoa hadharani majina ya wanachama wake watakaogombea ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) kupitia makundi mbalimbali.

A) Tanzania Bara Viti 20:

Waziri Mkuu,
Bw. Edward Lowassa - AMESHINDA

Bi. Shy-Rose Bhanji -AMEKOSA

Waziri wa Ulinzi,
Profesa Juma Kapuya - AMESHINDA

Naibu Waziri wa Miundombinu
Dk. Milton Makongoro Mahanga -AMESHINDA

Katibu Mkuu wa CCM,
Bw. Yussuf Makamba -AMESHINDA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,
Bw. Bernard Membe -AMESHINDA

Naibu Waziri wa Nishati na Madini
Bw. William Ngeleje,

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Siasa)
Bw. Kingunge Ngombale Mwiru - AMESHINDA

Waziri Mkuu Mstaafu
Bw. Frederick Sumaye -AMESHINDA

Bw. Wilson Masilingi,
Bw. Filbert Bayi,
Bw. Abrahaman Kinana -AMESHINDA

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma
Bw. William Lukuvi

Bw. Jaka Mwambi -AMESHINDA

Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mshariki
Bw. Deodarus Kamala -

Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na ushirika
Bw. David Mathayo -

Bw. Aggrey Mwanri -AMESHINDA
Bw. Isidore Shirima -
Bw. Enock Chambili -
Bw. Christopher Gachuma -AMESHINDA

Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii
Profesa David Mwakyusa -AMESHINDA

Profesa Samwel Wangwe -AMESHINDA

Waziri wa Miundombinu
Bw. Andrew Chenge -AMESHINDA

Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana
Bw. Capt. John Chiligati -AMESHINDA

Brigedia Jenerali Hassan Ngwilizi -
Kapteni John Komba -AMESHINDA

Bw. Novatus Makunga -
Bw. Tarimba Abbas -
Bw. Lucas Kisasa -AMEKOSA
Bw. Job Ndugai -
Bw. George Simba Chawene -
Bw. Abdul Sapi -
Bw. Uhahula -
Bw. David Holela -

Waziri wa Kilimo na Ushirika,
Bw. Stephen Wassira -AMESHINDA

Bw. Emmanuel Mwambulukutu,
Bw. Amos Makalla -AMESHINDA
Bw. Jackson Msomi (Msome?) -AMESHINDA
Dr. James Msekela,
Bw. Mohamed Mkumba,
Prof Idris Mtulia,
Bw. Pascal Mabiti,
Bw. Said Fundikira,
Bw. Abeid Mwinyimusa,
Bw. Charles Kagonji na
Dk. Ibrahim Msengi.

B) Zanzibar:

Dk. Ali Mohamed Shein -AMESHINDA

Waziri Kiongozi,
Bw. Shamsi Vuai Nahodha -AMESHINDA
Dk. Hussein Mwinyi -AMESHINDA
Dk. Gharib Bilal -AMESHINDA
Bw. Mohamed Seif Khatibu -AMESHINDA
Bi. Samia Suluh Hassan -AMESHINDA
Bi. Kidawa Hamid Saleh -AMESHINDA
Bw. Salim Msabah -AMESHINDA
Bi. Khajida Aboud -AMESHINDA
Bw. Mansour Yusuf -AMESHINDA
Bw. Mohamed Nassor Moyo -AMESHINDA
Bw. Makame Mnyae -AMESHINDA
Bi. Moudeleine Castico -AMESHINDA
Bw. Twaiba Kisaso -AMESHINDA
Bi. Ishao Abdallah Ussu -AMESHINDA
Bw. Vuai Ali Vuai -AMESHINDA
Bw. Omary Yusuf Mzee -AMESHINDA
Bw. Adam Mwakanjuki -AMESHINDA

C) Wanawake Zanzibar:
Bi. Mwajuma Abdallah Majid -AMESHINDA
Bi. Fatma Said Ali -AMESHINDA
Bi. Fatma Aloo -AMESHINDA
Bi. Amina Idi Mabrouk -AMESHINDA
Bi. Catherine Nao -AMESHINDA
Bi. Asha Abdallah Juma -AMESHINDA
Bi. Asha Bakari Makame -AMESHINDA

Baadhi ya wanaogombea ujumbe wa NEC kupitia Vijana Bara ni
Bi. Zainabu Kawawa -AMEPATA
Bw. Nape Nnaunye -AMEPATA
Bw. Deogratias Ndejembi -
Bw. Paul Kirigiri -
Bw. Maghembe Maghembe -
Bi. Violet Mzindakaya -AMESHINDA
Bi. Lucy Mayenga -AMEPATA
(majina yafuatayo sikuyaona August 2007)
Bi. Jerry Slaa -AMESHINDA
Bw. Salim M. Ali -AMESHINDA
Bw. Suleiman Mchabi -AMESHINDA
Bw. Beno Malisa -AMSHINDA
Bw. Edwin Sannda -AMESHIDA (hongera 'mate' - uclas!)

Vijana (UVCCM) Zanzibar:
Bi. Hawa Sukwa Saidi -AMESHINDA
Bw. Hamad Yusuf -AMESHINDA
Bi. Adika Vuai -AMESHINDA
Marco Charles Bundara -AMESHINDA
Ashura Abdallah Ismail -AMESHINDA
Suleiman M. Haji -AMESHINDA

Ujumbe NEC Wazazi Tanzania Bara baadhi ya majina mashuhuri ni yafuatayo:
Bw. Enock Kalumuna,
Bw. Salim Tambalizeni,
Bw. Richard Hizza Tambwe - AMEKOSA
Bw. Mustapha Yakub,
Bw. Mussa Hassan Zungu -AMESHINDA
Bw. Ruth Msafiri, .....(bwana au bi?)
Bw. Thomas Ngawaiya - AMEKOSA
Bw. Henry Shekifu,
Bw. Richarch Nyaulawa -AMESHINDA
Bw. Danhi Makanga - AMEKOSA
Bw. Dickels Shindika,
Dr. Zainabu Gama -AMESHINDA
Bw. Adam Kighoma Malima -AMESHINDA
Bw. Stella Manyanya -AMESHINDA
Bw. Athumani Mfutakamba -
(hili jina sikuliona Augosti 2007)
Bw. Mohamed Nondo -AMESHINDA

Wazazi Zanzibar:
Dogo Mabrouk -AMESHINDA
Hassan Rajab Khatibu -AMESHINDA
Fatma A. Haji -AMESHINDA
Mtumwa Pea -AMESHINDA

D) Wanawake (UWT) Bara:
Bi. Halima Mamuya -AMEKOSA
Bi. Sifa Swai -
Bi. Asha Baraka -AMEPATA
Bi. Khadija Kopa -AMEPATA
Bi. Jacqueline Liana -AMEKOSA
Bi. Anne Makinda -AMEPATA
Bi. Jane Mihanji -AMEKOSA
Bi. Fatuma Adam Mkwawa,
Bi. Rita Mlaki -AMEKOSA
Bi. Sofia Simba -AMEPATA
Bi. Margaret Sitta -AMEPATA
Bi. Kate Kamba -AMEPATA
Bi. Shamsa Mwangunga -AMEPATA
Bi. Anne Kilango Malecela -AMEPATA
Bi. Salome Mbatia -AMEFARIKI DUNIA
Bi. Zakia Meghji -AMEPATA
Dr. Rehema Nchimbi -AMEPATA
Bi. Halima Kihemba -AMEKOSA
Bi. Margaret Mkanga,
Bi. Lydia Boma,
Bi. Esther Nyawazwa,
Bi. Zainab Vullu ,
Bi. Esha Stima -AMEKOSA
Bi. Diana Chilolo -AMEPATA
Bi. Tatu Ntimizi -AMEKOSA
Dr. Aisha Kigoda -AMEPATA
Bi. Mwantumu Mahiza -
Bi. Beatrice Shelukindo -AMEKOSA
Bi. Pili Chana -AMEPATA (nimeliona leo, awali sikuliona hili jina!!)

Taarifa hiyo inaonyesha kwamba wana-CCM
60 wameteuliwa kuwania nafasi ya ujumbe wa NEC Taifa kwa upande wa Tanzania Visiwani,
18 kupitia UVCCM,
12 kupitia Wazazi na
21 kupitia UWT.

Wana-CCM kadhaa wameamua kutangaza rasmi kung’atuka katika uongozi wa chama. Waliochukua hatua hiyo ni:-
Dk. Chrisant Mzindakaya,
Bi. Maria Watondoha,
Balozi Isaack Sepetu,
Bw. Daniel Ole Njoolay,
Bw. Charles Keenja,
Profesa Philemon Sarungi,
Bw. Stephen Mashishanga,
Bw. Paul Kimiti,
Bi. Asha Makwega na
Bi. Shamim Khan.
Bw. Pancras Ndejembi (M/Kiti mkoa, Dodoma).


Kamati ya usimamizi wa uchaguzi CCM:
1. Spika Sitta -M/Kiti
2. Makamu wake Anna Makinda (?)
3. Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar,
Bw. Pandu Ameir Kificho,
4. Dk. Maua Daftari,
5. Dk. Mary Nagu,
6. Dk. Batilda Burian,
7. Bw. Rostam Azizi na
8. Bw. Emmanuel Nchimbi.

Halmashauri Kuu inakutana leo, 06/11/2007, kuteua Kamati Kuu ya CCM na secterarieti na jina la Katibu Mkuu wa CCM.


HABARI ZAIDI (KUTOKA KWA ISSAMICHUZI BLOG)
MANAIBU mawaziri watano, wakuu wa wilaya na viongozikadhaa wa zamani wa chama na serikali na wanasiasawatatu wa upinzani waliohamia Chama Cha Mapinduzi(CCM) hivi karibuni, ni miongoni mwa walioshindwakatika uchaguzi wa ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifaya chama hicho (NEC).

Wakati wanasiasa hao wakishindwa kuingia ndani yaNEC, watendaji wakuu wa chama hicho akiwamo KatibuMkuu, Yussuf Makamba na mawaziri kadhaa wakiongozwa naWaziri Mkuu Edward Lowassa, walishinda uchaguzi huouliofanyika juzi wakati wa Mkutano Mkuu wa Taifa waNane wa CCM uliomalizika jana alasiri kwenye Ukumbi wa Kizota hapa.

Manaibu mawaziri wa Serikali ya Awamu ya Nnewalioshindwa ni Rita Mlaki (Ardhi, Nyumba na Maendeleoya Makazi) na Mwantumu Mahiza (Elimu na Mafunzo yaUfundi) walioshindwa kwa kundi la viti 13 WanawakeBara.

Wengine ni Dk. Diodorus Kamala (Ushirikiano waAfrika Mashariki), Dk. David Mathayo (Chakula,Ushirikana Masoko) na William Ngeleja (Nishati na Madini)walioshindwa kupitia kundi la viti 20 Tanzania Bara.

Katika uchaguzi huo, walioanguka wengine waliopitia katika kundi la Wanawake Bara ni aliyewahi kuwa Waziri katika Serikali ya Awamu ya Tatu, Tatu Ntimizi, Katibu Mkuu wa zamani wa UWT, Halima Mamuya, wakuu wa wilaya;Halima Kihemba, Chiku Galawa, Fatma Kimario, Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Mrisho, wabunge; EstherNyawazwa, Zainab Vullu, Margaret Mkanga, BeatriceShelukindo na wanahabari Jacqueline Liana na Jane Mihanji, wote wa Uhuru/Mzalendo.

Walioshinda na kura zao katika mabano ni MargaretSitta (1,780), Zakia Meghji (1,207), Pindi Chana(1,203), Anne Makinda (1,146), Diana Chilolo (1,105),Dk. Aisha Kigoda (1,060), Anne Kilango-Malecela (983),Dk. Rehema Nchimbi (887), Shamsa Mwangunga (850),Khadija Kopa (842), Asha Baraka (766), Kate Kamba(706) na Sophia Simba (689).

Katika kundi la Tanzania Bara, mbali na akina Dk.Mathayo, Dk. Kamala na Ngeleja, wengine waliotupwa nje ni wakuu wa mikoa; Dk. James Msekela, Isdori Shirima, Abeid Mwinyimsa, wakuu wa wilaya; Pascal Mabiti, Frank Uhaula, David Holela, Dk. Ibrahim Msengi, waandishi wa habari Lucas Kisasa, Shy-RoseBhanji na Novatus Makunga.

Wengine ni Balozi Emmanuel Mwambulukutu, mawaziri wa zamani Wilson Masilingi, Hassan Ngwilizi, Mwenyekiti wa zamani wa Mkoa wa Mara, Enock Chambiri, Katibu Mkuu wa TOC, Filbert Bayi na wabunge; Profesa Idrisa Mtulia na Job Ndugai na mfanyabiashara wa Dar es Salaam, Salim Hamis Salim ‘Chicago’.

Katika kundi hilo la ‘kifo’, waliopenya ni Waziri Mkuu, Edward Lowassa aliyeongoza kwa kura 1,681, Andrew Chenge (1,530), Yussuf Makamba (1,510), Bernard Membe (1,281), Jaka Mwambi (1,239), Profesa Juma Kapuya (1,216), Abdulrahman Kinana (1,204),Christopher Gachuma (1,181), Stephen Wassira (1,107),Aggrey Mwanri (1,068), Milton Mahanga (1,067),Frederick Sumaye (1,065).

Pia wamo John Komba (1,056), Kingunge Ngombale-Mwiru(1,023), John Chiligati (910), Amos Makalla (871),Profesa Samuel Wangwe (817), Profesa David Mwakyusa(754) na Jackson Msome (747).

Wanasiasa waliojiunga na CCM kutoka vyama vyaupinzani; Richard Tambwe Hizza na Thomas Ngawaiya walikwama baada ya kushindwa katika Kundi la Wazazi Bara, huku kiongozi mwingine wa zamani wa upinzani,Salum Msabah Mbarouk akishinda kwa upande wa viti 20 kundi la Tanzania Visiwani.

Mbali na Tambwe na Ngawaiya, wengine walioshindwa kwa Wazazi ni mshairi maarufu Salim Tambalizeni, wakuu wawilaya; Danhi Makanga, Athuman Mfutakamba, Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Henry Shekifu, mbunge Ruth Msafiri(Muleba Kaskazini).

Walioshinda ni Stella Manyanya (948), Zainab Gama(818), Mussa Azzan Zungu (730), Adam Kighoma Malima(698), Mohammed Nondo (679) na Richard Nyaulawa (669).

Kwa upande wa Zanzibar kundi hilo la Wazazi, washindini Dogo Iddi Mbarouk, Fatma Abeid Haji, Mtumwa YussufPeya na Hassa Rajab Khatib.

Walioshinda kwa upande wa Umoja wa Vijana Kundi la Bara ni Zainab Kawawa (1,390), Violet Mzindakaya Mpogolo (1,165), Nape Nnauye (1,056), Jerry Silaa(994), Sarah Ally (935), Beno Malisa (857), EdwinSanda (804) na Lucy Mayenga (770).

Miongoni mwa walioshindwa katika kundi hilo ni mgombea Penias Kaindoa ambaye wakati akiomba kura,aliwasihi wajumbe wamnusuru ili asiwe mkimbizi kwenye nchi yake, akitokea katika Jimbo la Bukoba Mjini lenye upinzani mkali na Chama cha Wananchi (CUF), akidai akirudi bila kuchaguliwa, atakuwa katika wakati mgumu.

Washindi kwa upande wa Vijana Zanzibar ni Hawa SukwaSaidi (930), Hamad Masauni Yussuf (894), Adila HilalVuai (886), Michael Charles Bundala (845), AshuraAbdallah Ismail (808) na Suleiman Muhsin Haji (771).

Washindi kwa upande wa Tanzania Visiwani ni Dk. AliMohamed Shein (1,663), Shamsi Vuai Nahodha (1,525), Dk. Hussein Ali Mwinyi (1,496), Dk. Mohammed GharibBilal (1,366), Saleh Ramadhan Ferouz (1,352), Muhammed Seif Khatib (1,346), Samia Suluhu Hassan (1,281),Kidawa Hamid Saleh (1,212), Msabah (1,151), Khadija Hassan Aboud (1,076), Mansour Yussuf Himid (1,073),Omar Yussuf Mzee (1,022), Balozi Seif Ali Iddi (997),Mohamed Hassan Nassoro Moyo (959), Profesa Makame Mnyaa Mbarawa (958), Maudline Cyrus Castico (950),Vuai Ali Vuai (943), Brigedia Jenerali Adam Mwakanjuki(936), Thuwayban Edington Kissasi (860) na Dk. Ishau Abdula Khamis (840).

Kwa mujibu wa msimamizi wa uchaguzi huo, Spika wa Bunge, Samuel Sitta, kwa upande wa uchaguzi wa Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Pius Msekwa alipata kura za Ndiyo 1,879, na kura tano za Hapana, kati ya kura halali 1,887, huku kura moja ikiharibika na ushindi wake ni sawa na asilimia 99.78.

Sitta alisema kwa upande wa Makamu Mwenyekiti TanzaniaZanzibar, Rais Amani Abeid Karume alishinda kwa kupatakura 1,886 za Ndiyo, kati ya kura 1,887. Kura moja ilimkataa na ushindi wake ni sawa na asilimia 99.94.

Rais Jakaya Kikwete ambaye tangu Juni 25, mwaka jana alikabidhiwa mikoba ya uenyekiti wa CCM na Rais mstaafu Benjamin Mkapa, jana alikabidhiwa rasmi kipindi chake cha kwanza kwa kuchaguliwa kwa kura za Ndiyo 1,887, kati ya kura halali 1,892, kura tanozi kimkataa na hivyo ushindi wake ni sawa na asilimia 99.73.

Mwenyekiti huyo mpya wa CCM alitangaza kuwa leo Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho itakutana kwamara ya kwanza na kisha kuteua Kamati Kuu na kuundwakwa Sekretarieti mpya itakayoiongoza CCM kwa miakamitano hadi mwaka 2012.

Kumalizika kwa Mkutano Mkuu wa Taifa wa Nane wa CCMjana kulihitimisha mchakato wa uchaguzi ndani ya chamahicho ulioanza Januari mwaka huu kuanzia ngazi ya Shina.

Sir Alex celebrates 21 years at United

Sir Alex Ferguson today has celebrated his 21st season at Manchester United.
Though it is the happy day for him, he has had difficult moments in some parts of his life at Old Trafford. How hard was it? Yes, according to him, he had to let some of his important players in the United family leave for other clubs.
Although he mentioned Nicky Butt and Phil Neville as some of the hardest decisions he made in the past to let them go, but in the list, I would like to add such names like Ruud van Nistelrooy, David Beckham, Roy Keane, Jaap Stam to mention only few! These players really left United in a difficult time to find their replacements.
However, Sir Alex said, 'I always have to put that hat on when it comes to making those business decisions'.

By Mosonga

Monday 5 November 2007

Arsenal 2 Man Utd 2

The results gives United a slight edge over Arsenal as the game was an away one (for United). Both United goals were superbly created and well taken - a textbook material; compared to the opposition's.
United has played more tougher games than Arsenal, yet have same number of points and goal difference as Arsenal!

Man United Line-up:
Van de Sar, Brown, Ferdinand, Vidic, Evra, Hargreaves, Anderson, Ronaldo, Teves, Rooney, Giggs.
Subs used: Oshea for Brown, Carrick for Anderson, Saha for Teves

Did you hear Gallas admitting (in a post match interview, ss1) how tougher and better Man United were on Saturday? He was on the pitch sweating for over 90 minutes; how abaout you (Arsenal fan(s)) who were only sitting on the sofa watching?
I think you know now that Man United is above you footballwise!
Expect more from Manchester United as there is plenty from the lockers yet to come! The Premiership will be won in style, again, this season!
By Mosonga

Man United: Fixtures & Results 2007/08

August 2007
12 August 2007 Reading H k.o.1600BST Draw 0 - 0
15 August 2007 Portsmouth A KO19:45BST Draw 1-1, Scholes
19 August 2007 Man City A KO13:30BST Lost 0-1
26 August 2007 Tottenham H KO16:00BST Win 1-0, Nani

September 2007
01 September 2007 Sunderland H k.o. 17:15 W 1-0, Saha
15 September 2007 Everton A KO12:00 BST W 1-0, Vidic 83'
19 September2007 Sporting Lisbon A KO19:45BST W 1-0, Ronaldo 62'
23 September2007 Chelsea H KO1600BST W 2-0, Tevez 45', Saha 89'
26 September2007 Coventry City H KO20:00BST L 0-2
29 September2007 Birmingham A KO17:15BST W 1-0 Ronaldo 51'

October 2007
02 Oct UEFA Champions League United Vs Roma H KO19:45BST W 1-0, Rooney 51' (itv 1)
06 Oct Prem Vs Wigan 12:45 H W 4-0, Tevez 54' Ronaldo 59'&76', Rooney 82'
20 Oct Prem Vs A Villa 17:15 A W 4-1, Rooney (36, 44), Ferdinand (45), Giggs (75)
23 Oct UEFA Champ Lg Vs Dynamo Kiev 19:45 A W 4-2 Ferdinand,Rooney, Ronaldo(2)
27 Oct Prem League United Vs Middlsbro 15:00 H W 4-1 Nani, Rooney, Tevez (2)

November 2007
03 Nov Vs Arsenal A KO12:45BST A D 2-2 Gallas (OG) 45', Ronaldo 84'
07 Nov UEFA Champ Lg Dynamo Kiev 19:45 H W Pique 31', Tevez 37', Rooney 76', Ronaldo 88'
11 Nov Barclays Prem Vs Blackburn 15:00 H W 2-0 Ronaldo 34', 35'
24 Nov Barclays Premier League United Vs Bolton 15:00 A L 0-1
27 Nov UEFA Champions League United Vs Sporting Lisbon 19:45 H W 2-1 Tevez, Ronaldo


December 2007
03 Dec Barclays Premier League United Vs Fulham 20:00 H W 2-0 Ronaldo (twice)
08 Dec Prem Lg United Vs Derby County 15:00 H W 4-1 Giggs, Tevez(2), Ronaldo(p)
12 Dec UEFA Champions League United Vs Roma 19:45 A Draw 1-1 Pique
16 Dec Barclays Premier League United Vs Liverpool 13:30 A W 1-0 Tevez
23 Dec Premier League United Vs Everton 12:00 H W 2-1 Ronaldo, Ronaldo(p)
26 Dec Prem Lg Vs Sunderland 15:00 A W 4-0 Rooney, Saha, Saha(p), Ronaldo
29 Dec Barclays Premier League United Vs West Ham 15:00 A L 1-2, Ronaldo

January 2008
01 Jan Barclays Premier League United Vs Birmingham 15:00 H
12 Jan Barclays Premier League United Vs Newcastle 17:15 H
19 Jan Barclays Premier League United Vs Reading 15:00 A
30 Jan Barclays Premier League United Vs Portsmouth 20:00 H

February 2008
02 Feb Barclays Premier League United Vs Tottenham 15:00 A
10 Feb Barclays Premier League United Vs Man City 12:00 H
23 Feb Barclays Premier League United Vs Newcastle 15:00 A

March 2008
01 Mar Barclays Premier League United Vs Fulham 15:00 A
08 Mar Barclays Premier League United Vs Bolton 15:00 H
15 Mar Barclays Premier League United Vs Derby County 15:00 A
22 Mar Barclays Premier League United Vs Liverpool 12:00 H
29 Mar Barclays Premier League United Vs Aston Villa 15:00 H

April 2008
05 Apr Barclays Premier League United Vs Middlsbro 15:00 A
12 Apr Barclays Premier League United Vs Arsenal 15:00 H
19 Apr Barclays Premier League United Vs Blackburn 15:00 A
26 Apr Barclays Premier League United Vs Chelsea 15:00 A

May 2008
03 May Barclays Premier League United Vs West Ham 15:00 H
11 May Barclays Premier League United Vs Wigan 15:00 A


Latest change: 31/12/2007, Mon
GOALS!!!!!!
Saha-Prem:1+1=2=4
Scholes-Prem:1+ =1
Nani-Prem:1+1 Champ Lg: =2
Vidic-Prem:1+1 =2
Ronaldo-Prem:1+2+1+2+2+1+3+1 Champ Lg:1+2+1+1 =18
Tevez-Prem:1+1+2+2+1 Cham Lg:1+1 =9
Rooney-Prem:1+2+1+1 Champ Lg:1+1+1 =8
Giggs-Pre:1+1 Champ Lge: =2
Ferdinand:Prem:1+ Champ Lg:1+ =2
Gerard Pique- Prem: Champ Lg:1+1 =2

Saturday 3 November 2007

Nipashe na Katiba ya CCM!

Nadhani waandishi habari na wahariri wa gazeti Nipashe wamepitiwa kidogo kuhusu utaratibu wa CCM kupitisha maamuzi kwa kufuata katiba yao.
Gazeti la leo (Nipashe) linasema Kamati Kuu ya CCM imeteua majina ya wagombea nafasi uenyekiti na makamu (Zanzibar na Bara); na kwamba yanaenda moja kwa moja Mkutano Mkuu wa Chama.
Kiutaratibu yanatakiwa yapewe baraka na Halmashauri Kuu ya CCM (na ndivyo ilivyokuwa).
Hakuna sehemu yoyote ktk habari ya Nipashe ambapo kikao cha H/Kuu imetajwa.

Nimenukuu baadhi ya sehemu kutoka gazeti hilo:
'Kamati Kuu ilikutana katika kikao cha siri jana chini ya Mwenyekiti wake, Rais Kikwete kupitisha majina ya watu watakaogombea nafasi ya Umakamu Mwenyekiti wa CCM kutoka Tanzania Bara na Visiwani.
Wateule hao majina yao leo yatawasilishwa katika Mkutano Mkuu wa Uchaguzi tayari kwa kupigiwa kura.' - Nipashe 03/11/2007

Na Mosonga

Ecological footprint

Ecological footprint:
Ecological footprint (EF) analysis measures human demand on nature. It compares human consumption of natural resources with planet Earth's ecological capacity to regenerate them.
It is an estimate of the amount of biologically productive land and sea area needed to regenerate (if possible) the resources a human population consumes and to absorb and render harmless the corresponding waste, given prevailing technology and current understanding.
Using this assessment, it is possible to estimate how many planet Earths it would take to support humanity if everybody lived a given lifestyle.
While the measure is widely used, some also criticize the approach.

From: wikipedia

Food miles

Food miles
The concept of food miles is part of a broader issue of sustainability which deals with a large range of issues, including local food.

Recent findings indicate that it is not only how far the food has travelled but how it has travelled that is important to consider.
The positive environmental effects of specialist organic farming may be offset by increased transportation, unless it is produced by local farms.
But even then the logistics and effects on other local traffic may play a big role. Also, many trips by personal cars to external shopping centres would have a negative environmental impact compared to a few truck loads to neighbourhood stores that can be easily accessed by walking or cycling. A locavore endeavors to eat food from within a foodshed having a radius of 100 miles.

Criticism of food miles
Critics of food miles point out that transport is only one component of the total environmental impact of food production and consumption. In fact, any environmental assessment of food that consumers buy needs to take into account how the food has been produced and what energy is used in its production. A recent DEFRA case study indicated that tomatoes grown in Spain and transported to the United Kingdom may have a lower carbon footprint in terms of energy efficiency than tomatoes to be grown in the United Kingdom because of the energy needed to heat greenhouses in the UK.

An 2006 research report from New Zealand's Lincoln University counters claims about food miles by comparing total energy used in food production in Europe and New Zealand, taking into account energy used to ship the food to Europe for consumers. The report states, "New Zealand has greater production efficiency in many food commodities compared to the UK. For example New Zealand agriculture tends to apply less fertilisers (which require large amounts of energy to produce and cause significant CO2 emissions) and animals are able to graze year round outside eating grass instead of large quantities of brought-in feed such as concentrates. In the case of dairy and sheepmeat production NZ is by far more energy efficient, even including the transport cost, than the UK, twice as efficient in the case of dairy, and four times as efficient in case of sheepmeat. In the case of apples NZ is more energy efficient even though the energy embodied in capital items and other inputs data was not available for the UK."

Further study on the total carbon footprint of food is required, of which transport may or may not make a large contribution. However, "Food Miles" signals more than just carbon footprint - which came into being several years later, and also includes transport of virtual water, life cycle assessments, land use and the craziness of moving similar foods backwards and forwards over the same ground.

A commonly ignored element is the local loop. The act of driving further to a more "right-on" food source increases the total carbon footprint. A shopper may buy say 5kg of meat and use about a gallon to get it. That piece of meat could have gone over 60,000 miles by road (40tonner at 8mpg) to require the same carbon in transportation.

From: wikipedia

NEC CCM: Ni Kikwete, Karume na Msekwa

Hongera sana waheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na M/kiti wa Baraza la Mapinduzi Amani Abeid Karume na Pius Msekwa kwa kuteuliwa kwenu kuwa wagombea wa nafasi za Mwenyekiti wa CCM, Makamu M/kiti Zanzibar na Bara.
Na Mosonga

MSEKWA ATEULIWA MAKAMU WA MWENYEKITI WA CHAMA CHA MAPINDUZI BARA

Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi imepitisha kwa Kauli moja jina la Mheshimiwa Rais JAKAYA MRISHO KIKWETE kuwa Mgombea Pekee wa nafasi ya Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi.

Halmashauri Kuu ya CCM imepitisha majina mawili katika nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara na Zanzibar.

Rais ABEID AMANI KARUME ameteuliwa kugombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa CCM zanzibar na Ndugu PIUS MSEKWA ameteuliwa Kugombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara.

Wagombea wote watapigiwa kura leo kwenye Mkutano Mkuu wa CCM unaoanza leo Kizota nje kidogo ya Mji wa Dodoma.

Pia Halmshauri Kuu ilimteua Ndugu Khadija Faraji Kuwa Katibu wa CCM mkoa wa Unguja Kaskazini.
03 Nov 2007

From: www.ccmtz.org

Friday 2 November 2007

Organic food

Organic food
Organic foods are produced according to certain production standards.
-For crops, it means they were grown without the use of conventional pesticides, artificial fertilizers, human waste, or sewage sludge, and that they were processed without ionizing radiation or food additives.
-For animals, it means they were reared without the routine use of antibiotics and without the use of growth hormones. In most countries, organic produce must not be genetically modified.

Increasingly, organic food production is legally regulated. Currently, the United States, the European Union, Japan and many other countries require producers to obtain organic certification in order to market food as organic.

Historically, organic farms have been relatively small family-run farms — which is why organic food was once only available in small stores or farmers' markets. Now, organic foods are becoming much more widely available — organic food sales within the United States have grown by 17 to 20 percent a year for the past few years while sales of conventional food have grown at only about 2 to 3 percent a year. This large growth is predicted to continue, and many companies are jumping into the market.

Types of organic food
Organic foods can be either fresh or processed, based on production methods.

Processed food
Often, within the same supermarket, both organic and conventional versions of products are available, although the price of the organic version is usually higher (see modern developments). Most processed organic food comes from large food conglomerates producing and marketing products like canned goods, frozen vegetables, prepared dishes and other convenience foods.

Processed organic food usually contains only organic ingredients, or where there are a number of ingredients, at least a minimum percentage of the plant and animal ingredients must be organic (95% in Australia). Any non-organically produced ingredients must still meet requirements. It must be free of artificial food additives, and is often processed with fewer artificial methods, materials and conditions (no chemical ripening, no food irradiation, and no genetically modified ingredients, etc.).

They may also be required to be produced using energy-saving technologies and packaged using recyclable or biodegradable materials when possible.


Identifying organic food
At first, organic food comprised mainly of fresh vegetables. Early consumers interested in organic food would look for chemical-free, fresh or minimally processed food. They mostly had to buy directly from growers: "Know your farmer, know your food" was the motto. Personal definitions of what constituted "organic" were developed through firsthand experience: by talking to farmers, seeing farm conditions, and farming activities. Small farms grew vegetables (and raised livestock) using organic farming practices, with or without certification, and the individual consumer monitored.

Consumer demand for organic foods continues to increase, and high volume sales through mass outlets, like supermarkets, is rapidly replacing the direct farmer connection. For supermarket consumers, food production is not easily observable, and product labelling, like "certified organic", is relied on. Government regulations and third-party inspectors are looked to for assurance.

A "certified organic" label is usually the only way for consumers to know that a processed product is "organic".

from: wikipedia

Organic farming

Organic farming is a form of agriculture which avoids or largely excludes the use of synthetic fertilizers and pesticides, plant growth regulators, and livestock feed additives. As far as possible, organic farmers rely on crop rotation, crop residues, animal manures and mechanical cultivation to maintain soil productivity and tilth to supply plant nutrients, and to control weeds, insects and other pests.

What is organic farming?

Organic farming can be defined as an approach to agriculture where the aim is to create integrated, humane, environmentally and economically sustainable agricultural production systems. Maximum reliance is placed on locally or farm-derived renewable resources and the management of self-regulating ecological and biological processes and interactions in order to provide acceptable levels of crop, livestock and human nutrition, protection from pests and diseases, and an appropriate return to the human and other resources employed. Reliance on external inputs, whether chemical or organic, is reduced as far as possible. In many European countries, organic agriculture is known as ecological agriculture, reflecting this reliance on ecosystem management rather than external inputs.

The objective of sustainability lies at the heart of organic farming and is one of the major factors determining the acceptability or otherwise of specific production practices. The term 'sustainable' is used in its widest sense, to encompass not just conservation of non-renewable resources (soil, energy, minerals) but also issues of environmental, economic and social sustainability. The term 'organic' is best thought of as referring to the concept of the farm as an organism, in which all the component parts - the soil minerals, organic matter, micro-organisms, insects, plants, animals and humans - interact to create a coherent and stable whole.

The key characteristics of organic farming include:

1. protecting the long term fertility of soils by maintaining organic matter levels, encouraging soil biological activity, and careful mechanical intervention;

2. providing crop nutrients indirectly using relatively insoluble nutrient sources which are made available to the plant by the action of soil micro-organisms;

3. nitrogen self-sufficiency through the use of legumes and biological nitrogen fixation, as well as effective recycling of organic materials including crop residues and livestock manures;

4. weed, disease and pest control relying primarily on crop rotations, natural predators, diversity, organic manuring, resistant varieties and limited (preferably minimal) thermal, biological and chemical intervention;

5. the extensive management of livestock, paying full regard to their evolutionary adaptations, behavioural needs and animal welfare issues with respect to nutrition, housing, health, breeding and rearing;

6. careful attention to the impact of the farming system on the wider environment and the conservation of wildlife and natural habitats.

Organic systems
The main components of organic farming are avoiding the use of artificial fertilisers and pesticides, and the use of crop husbandry to maintain soil fertility and control weeds, pests and diseases.

Arable
The main aspects of organic arable systems are:
-soil fertility
-crop rotation
-crop protection
-organic seed
-organic crop storage

Livestock
Livestock systems often form an integral part of an organic farming system.

The main aspects of organic livestock systems are:
-feeding
-housing
-health management
-use of manures

From:
www.wirs.ac.uk
www.defra.gov.uk
wikipedia

Yanga 2007/08

Kikosi cha Yanga msimu huu 2007/08:

Walinda mlango
1.Benjamin Haule, Ivo Mapunda, Jackson Chove

Walinzi
2.Fred Mbuna,
3.Amir Maftaha, Abuu Mtiro
4.Lulanga Mapunda, Hamis Yussuf
5.Wisdom Ndlovu, Nadir Haroub (Cannavaro)

Viungo
6.Athumani Idd, Edwin Mukenya, Waziri Mahadhi
7.Mrisho Ngassa, Credo Mwaipopo,
8.Laurent Kabanda, Abuu Ramadhan

Washambuliaji
9.Ben Mwalala, Hussein Sudi, Gaudence Mwaikimba,
10.Maurice Sunguti, Hamis Suedi
11.Abdi Kassim, Aime Lukunku, Mrisho Ngassa

Prisons 1 Yanga 2

Yanga `yaikata ngebe` Prisons

2007-11-02 08:59:15
By Jacqueline Massano, Mbeya


Yanga jana iliweza kupunguza kasi ya Prisons ya Mbeya baada ya kuibuka na ushindi wa 2-1 katika mchezo wa Ligi Kuu ya soka ya Tanzania Bara uliochezwa kwenye uwanja wa Sokoine mjini Mbeya.

Kwa matokeo hayo sasa, Yanga imeweza kufikisha pointi 18 na kutofautiana pointi sita na Prisons.

Yanga iliweza kuondoka na ushindi baada ya kucheza soka ya kuvutia na ingeweza kuondoka na ushindi mkubwa kama washambuliaji wake wangekuwa makini.

Ni tofauti na Prisons, ambayo ilikosa uelewano katika mchezo huo, hasa upande wa beki.

Kuna uwezekano kunaweza kukawa kwa kiasi kikubwa kulichangiwa na hofu ya kucheza na Yanga, ambayo katika siku za karibuni imeonekana kutulia na kuanza kukusanya pointi.

Yanga iliweza kujipatia bao la kwanza katika dakika ya 38 lililofungwa kwa `tik tak? na mshambuliaji mkongwe, Mkenya Maurice Sunguti.

Mrisho Ngassa, hata hivyo, aliyeingia katika kipindi cha pili, aliihakikishia Yanga ushindi baada ya kufunga bao maridadi katika dakika ya 73.

Alifunga bao hilo baada ya kumlamba chenga beki Sam Kamtande na Kipa Frank Mutego kabla ya kuzamisha mpira wavuni akiwa peke yake na goli.

Stephen Masika, hata hivyo, aliipatia Prisons bao la kufutia machozi katika dakika ya 85.

Akizungumza baada ya mchezo huo, Kocha Jack Chamangwana alieleza kufurahishwa na ushindi wa timu yake.

Chamangwana alidai zilikuwa pointi tatu muhimu na pia alifurahishwa timu yake kuweza kupunguza kasi ya Prisons iliyoonekana kupaa kwenye msimamo wa ligi wakati ilipoanza.

Naye Kocha Juma Mwambusi wa Prisons alieleza masikitiko yake baada ya timu yake kupoteza mechi ya kwanza nyumbani.

Timu zilikuwa:
Prisons: Frank Mutego, Lusajo Mwakifamba, Stephano Masika, Aloyce Adam, Sylvester Kamtande, Godfrey Bonny, Said Mtupa, Misango Magai, Oswald Morris, Yonah Ndabila (Shabaan Mtupa dk.65) na Fred Chudu.

Yanga: Jackson Chove, Fred Mbuna, Abuu Mtiro, Wisdomu Ndlovu, Hamisi Yussuf, Credo Mwaipopo, Waziri Mahadhi (Mrisho Ngassa dk.46), Abuu Ramadhan, Gaudence Mwaikimba, Maurice Sunguti (Hamisi Suedi dk.76) na Abdi Kassim (Nadir Haroub `Cannavaro` dk.65).

Wakati huo huo, Victor Kwayu wa PST-Moshi anaripoti Toto African ya Mwanza ilipata pointi tatu za ugenini baada ya kuilaza Ashanti 2-0 kwenye mchezo uliofanyika kwenye uwanja wa Ushirika kwa mabao yaliyopachikwa na Castory Mubala na Joseph Lindo.

Naye Idda Mushi wa PST-Morogoro anaripoti kuwa mechi kati ya Polisi Morogoro na Kagera Sugar iliyokuwa ifanyike jana itachezwa leo badala ya jana kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro

From: Nipashe

Vidic aims to keep clean sheet at Arsenal

Vidic aims to keep Arsenal out
Serbian centre-back Nemanja Vidic has the specific aim of not conceding against Arsenal this weekend, but he has also warned the Gunners that they face a tough task containing the Reds’ firing front men.

Wayne Rooney and Cristiano Ronaldo lead the goalscoring stakes with six apiece, while Carlos Tevez has chipped in with four and Ryan Giggs, Rio Ferdinand, Louis Saha and Nani have all scored two.

"Rooney and Tevez are playing so well at the moment, but it’s not just them; Ronaldo, Nani, every one of the attackers,” he was quoted as saying in The Sun.

The Reds travel to the Emirates Stadium for Saturday’s lunchtime kick-off level on 26 points with the current league leaders, who have a game in hand, and United don’t want to let the Londoners edge any further ahead.

Vidic, himself with one league goal this term, is determined to put up formidable resistance to Arsene Wenger’s forwards.

“Arsenal have been playing very well. They are not just winning but playing good football too,” he said. “I watched their match against Liverpool and thought they were especially good in the first half.

“But, at the back, we will take just as much pride from a clean sheet as our strikers will from scoring a goal. Arsenal will be a big test but I believe we can stop them and have another clean sheet to our names.”

From: www.manutd.com

Thursday 1 November 2007

Manchester United Fixtures & Results

August 2007
12 August 2007 Reading H k.o.1600BST Draw 0 - 0
15 August 2007 Portsmouth A KO19:45BST Draw 1-1, Scholes
19 August 2007 Man City A KO13:30BST Lost 0-1
26 August 2007 Tottenham H KO16:00BST Win 1-0, Nani

September 2007
01 September 2007 Sunderland H k.o. 17:15 W 1-0, Saha
15 September 2007 Everton A KO12:00 BST W 1-0, Vidic 83'
19 September2007 Sporting Lisbon A KO19:45BST W 1-0, Ronaldo 62'
23 September2007 Chelsea H KO1600BST W 2-0, Tevez 45', Saha 89'
26 September2007 Coventry City H KO20:00BST L 0-2
29 September2007 Birmingham A KO17:15BST W 1-0 Ronaldo 51'

October 2007
02 Oct UEFA Champions League United Vs Roma H KO19:45BST W 1-0, Rooney 51' (itv 1)
06 Oct Prem Vs Wigan 12:45 H W 4-0, Tevez 54' Ronaldo 59'&76', Rooney 82'
20 Oct Prem Vs A Villa 17:15 A W 4-1, Rooney (36, 44), Ferdinand (45), Giggs (75)
23 Oct UEFA Champ Lg Vs Dynamo Kiev 19:45 A W 4-2 Ferdinand,Rooney, Ronaldo(2)
27 Oct Prem League United Vs Middlsbro 15:00 H W 4-1 Nani, Rooney, Tevez (2)

November 2007
03 November 2007 V Arsenal A KO12:45BST A D 2-2 Gallas (OG) 45', Ronaldo 84'
07 November 2007 V Dynamo Kiev H KO19:45
11 November2007 V Blackburn H KO15:00



GOALS!!!!!!
Saha-Prem:1+1=2
Scholes-Prem:1+ =1
Nani-Prem:1+ =1
Vidic-Prem:1+1 =2
Ronaldo-Prem:1+2+1 Champ Lg:1+2+ =7
Tevez-Prem:1+1+2 Cham Lg: =4
Rooney-Prem:1+2+1 Champ Lg:1+1 =6
Giggs-Pre:1+ Champ Lge: =1
Ferdinand:Prem:1+ Champ Lg:1+ =2