Saturday 30 May 2009

Jicho la 3

Ili tuendelee watanzania tunatakiwa tuwe wawazi na wakweli. Hakuna kitu kibaya kama unafiki wa kusifia hata pale panapoonekana kabisa kuna dosari.

Wananchi, ambao kwa kweli ni wanyonge, wanahitaji watu ambao watasimama kidete kuwatetea na kulinda haki zao. Wananchi hawahitaji mtu wa kuwagawia hela njiani. Wananchi wahitaji haki yao iwepo wazi. Kila stahili yao ni lazima ipatikane kwa uwazi bila kuzungushana hasa hasa huduma za kijamii kama vile hospitalini, shuleni, maofisini n.k. Watendaji wasizitoe kama vile ni 'favour'. Kuzungushana-zungushana ndio mwanzo wa kuchochea rushwa.

Serikali yetu nayo inahitaji msukumo kutoka pembeni. Tusijidanganye eti kwa kuisifia ndio tutaonekana 'wazuri' mbele yake. Tena wakati mwingine serikali hushukuru inapomulikwa utendaji wake. Kama kuna udhaifu ndani ya vyombo vya utendaji au watendaji serikalini, ni lazima usemwe na kukemewa vikali.

Kama serikali yetu inafanya vizuri kazi yake mimi nitakuwa mtu wa kwanza kuisifia au kuipongeza. Lakini kama serikali inafanya 'madudu' na kukiuka ahadi ilizozitoa ktk ilani ya chama chake wakati wa uchaguzi mkuu, mimi nitakuwa miongoni mwa wataoisema na kuilaumu. Hakuna cha urafiki ktk kulinda maslahi ya Taifa letu. Wale wenzetu walioko serikalini wakumbuke kuwa wako pale kwa ajili ya kusimamia rasilimali za Taifa na kutuongoza ili tujikomboe kiuchumi na kimaendeleo. Na tunataka maendeleo ya Taifa yatafsiriwe kupitia ustawi wa maisha ya wananchi kwa ujumla.

Ndio maana nasema kuwa ni wajibu wa serikali kuongoza nchi kwa misingi inayokubalika. Haki, uhuru na stahili za wananchi zisitolewe kama fadhila.

Mwisho, tusisahau kujikumbusha hotuba muhimu za watangulizi wetu. Kwa ujumla karibu hotuba zote za Baba wa Taifa Mwalimu JK Nyerere ni nzuri, ila kama nafasi hairuhusu napendekeza turejee hotuba mbili. Ya kwanza ni ile aliyokuwa anaongea na waandishi wa habari mwaka 1994, na hotuba ya pili, kwa mapendekezo yangu, ni ile ya kilele cha maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani iliyofanyika kitaifa mjini Mbeya (Uwanja wa Sokoine) mwaka 1995. Naye Rais mstaafu Mheshimiwa Benjamin William Mkapa aliwahi kutoa hotuba nzuri ktk NEC ya Chama Cha Mapinduzi au Bungeni (sina hakika) -aliipa hotuba hiyo kichwa cha 'The Courage of Leadership' (na inapatikana ktk tovuti ya Chama Cha Mapinduzi). Huu ni urithi mzuri kwetu na kwa vizazi vijavyo.

Friday 29 May 2009

Siku Simba na Yanga walipotozwa faini

-Ilikuwa tarehe 30/10/2007
watani wa jadi simba na yanga leo wamezabwa faini ya shilingi 500,000 kila mojakutokana na timu hizo kufanya vurugu wakati wa mechi yao iliyochezwa Jumatano iliyopita mjini Morogoro.

katika mchezo huo ambao Simba ilishinda bao 1-0 mashabiki wa Yanga waliwekavizuizi vya viti kwa lengo la kuzuia magari ya viongozi wa Simba nawachezaji tukio ambalo lilisababisha kushambuliwa kwa mawe, chupa za maji navimiminika vingeni gari la wachezaji wa Simba na mchezaji Haruna Moshialijeruhiwa.

yanga imepigwa faini ya shilingi 500,000 na imetakiwa kulipa gharama za uharibifu uliotokana na vurugu hizo ikiwa ni pamoja na matibabu ya mchezaji Haruna Moshi baada ya kuwasilishwa na kuthibitishwa na tff.

simba, ambao nao walihusika na vurugu kwa kurusha mawe, chupazilizojaa maji na vimiminika vingine na kusababishwa mchezo kusimama nayo imetozwa faini ya shilingi 500,000 na faini hizo ni kwa mujibu wa kanuni ya 31(1) na 66 ya tff.


......................................................
Maoni:
Tarehe October 30, 2007 9:11 PM, Mtoa Maoni: MOSONGA

Hiyo sheria ifanyiwe marekebisho haraka sana.
Sh 500,000/= haiwaumizi hawa simba na Yanga! Inatakiwa iwe sh. mil.5 as a minimum ili iwe fundisho!

........................................................

source: Michuzi | Monday, October 29, 2007

Watchout! "She" wants you all!

Subject: Hello!!!
Date: Thursday, May 28, 2009 6:46 PM
From: "lyn gitchel"
To: undisclosed-recipients

Hello,
My name is Lyn Gitchel I am 23 years old (Vig), Single, Native of American, Caucasian, Heterosexual, Female, 5'11" (149cm), 105lbs (47kg), located in Baltimore, Maryland United States. Christian by religion.
I'm a full time Student and I'm majoring in marketing and getting a minor in International financing.
My body style is average weight I am physically active, I never smoke and drink. I am the only girl in the family of three children, am the second child.
My father and mother are still alive. My father is 55 years old, why my mother is 48 My elder brother is 26 and younger brother is 20.
Get in touch at
lyn_gitchel4u@yahoo.com,
With Love,
Lyn Gitchel

Favourite Books

Architecture:
Architect's Pocket Book, 3rd edition
Charlotte Baden-Powell, Jonathan Hetreed, Ann Ross
Architectura Press
ISBN 978-0-7506-8617-4

Landscape Architect's Pocket Book, 1st edition
Siobhan Vernon, Rachel Tennant, Nicola Garmory
Architectura Press
ISBN 978-0-7506-8348-7

Building Construction Handbook: incorporating current building and construction regulations, 7th edition.
Roy Chudley and Roger Greeno
ISBN 978-0-7506-8622-8


English/General:
Oxford Advanced Learner's Dictionary, 7th Edition
A S Hornby
OUP
ISBN 978-0-19-400116-8
£25.00


(price, and book titles as seen at Waterstones Bookshop, Broad street, Reading on Thursday 28 May 2009)

Thursday 28 May 2009

Do not short-change the future!

................................
'don't short-change the future because of the fear in the present'
-US President Barack Obama, his response to worried voters
10:59 BST, April 01, 2009. Joint Press Conference with PM Gordon Brown in London (shortly before g20 summit)

................................

................................
'overtime good policies is good politics'
-President Obama, 11:02 BST, April 01, 2009
................................

Tawi la MU Dar lazinduliwa

Mashabiki wa Manchester United FC nchini (Tanzania) wameunda tawi na kulifungua leo katika hoteli ya Regency.

Uongozi wa Tawi:
-Bernard Mbwana (m/kiti)
-Ngallo (katibu wa muda)
-Dennis Ssebo (mratibu wa tawi)

Sherehe ya uzinduzi wa tawi ilifanyika usiku huu na kuhudhuriwa balozi wa Uingereza nchini Mh. Diane Corner ambaye pia alizindua rasmi tawi la Manchester United FC Dar.


chanzo: lukwangule blogspot, 28/05/2009

It was a good season for Man Utd!

Despite losing to Barcelona in the final of Champions League, Manchester United had a good season in general. We won 3 trophies, reaching in the semis of FA Cup, and finals of UEFA Champions League. That's something we should be proud of.

We win matches and titles together and when we don't, we lose together!!

This is Manchester United. I have no doubt we will be back stronger next season.

Glory, Glory Man United!

Tuesday 26 May 2009

Kukubali kushindwa ni ushujaa pia

Napenda kuwasihi watanzania wenzagu kuwa na moyo wa kweli kiushindani. Ktk mashindano yoyote yale ni lazima apatikane mshindi na kwa matokeo hayohayo ambaye hakushinda atapatikana pia.
Wenzetu waliogombea kule Busanda walikuwa na wiki takribani 4 za kujinadi. Baada ya muda huo, ikaja zamu ya wapiga kura kuamua na WAMESHAAMUA ni nani awe mbunge wao. Ni mategemeo yangu kuwa wagombea walioshindwa wangekubaliana na kauli ya wananchi. Huo ndio ukomavu wa kidemokrasia.
Hongera sana Mheshimiwa Lolensia Bukwimba wa Chama Cha Mapinduzi. Wananchi wameonyesha imani nawe kwa kukuchagua kuwa mwakilishi wao. Ninakutakia kila la heri katika majukumu yako. Moja ya kazi ninazokutuma Bungeni ni kufuatilia utaratibu mbaya uliopo ktk sheria za uchaguzi uliosababuisha wewe na wagombea wengine kutopiga kura kwa kuwa mlijiandikisha sehemu nyingine tofauti na Busanda. Hebu fuatilia hilo, inauma mtu kugombea halafu usiruhusiwe kupiga kura!

Nani aitangaze nchi yetu nje?

Ni kawaida yetu sisi kulaumu serikali zetu hazifanyi jitihada yoyote kuitangaza nchi yetu ughaibuni (nchi za nje). Tumekuwa tunalaumu pia wizara husika ya Utalii ni kwa nini haitangazi vivutio vya utalii vilivyoko nyumbani n.k.

Kwa upande wangu naona suala hili ni la pande zote. Sio la serikali pekee. Hata wale wanaopata nafasi ya kufika au kuishi huku japo kwa muda kidogo, no wana wajibu pia kwa kiwango chao. Naweza kusema ni wadau wa ktk kutangaza nchi yetu pale walipo na kwa uwezo walio nao.

Kwa bahati mbaya, ninashangaa sana kuona hawa wadau (watanzania walio ughaibuni) hawatekelezi linalowahusu ktk kuitangaza nchi.

Natoa mfano mdogo tu.
-Je watanzania walioko nje (wa kiume na kike) wanavaa mavazi gani? Wanavaa vito gani?
-Je wanasikiliza muziki wa aina gani majumbani kwao na vyombo vyao vya usafiri (ndani ya magari yao)?
-Majumbani kwao ukutani kuna picha za mandhari za wapi?

Mara nyingi utakuta tunasikiliza miziki ya nje hadharani, mavazi ya mitindo ya nchi za nje, picha za huko Marekani n.k.

Huu ni wakati wa kuamka ili tuweze kuchangia ktk kuitangaza nchi yetu hasa kwa kupitia utamaduni wetu na mali asili zetu! Kwa kufanya hivyo tutaweza kuiweka nchi yetu hadharani, maana sisi ndio tulioko mitaani na watu wanakutana nasi kila siku. Sisi ni kioo cha nchi yetu, na ndio maana nasema kuwa mchango wetu ni mzito zaidi kuliko matangazo kwenye luninga na majarida mbalimbali.

Maisha Uingereza -2

26/05/2009
Utamaduni wa wenzetu ni tofauti na wa kwetu Afrika. Nyumbani tumezoea kusalimiana kila tunapokutana hata kama mtu hamfahamiani. Huku sio hivyo. Ukifika, kwa mfano, kituo cha basi au hospitali unakuta watu kimya kila mmoja na lake. Wengine wanacheza game na simu zao, wenye vitabu wako bize wanasoma au mtu na mwenzi wake wanabusiana hapo n.k. Hakuna cha jambo wala nini. Muda ukifika wa kupata kilichokupeleka hapo unafanya na kupotea!
Na ule utamaduni wetu wa kumwita mtu dada, shangazi, kaka, mzee n.k. haupo hapa. Ukimwita mtu kaka -atashangaa anaweza kukwambia mimi sio kaka yako au sio ndugu yako. Kama mtu unamfahamu unatakiwa kumwita jina lake la kwanza hata kama ana umri sawa na babu yako. Hakuna cha Mr. fulani, au Mrs. fulani. Hapo ndipo pagumu maana unaona kama utamdhalilisha kumwita kwa jina! Mtoto wa miaka 4 anamwita mtu wa miaka kama 50 kwa jina mfano Peter, Sarah n.k. Mtoto atamwita mama yake tu kama 'mama' lakini sio kwa watu wenye umri wa mama yake!
Ule utamaduni wetu wa kuwapenda na kuwajali watoto njiani huku ni mwiko! Usije jaribu kumsaidia kitu mtoto njiani hata kama anahitaji msaada. Hilo ni kosa kubwa mno kwa huku. Ukimshika mtoto tu ni kosa na tena unaweza kushitakiwa na kufungwa kwa kumdhalilisha mtoto. Kwa hiyo kaa mbali na watoto wa watu wengine. Kama ni mwanao sawa, lakini hakuna cha kusema huyu ni mtoto wa jirani.
Hakuna utamaduni wa kuazimana magazeti ndani ya basi, kama tufanyavyo nyumbani kwa kugawana kurasa za gazeti! Kama kitu si chako itabidi uangalie kijanja sio shingo feni!
Ila wana kautamaduni poa sana ka ustaarabu wa kupanga foleni kila panapotakiwa. Mfano kupanda basi au treni, au wakati wa kushuka watu hufuata utaratibu wa foleni tena kwa taratibu bila kusukumana. Wakati wa kulipia huduma dukani au huduma za benki n.k. wateja hujipanga foleni kwa kuzingatia aliyekuwa wa kwanza kufika eneo husika. Na kama wote mmefika kwa wakati mmoja haina tatizo watu hupeana nafasi ili kujipanga. Hapo ni raha sana na huu ustaarabu inabidi tujifunze na sisi huko nyumbani. Nadhani wanapokuja kutalii huko nyumbani huwa wanatushangaa tunavyombania kuingia ktk usafiri hasa wa daladala, mpaka wengine hupitia dirishani!

Maisha Uingereza -1

May 26, 2009
Nimeishi ugenini UK kwa muda mfupi kidogo. Kwa maana hiyo siwezi kujiita mwenyeji au 'al-watan'! Hata hivyo, ktk muda huo mfupi ni mengi nimeyaona; mazuri, ya kawaida na mengine yasiyo ya kuvutia! Leo, nimeamua kujipa zoezi (au 'assignment' kwa lugha ya kigeni) - kutoa tathimini ya maisha ya UK kutokana na uzoefu wangu wa muda mfupi wa kuishi hapa.

Hawa wenzetu huku Uingereza wanajali sana muda. Ndio maana huko nyumbani tumezoea kusikia msemo maarufu 'time is money'. Lakini maana halisi ya msemo huo utaiona huku. Mambo yao yote yako kwa ratiba ya muda (siku, saa hata dakika). Kazini wanaingia kwa kuweka sahihi (signing in) na mtu akitoka nje mapumziko au kwa shughuli zisizo za kikati anasaini kutoka ktk mtambo mdogo wa kunakili muda wa kila mfanyakazi (wao wanaita clocking in and out). Kwa hiyo mwisho wa wiki au mwezi masaa yako huhesabiwa na kompyuta na kulipwa masaa ambayo umefanya kazi 'kikweli kweli'. ule utaratibu wetu Afrika wa kuripoti kazini kisha kutoweka hapa haupo. Na ukiwa mtorokaji au mkwepaji kibarua chako kitaota majani haraka sana maana uthibitisho upo kitaalamu kuwa tija yako ni ndogo na ni hasara kwa kampuni au mwajiri wako.
Karibu kila mtu ana kitabu cha mambo yake (diary) ambapo hurekodi kumbukumbu zake zote ikiwa ni pamoja na masaa na siku za shifti zake. Muda wa kuanza kazi sharti uwepo kazini na muda wa kutoka tu ukifika mtu unafunga vilivyo vyako na kuondoka, na kila mmoja na njia yake! Sio kawaida mtu kudandia lifti huku, kama hauna usafiri wako itabidi upitie kituo cha basi au treni kwa ajili ya kurejea kwako. Ama kama ni karibu utaswaga mguu (sio aibu ni jambo la kawaida huku).

Zipo kazi mbalimbali huku. Lakini watu wengi kule nyumbani TZ wanaelewa moja tu -ya 'kubeba box'. Hii moja ya kazi ambazo kwa UK hujulikana kama Industrial (Pick&Packing). Pamoja na watu huko nyumbani kuiona kama kazi rahisi lakini inahitaji mafunzo ya awali ktk kuifanya, na inabidi mtu apitie kozi ndogondogo ili aweze kuruhusiwa kuifanya. Baadhi ya kozi ni za 'first aid', 'manual handling', 'Control of substances hazardous to health (COSHH)', 'fire fighting' n.k. Nguvu na akili yako huhitajika pia.
Kazi zingine ambazo watu hujihusisha ni za kijamii, kwa mfano kulea watoto au watu wazima (wazee au wale wenye matatizo ya kitabia yaani challenging behaviour). Hizi za wazee sana kiumri hujulikana kama Nursing. Ktk 'Nursing' mtu huajiriwa kufanya kazi kwenye 'nursing homes' ambapo wazee (vikongwe) husaidiwa ktk mahitaji yao ya kila siku (mfano kupikiwa na kulishwa chakula, kuogeshwa, kuvalishwa, kunyanyuliwa kitandani au kitini n.k.). Inabidi upate mafunzo kama yale ya industrial na ya nyongeza kama food hygiene.
Ktk kulea watoto, watu huajiriwa ktk shule za watoto watukutu ili kusaidia kuwaangalia na kuwatuliza. Zipo kazi zingine za kijamii za kuwaangalia watu wenye akili taahira na mtindio wa ubongo ktk 'Residential Care homes'. Utasikia watu wanaziita kazi za 'care'. Kundi hili ni la watu wa rika zote. Zipo kozi zake pia (hizo nilizotaja hapo juu nazo ni lazima uzifanye. Kozi za care ni pamoja na NVQ level 1-3 kwa kutegemea majukumu mtu aliyoajiriwa nayo au atakayopewa kama 'promotion' kazini). Kazi za care huhusiana na kuwaangalia, kusaidia kuwapatia huduma mbalimbali za kimahitaji ya kila siku na pia kuwapatia dawa za matibabu walizoandikiwa na daktari. Kabla ya kuruhusiwa kufanya kazi zozote za kijamii ni lazima ufanyiwe uchunguzi wa kipolisi kuona kama una kosa lolote la jinai. Watu waliohukumiwa kwa makosa fulani ya jinai hawaruhusiwi kuchanganyikana na makundi ya watu wanaohitaji kusaidiwa kwa mfano wazee vikongwe, watoto wadogo na wenye ulemavu wa taahira ya akili na mtindio wa ubongo (vulnerable people).

Zipo pia kazi za kufanya usafi ktk mahoteli na maofisi (cleaning). Hizi hufanyika zaidi nyakati za jioni au alfajiri sana ama siku za mwisho wa juma (pale ofisi zinapokuwa wazi). Pia watu hupelekwa kufanya usafi maeneo yenye mkusanyiko mkubwa wa watu mfano kwenye viwanja vya michezo (mpira wa miguu, ragbi, mbio za farasi, kumbi za starehe n.k.).

Kazi zingine zinahusu usimamizi wa watazamaji (crowd safety/control) ktk matukio mbalimbali (events organizing). Kwa mfano siku za mashindano ya farasi, siku za mechi za mpira wa miguu (premier league, championship au mechi Euro uwanja wa Wembley). Hii ni mifano michache ya matukio ambayo watu huchukuliwa kusaidia -watu hawa wanaitwa 'stewards'. Polisi hukaa pembeni, wakisubiri kama kuna matukio yanayoweza kuwahitaji wao kuingilia.

Kwa ufupi, hizi ndizo baadhi ya kazi ambazo watu waendao UK hufanya ili kuweza kujikimu mahitaji yao mbalimbali. Kusema kweli kazi hizi hufanywa zaidi na wale tunaotoka nje ya UK; kama vile Afrika, Asia, Amerika ya Kusini, visiwa vya karibean n.k. Kwa wazawa wa UK wengi wao hawapendi kuzifanya kazi hizi na kama wapo wanaozifanya ni wale ambao hawakwenda shule au hawana elimu ya sekondari; kwani kwa wazawa wa hapa UK elimu ya sekondari inatosha kabisa kumpa mtu kazi nzuri.

Chai na sukari. Usije kushangaa mtu anakukaribisha chai na kukuliza 'how many sugar?'. Watu hunywa chai kwa kutumia sukari zilizo katika vipakiti vidogovidogo sawa na kijiko kimoja cha cha chai. Na wengi hutumia kipakiti kimoja au kijiko kimoja cha chai. Wengine hutumia viwili au hawatumii kabisa sukari. Wanakunywa chai kavu (bila sukari na maziwa kidogo sana!). Sisi tuliotoka Afrika mara nyingi hutumia vitatu au vinne! wazungu hushangaa sana wanaposikia tunasema 3 au 4 sugars!!! Kwa hiyo ukisikia unaulizwa 'how many sugars' ujue wanakuuliza unatumia vijiko (au vipakiti)vingapi vya sukari.

Hawa jamaa (wazungu) hawana cha siri. Uki'muuma mtu sikio' uelewe kabisa hiyo sio siri - itaanikwa hadharani muda wowote! Ndivyo walivyo, hawana kitu cha siri! Wanapenda sana kufuga wanyama wadogo (mbwa, paka, ndege n.k.) kama mapambo. Na wengine huwaita hao wanyama kama wenzi wao (companion).

Kwa tuliotoka Afrika kwenye maeneo ya joto, mbu na nzi ni wadudu wa kawaida. Pia magonjwa yatokanayo na wadudu hao ni ya kawaida - malaria, kipindupindu kuhara n.k. Kwa kweli hali ya hewa ya ubaridi huku UK hairuhusu wadudu hao kuishi ama kuzaliana. Kuna wakati huwa naona nzi wale wa kijani mara moja moja, na mbu husikika pia kwa mbali lakini sio mara kwa mara. Cha muhimu ni kuwa hakuna madhara yoyote yanayoletwa na kelele zao. Sijawahi kuona neti madukani wala ktk miji ya watu, hiki ni kiashirio kuwa hakuna tishio la malaria. Pia watu wa huku huwa hawazingatii sana usafi wa kunawa mikono (achilia mbali kunawa kwa sabuni!). Watu wanaweza kuwa wako kazini bize lakini wakati wa mapumziko wananunua mkate (sandwich) na kushika na mikono michafu na wakati mawingine mtu anaweka chini kipande cha mkate halafu anaendelea kula baadae! Kipindupindu na magonjwa mengine ya tumbo hayapo huku.

Baadhi ya vijana wadogo wa huku (miaka kati ta 16 hadi 30 hivi) wana tabia mbaya ya kugombana na kuchomana visu. Wengi wao wako ktk magenge na kila genge huwa na uongozi wao na eneo wanalotawala. ikitokea kundi moja (genge) likaingia himaya ya wengine fujo hutokea na aghalabu matokeo ya fujo hizo ni kuuana. miji mikubwa kama London na Manchester hali ni mbaya mno!

Kwa upande mwingine UK kuna hali ya ustaarabu au maendeleo ya namna fulani tofauti na nyumbani. Kwetu Afrika, nyumba au ofisi huwa hazijakamilika bila kuwa na mageti ya chuma milangoni na madirisha ya nondo. Kwa UK mambo sio hivyo. Milango ya nyumba, ofisi hata mabenki huwa ni ya vioo na hata madirisha ni ya vioo - hakuna vibaka wa kuvunja na kuingia kuiba,na kama matukio hayo yapo ni kwa asilimi ndogo sana. Hata magari hulazwa nje, tena barabarani kila siku - hakuna tatizo.

Shrika la Posta chini ya 'Royal Mail' wana utaratibu wa kusambaza barua au vifurushi vya wateja kwa kuwapeleakea ktk makazi yao. Ndio maana anuani za UK huwa zina jina la mpokeaji barua/kifurushi, namba ya nyumba anayoishi, mtaa na post code (mfano RG2 7HT, SL5 0TP, W7 3CX n.k.). Lakini ni lazima niseme kuwa kuna baadhi ya matatizo yanayojitokeza ktk nyumba za kuchangia. Barua zikishaletwa na watumishi wa Royal Mail, hupitishwa ktk kitundu kidogo kilichoko ktk mlango wa mbele. Mara nyingi ktk nyumba za kuchangia sio wakazi wote wa nyumba huwa wapo nyumbani wakati wote, na kwa hiyo barua hukusanywa toka pale chini ya mlango na yeyote aliyepo nyumbani kwa wakati huo. Baadhi yetu uaminifu wetu ni mdogo na inatokea mara kwa mara barua hupotea kwa mazingira ya kutatanisha! Hapa tatizo linakuwa ni mtu kufungua na kusoma barua isiyomhusu na kuitupa. Hii hutokea kwa barua zenye statement ya akaunti za benki au bank/credit cards, risiti ya malipo kazini (pay slip), n.k. Sijui ni kwa nini watu wengine hupenda kufungua barua ama nyaraka za siri za mambo yasiyowahusu! Ubongo na uafrika wetu haupotei hata kama mtu anaishi Ulaya!! Kwa hili inabidi tubadilike kifikra na kiupeo, maana wengi wa wanaoishi hapa toka nje ya Ulaya (mfano Afrika) ni wasomi tena wa kiwango cha elimu ya juu.

Wazawa wa UK wanapenda sana michezo na utamaduni. Michezo ipo mingi sana. Na michezo yenye ushabiki wa kiwango kikubwa ni kama mpira wa miguu, mpira wa ragbi, tennis, mchezo wa kriketi, mbio za magari, pikipiki, farasi na mbwa. Ktk michezo hii watu hupenda kucheza kamari za kubashiri matokeo ktk michezo mbalimbali.

Ktk uwanja wa habari ndugu zetu hawa hawako nyuma. Kuna vituo vingi sana vya televisheni na redio. Ktk tv kuna stesheni za bure na za kulipia (za kulipia ni nyingi zaidi na hurushwa kwa kupitia satellite na cable). TV za bure huruhwa kwa njia ya kawaida (terrestrial). Mtu yeyote mwenye tv anaweza kupokea matangazo ya bure ya tv ktk mtindo wa 'analogy' au pia mtu anaweza kuyapata kupitia box (freeview box) ambalo hupokea matangazo ya tv na redio ktk hali ya 'digital'. Free view box in stesheni (channels) zaidi ya 50. Stesheni za bure ktk tv ni kama ifuatavyo: BBC One, BBC Two, ITV, Channel 4 na Channel 5. Hata hivyo hakuna cha bure ktk kuangalia tv. Mtu yeyote anayetumia TV ya rangi au 'black and white', DVD player/recorder, Video player/recorder n.k. ni lazima alipe leseni ya TV (TV Licence) kwa BBC ambayo ni Paundi za Uingereza 145 (GBP 145) kwa mwaka, pia inaweza kulipwa kwa awamu kulingna na uwezo wa mtumiaji. Hii hela ndiyo inayotumiwa na BBC kuendesha shughuli zake pamoja na mishahara ya wafanyakazi wake. Na ndio maana Stesheni zote za BBC (radio na TV) huwa hazina matangazo ya biashara. Mapato ya BBC ni kupitia karo (fee) ya leseni ya TV ambayo hulipwa na kila familia UK.

26 May: Blog is 2 yrs (Happy Birthday!)

This is the 109th post in this blog. And I am glad to announce that today 26 May 2009 the blog is marking its second anniversary!

Uuuu ye, I wish you a happy birthaday,
uuuu uuuye many many happy returns* ....


*Sophia George song

Friday 22 May 2009

"Jengeni kwenu kwanza ..." - Kikwete

Friday, 22/05/2009
Rais Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa wajibu mkubwa wa Watanzania wanaoishi nchi za nje ni kufanya jitihada za kujenga na kuendeleza kwao, ili kuthibitisha ubora wa kuishi kwao nje.

Rais amesema kuwa na wala Watanzania hao wasihangaike na kutafuta jinsi ya kusaidia kuendeleza miradi mikubwa ya maendeleo kwa sababu shughuli hiyo ni wajibu wa Serikali na wanaweza wasiwe na uwezo wa kushiriki katika kuendeleza miradi hiyo mikubwa ya maendeleo.

“Mkiweza kupata mwekezaji mzuri, leteni tu. Mkipata mtu mwenye fedha za kusaidia ujenzi wa miradi mikubwa kama mabarabara na shule leteni, lakini ushauri wangu mkubwa kwenu ni huu… jengeni na endelezeni kwenu kwanza, ili mthibitishe kwa nini ni bora kuishi nje,” Rais Kikwete amewaambia Watanzania wanaoishi katika eneo la Kusini mwa Jimbo la California.

Akizungumza na Watanzania hao leo, Jumanne, Mei 19, 2009, kwenye Hoteli ya Beverly Hills Hilton mjini Los Angeles, Rais Kikwete amesema:

“Ujumbe wangu kwenu ni kwamba msisahau kwenu. Wathibitishie mliowaacha nyumbani kuwa ni bora zaidi kuishi huku mliko kuliko nyumbani. Jengeni kwenu, endelezeni kwenu. Msije kufikia mahali mnarudi nyumbani mkakosa hata mahali pa kufikia,” amewaambia Watanzania hao wanachama wa Chama cha Watanzania Wanaoishi Kusini mwa California.

Rais amewasisitizia Watanzania hao wakati akijibu maswali yao: “Tengenezeni kwenu. Haya makubwa ya ujenzi wa mabarabara, tuachie sisi wa Serikali, ndio maana tupo. Hatutaki kuwasumbua kwa masuala ya ujenzi wa barabara na shule. Hii ndiyo kazi na wajibu wetu. Nyie jengeni kwenu, ili ndugu zenu wajue kuwa kuishi kwenu nje kuna maana.”

Rais Kikwete ambaye amekutana na kuzungumza na Watanzania hao baada ya kuwa amewasili mjini Los Angeles akitokea mjini San Francisco ambako alianzia ziara yake ya Marekani pia ametumia muda mwingi kuelezea mambo makubwa yaliyofanywa na Serikali yake ikiwa ni pamoja na ujenzi wa shule 2,700 za sekondari katika miaka mitatu iliyopita.

Rais amezungumzia mafanikio makubwa yaliyopatikana katika sekta za elimu, afya, ujenzi wa barabara, akisisitiza kuwa, kwa mfano, kiwango cha malaria nchini kimepungua kwa kiasi cha asilimia 38 katika miaka mitatu kutokana na maamuzi ya Serikali tokea iingie madarakani.

“Ni kweli kuwa malaria inabakia ugonjwa unaoua watu wengi zaidi nchini, lakini hatua tulizozichukua katika miaka mitatu, minne iliyopita, zimepunguza kiwango cha malaria kwa asilimia 38. Katika Zanzibar ni kama tumemaliza ungonjwa huo kabisa.”

Rais pia amewaeleza Watanzania hao kuhusu mpango mkubwa wa Serikali kujenga zahanati kila kijiji na kituo cha afya kila kata nchini akiongeza:

“Hata kwa yale magonjwa ambayo tumekuwa tunalazimika kuwapeleka watu nje, tunachukua hatua. Kwa mfano, Wachina wamekubali kutujengea hospitali kubwa ya kutibu magonjwa ya moyo.”



(Source: Ikulu Mawasiliano (Blog). Tuesday, May 19, 2009)

Thursday 21 May 2009

Ushauri mnyenyekevu

Alhamis, 21/05/2009
Juma hili nilitembelea ubalozi wetu pale Stratford Place, jijini London. Nilifurahi kuona nyumbani kwetu 'mbali na nyumbani', maana pale ndio kimbilio; kwa mema au mabaya! Pale ndio baba, ndio mama, ndio mjomba na ndio kila kitu.

Nilifurahi pia kuona wafanyakazi wakarimu na wachapakazi.

Kwa vile pale ni nyumbani, sio vibaya kutoa maoni au ushauri wa kinyenyekevu (polite advice).

1. Nje: Ngazi za kuingia kwenye basement (eneo la hati za kusafiria) pamoja na eneo chini ya ngazi hizo za chuma panahitaji matengenezo au matunzo mazuri zaidi (TLC). Pale chini ya ngazi sio pasafi na panaonekana kama ni 'ka-stoo' ka kienyeji. Nashauri makorokoro yote pale chini yaondolewe na ukarabati mdogo ufanike na pia kupiga rangi kidogo ili papendeze. Marumaru sakafuni nazo zitupiwe macho ili ikiwezekana zishughulikiwe. Lile eneo la ngazi na 'landing yake' ni muhimu sana kwa kutangaza sura (image) ya nchi yetu. Ndio maana nashauri lifanyiwe kazi ili kuliinua kimuonekano. Zile railings za nje nazo zipigwe 'soap-soap' kidogo!
Pale mahala (ubalozini) pako karibu kabisa na mtaa ulio-bize wa Oxford na pia kituo cha treni za ardhini (Bond Street) kiko pale mlangoni kabisa!

2. Mlangoni: Mlango wetu pale 'basement' sio wa kiwango kinachostahili (hadhi ya ubalozi). Nilipokuwa nabisha hodi na kuingia ndani, vipeperushi vilidondoka kwa ndani. Kumbe vilikuwa vinaning'inia kati ya upenyo wa mlango na fremu yake. Hii inaonyesha kuwa kuna watu ambao hutembeza na kudondosha vipeperushi vya biashara ktk milango ya nyumba (note: ni kawaida kwa Uingereza kitu kama hicho)! Ila mimi nadhani ubalozi wetu hauwezi kuwaruhusu wachuuzi wa mitaani kudondosha 'vikaratasi' au vipeperushi vya kibiashara/matangazo ndani ya ofisi ya ubalozi wa nchi. Wote tunaelewa mahala pale ni nyeti. Kwa hiyo tuwe makini na hilo.

3. Ndani: Nitaongelea 'interior design'. Kuna kuta nyingi mno zisizo na sababu. Mfano ukuta kati ya meza za maulizo na pale wateja husimama. Nashauri ule ukuta na kidirisha chake viondolewe kabisa, na badala yake iwekwe meza iliyonyanyuka kama mita 1.2 kutoka usawa wa sakafu na wafanyakazi watumie viti virefu au wasimame. Pia ukuta kati ya kile chumba cha mapumziko na meza ya maulizo uondolewe. Kwa kuafanya hivyo eneo litaonekana kubwa na kutakuwa na mwanga wa kutosha pale ndani. Kwa sasa mtu akiingia panaonekana pafinyu sana na mwanga sio mzuri kwa standard ya ofisi. Na panaonekana pamejengwa kwa 'scale' ya nyumba ya kuishi (residential) na sio public space!

4. Ndani. Matangazo na 'Info': Pale maulizo pawekewe tray ya vipeperushi vya huduma mbalimbali zinazopatikana hapo ofisini. Hii itasaidia kuondoa utata wa maelezo ya wafanyakazi. Mfano mfanyakazi mmoja anaweza kukupa maelezo fulani (Facts) na mwingine akakupa ukweli mwingine! Naelewa hii inaweza kutokea kwa bahati mbaya, lakini kama kuna vipeperushi, ni rahisi kwa mfanyakazi kumpa mtu kipeperushi kwa ajili ya rejea anapokuwa na shida wakati wowote. Na pia tukumbuke kuwa sio kila mteja wenu anaewatembelea anapata huduma ya mtandao (internet). Kwa hiyo tusiwalazimeishe wateja wetu kwenda kusoma website kwani hiyo sio njia pekee ya kupata habari za ubalozi wetu.

Mwisho ninawapongeza wafanyakazi wote pale ubalozini kwa kazi nzuri wanayoifanya. Wanao ushirikiano wa hali ya juu na watanzania walioko nje ya nchi, na hiki ndicho kitu muhimu zaidi. Pia wanajitahidi kwa uwezo wao wote kuitangaza nchi yetu kwa nafasi walioyo nayo. Inawezekana kuwa moja ya matatizo makubwa yanayowakabili ni ufinyu wa bajeti, kwa hiyo tusiwe wepesi kuwarushia makombora ya lawama. Na wanaweza kuwa wanafanya kazi ktk mazingira magumu. Kwa ujumla kazi yao inaridhisha kwa kiwango kizuri. Hongera pia balozi wetu Mama Maajar, wewe ni shujaa na tunakupenda!

Wednesday 20 May 2009

'Hapo zamani ...'

Jumatano 20/05/2009
Nakumbuka zile hadithi ktk vitabu nilizozisoma wakati nilipokuwa mdogo. Karibu kila kitabu nilichosoma kilianza na huu msemo; 'hapo zamani za kale paliondokea ....'

Hasa nakumbuka hadithi za kitabu fulani kilichokuwa na hadithi 3 nzuri! Sura ya kwanza ilikuwa na kichwa 'Mkataa pema pabaya panamwita'. Sura ya pili ilikuwa na ' ... jamani fungeni mkutano wengine zimeyeyika' - ile ambayo fisi alihudhuria mkutanao wa wanyama wenye pembe huku yeye akiwa amejiwekea pembe bandia na kugundisha na nta. Muda ulipokwenda sana nta ikaanza kuyeyuka na akahofia kuwa 'pembe' zitadondoka na hivyo akatoa hoja mkutano ufungwe! Sura ya tatu ilikuwa na kichwa 'usitukane wakunga na uzazi ungalipo'.

Kitabu kingine kilihusu hadithi za usukumani ambako kuma mtu alikuwa akisafiri anaaacha maziwa 'fresh' kwenye kibuyu au bakuli, na kwa muda wote atakapokuwa safarini 'salama' maziwa yanabakia 'fresh' na kama akipata tatizo au kufariki maziwa yanaganda! Hii ni hadithi ya Mwanamalunde. Siikumbuki vizuri ila kwa mbali nakumbuka maudhui yake!

Natamani wanangu kama angepata nakala moja ili aone tulichosoma enzi zetu tulipokuwa na umri kama wake. Na kwa kweli vitabu hivi na vingine vya aina hiyo vyafaa kuhifadhiwa kwa ajili ya kumbukumbu ya vizazi vijavyo.

Kila kizazi kinanao wajibu wa kutunza mabaki ya kumbukumbu za shughuli na maendeleo yake (legacy) kwa ajili ya vizazi vijavyo. Na huu ni wajibu wa kila mtu binafsi na wadau mbalimbali! Kwa kuanzia mie nina kumbukumbu za kazi zangu zote za darasani (daftari za mazoezi na karatasi za mitihani) kuanzia nilipokuwa darasa la kwanza elimu ya msingi. Na bado ninaendelea kuhifadhi kumbukumbu zaidi za kazi zangu. Tayari mwanangu ameshaanza kunicheka sana kila anapoona kazi yangu ya darasa la pili (analosoma sasa), kwa sababu anaona nimekosa maswali rahisi mno au mwandiko wangu wa ajabu enzi hizo! Nadhani mwanangu atajifunza kutokana na makosa yangu kama anavyoyaona mwenyewe kwa macho yake bila kusimuliwa au kuambiwa!

Tuesday 19 May 2009

Tumege uzoefu wa wazee wetu

19/05/20009
Ni rahisi kusikia mashirika yanaanzishwa kusaidia kina mama fulani -wajane kwa mfano, au walioachika au waliokatiza masomo yao n.k. Pia yapo ya kusaidiwa watoto ambao mara nyingi wanatokana na matatizo yaliyowapata kinamama hapo juu.

Nadhani wakati umefika kuwakumbuka watu wazima hasa wastaafu ambao wameamua kupumzika kwa sababu za kiafya au kisheria (umri wa kustaafu).

Wazee wetu hawa wanapoacha kazi, mara nyingi huwa wanabaki kuwa wapweke sana. Walizoea kutoka kila asubuhi na kurudi nyumbani jioni au usiku lakini inapotokea siku ya siku imefika na wakastaafu mabadiliko haya ya ghafla huwagharimu sana kifikra.

Ni vema ndugu zetu hawa nao wakakumbukwa hasa ktk namna ya kuwafanya waendane na hali halisi ya mabadiliko ya kimajukumu. Hapo nazungumzia afya ya akili.

Ushauri wangu ni kwamba serikali za mitaa zikisaidiana na asasi mbalimbali waanzishe vyombo (facilities) vya kusaidia kuwajumuisha watu wa kundi hili ili wajione wako ndani ya jamii. Wastaafu walio wengi kwa kweli hujiona kama ndio umuhimu wao ktk jamii umefikia ukingoni. Ni jukumu la kila mwanajamii kuhakikisha wakubwa zetu au wazazi wetu hawa wanaonekana kama wenzetu na kuwa mchango wao ktk jamii bado unahitajika, tena zaidi.

Ebu tuangalie namna ambayo tutachuma uzoefu wao kimaisha ili utusaidie ktk maendeleo yetu kwa ujumla. Tusiwaachie maarifa yao wakae nayo peke yao. Kundi hili ni muhimu sana ktk jamii na lina mengi ya kutusaidia. Kwa hiyo tusilale, tuwahusishe ktk mambo yote ili nasi tuupate uzoefu na utajiri wa fikra zao njema. Kwa kufanya hivi tutakuwa tunawasaidia kuwaweka 'fit' kiafya (mwili na akili) na bila shaka watafaidi maisha na kurefusha maisha yao pia.

Lakini yote haya tutayapataje ikiwa kila mstaafu yuko nyumbani kwake na familia yake? Mimi nasema, tunahitaji vituo vya kutukutanisha wote ili waweze kutoa mchango wao chanya. Serikali za mitaa na asasi za binafsi zina nafasi kufanya kitu cha maana hapa.

Hivyo ndivyo nionavyo mimi kwa ufupi tu.

Umuhimu wa maktaba

19/05/2009
Mbali na kutenga maeneo ya bustani za kustarehe ktk miji na vitongoji, maktaba ni sehemu murua pia kwa watu kupumzika huku wakijisomea vitabu magazeti na kupitia mtandao wa kompyuta.

napendekeza kuwa kila kata nchini iwe na maktaba yake kwa manufaa ya wananchi. Ipo kasumba kwamba baada ya masomo ya elimu ya msingi au sekondari basi hakuna tena kusoma au kujisomea.

Maktaba zinasaidia kuwafanya watu wawe na nguvu (active) hasa kutokana na kuchamsha ubongo ambao ndio dereva wa shughuli zote za viungo vya mwili. Akili ikichangamka mtu hupata furaha lakini ikidumaa mwili huchoka na kuweza kukata tamaa haraka.

Pia maktaba ni sehemu ya watu kukutana na kujuliana hali, kitu muhimu sana ktk jamii.

Watoto wetu pia watapata nafasi kujisomea, kujifunza pamoja au kucheza na wenzao wakutanapo maktaba. Na maktaba zinapokuwa karibu na maeneo tunayoishi inakuwa rahisi kwa kila mmoja wetu kuzitembelea kwa vile hakuna haja ya kusafiri masafa marefu (kitu ambacho hukatisha tamaa kwa wengi wenye nia ya kujiendeleza au kupata huduma za husika)

Chagua Finias Magesa kuwa MBUNGE

19/05/2009
Kwenu wana Busanda. Uchaguzi ujao mpigieni kura Finias Magesa;
-Mchapakazi (anafanya kazi kwa kuipenda sio 'bora liende')
-Mpenda maendeleo
-Mpenda mabadiliko ya kimaendeleo
-Mwakilishi na mtetezi imara popote atumwapo
-Mwaminifu, msikivu na mcheshi
-Mwenye upeo wa hali ya juu ktk masuala mbalimbali ya kitaifa na kimataifa, kisiasa na kisayansi + teknolojia yake.

Hakika Busanda itamfaa Finias na Finias ataifaa Busanda.

Nampitisha kuwa anafaa kuwawakilisheni Bungeni.

Mpeni kura muone matunda ya kazi yake! Atasaidia kusukuma gurudumu la Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii kwa ujumla sio hapo jimboni pekee bali pia TAIFA litanufaika na mchango wake ktk jukwaa la siasa akiwa kama Mbunge au hata Waziri ndani ya serikali zijazo!

Huo ni ushuhuda wangu kuhusu huyu mgombea Finias Magesa, na ndio maana nawaomba mmkubali awe mwakilishi wenu Bungeni siku ya Jumapili.

Kamwe hamtajutia uamuzi wa kumchagua Finias MAGESA.

Busanda Oyeeeee! Tanzania Oyeee!

Message to Busanda constituents

Tue 19/05/2009
As you understand, this coming Sunday you will be voting for your next Member of Parliament.

I am not from Busanda, but I know someone from Busanda who can work for you.

You need someone whom you can trust, see and contact as freely and conveniently as you would like.

I know someone who;
- can work with you to sort out problems and bring success,
- can present your issues, views, requests and questions before the government,
- is tireless, intelligent, brave and honest,
- you've been longing for!

This is none other than MAGESA, Finias.

Remember, the formula to get Finias Magesa as your MP is very simple -just vote for him on Sunday. Do not stay at home. You have vote to get him.

If you vote Finias Magesa, Busanda won't be the same again.

Here comes the change. We all need change. Don't let it passby.

Finias Magesa is the man to bring the change!

Vote for MAGESA, Finias on Sunday, 24 May 2009
..........................................................

M

Tuesday, May 19, 2009
Yesterday this small blog marked its 1,000th post since it was born (May 26, 2007), -exactly ONE week before its second anniversary. This is an historic milestone and/or an achievement of some sort.

Entries are seldom prepared in advance. Therefore, mistakes or errors are inevitable. However, I always try to present my views, comments or points of support in an honest way.

As the journey of life continues, this small blog will also be on the move. It won't lag behind at all.

The first 500 posts milestone was marked on Tuesday May 06, 2008. This reading shows that only 500 posts are managed per year. NOT a bad record, is it?

Monday 18 May 2009

'Mama' la madai yote!

Ktk sakata la kisiasa linaloendelea ktk visiwa vya Uk kuhusiana na madai 'hewa' au 'feki' ya gharama za matumizi ya wabunge ktk shughuli zao za kikazi, hii ya waziri wa mambo ya ndani ni kali zaidi.

Mume wa waziri huyo wa mambo ya ndani (home office) aliangalia picha za ngono za kulipia ktk luninga na kisha mke wake (ambae ni mbunge/waziri) akaenda kudai bungeni arejeshewe hela yake (paundi 10 za kuangalia picha 2 za ngono)!!!

Waziri anadai kuwa alipitiwa kwa bahati mbaya kuambatanisha risiti ya mambo ya ngono ktk madai.

Hata hivyo sijui kama waziri huyo atapona panga la waziri mkuu, ktk mabadiliko ya baraza la mawaziri yanayotarajiwa kufanyika baada ya uchaguzi wa serikali za mitaa na wabunge wa bunge la ulaya hapo Juni 04 mwaka huu ambapo chama tawala cha Labour kinatabiriwa kuanguka vibaya ktk chaguzi hizo.

Kwa habari zaidi kuhusiana na madai ya wabunge yasiyo na kichwa wala miguu, fuatilia matoleo ya gazeti la 'the daily telegraph'!

Blame game

Monday, May 18, 2009

................................
'when I was leader of the trade unions, I blamed the management
when I was leader of the opposition, I blamed the government
when I was the government, I blamed Europe and America'
-UK PM Gordon Brown, quoting the Brazil president
10:32 BST, April 01, 2009
................................
'some are to blame, but all are responsible'
-Brack Obama, US President in London
10:33 BST, April 01, 2009
.................................

Champs 2008/09: Glory, glory Man United

Manchester United are English Premier League champions (sponsored by Barclays) for the 18th time.

..............
01. 1907/08
02. 1910/1911
03. 1951/52
04. 1955/56
05. 1956/57
06. 1964/65
07. 1966/67
..............

under Sir Alex Ferguson (below)
08. 1992/93
09. 1993/94
10. 1995/96
11. 1996/97
12. 1998/99
13. 1999/00
14. 2000/01
15. 2002/03
16. 2006/07
17. 2007/08
18. 2008/09

Manchester United Player of the year Awards 2009

Monday May 18, 2009
Yesterday Manchester United players had an enjoyable night. It wasn't a party to celebrate the 2008/09 Premierships title per se, but the one for the recognition of outstanding individual players throughout the season voted by fans or players themselves. The Awards ceremony was shown live by Manchester United own TV Channel (MUTV) from 19:30 BST.

And the winners are...

Nemanja Vidic - Sir Matt Busby Player of the Year. (voted by fans).
Nemanja Vidic - Players' Player of the Year.
Cristiano Ronaldo - Goal of the Season, v FC Porto. (voted by fans).
James Chester - Denzil Haroun Reserve Player of the Year
Federico Macheda - Jimmy Murphy Academy Player of the Year

Vingunge wetu eee, wapi vitendo?

Mzee wa Changamoto ameniunga mkono kuhusu tabia za viongozi wetu kupiga domo tu bila kuzingatia hali halisi ya maisha ya mwananchi na ahadi hewa kila baada ya miaka mitano (wanaonekana kabla/kwenye kampeni za chaguzi, na baada ya chaguzi wanatokomea!)
Kuna vitu vingine ni vidogo sana lakini vya muhimu kwa maisha ya mwananchi. Sio vizuri kuvipuuza kwa sababu ya udogo wake. Kinachotakiwa ni usimamizi wa karibu, uwepo wa sera zenye umakini, uaminifu kitaaluma (professionalism) na utekelezaji wa ahadi kivitendo. Wananchi sio wajinga, wanaelewa kile kinachosemwa na viongozi wetu na pia wanajua kutofautisha mbivu na mbichi!

..............................................

Mzee wa Changamoto anena zaidi:

Amani, Heshima na Upendo kwako Ndugu.
Wanachonishangaza Ndugu hawa wakuu ni namna ambavyo wanaangalia "nje ya ulingo waliomo" ambao ndio uliooza.
Hakuna atakayegoma kukaa kijijini kama huduma zote muhimu zitapatikana. Kama kutakuwa na mazingira ya kumfanya aweze kuuza japo bidhaa zake. Lakini wanaendekeza siasa na kujiandaa kusikika kuliko kutekeleza. Hashangai kwanini watu wanauza pombe badala ya shughuli ambazo wao wanaweza kudhani ni za kuwapatia kipato zaidi? Hawaoni kwanini watu wamechoka kuwasiliza, wanawazomea na kuwaona waongo kama niwaonavyo mimi. Ni kwa kuwa wanasema wakijua TBC iko pale lna hakuna atakayehoji wala kutaka ufafanuzi wa ahadi walizotoa wiki mbili zijazo.
Ni upuuzi kuona Waziri Mkuu hamuwajibishi mkuu wa sehemu hiyo (awe wa wilaya ama mkoa) kujua ni kipi kinachokwamisha maendeleo ya wananchi.
Ni lazima tuwe na mikataba, kuwa mtu anapokubali kuchukua kazi kama ya ukuu wa mikoa awe na ahadi ya kufanya vitu kadhaa ndani ya muda fulani, na akishindwa na aachie ngazi. Wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya ni kati ya watendaji wabovu zaidi nchini Tanzania.
Waziri aanze na wasaidizi wake kabla hajawaendea wale walioshindwa kuwezeshwa wakaamua kujiwezesha.
Shukrani kwa kazi njema

believe in yourself

"be yourself; you can not be somebody else!"

Friday 15 May 2009

Hii sio haki

Ijumaa mei 15, 2009
“.... Pombe zote hakuna kuuzwa katikati ya wiki isipokuwa Jumapili na siku za sikukuu, ni lazima turudishe nidhamu ya kilimo bora, kilimo cha kufa na kupona,” alisema Waziri Mkuu (Mizengo Pinda).

Kama pombe anazozungumzia mheshimiwa WM ni halali, basi hakuna haja kuwapiga vita wajasiamali wanaopika pombe hii. Hii ni biashara ya mtu inayompa kipato cha kuhimili gharama na makali maisha kila siku.

Waziri mkuu anapopiga marufuku pombe, hakomoi wanywa pombe bali pia wapika pombe ambao hutegemea kipato kupitia hiyo biashara.

Enzi za kulazimisha watu kulima ilishapitwa na wakati. Serikali isaidie ktk kuandaa au kuweka mazingira ya kuvutia kilimo vijijini ili mwananchi aweze kuwekeza mali, nguvu na muda wake ktk kilimo kwa hiyari yake. Kadhalika serikali iwe na mkakati endelevu wa kutoa ruzuku ktk bei za pembejeo za kilimo ili wananchi wajikomboe na kuinama shambani kwa kutumia jembe la mkono au la ng'ombe.

Sio busara kuswaga watu kwenda shambani pasipo kuwaandalia mazingira mazuri ya kupenda kilimo. Ktk hotuba ya WM sikuona anataja suala la mapinduzi ya kilimo kwa utumiaji wa mashine za kisasa ili kuwarahisishia wananchi utendaji kazi za shambani.

Ni nani apendaye kupinda mgongo shambani kwa kutumia zana za miaka ya sitini? Na kwa serikali yetu, acheni kuwatisha wananchi, cha muhimu ni serikali kuwasaidia ktk kufanya mapinduzi ya kilimo.

Hapo ndipo kila mtu atapenda kwenda shambani.

Finias Magesa for MP Busanda!

Friday May 15, 2009
Honourable Finias Magessa: Is this the one I know? UDSM graduate, BSc Mechanical Engineering in the late 1990s, a friend of my friend Ernest Mayombya?

If that's the case, I congratulate you for earning the nomination via your party ticket (chadema) and wish you all the best, mate!

Kaka Miye!

Ijumaa Mei 15, 2009
Miaka ya 1980 nilikuwa napenda kupitia makala za Kaka Miye, ukurasa mmoja maarufu enzi hizo ktk gazeti la Jumapili la Chama Cha Mapinduzi (Mzalendo).

Sijui kama siku hizi makala hizo zinaendelea.

Pia Radio Tanzania (RTD) nao walikuwa na vipindi fulani vya ucheshi - Mahoka, sijui kama navyo viko hewani ktk muundo wa TBC ya sasa. Bahati mbaya hawa TBC hawana tovuti, ningeweza kufuatilia vipindi vyao vyote!

Tuesday 12 May 2009

FACT: Men and sex!

.................................
'guys think about sex every 5 minutes'

source: smokefree guide; no chance get lucky (NHS), page 8
................................

Maajabu: Mbwa anavyothaminiwa!

Tuesday, May 12 2009
Nimeshawahi kuandika mara kadhaa kuhusu mbwa wa Ulaya hasa Uingereza wanavyothaminiwa na hata kuliko binadamu. Sina haja kurudia hayo kwa leo, ila hebu sikia mkasa uliotokea wiki hii.

Bwana mmoja, mkewe pamoja na mtoto wao mchanga wa miezi saba na mbwa wao wawili walikuwa matembezini kando ya mto. Mara mbwa mmoja akajirusha mtoni, na wa pili nae akaingia mtoni. Mto ulikiwa umejaa maji na yanaenda kwa kasi baada ya mvua kunyesha siku za karibuni. Kuona hivyo, mke wa jamaa akajitosa majini kuokoa mbwa. Unajua maji yatiririkayo mitoni huku Uingereza ni ya ajabu sana. Unaweza kuona kama yametuama au kina si kirefu lakini mtu akianguka mtoni mara nyingi huwa anapoteza maisha! Sababu hasa ni kuwa maji huwa yana mkondo uendao kwa kasi ambao hauonekani kwa juu. Pili maji huwa ni ya baridi sana kiasi kwamba hata kama mtu ni mtaalamu wa kuogelea, inamuwia vigumu kuhimili ubaridi na kusababisha viungo muhimu vya vya mwili hushindwa kufanya kazi ipasavyo kutokana na ubaridi - matokeo yake ni mtu kuzama na kupoteza maisha!

Baada ya mama mtu kujitosa majini, alizidiwa nguvu na mkondo wa maji na hivyo kumfanya mzee mzima naye ajitose mtoni kusaidia mama na mbwa wao! Jamaa nae baada ya kuingia majini mambo yakawa yaleyale, alizidiwa na kusombwa na maji! Wote na mbwa wao wakamezwa na kondo mkali wa mto. Baada ya jitihada za uokoaji kufanyika, mama mtu alipatikana huku akiwa hoi bin taabani, na mwili wa mzee ulipatikana mtoni baadae akiwa ameshafariki. Mbwa wao pia walikufa! Hata hivyo mama mtu nae alifariki dunia hospitalini kutokana na madhara ya ubaridi.

Kando ya mto alibakia mtoto mchanga wa miezi saba, akiwa kwenye kitoroli cha kusukumia watoto! Ndie tu aliyebaki, na bahati mbaya hawezi hata kusimulia kilichotokea maskini!!

Kutokana na mkasa huu, Waingereza wameanza kuuulizana inakuwaje wanyama wafugwao (pets) wawe na umuhimu kuliko maisha ya binadamu? Je huyu mtoto atakapokuwa mtu mzima na kusimuliwa kilichotokea atawaelewaje wazazi wake?
.....................................

Saturday 9 May 2009

Hali ngumu ya Uchumi: Bunge lifupishwe

Saturday May 09, 2009
Bunge la Jamhuri ya Muungano liko mbioni kukutana ktk marathoni ya vikao vya kujadili na kupitisha bajeti ya serikali ya mwaka wa fedha 2009/10.

Kama wote tujuavyo, hiki ni kipindi kigumu sana kiuchumi duniani kote. Ni vizuri viongiozi wetu na wawakilishi wetu wakazingatia hali tuliyonayo na kuchukua hatua za kusaidia kupunguza makali ya uchumi.

Mojawapo ya hatua za kuchukua ambazo ziko ndani ya uwezo wetu ni kufupisha urefu wa vikao vya Bunge. Kwa kawaida vikao vya bajeti huchukua miezi miwili (Juni hadi Agosti kila mwaka).

Napendekeza kwa waandaaji wa ratiba za
1. hotuba za mawaziri kuwasilisha bajeti na
2. muda wa waheshimiwa wabunge kujadili bajeti hizo,
zifupishwe kwa asilimia 10 au zaidi.

Hotuba kuu ya waziri wa fedha na wa mipango kuhusu hali ya uchumi wa nchi ndizo zipewe muda wa kawaida, lakini hotuba zote za wizara zinazofuata zifupishwe kama nilivyopendekeza kwa manufaa ya wananchi wa Tanzania.

Haitakuwa uamuzi wa busara kutumia gharama kubwa kuendesha vikao wakati huduma muhimu kwa wananchi zinayumba kwa kukosa fedha za kuziendesha. Kama wananchi wanaambiwa wafunge mikanda kila siku, inakuwaje wakubwa waendelee kulegeza ya kwao?

Kila mtanzania ana wajibu wa kubana matumizi ktk nafasi yake aliyoko, na nyie wawakilishi wetu fanyeni vivyo hivyo!

Stesheni za TV na Redio za BBC (UK)

TV
01. BBC One (24Hrs, joining with BBC News 06:00-08:30, 18:00&22:00 news bulletins)
02. BBC Two (24 Hours)
03. BBC Three (19:00-06:00) (joins CBBC 06:00-19:00)
04. BBC Four (19:00-06:00) (joins CBEEBIES 06:00-19:00)
05. BBC News (24Hours)
06. BBC Parliament (24 Hours, Pure Politics; covering Westminster (House of Commons and Lords) and Wales, Scottish, Northern Ireland Assemblies)
07. CBBC (06:00-19:00 for older children, over 6 years of age)
08. CBEEBIES (06:00-19:00 for children under 6)

Radios
01. BBC One
02. BBC 1 X-tra (music)
03. BBC 2
04. BBC 3
05. BBC 4
06. BBC 5 Live (sports)
07. BBC Spirts Extra (occassionally, to cover BBC 5 Live)
06. BBC 7
07. BBC Asia network
08. BBC World Service (Not available these days?)

BBC Parliament (mpya?)

Sat 09 May, 2009
BBC Parliament TV channel, wamebadili mfumo wa mpangilio (usanifu) na rangi za TV yao tangu April 22, 2009.
Awali walikuwa wanatumia rangi kama ya chungwa ila sasa wanatumia rangi ya udongo mwekundu sawa na ile inayotumiwa na wenzao wa BBC News (zamani BBC News 24).
Maandishi ya utambulisho yalikuwa yanaandikwa kushoto kwa screen na picha kubanwa upande wa pili, lakini sasa maandishi yote huwa chini ya picha kuu. Na kwa kusema kweli hivi sasa wanatumia mfumo na mpangilio wa BBC News.

Zile alama na rangi za 'logo' kuonyesha aina ya kikao kinachoonyeshwa hazipo tena. Kabla ya April 22, 2009 walitumia logo za House of Commons, za House of Lords, Za Wales, Scottish na Northern Ireland Assemblies kuonyesha kikao kinachoonyeshwa (sasa hazipo tena, nadhani hapo wahusika wamechemsha!)

Bajeti ya Uingereza mwaka huu ilitangazwa tarehe 22/April/2009 na waziri wa fedha wa UK, Chancellor of Exchequer mheshimiwa Alistair Darling.

Wednesday 6 May 2009

Ucheshi wa kiafrika

Wed. May 06, 2009
Ni kawaida kuona viongozi (hasa marais) kutoka nje ya nchi wanapotutembelea, hukaribishwa na wenyeji wao (rais wetu, makamu, waziri mkuu na wasaidizi wao) kwa ucheshi na ukarumu wa hali ya juu!

Pale uwanja wa ndege huwa kuna watoto chipukizi tayari kuwavisha mashada wageni wetu na pia vikundi vya ngoma, sanaa na utamaduni huwepo kuwaburudisha wageni.

Barabarani watu hujipanga msururu wakiwa na bendera za nchi yetu na za mgeni husika! Shamrashamra huendelea njiani kote hadi ikulu ambako nako hupokewa na vikundi mbalimbali na wenyeji zaidi kwa furaha na chereko!

Vyombo vya habari nchini (TV, magazeti na redio hutangaza habari za ujio wa mgeni wetu nchi nzima!

Furaha na chereko kwa mgeni huendelea muda wote anapokuwa nyumabani kwetu (nchini) hadi anapoondoka na kutia mguu kwenye ndege na kupaa, huwa tunampungia mkono na kumtakia safari njema!

Kwa kweli ukarimu wetu waafrika ni wa kweli.

Kwa upande wa pili, viongozi wetu (rais, makamu na waziri mkuu) wanaposafiri nje ya Afrika hali huwa tofauti. Kwanza Rais wetu anaweza asipokelewe na mwenyeji wake uwanja wa ndege. Pili hakuna nderemo wala shamrashamra zozote na ataelekea hotelini kwake moja kwa moja. Anaweza kuonana na mwenyeji wake kwa dakika chache au akiwa na bahati masaa machache tu, na hawaonani tena! Vyombo vya habari ndio usiseme hata havitaji au kutangaza ujio wa Rais wetu huku ughaibuni!

Mungu ametujalia wema na ukarimu, na nina uhakika wenzetu wanautamani!

Tony Blair is 56 years young today

Wed. May 06, 2009

Happy Birthday to you, Tony!

Regards,
M.R.

Tuesday 5 May 2009

Tume ya Mabomu: ongezeeni hadidu yangu!

Tuesday May 05, 2009
Serikali imeunda tume ya wataalamu kuchunguza na kubaini yaliyotokea ktk ile ajali ya mabomu ktk kambi ya jeshi kule Mbagala Kizuiani.

Hadidu rejea kwa baraza hilo ni:
1. kuchunguza na kubaini chanzo, madhara, hasara
2. kupendekeza hatua za kuchukuliwa ili kuzuia tukio kama hilo lisitokee tena.
3. kupendekeza hatua za ziada zitakazochukuliwa ili kuepusha tukio kama hilo lisitokee katika maghala mengine.

Kwa maoni yangu naona serikali ingeongeza hadidu moja nyeti. Tukio kama hili linapotokea ni nini kifanyike - kwa vile ajali haina kinga!

Nimesikitika kusoma ktk vyombo vya habari kuwa wananchi walikimbia huku na kule wasijue nini cha kufanya na hatima yake wakajitosa majini (mtoni) ambapo baadhi yao walipoteza maisha yao. Wanafunzi wa shule za msingi na watoto wadogo walitawaniyika na kutokomea kusikojulikana! Watu wazima wengine walikimbia kutafuta hifadhi maeneo ya mbali kama vile Buza!

Kwa hiyo kinachotakiwa ni kuweka utaratibu au mpango (kwa lugha ya kigeni wanaita plan) inapotokea hatari au dharura ya namna hii watu wafanye nini. Serikali kupitia taasisi au chombo husika kitoe elimu na mafunzo kwa wananchi ili kuondoa uwezekano wa raia kupoteza maisha kwa hofu tu (mfano kujitosa mtoni). Kwa hiyo nashauri mafunzo yatolewe kwa wananchi namna ya kujiweka ktk hali ya usalama (health and safety) pindi ajali za namna hii zinapotoea au hata ajali ya moto. Wakishapewa elimu na mafunzo, ni vizuri pia kuwa kila baada ya kipindi fulani, mathalani miaka 3, wawe wanapigwa msasa na kufanya majaribio (drills) ili kujiweka ktk utayari kukabiliana na maafa. Hii ni muhimu sana hasa wananchi wanaoishi maeneo yanayozunguka kambi za majeshi yetu ya ulinzi na usalama.

Wananchi waelemishwe pia jinsi ya kutoroka (how to escape) moto unapotokea majumbani au maeneo ya kazini na maeneo ya kukusanyika yaeleweke (assembly point) ili watu waweze kujuana ni nani ametoka ndani na ni nani amebakia ndani ya nyumba au jengo. Hii staili ya kuondoka baruti kila mtu kivyake sio nzuri, kwa sababu ni vigumu (hasa kwa zimamoto) kujua kama wanaokoa maisha ya watu (rescue) ktk jengo ama ni jengo tupu linawaka! Hii ni muhimu sana -hasa kwa usalama wa wazima moto. Kama hakuna mtu ndani ya jengo wana-zimamoto hawatakuwa na haja ya kuhatarisha maisha yao kuingia ndani ya jengo kutafuta watu 'walionaswa' ndani ya moto. Lakini huyu zimamoto atajuaje kama ndani ya jengo au nyumba inayoungua kuna mtu au watu kama kila mtu alitoka na kutokomea kusikojulikana? Hii ilitokea katikati ya jiji baada ya mlipuko wa mabomu, wafanyakazi walijitokea kiennyeji na kwenda wanakotaka wenyewe (nadhani hakuna walioitisha majina ya wafanyakazi waliotoka ndani ya jengo (roll-call)). Kwa hiyo kama maofisi yangeporomoka ingekuwaje, wakati wengine wako wanakojua wenyewe?

Ndio maana nasema hii tume itoe mapendekezo ya ni nini cha kufanya kwa wahanga endapo tukio kama hili au la moto mkubwa litatokea tena? Hatuwezi kusema kwa uhakika kuwa tukio kama hili au la aina hiyo haliwezi kutokea tena kwa sababu hii ni ajali (ni nani ajuaye ajali itatokea lini!). Kwa hiyo tujiandae na kisichotarajiwa. Na je kitakapotokea kisichotarajiwa wananchi tufanyeje?

Mimi naamini jibu sio kutokomea mitini!

Sorry, I have got Mine!!!*

Hello….Saturday, May 2, 2009 9:39 PM

From: "jackline francois"
To: undisclosed-recipients

Hello,

My name is Jackline Francois I am 23 years old (Vig), Single, Native of American, Caucasian, Female, 5'11" (149cm), 105lbs (47kg), located in Baltimore, Maryland United States. Christian by religion. I'm a full time Student and I'm majoring in marketing and getting a minor in International financing.

My body style is average weight I am physically active, I never smoke and drink. I am the only girl in the family of three children,I am the second child. My father and mother are still alive. My father is 55 years old, while my mother is 48, My elder brother is 26 and younger brother is 20. Get in touch at


jacklinfran08@yahoo.com

With Love,
JACKLINE FRANCOIS.


*letter via my e-mail address, to unnamed and loved(?) recipient!
(NOTE: this is from con-men, be careful!)

Saturday 2 May 2009

Fixtures (Man Utd): May 2009

May 2009
02 May Barclays Premier League Middlesbrough A 12:45 W 2-0 giggs, park
05 May UEFA Champions League Arsenal A 19:45 W 3-1 park, ronaldo(2);(aggregate:4-1)
10 May Barclays Premier League Man City H 13:30 W 2-0 ronaldo, tevez
13 May Barclays Premier League Wigan A 20:00 W 2-1 tevez, carrick
16 May Barclays Premier League Arsenal H 12:45 D 0-0 Man Utd Champions 2008/09
24 May Barclays Premier League Hull City A 16:00 W 1-0 Gibson
27 May UEFA Champions League Barcelona N* 19:45 L 0-2

*Roma: Stadio Olimpico, Italy

Fixtures updated 16 April 2009. Fixtures are subject to change and may be selected for live TV broadcast (and subsequently not played at 15:00 Saturday). Fans are strongly advised not to make travel or accommodation arrangements too far in advance.

(courtesy: www.manutd.com)