Friday 29 June 2007

Man Utd: Goals 2006/07*

ROONEY- 25
RONALDO- 24
SAHA- 13
SOLSKJAER- 11
SCHOLES -7
GIGGS -6
CARRICK -6
O'SHEA -5
J S PARK -5
VIDIC -4
K RICHARDSON -3
FLETCHER -3
LARSSON -3
EVRA -2
FERDNAND -1
SYLVESTRE -1
K LEE -1
HEINZE -1
BROWN -1
SMITH -1
C EAGLES -1

Goals came from a variety of players, except goalkeepers. It is good to get scorers from different sources, rather than depending on specific players!

*Matches involved are:
Premieship
FA Cup
League Cup
UEFA Champions League
Man Utd v. Europe IX Friendly on 13/3/2007 where Man Utd won 4-3. Rooney's double, Ronaldo and Wes Brown won the match.
A total of 124 goals were scored.

By Mosonga

Man utd: 2006/07 General Perfomance

August 19 - December 23, 2006
P W D L F A Pts
19 15 2 2 41 10 47

Dec 23, 2006 - May 13 2007
P W D L F A Pts
19 13 3 3 42 17 42

The first half performance of the season gave Man Utd the Title without any doubt! Also the December performance was crutial for the title charge. I always believe if the team does well in December and April -May there is the great chance to take the title (Premiership).
Hopefully this coming season again Man Utd can do the same to make it a double!!
By Mosonga

Kifo cha Amina Chifupa (MB -Vijana CCM)

KIFO CHA AMINA CHIFUPA…
Bunge laahirisha shughuli zake
Na Mwadini Hassan, Dodoma
BUNGE la Jamhuri ya Muungano, jana liliahirisha shughuli zake zote kwa heshima ya Mbunge wa Viti Maalum, Amina Chifupa, aliyefariki dunia juzi.Ukumbi mzima wa Bunge mjini hapa, ulilizima simanzi baada ya Spika wa Bunge, Samuel Sitta, kuwatangazia wabunge kifo cha mbunge huyo aliyekuwa akiwakilisha vijana. Ujumbe wa wabunge wasiopungua 32 ukiongozwa na Spika Sitta, uliondoka hapa jana saa nane mchana kwa ndege maalum ya kukodi, kwenda Dar es Salaam, kuliwakilisha Bunge na serikali katika msiba huo.“Kwa masikitiko makubwa nawatangazia kifo cha mbunge mwenzetu, Amina Chifupa, kilichotokea jana (juzi) saa 2.43 usiku katika hospitali ya jeshi Lugalo, Dar es Salaam. “Katika dakika zake za mwisho baba yake mzazi, mama yake mzazi na mumewe walikuwa naye,” alieleza Spika mara baada ya kusomwa dua za kuiiombea nchi na Bunge, wakati bunge lilipoanza shughuli zake saa tatu kamili asubuhi.Wakati tangazo hilo likiendelea, baadhi ya wabunge akiwemo Spika mwenyewe, walionekana wakifuta machozi, na baada ya tangazo hilo bunge liliahirishwa kwa saa moja hadi saa nne asubuhi, kutoa nafasi za kufanya maandalizi ya Bunge kwa msiba huo.Baada ya kuahirishwa bila kuwepo kipindi cha maswali na majibu, baadhi ya wabunge walishindwa kujizuia na kulia kwa sauti ndani ya ukumbi, na hasa wabunge wanawake, ambao baadaye walikutana kwa kikao cha dharura.Kamati ya Uongozi na Tume ya Huduma za Bunge, zilikutana mara moja baada ya Bunge kuahirishwa kupanga taratibu zitakazofuata kufuatia msiba huo.Bunge liliporejea katika kikao chake saa nne asubuhi, Spika alitangaza kwamba kikao cha Kamati ya Uongozi na Tume ya Huduma za Bunge kimeamua: “Baadhi yetu twende Dar es Salaam leo (jana) saa nane mchana, tukaungane mkono na familia ya marehemu kuwafariji kwa msiba huu."Tumeamua tuwe na uwakilishi wa vyama vya siasa, uwakilishi wa maeneo ya nchi, kwa maana ya Tanzania Bara na Zanzibar na maeneo ya kijinsia," alitangaza Spika huku ukumbi ukiwa katika ukimya mkubwa na majonzi yakionekana nyusoni mwa wabunge ambao baadhi yao walikuwa wakifuta machozi."Wabunge wanawake wamepitisha azimio waende wote (kwenye msiba), nasikitika hilo halitawezekana," alisema na kuongeza kuwa kufanya hivyo kutaweka utaratibu ambayo baadaye inaweza kukwamisha shughuli za bunge siku zijazo.Akifafanua uwakilishi uliopangwa kwenda Dar es Salaam kuwakilisha Bunge na serikali kwenye msiba wa Amina, Spika Sitta alisema utakuwa na wabunge wote Iringa, ambao ndiyo mkoa wake kwa kuzaliwa na wabunge wote wa Dar es Salaam.Serikali itawakilishwa na Waziri wa Usalama wa Raia, Harith Bakari Mwapachu, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Hawa Ghasia na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba.Alisema watakuwemo wabunge wanne wa vyama vya upinzani watakaoongozwa na kiongozi wa upinzani bungeni, Hamad Rashid Mohammed.Spika alisema baada ya ujumbe huo ambao pia utajumuisha Katibu wa Bunge na makatibu wasaidizi wawili na wabunge wengine kadhaa, alisema leo ujumbe mdogo utakaoongozwa na Mbunge wa Singida Kaskazini, Mohammed Missanga, utakwenda Njombe kuhudhuria mazishi.Marehemu Amina aliyezaliwa Mei 20, 1981 na kuapishwa kuwa mbunge Desemba 29, 2005, atazikwa leo katika kijiji cha Lupembe, wilayani Njombe, Iringa.

…Vilio na simanzi vyatawala bungeni
Na Mwadini Hassan, Dodoma
VILIO, simanzi na majonzi vilisikika na kuonekana waziwazi bungeni jana, baada ya Spika wa Bunge, Samuel Sitta, kutangaza habari za kifo cha mbunge Amina Chifupa.Karibu kila mbunge alionekana kuguswa na habari hizo, akiwemo Spika mwenyewe ambaye wakati akitangaza taarifa za kifo hicho, alishindwa kujizuia na kuonekana akifuta machozi akiwa amesimama mezani pake ndani ya ukumbi wa Bunge.Hali ilikuwa tete zaidi kwa wabunge wanawake, ambao walionekana wakimwaga machozi huku wakiwa na vitambaa mikononi wakifuta machozi mara kwa mara wakati Spika akiendelea kutoa tangazo la kifo hicho, kilichotokea juzi saa 2.43 usiku.Amina Chifupa aliyekuwa mbunge wa viti maalum kupitia Umoja wa Vijana wa CCM, alifariki dunia katika hospitali ya jeshi Lugalo, jijini Dar es Salaam, alikokuwa amelazwa kwa matibabu.Hali ya majonzi ilizizima zaidi baada ya Bunge kuahirishwa moja kwa moja kwa siku ya jana karibu saa 4.25 asubuhi, ambapo baadhi ya wabunge wanawake walisikika wakilia kwa sauti huku wakifarijiana kwa kukumbatiana.Habari za uhakika kutoka ndani ya Bunge zilithibitisha jana kwamba, hii ni mara ya kwanza kwa historia ya karibuni ya Bunge, kuahirisha shughuli zake kutwa nzima kwa sababu ya kifo cha mbunge.Hali ya simanzi kutokana na kifo cha mbunge huyo machachari aliyejipatia jina kutokana na michango, hoja na maswali yake bungeni, ilianza kuonekana mapema wakati wabunge walipokuwa wakiingia maeneo ya viwanja vya bunge, kutokana na habari hizo kuanza kufahamika kwa baadhi yao mapema.Kama ilipangwa, baadhi ya wabunge waliingia ndani ya Bunge wakiwa wamevaa nguo nyeupe, ambazo siku hizi zimekuwa maarufu kuvaliwa na wanawake wakati wa misiba.

JK amlilia Amina Chifupa
Na Mwandishi Wetu
RAIS Jakaya Kikwete, ameeleza kupokea kwa mshituko mkubwa taarifa ya kifo mbunge wa CCM Viti Maalum, Amina Chifupa.Taarifa ya Ikulu kwa vyombo vya habari, ilisema kifo hicho kimetokea wakati usiotarajiwa, huku akihitajika, lakini vivyo hivyo alikuwa ameanza kuvuma kisiasa."Wengi tutamkubuka marehemu Amina Chifupa kwa mchango wake muhimu alioutoa bungeni na katika jamii hasa mongoni mwa vijana."Alikuwa hodari katika kujkenga hoja na kutetea maslahi ya vijana wenzake na taifa kwa ujumla. Alikuwa kijana msema kweli na jasiri katika kutoa maoni yake kwa jambo analoliona," alisema Rais Kikwete.Huku akinukuu misemo mbalimbali ya kijamii, Rais Kikwete alieleza kusikitishwa kwake na kifo cha mbunge huyo katika umri wa ujana wake."Kwa hakika kifo chake kinawagusa na kuwasikitisha watu wengi nchini. Wabunge wamempoteza mbunge mwenzao kipenzi, CCM wamempoteza nyota yao."Familia yake imempoteza nyota yao. Familia yake imempoteza mtoto na ndugu wa karibu. Mwanawe amempoteza mama. "Mzazi mwenzake amempoteza mzazi mwenziwe wa kusaidiana naye kulea mtoto wao mdogo. Jamii imempoteza mwana jamii mwema, mkarimu na mwenye moyo wa huruma," alisema Rais Kikwete. Aliwahakikishia jamaa za karibu wa marehemu, huzuni hiyo haikuwa peke yao, bali ni ya wote wanaoguswa na kifo hicho, huku akisisitiza ni "Mapenzi ya Mungu."Katika hatua nyingine, Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), umetoa rambirambi kutokana na kifo hicho cha Amina.Rambirambi za UVCCM zilizotolewa katika taarifa iliyotiwa saini na Mwenyekiti wa Taifa, John Nchimbi, zilisema hawataweza kumsahau kutokana na uwakilishi wake hasa wa kutetea maslahi ya vijana nchini wakati wote."Amina alikuwa ni mchapakazi hodari, mkweli na ambaye siku zote alitetea masuala ya vijana, sifa ambayo ilimfanya apendwe na wengi," ilisema taarifa hiyo.Nchimbi katika taarifa yake, alibainisha kwamba wakati wote wataendelea kukumbuka kwa utashi aliokuwa nao katika utumishi wa uwakilishi wa jamii katika chombo hicho cha kutunga sheria."Tunaungana na wabunge, familia, ndugu na jamaa za Amina Chifupa, kuomboleza kifo chake na tunamwomba Mwenyezi Mungu awape uvumilivu, nguvu na afya katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo," ilihitimisha taarifa hiyo.Wakati huo huo, Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, alisema chama hicho na yeye binafsi wameshitushwa na kifo cha Amina.Walimsifu marehemu kama mtetezi wa jamii ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na hivyo Watanzania wamempoteza kiongozi shupavu."CUF - tunatoa pole kwa Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi, Jakaya Kikwete, Spika Samuel Sitta, wabunge, ndugu na jamaa wa marehemu na tunaungana nao katika kipindi hiki kigumu cha majonzi,” ilisema taarifa ya CUF, iliyotiwa saini na msemaji Mbaralah Maharagande.

Naye Mwadini Hassan, anaripoti kutoka Dodoma kuwa, Chama cha Mapinduzi kimesema kimepokea kwa masikitiko makubwa habari za kifo cha Mbunge wa Viti Maalum, Amina Chifupa, na kusema namna ya kumuenzi ni kutetea na kuyasimamia yote aliyokuwa akiyatetea.Kauli hiyo ya CCM ilitolewa hapa jana na Katibu Mkuu wa CCM, Yussuf Makamba, alipozungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, makao makuu ya chama.Alisema, marehemu Amina alikuwa kiongozi imara katika kutetea hoja, na hasa kupambana na dawa za kulevya, ambapo alidiriki kueleza hadharani kuwa "hata kama ni mumewe au yeye mwenyewe anajihusisha na biashara ya dawa hizo, watajwe ili wafikishwe katika vyombo vya sheria."Makamba alisema, Amina alichukia biashara ya dawa za kulevya, ambayo imekuwa chanzo cha kuwaharibu vijana wengi nchini, ambao ndiyo nguvu kazi ya taifa.Makamba alitaja eneo jingine ambalo marehemu alilisimamia imara kulitetea, ni la watoto wa mitaani na wanaoishi katika maisha magumu, ambapo licha ya yeye kujitolea kwa hali na mali kupambana na tatizo hilo, alikuwa mara kwa mara akiitaka serikali kuchukua hatua madhubuti kuwasaidia kwa kuwapatia makazi ili waondokane na hali zao.Marehemu Amina alisema Makamba, aliwahi kulia alipowatembelea watoto wanaoishi katika mazingira magumu, hali ambayo ilionyesha alikuwa akiumizwa na hali hiyo na aliahidi kujitahidi kuwasaidia. "Namna nzuri ya kumuezi, ni kuyaendeleza aliyokuwa akiyasimamia na kuyatetea, na hasa kwa Umoja wa Vijana ambao alikuwa akiuwakilisha bungeni," alisema.

(source: uhuru, 28/6/2007)

Thursday 28 June 2007

Majibu!?

Lady: I wonder men in this town?
Bogi: What do you mean?
Lady: I have been here (in the bar) all night but no one has bought me a beer!
Bogi: You have stayed in this town for a long time; you should know the answers.
Lady: The problem is that once you know the answers, there is no one to ask you questions!!!???
Bogi: !!!!!!?????

Just keep on exercising!!!

You might not look overweight but that doesn't mean you don't need to exercise.
(You could be 'Thin on the Outside and Fat on the Inside -TOFI')
People who look slim can have large amounts of internal fat which can accummulate around vital organs and put them at risk of heart disease and Type 2 diabetes.

Quotes

'Most of us don't design our career, we fall into it by chance than design'
-Lenny Henry

'The secret of happiness is accepting some miserable times are inevitable'
-Researchers in US varsity (Virginia)

Amina Chifupa: Mwanamke Jasiri na 'Time Taker'*

Nilifahamu katika kipindi kifupi Amina Chifupa(26), japo hatukuwa tumezoeana lakini kutokana na majukumu yangu hasa katika nyanja ya michezo na burudani, tuliweza kugongana mara chache. Amina alifariki juzi usiku majira ya saa tatu kwenye hospitali ya Lugalo na kufanya taifa kuzizima kutokana na masikitiko ya kifo chake. Alikuwa mtu, ambaye aliweza kugusa kila nyanja na hasa kwenye burudani, michezo na siasa, ambako ndiko alikokutwa na mauti yake. Chifupa alikuwa Mbunge wa Jamhuri ya Muungano kupitia tiketi za vijana, ambapo alionyesha cheche mara baada ya kuchaguliwa kwake mwaka 2005. Mara ya mwisho kukutana naye ilikuwa mwezi Februari, mwaka huu wakati alipoandaa sherehe maalum ya kutimiza miaka mitano yake na ndoa na mumewe Mohammed Mpakanjia `Medi`. Pia mtoto wao, Rahman, alikuwa akitimiza miaka mitano kwenye sherehe hiyo iliyofanyika nyumbani kwao Sinza. Bahati mbaya kwenye sherehe ndio kulikuwa kumeanza kutokea minong?ono ya kuwepo mpasuko kwenye ndoa yake na Mpakanjia. Walichukua nafasi hiyo kuwadhihirishia marafiki, ndugu na majirani zao kuwa walikuwa bado kitu kimoja. Bahati mbaya sana yakatokea mengi yaliyotokea ndoa yake kuvunjika baada ya kutalikiwa na mumewe. Kitu kimoja kuhusu Amina, alikuwa akigonga vichwa vya habari kila mara, na kufanya kila mmoja katika jamii ya watanzania kumchukulia kivyake. Wengine walimwona mtu safi,kutokana na jinsi alivyopenda kusaidia walemavu, yatima na wale wote wenye shida. Alichukuliwa mpiganaji wa haki za wanyonge na hasa walipoingia kwenye vita ya kupambana na wauza madawa ya kulevya na wala rushwa na wabadhirifu kwenye serikali. Hiyo haikuzuia watu wengine kumwona kama mpenda sifa na mwenye kiherehere. Ukiachia yote hayo ya mitaani, Amina alikuwa na msimamo na alikuwa akifanya kile alichokiamini kilikuwa sawa kwake. Kutokana na msimamo huo, aliweza kutoa mchango mkubwa kwenye nyanja hasa za taarabu na michezo. Amina hakujali jamii ilikuwa inamchukulia vipi, bali mara zote alisimama kufanya kile alichokuwa anakiamini na kwa maneno mengine ya Kiingereza ungeweza kumwita `timetaker`. Kupitia vipindi vya burudani na hasa kwenye Redio ya Clouds alikoanzia kazi alikuwa na kipindi cha Unavyojisiki, ambapo alikuwa akipiga taarabu zaidi na kuzifanya kupanda kwenye chati za burudani. Nani atasahau mwaka 1999 hadi 2001, wakati muziki wa `Rusha Roho` ulipokuwa `matawi ya juu` na kufanya pambano la vikundi vya taarab vya TOT na Muungano kwenye miaka hiyo kuingiza kiasi cha Sh. milioni 20 katika onyesho moja. Akiwa mtangazaji wa kipindi cha African Bambataa kwenye miaka hiyo, ambapo akishirikiana na DJ Charles waliweza kuinua bendi za nyumbani. Hapo ndipo tulipoanza kushuhudia muziki wa Congo ukianza kuwekwa pembeni na watu wakaanza kupenda bendi zetu za nyumbani na pia kuibuka kwa `bongo fleva.` Chifupa ni mwaka huu baada ya kuwa Mbunge, alianza kujitokeza katika nyanja za michezo na hususan soka. Bila shaka kipindi hicho huku kukiwa hakuna makampuni yaliyojitokeza, alijitolea kutangaza zawadi kwa wachezaji wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars walipokuwa wanajiandaa kucheza na Burkina Fasso na Msumbiji kwenye mechi za Kombe la Mataifa ya Afrika, mwaka jana. Alionyesha uzalendo wa hali ya juu alipotinga na track suit ndani ya Uwanja wa Taifa wakati Stars ilipocheza na Burkina Fasso. Pia alionyesha ukereketwa wake wakati alipokwenda Msumbiji na kuahidi kutoa motisha ya fedha ya Sh. 500,000 kwa kila goli, ambalo lingefungwa. Chifupa alionyesha uzalendo wa hali ya juu kutokana na kuwa kati ya watu wa mwanzo kujitokeza kuisaidia Stars katika kipindi ambacho kila mwanzo ilikuwa haina wadhamini. Ndio maana mara baada ya kifo chake kutangazwa jana kwenye redio na televisheni, jamii ya watanzanzia imeweza kuwagusa watu kwa njia moja ama nyingine. Kutokana na ukweli kuwa Amina kutokana na ujasiri wake na kutojali maneno ya watu, aligusa nyanja za siasa na michezo akiwa Mbunge na pia kutoa mchango mkubwa katika kukuza sanaa na burudani za Kitanzania akiwa mtangazaji wa redio ya Clouds. Anazikwa leo kijijini kwao Lupembe wilaya ya Njombe mkoa wa Iringa. Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi! Amen.

*Source: Nipashe; imeandikwa na Samson Mfalila.

Man Utd: Fixture changes (For matches to be shown live on TV)

Sky Sports and Setanta are set to announce their listings for the first half of the season, which will move some games away from their traditional 3pm Saturday slots.
Sky have four packages, while Setanta have two, taking over those previously occupied by Prem Plus pay per view.
Games on Sky will be switched to Sunday at 1pm and 4pm and Saturday at 12.45pm.
Games on Setanta will be switched to Saturday at 5.15pm and Monday at 8pm.
Under the terms of the television deal, fans can expect a minimum of five and maximum of 26 league games to be switched for television coverage across the season.
Supporters are advised not to book travel or accommodation for games until the finalised fixture list has been confirmed.

Tuesday 26 June 2007

Mweusi, shule na lupango!

Mtoto au kijana mweusi (UK) ana uwezekano mkubwa maishani mwake kwenda jela (gerezani) kuliko kujiunga na masomo ya Chuo Kikuu!
-Hii ni ripoti ya hivi karibuni, na watu weusi wamelaani vikali hali hii na kuiita ni institutional racism!

Mhe Mzindakaya; habari zaidi za nyumbani leo.

MBUNGE wa Kwela (CCM), Dk. Chrisant Mzindakaya, amekana kuwa sehemu ya ubadhirifu ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kama ilivyodaiwa na Mbunge wa Karatu, Dk. Wilbrod Slaa (CHADEMA).
Akitoa maelezo bungeni juzi, baada ya Dk. Slaa kueleza hayo, Mzindakaya alikiri kukopa katika benki ya biashara kwa dhamana ya serikali na kwamba hajakopaau kudhaminiwa na BoT.Alisema mwaka 2004, serikali ilianzisha sera yakuwawezesha Watanzania ambao miradi yao inaonekana ina manufaa kwa uchumi wa nchi.
"Ingawa nia ya serikali wakati ule ilikuwa ni kuitumia Benki ya Rasilimali nchini (TIB) kwa miradi ya kilimo na ile ya ufugaji, benki hiyo ilikuwa bado haijajiandaa kikamilifu. Kwa hiyo serikali ilitoa mwongozo kuwa, kwa wakati ule wenye miradi waende katika benki watakazokuwa wamechagua na benki hizo kuwakubalia."... benki husika ndiyo zitaandika barua serikalini na kwa Benki Kuu na badala ya serikali kutoa udhamini kwa benki iliyotoa mkopo, serikali ilitoa dhamana kwaBenki Kuu," alisema Dk. Mzindakaya.Alisema mdhamini wa mkopo wake si BoT, ni serikali kupitia Wizara ya Fedha na kuongeza: "Mkopo wa Standard Chartered Bank si wa muda mrefu, mara nyingiwanatoa mkopo wa muda mfupi usiozidi miaka mitano".
Dk. Mzindakaya alisema mradi alioombea mkopo ni wa ufugaji wa ng'ombe wa nyama, ujenzi wa machinjio na kiwanda cha kisasa, ambao ulipaji wake hauwezi kuwa wa muda mfupi."Kwa kuwa Standard Chartered waliridhika kwamba mradi huu ni mzuri walikubali kutoa mkopo huo, na kwa kuwa muda wao ni miaka mitano, baada ya mradi wenyewe kuanza kutekelezwa... walitoa pendekezo kwa serikalikwamba ni mzuri, lakini mkopaji hawezi kulipa kwa miaka mitano."Walipendekeza serikali ipeleke katika benki nyingine Mambayo muda wake utakuwa mrefu kwa mkopaji. Baada ya hayo benki niliyokopa ambayo sina haja ya kutoa maelezo mengi, ilipopeleka mapendekezo yake, serikaliilikubali kwa kuzingatia umuhimu na faidia ya mradi huo."Baada ya kukubali, serikali yenyewe ndiyo iliagiza BoT kwamba mimi sasa nihamie TIB. Kwa hiyo mkopo niliokopa mimi na dhamana ni ya Serikali Kuu na si ya BoT," alisema Dk. Mzindakaya.Alisema BoT haiwezi kumkopesha kwa sababu haiwezi kukopesha mtu, haina hela ya kukopesha. Aliongeza: "Fedha nilizokopeshwa, mdhamini wake narudia ilikuwa Serikali Kuu na fedha ambazo ilionekana lazima nihamie TIB, serikali ndiyo imelipa katika benki niliyokopa na siyo Benki Kuu kama inavyoelezwahapa."Mzindakaya ambaye ni mbunge wa Kwera-CCM, alisema hawezi kueleza kuhusu kiwango cha deni la kampuni yake na kuwa deni ni siri kati yake na benki,hivyo takwimu zilizotolewa hawezi kizithibitisha kwa sababu ni siri ya mkopaji na mkopeshaji.Dk. Mzindakaya alisema kiwanda kilichojengwa kitatoa ajira kwa wafanyakazi 180 na wale wasiokuwa wa moja kwa moja watakuwa 2,300, hivyo kuwa na manufaa kwa Watanzania.
"Ninaweza sasa nikatambua kwamba mtu mweusi kufanya maendeleo ya aina hii tuliyofanya ni dhambi kwa sababu hakuna atakaye- appreciate jambo kama hilo, na leo (juzi) maelezo haya ni ushahidi. Si kweli kwamba kampuni yangu imeomba mkopo mwingine wa mabilioni kutoka Benki Kuu."Sikujua kama lengo la maelezo ya Dk. Slaa ni gavana kwa jina la Ballal. Nilisema baadhi ya mambo mazuri, ambayo BoT imeyafanya katika kipindi cha miaka 10 iliyopita.
"Sijatetea maovu yoyote ambayo yanamlenga gavana kwa sababu mimi sikujua hayo.
Nilisifu serikali kwamba imekubali na itafanya ukaguzi wa yanayozungumzwa kuhusu Benki Kuu. Nimekuwa mtetezi na nimeendelea kuwamtetezi wa wananchi kupitia sera za chama changu," alisema.Alisema katika kipindi cha miaka 40 alichofanya kazi hiyo, hajawahi kuhusishwa na kashfa yoyote katika maisha yake na kuongeza kuwa kuwa: "Nimekopa katika benki sikuiba, wala siku- Collude na Benki Kuu."
Dk. Slaa akiwasilisha hotuba ya kambi ya upinzani kuhusu makadirio ya matumizi ya fedha ya ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka 2007/08, alisema kwa mujibu wa kanuni za Bunge kifungu cha 49 (7), ambacho kinamzuiambunge kuzungumzia jambo ambalo ana maslahi nalo kifedha, isipokuwa baada ya kutaja jinsi anavyohusika na kiwango cha maslahi hayo, Dk. Mzindakaya hakutaja maslahi yake kuhusu BoT.
Alisema utafiti wao umeonyesha kuwa mwaka 2004, Dk. Mzindakaya alichukua mkopo kwa shughuli za kampuni yake binafsi ya SAAFI wa sh. bilioni 6.217 kutoka benki ya Standard Chartered.Dk. Slaa alisema BoT ilidhamini mkopo huo na kwamba mwaka huu, benki hiyo kutokana na mdhamana tayari imelipa sh. bilioni 8.1 kwa niaba ya Dk. Mzindakaya na fedha hizo na riba zinakisiwa kufikia sh. bilioni 9.7, deni ambalo limehamishiwa TIB, ambako anatakiwa kulipa deni la BoT."Hivi sasa ameomba adhaminiwe na BoT mkopo mwingine wa sh. bilioni mbili. Mkopo huo uko katika hatua ya kujadiliwa na BoT," alisema Dk. Slaa.
Spika wa Bunge, Samuel Sitta alihitimisha hoja hiyo akisema: "Naridhika kwamba kwa kuwa mkopo ulikuwa wa kibiashara, alikuwa hana haja ya ku-declare conflict of interest yoyote kwa sababu hata guarantee yenyewe kumbe ni ya serikali. Kwa hiyo hakuathiri Kanuni ya 49 (7)."


JK: Sheria ya dawa za kulevya ifanyiwe marekebisho haraka 'Mateja' sasa kupewa matibabu kwa nguvu

RAIS Jakaya Kikwete amesema sheria inayotoa adhabu ndogo kwa watuhumiwa wa dawa za kulevya itaangaliwa upya na kutupilia mbali hoja za wanaodai kutetea haki za binadamu.Alisema watuhumiwa hao wamekuwa wakiharibu watoto, lakini wanapofikishwa kwenye vyombo vya sheria hupewa adhabu ndogo kuliko makosa yanayofanywa kwa kigezo cha kuheshimu haki za binadamu.Akizungumza kwenye maadhimisho ya kitaifa ya siku ya kupiga vita dawa za kulevya duniani yaliyofanyika katika uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga jana, Rais Kikwete alisema inashangaza kuona mtu anakamatwa na dawa za kulevya zenye thamani ya milioni 30, lakini anapewa adhabu ya kulipa sh. milioni moja."Naomba niseme sifurahishwi sana na sheria kwamba mtu anakamatwa na dawa za sh. milioni 30, lakini anatozwa faini ya sh. milioni moja. Hii inashangaza sana kwa nini huyu mtu asifungwe jela miaka ya kutosha ili akitoka awe amezeeka na hiyo itatusaidia kuinusuru jamii yetu," alisema.Rais Kikwete alisema kama mtu ameweza kununua dawa zenye thamani ya mamilioni anapaswa kuogopwa na kupewa adhabu kubwa na kwamba akiachiwa ataendelea kufanya biashara hiyo na kuiharibu jamii ya Watanzania.

Watendaji walaumiwakukwamisha maendeleo

BAADHI ya wabunge wamewashutumu watendaji wa serikali kwa kukwamisha kasi ya maendeleo ya wananchi, kwa kutumia fedha kinyume cha malengo yaliyokusudiwa.Wabunge Mudhihir Mudhihir (Mchinga-CCM), Diana Chilolo (Viti Maalum-CCM), Vedastusi Manyinyi (MusomaMjini-CCM) na Omar Kwaangw' (Babati Mjini-CCM), kwa nyakati tofauti walilalamikia baadhi ya watendaji wanaokwamisha maendeleo.Mudhihir alimlalamikia katibu tawala wa mkoa kwa kukwamisha mradi wa ujenzi wa hospitali, ambao uliwahi kutengewa sh. milioni 300, zilizohamishiwa kwenyemradi mwingine, wakiambiwa kuwa wao ni 'sikio katika uso'.Alisema baadhi ya watendaji wamekuwa wababe na wanakiuka Katiba. Alisema hospitali hiyo ni muhimu kama ilivyo ya Tumbi, Kibaha, ambayo itasaidia hatamajeruhi.Akizungumzia kuhusu umeme kutoka Mnazi Bay, Mudhihir alisema sh. milioni 320 zilitengwa kwa ajili ya kazi hiyo, lakini ofisa mmoja wa Wizara ya Fedhaamekwamisha kazi hiyo.Diana kwa upande wake, alisema mwaka 2005 walitengewa sh. milioni 200 na mwaka 2006 walipewa sh. milioni 165 kwa ajili ya ununuzi wa gari la zimamoto, lakini sh.milioni 165 zilitumiwa kwa shughuli tofauti.Alisema Singida imekuwa ikikabiliwa na majanga ya moto kama ilivyotokea hivi karibuni kwa basi la Mohamed Trans kuungua, lakini walishindwa kuwasaidia kutokana na kutokuwepo kwa gari la zimamoto. Alitaja majengo mengine yaliyowahi kuungua kuwa ofisi ya CCM, stendi ya mabasi na nyumba ya mfanyabiashara."Tutaendelea kuipaka matope serikali hadi lini. Wanajua taratibu za fedha, tuwatazame kwa macho mawili watu wa aina hii. sh. milioni 200 zilizobakituongezewe tupate gari la zimamoto," alisema. Manyinyi alisema wako baadhi ya watendaji ambao wamekuwa wakisababisha kero kwa wananchi pasipo sababu, moja kati ya hizo ikiwa magari kukamatwa kwa kutokufungwa vidhibiti mwendo, ambavyo havipo.Kwa upande wake, Kwaangw' alisema ubadhirifu uko kwenye manunuzi ya vifaa, huduma na ujenzi, alishauri Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi (PPRA) ifanye kazi hiyo na si Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikalipekee. Katika hatua nyingine, wabunge wameishauri serikali kuwa posho ya madiwani ya sh. 60,000 kwa mwezi itolewe kwa halmashauri zote na si kwa kulingana na uwezo wake.Wabunge hao Diana, Jenista Mhagama (Peramiho- CCM), Estherina Kilasi (Mbarali- CCM) na Manyinyi walisema hayo walipokuwa wakichangia hotuba ya Waziri Mkuu, Edward Lowassa kuhusu mapitio na mwelekeo wa kazi za serikali na makadirio ya matumizi ya fedha ya ofisi yake na ofisi ya bunge kwa mwaka 2007/08.
Lowassa katika hotuba yake juzi alisema serikali imekubali kuongeza posho za madiwani kutoka sh. 30,000 hadi sh. 60,000 kwa mwezi, kulingana na uwezo wa halmashauri. Alisema kazi ya kutathmini halmashauri zisizo na uwezo inaendelea kufanyika. Diana aliishauri serikali kuongeza kiasi hicho kifikie sh. 100,000 na kwamba posho hizo zilipwe na serikali kuu.Katika hatua nyingine, Estherina aliishauri serikali nusu ya fedha kwa ajili ya wajasiriamali zitolewe kupitia Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo Vidogo(SIDO) kutokana na benki kushindwa kuwapatia mikopowakulima.Baadhi ya wachangiaji kwa nyakati tofauti, waliwataka mawaziri kwenda majimboni kujibu kero za wananchi, kwa kuwa wao wamekosa majibu.

Nyimbo za Watoto (Nursery Rhymes)

THE WHEELS ON THE BUS
The wheels on the bus go round and round,
Round and round, round and round,
The wheels on the bus go round and round,
All the day long.

The horn on the bus goes beep, beep, beep!
Beep, beep, beep! Beep, beep, beep!
The horn on the bus goes beep, beep, beep
All the day long.

TWINKLE, TWINKLE, LITTLE STAR
Twinkle, twinkle little star,
How I wonder what you are!
Up above the world so high,
Like a diamond in the sky.
Twinkle, twinkle little star,
How I wonder what you are.

LONDON BRIDGE
London Bridge is falling down,
Falling down, falling down,
London Bridge is falling down,
My fair lady.

GOOD MORNING TO YOU (as happybirthday to you ...!)
Good morning to you,
Good morning to you,
Good morning, dear Toby,
Good morning to you!

Monday 25 June 2007

Napendekeza ...

Ipo haja ya viongozi wa vyama vikubwa vya upinzani nchini kuwemo ktk Bunge la Jamnhuri ya Muungano au Baraza la Wawakilishi.
Kwa hiyo napendekeza kuwa sheria husika zipitiwe ili viongozi wa vyama vinavyopata 5% au zaidi ya kura zote ktk uchaguzi Mkuu (wa Rais), waweze kuingia Bungeni moja kwa moja. Hii itaimarisha zaidi demokrasia yetu changa nchini. Au vyama vyenye sifa ya kupata ruzuku toka serikalini viweze kuwakilishwa bungeni na viongozi wao. Lengo ni kuimarisha demokrasia na kuvipa uhai 'zaidi' vyama vya upinzani.
Kwa maana hii, viongozi wa vyama vya CUF -Ibahimu Lipumba (na Maalimu Seif -wawakilishi Z'bar), Chadema -Freeman mbowe, TLP - Augustine Mrema wangeweza kuingia Bungeni moja kwa moja kwa kuzingatia matokeo ya uchaguzi Mkuu uliopita!
Natumaini Bunge lingepata msisimko zaidi!!!

Maoni: Yanga Tuamke Kumekucha!*

(Natoa) Hongera kwa Yanga kutwaa ubingwa 2006. Nawatakia kila la heri mwakani Champions League ya CAF.
Yanga hawana haja kuleta kocha mpya kwa sasa, waliopo wanafaa.
Wanachotakiwa kufanya ni kukarabati uwanja wa Kaunda ili utumike itasavyo (kibiashara) kama kitega uchumi. Pia Yanga wanatakiwa waweke au waongeze facilities za kisasa za mazoezi kwa wachezaji na huduma nyingine (e.g. hospitality) klabuni.
Long term plans:
Yanga watafute site kwa ajili ya uwanja wao kwa mechi za nyumbani wenye capacity kati ya watu 20,000 hadi 25,000 (au zaidi ya hapo). Kama kampuni, wana nafasi ya kupata mkopo kwa ajili hiyo. Faida nyingine ni kuwa uwanja utakuwa unaazimwa/unakodiwa na TFF au timu yoyote ya Tanzania kwa mechi za kimataifa na za CECAFA, CAF au FIFA na timu itapata fedha (hata za kigeni). Pia itaondokana na kuilalamikia TFF kupunjwa mapato hasa mgawanyo wa ki-asilimia wa viingilio, maana itapanga viingilio vyake na kuuza tiketi yenyewe. Kwa hiyo itadhibiti udokozi na ubadhilifu unaofanywa U/Taifa kwa sasa.
Hebu fikiria Man Utd ktk uwanja wake wenye uwezo wa watazamaji zaidi ya 76,000, wanatoa tiketi kwa timu pinzani inayokuja kucheza Old Trafford tiketi 3,000 - 6,000 tu. Hii ina maana kuwa tiketi zilizobaki 70,000 - 73,000 zinauzwa na timu yenyewe (Man Utd). Tuchukulie kwa mfano, kwa wastani, tiketi moja ni GBP 20 kwa hiyo Man Utd wanapata, angalau, GBP 1,400,000 ktk mechi moja ya nyumbani (hizo ni paundi!!!).
Nadhani Yanga nao waige hili maana ni zuri na ni endelevu. Mathalani, ktk uwanja wa viti 20,000 kwa bei ya sh.2,500 kiingilio, Yanga wanaweza kuingiza sh.50,000,000/= ktk mechi moja ya kawaida mfano dhidi ya Mtibwa au Prisons. Siku ya mechi dhidi ya Simba kwa kiingilio cha sh.4,500 itakuwa jumla sh.90,000,000/=.
Ukipata hiyo hela ya 1. viingilio, 2. ukodishaji uwanja na 3. ukiongezea hela inayoingia ktk udhamini mbali mbali na matangazo Uwanjani, timu itapata mapato makubwa na itaweza kujiendesha kibiashara zaidi badala ya kutegemea kina ''Yanga Family'' wagharamie usajili wa timu kila mwaka. Au kutegemea kina Aaron Nyanda watoe hela ya nauli/posho kwa wachezaji baada ya mazoezi; kisa, eti hakuna hela ya posho kwa wachezaji kambini!!! Hii hali inasikitisha hususan kwa timu kama Yanga, mabingwa kwa mara ya tatu chini ya Chamangwana.
Pia ikumbukwe timu inahitaji kuwa na chemichemi ya wachezaji wa siku zijazo (academy). Watoto wenye vipaji wa makundi ya kiumri kuanzia miaka 11-14, 15-17 na 18-21. Kundi la muhimu zaidi ni la miaka 16-19 maana wanakuwa wanamalizia au wamemaliza elimu ya sekondari.
Inabidi kufanyike mabadiliko ya haraka kimaendeleo ili timu isonge mbele ktk enzi hizi za kiteknolojia. Hapo tunaweza tukafanya vizuri kimataifa na hata kuuza wachezaji nje ya nchi hasa kwenda nchi za EU na timu itapata hela nyingi za kigeni kwa kuuza vipaji.

*Hii ni sehemu ya barua zangu mwaka jana (2006) kwa mashabiki wenzangu baada ya Yanga kutwaa ubingwa chini ya kocha Jack Chamangwana kutoka Malawi. Sijui kwa sasa Chamangwana yuko wapi na anafanya nini. Nampongeza sana kwa kazi yake Yanga.

Arsenal: Niliyatabiri April 2006!!*

Hongera kwa ushindi dhidi ya Juve, unajua ktk mchezo pamoja na vipaji, ufundi, nguvu, speed n.k. kitu kingine muhimu ni BAHATI. Safari hii Arsenal bahati imewaangukia.
Zipo bahati za aina nyingi mfano;
1. refarii na kipenga:
kupewa au kunyimwa penalti ktk mchezo, mchezaji kupewa au kutopewa red card, maamuzi ya utata kuhusu goli au kukataa goli n.k.
2. game:
ziko siku nzuri na mbaya ktk game lakini timu inashinda hata bila kucheza vizuri.
Kwa upande wenu Arsenal timu bado ni changa na bahati inawasaidia. Bado siamini kuwa mtafika fainali (au kuchukua kombe) kwa sababu hamna uzoefu.
Kuhusu mechi ya kesho Old Trafford, Man Utd itashinda. Uzoefu, Nguvu, Ushambuliaji wa Man U ni mkubwa kuliko Arsenal. Nafasi yenu kushinda au kuambulia sare ni ndogo sana.
Ktk kiungo hali yenu sio mbaya tunaweza kulingana. Ulinzi tunawazidi, Golini tuko sawa kwa hiyo washambuliaji + viungo ndio wataamua mechi - vitu ambavyo Man U ipo juu yaArsenal.

* Ujumbe huu niliuandika tarehe 08/4/2006, na maoni haya ni yangu binafsi kutokana na tathmini yangu ktk soka la Uingereza.
Hivi sasa mambo si shwari Arsenal na msimu uliopita nusura wakose hata nafasi ya 4 (champions league positon)!!
Thiery Henry nae uzalendo umemshinda kaona bora ajiondokee.
Hatma ya Arsene Wenger iko ktk hatihati huenda nae yuko njiani kuondoka Arsenal mwishoni mwa msimu ujao (mkataba wake utakapoisha)!!
Ujenzi wa uwanja mpya wa Emirates umeigharimu Arsenal hela nyingi na hivi sasa wanarudisha deni kwa wakopeshaji (creditors); ila hali itarejea shwari baada ya miaka 5 hivi. (Wenger aliwahi kusema, mwaka 2003, kuwa hali ya kifedha Arsenal itarejea ktk hali nzuri baada ya miaka 8 na hivi sasa imeshapita miaka 4 tangu kauli ya Wenger). Ndio maana Arsenal kwa sasa hawana hela ya kununua wachezaji wazuri ambao wanagharimu zaidi ya £15mil. Utaona mara nyingi wachezaji wa Arsenal wanagharimu chini ya £10mil. na sio kwamba wanapenda au kubana matumizi; jibu ni kwamba hawana hela za kushindana na timu za Man Utd, Chelsea na Liverpool. Na kwa sasa hata West Ham inawashinda Arsenal ktk soko la kununua wachezaji!!!
Ni lazima Arsenal iamue sasa kutumia hata kama ni kukopa zaidi au kumkubali owner mwingine ambae atawekeza hela zaidi.

Friday 22 June 2007

Shirikisho la afrika Mashariki*

Nimesoma makala yako kuhusu viongozi wetu na shirikisho.
Ninakubaliana nawe hasa uchambuzi wa kisiasa na kiuchumi ulioufanya. (Naona kama ulisahau kuongelea Rwanda na Burundi ambazo zimeongezwa ktk jumuiya ya A. Mashariki)
Uzoefu wako hasa ktk jumuiya ya zamani ni wa kipekee kwa vile kizazi cha viongozi/wabunge wa sasa wamesahau mabaya yaliyosababisha kuvunjikka jumuiya na jinsi Kenya ilivyotudhulumu.
Pamoja na makundi yote uliyobainisha kuwa yashirikishwe kikamilifu, mimi napenda kuongezea kundi ambalo ni muhimu kisiasa na ki-ushawishi. Kundi hili ni Vyama Vya Siasa. Unaonaje viongozi wa vyama hivi nao wakipiga kampeni kuwaelimisha wananchi juu ya madhara ya shirikisho kwa nchi yetu?
Nimejaribu kuongea na watu mbalimbali na nimegundua kundi la watu wanaotaka shirikisho ni wanasiasa ambao wana nafasi ya kupata ulaji/uongozi ktk shirikisho hasa marais wetu mfano hao waliobadilisha katiba zao ili wawepo madarakani ktk kipindi cha kuanzisha shirikisho!!
Watu wengine wanaotaka shirikisho ni wafanyabiashara (wachache) wakubwa ambao watanufaika na kutangaza/kusambaza biashara zao ktk nchi hizo zote.
Ninaamini wananchi walio wengi Tanzania hawatanufaika.
Ningependa kuona unaazishwa mtandao wale wananchi wanaopinga kuanzishwa kwa shirikisho ili wawe msitari wa mbele kuwaelemisha wananchi na kuwashinikiza viongozi wetu wawasikilize wananchi. sidhani kama ni vibaya huo mtandao kuwepo!
Tunaomba pia wabunge wetu watuwakilishe kikamilifu ktk hili.
Kuna mambo mengi ambayo tungependa serikali yetu iyashughulikie badala ya kupoteza nguvu na muda kwa hili la shirikisho.


*Barua hii niliiandika tarehe 27/12/2006 kama maoni yangu binafsi.

Maoni: Mafao Kwa Wastaafu Tanzania*

Mheshimiwa Mzee J S Malecela.
Napenda kutoa pongezi kwa mchango wako bungeni kuhusu mafao kwa wastaafu. Nimefurahi hasa ulipoamua kuwa, pamoja na serikali kulifuatilia, wewe mwenyewe na wabunge kwa ujumla kuchukua jukumu la kuwaorodhesha majimboni ili mafao yao yashughulikiwe.
Ni matumaini yangu kuwa waheshimiwa mkishakabidhi orodha hizo, waziri atakeshughulia hizo orodha awe anatoa update ya malipo mafao hayo kila mara (hasa kila baada ya miezi 2 hadi 3) bungeni.
Hongera pia kwa mchango wako kuhusu kauli na kitabu cha Profesa Malyamkono -'the promise'. (Mimi) ninakuunga mkono kwani viongozi mlioweka msingi imara wa taifa hili ni vizuri kazi yenu itambuliwe na kuthaminiwa.
Nakutakia kila la heri.
Edison

*Hii ni barua yangu kwa Mheshimiwa John Malecela (MB Mtera, Makamo wa M/Kiti CCM Taifa) tarehe 28/9/2006

Maoni: Waliooana*

Hi Anti Flora!!!!
Asante kwa kutoa nafasi kwa wasomaji wako kutoa au kuchangia mada ktk 'maisha ndivyo yalivyo'.
Napenda kuchangia hoja ya msomaji wako aishie Oxford, Uingereza.
Kwanza napenda kukupongeza wewe binafsi kwa mafundisho yako ktk jamii. Kila mara unasisitiza mambo muhimu katika kudumisha ndoa kwa mfano upendo, uaminifu, uvumilivu, kusameheana, kukosoana n.k. Naamini mada unazoandika kila wiki unazitumia kama mifano ktk kufikisha ujumbe kwa jamii.
Msomaji wako 'aliponda' moja kwa moja juhudi za mwanandoa uliyemzungumzia ktk kunusuru ndoa yake (rejea mada ya 17/09/2006). Kwa upande wangu na kwa mazingira ya kwetu Tanzania, juhudi hizo hazikuwa bure, kwa sabababu huyo mama alifanikiwa kulipatia jibu lile tatizo la mumewe! Kama kuna mambo ya virusi yameingilia ktk suala hili, basi, hilo ni suala lingine. Lile kubwa la msingi limepata jibu.
Hili suala la kudhibiti/kuzuia maambukizi (STDs & Infections) tukiliangalia kwa karibu kabisa kabisa linaweza kupata dawa/kinga kabla mtu hajapata magonjwa/maambukizi haya. Ktk ndoa kama kuna uaminifu wa kweli, upendo, uvumilivu n.k. mtu hawezi kwenda nje ya ndoa kimapenzi. Kila anapopata tamaa kimwili atamkumbuka mkewe kama vile anamwona kile anachofikiria au kutamani (ngono ya nje!!)
Yule mama uliyemsimlia 17.09.06, hana makosa na yeye alifanya kile kilicho ktk uwezo wake na akafaulu. Kuna msemo, mtu hujikuna pale anapofikia! Hapa tatizo liko kwa 'baba'aliyekuwa na kimada Morogoro.
Wanaume wengi tuna jeuri ya kufanya tutakavyo hasa kuhusu nyumba ndogo kwa vile wake zetu (wengi wao) ni kina mama wa nyumbani na wanatutegemea kwa kila kitu kimatunzo. Kwa mwanamke anayemtegemea mumewe kimaisha(kiuchumi) anakuwa ni mnyonge pale mumewe anapomkosea maana dume litasema ''leo nakurudisha kwenu'' sasa huyu mwanamke atasemaje, sanasana atanywea tu. Ninachotaka kusema ni kuwa ni wanawake wangapi Tanzania wanaweza kuwafumania waume zao na wakawa na jeuri ya kudai mume aende au wote waende kwa pamoja kupima maambukizi kabla ya kuendelea na mahusiano ya mwili?

Huyu msomaji wako wa Oxford amesahau kutofautisha mazingira aliyopo kwa sasa (Uingereza) na Tanzania, dunia ya tatu.

Mwanamke wa Uingereza ndie huyu hapa;

sheria inamlinda sana na watoto. (na kwa taarifa yako anti Flora, wanaume wengi kutoka Afrika wanaojifanya vijogoo kwa wake zao wanaipata joto ya jiwe Uingereza).

kama hana kazi, atalipwa 'job seeker's allowance', incapacity benefit.

kama hana mahali pa kuishi (hasa baada ya umri wa miaka 18 na kuendelea) atalipwa housing benefit au kutafutiwa nyumba ktk halmashauri ya serikali ya mtaa anayoishi(council house). Council zote zina nyomba kwa ajili ya 'wanyonge' kimapato, wenye kipato cha chini na wasio na makazi.

kama akiachika kwa mumewe na ana mtoto/watoto, atapata mafao kupitia Child Support Agency, child support scheme.

kuna kadi (credit) ya matibabu ya mama na mtoto ktk hospitali zote za serikali na binafsi ambapo watapata matibabu au kupima afya zao bure (hospitali zitaidai serikali gharama).

mtoto atapata nafasi ya kusoma chekechea, msingi, sekondari hadi A-level bure. Chuo kikuu kuna mikopo kwa kila mwanafunzi aliyepata nafasi chuo kikuu.

kama ana ulemavu atapata Disability and Carers service benefits.

kama ni mzima na ana uwezo wa kufanya kazi, atatafutiwa kazi kupitia vituo vya kutafuta kazi, Jobcentre Plus vilivyoko ktk miji yote Uingereza. Kazi zipo tele za wasomi na wasio wasomi.

Anti Flora ninajaribu kujenga hoja kwa hiyo naomba univumilie kwa porojo zangu hizi.

Ninataka nijenge mazingira ambayo mwanamke mtanzania kama yule wa tarehe 17.09.06 anaweza kusimama kidete na kumpeleka mumewe 'ANGAZA' wakapime.

Nimetoa mfano wa mama aishiye Uingereza na tumlinganishe na huyu wa Tanzania. Naamini utakubaliana nami kuwa huyu mama wa Uingerreza anaweza kumwambia mumewe wakapime ikiwa mume atafanya mambo nje ya ndoa. Na ikiwa mume wake atagoma au kubisha na mama akawa na msimamo kulinda afya yake asijeambukizwa
mama anaweza kusema watengane kwa kuhofia virusi. na wakitengana anaweza kuendelea na maisha bila wasiwasi kama nilivyoelezea hapo juu. Huyu mama wa Kiingereza hatapata tatizo lolote kimaisha.

Je yule mama wa kitanzania akimwambia mumewe wakapime na mume akagoma, mama ataamua nini; aondoke au akae na kuambukizwa?

Matatizo mengi kwa kina mama chanzo chake ni utegemezi kiuchumi kwa mume au ndugu.

* Barua yangu ya 28/9/2006 kwa Flora Wingia wa Magazeti ya Guardian na mwandishi wa makala ya 'Maisha Ndivyo Yalivyo' Nipashe Jumapili.

'Haters'**

ONLY THE STRONG SURVIVE*

SHAKE THEM HATERS OFF!

A hater is someone that is jealous and envious and spends all their time
trying to make you look small so they can look tall. They are very negative
people.
Nothing is ever good enough!

When you make your mark, you will always attract some haters...
That's why you have to be careful who you share your blessings and your
dreams with because some folk can't handle seeing you blessed...

It's dangerous to be like somebody else... If God wanted you to be like
somebody else. He would have given you what He gave them.

You don't know what people have gone through to get what they have...
The problem I have with haters is that they see my glory, but they don't
know my story...
If the grass looks greener on the other side of the fence, you can rest
assured that the water bill is higher there too.

We've all got some haters among us: Some people don't like it that you can:
* Have a relationship with God
* Light up a room when you walk in
* Start your own business
* Tell a man/woman to get lost (if he/she ain't about the right thing)
* Raise children without both parents being around
* And not ask for a dime from Anyone

* Haters don't want to see you happy
* Haters don't want to see you succeed
* Haters don't want you to get the victory

Most of our haters are people that are supposed to be on our side. How do
you handle the haters who you at least expect to have your guard up
against?
You can handle your haters by:

1. *Knowing who you are & who your true friends are * (VERY IMPORTANT!!)
2. *Having a purpose to your life *
3. *By remembering what you have is by divine prerogative and not human
manipulation.*

Purpose does not mean having a job.
You can have a job and still be unfulfilled.
A purpose is having a clear sense of what God has called you to be.
Your purpose is not defined by what others think about you.

Fulfill your dreams!
You only have one life to live................when its your time to leave
this earth, you want to be able to say,"I've lived my life and fulfilled my
dreams, .........I'm ready to go HOME!

When God gives you a favor, you can tell your haters, "Don't look at me...
Look at who is in charge of me..."

Pass this to all of your family & friends who you know are not hating on
you including the person who sent it to you.
If you don't get it back, maybe you caught somebody out!
Don't worry about it, it's not your problem, it's theirs. Just pray for
them, that their life can be as fulfilled as yours!

Watch out for Haters............................BUT most of all don't
become a HATER yourself!

If you received this from me then you are on my FRIENDS list!

Take Care

**Ni ujumbe kutoka kwa mmoja wa wasomaji wangu Donald Bituro (wa August End, Reading)

Heshima zenu (Masange & Luwa JKT)*

1. Alphonce Kiheri B/C Coy- Masange/Luwa
2. Robinson Magambo HQ/B Coy-M/L
3. Jumanne Sandda -m/L
4. Happyness Temu a/A Coy- M/L
5. Isabela Akaro B Coy- Masange
6. Audrey Komeka B Coy- Luwa

*Orodha ya kuruta & servicemen/women wenzangu JKT 1990/91, Operation Kambarage.

Heshima Zenu, Mazengo High School**

Mazengo H/S
1. Maulid Gakore PGM- Mwongozo (my dorm. mate)
2. Bosco Kitura PGM-Azimio
3. Alphonce Kiheri PGM-Muungano
4. Shadrak Metili-
5. Ali ... -PGM, G3
6. Siston Makafu -PGM, G3 roomate R.09 Down
7. Godfrey Mmari -PGM, G2 -Roommate R.09 &14 Down
8. Fikeni Yona, -PGM, G2 -Room mate -do-

* Orodha ya Wanafunzi wenzangu (classmates) 1988-90.
Mabweni ya Mazengo
Mwongozo
Azimio
Muungano
Mwenge
Ujamaa

Manchester United: Fixtures july - Dec 2007

FULL FIXTURES & RESULTS: 2007/08

July 2007
17 Jul
Pre-season
United Vs Urawa Red Diamonds
12:00
A
-
20 Jul
Pre-season
United Vs FC Seoul
12:00
A
-
23 Jul
Pre-season
United Vs Shenzhen FC
12:00
A
-
August 2007
01 Aug
Pre-season
United Vs Inter Milan
20:00
H
-
05 Aug
FA Charity Shield
United Vs Chelsea
15:00
N
-
11 Aug
Barclays Premiership
United Vs Reading
15:00
H
-
14 Aug
Barclays Premiership
United Vs Portsmouth
20:00
A
-
18 Aug
Barclays Premiership
United Vs Man City
15:00
A
-
25 Aug
Barclays Premiership
United Vs Tottenham
15:00
H
-
September 2007
01 Sep
Barclays Premiership
United Vs Sunderland
15:00
H
-
15 Sep
Barclays Premiership
United Vs Everton
15:00
A
-
22 Sep
Barclays Premiership
United Vs Chelsea
15:00
H
-
29 Sep
Barclays Premiership
United Vs Birmingham
15:00
A
-
October 2007
06 Oct
Barclays Premiership
United Vs Wigan
15:00
H
-
20 Oct
Barclays Premiership
United Vs Aston Villa
15:00
A
-
27 Oct
Barclays Premiership
United Vs Middlsbro
15:00
H
-
November 2007
03 Nov
Barclays Premiership
United Vs Arsenal
15:00
A
-
10 Nov
Barclays Premiership
United Vs Blackburn
15:00
H
-
24 Nov
Barclays Premiership
United Vs Bolton
15:00
A
-
December 2007
01 Dec
Barclays Premiership
United Vs Fulham
15:00
H
-
08 Dec
Barclays Premiership
United Vs Derby County
15:00
H
-
15 Dec
Barclays Premiership
United Vs Liverpool
15:00
A
-
22 Dec
Barclays Premiership
United Vs Everton
15:00
H
-
26 Dec
Barclays Premiership
United Vs Sunderland
15:00
A

Monday 18 June 2007

Heshima Zenu 2!! Musoma Sec School*

MUSS Boys
1. Haruna Mohamed -Class monitor IB, IIB, Dormitory Leader -Shaaban Robert
2. Deogratius Mwema Thomas
3. Nyanda Gapale
4. Raphael Jowel
5. Venance Ndunga Power
6. Paul Mshimo
7. Paul Kamalamo
8. Leonard William Fweja -Amri Abeid (my dorm. mate)
9. Marco Waryoba
10. Ponsian Constantine
11. Emmanuel Ernest
12. Muungano James
13. Sophareth Magessa Kataso
14. Niva Michael -Lumumba
15. Maulid Gakole -Amri Abeid
16. Robinson Magambo -A.A
17. Patroba Materere -Shabaan Robert
18. Kasambalala Evaristi -Lumumba
19. Kizito Nkwabi- Lumumba
20. Alfred Andrew Auma -Mkwawa
21. Yusto sylvester 'VC' -
22. Mayunga ng'home -Amri abeid
23. ...........Kicheche (kamnyama) - Amri Abeid
24. (Super Short) Nyasanda -
25. ......Bondo -
26. Marwa Kenani - Amri Abeid
27. Msafiri (Traveller) -A.A
28. Chongo Cosmas -
29. Bartazar Chilato -Amri Abeid
30.Aruni Kitomwa (Form IB)-A.A
Zakayo Richard*

*Orodha ya wanafunzi wenzangu (classmates) 1984-87, MUSS.

Mabweni MUSS:
Amri Abeid
Shaaban Robert
Makongoro
Kimweri
Mkwawa
Milambo
Lumumba

Let's Share This ...

Your body is a bit slow when it comes to registering dehydration. By the time you feel thirsty you are already dehydrated.
The best advice is to sip some water little and often.
Don't wait till you are thirsty before drinking water!!!

G55

'Jamaa mmoja aliyekuwa anajitapa anajua sana kiingereza aliingia katika baa moja akawa anawaambia wenzake;
"do you know that SUGAR is the only word in english which starts with an S and U and yet it sounds like S, H & U?"'
Jamaa mmoja aliyekuwa amekaa pembeni akauliza 'are you SURE?'
-Jenerali Ulimwengu, MB (Vijana,CCM) 1990-95

Darasa la nne/tano

Natoa changamoto kwa mtoto yeyote aliye darasa la tano (kwa sasa) ambae atajaribu hili swali peke yake, halafu atoe comment zake hapo chini.
Mimi nilipokuwa darasa la nne au la tano nilipata shida sana kufanya hili swali na bado nalikumbuka sana!!!!

Swali:

Tafuta thamani ya a;

a/2 + 1 = a - 1

Onyesha njia na jawabu.

Heshima zenu!!!! BARANGA**

Baranga Boys/girls original
1. Marwa Richard -Std VIIB (my class mate)
2. Juma Marwa Chogoro -A
3. Naomi Matutu -B
4. Mbusiro Michael Kehengu-B
5. Rhobi Chacha Mosenye(?) -B
6. Chacha Nyamonge -Std VIA
7. Severina Joram -Std VIIA
8. Nyamahemba Washiki -B
9. Wesiko Marwa -B
10. Mwita Gati -B
11. Ogunya Mkama -B
13. Bhoke Magabe -B
14. Mtatiro Marwa Tyenyi -B
15. Bhoke Nyakorema -B
16. Rhobi Msoba -B
17. Chacha Nyamaranya -A
18. Nyawasha Machela -A
19. Elizabeth Wanda -A
20. Marwa Gati -A
21.Bhoke Sarya Mrisya -A
22. Charles Messanga -A
23. Mwita Magabe -A
24. Bhoke Magweiga Kisyeri -B
25. Nyamahemba Washiki-B
26. Chacha Mwita -A
27. Chacha Mwita -B
28. Mwita Mashauri -B
29. Chacha Mashauri -A
30.Mwita Marwa Kisyeri -B
31. Mwema Mnanka Samo -Std IVB
Musoma Wanda* - Std VIIA
Wegesa Wambura Nyakubhilela* -A
Ghati Magweiga Kisyeri* -A

*Orodha ya wanafunzi wenzangu Baranga Shule ya Msingi, Musoma (V), 1977-83

Usinichekeshe

Friend: Before my uncle became rich, he had nothing in his purse!
Bogi: My uncle didn't have even a purse!!!
(Courtesy: James Tumusiime, Bogi Benda)

Friday 15 June 2007

Manchester United

Fixtures 2007/08

Friendly Matches:
Tue 17/July Urawa Red Diamonds A 12:00
Fri 20/July FC Seoul A 12:00
Mon 23/July Shenzhen Jianlibao A 12:00
Wed 25/July Port Vale A 19:30
Wed 01/Aug Inter Milan H 19:45
Fri 03/Aug Doncaster Rovers A 19:45

Premier League
August
Sat 11 Reading H 15:00
Tue 14 Portsmouth A 15:00
Sat 18 Man City A 15:00
Sat 25 Tottenham H 15:00

September
Sat 01 Sunderland H 15;00
Sat 15 Everton A 15:00
Sat 22 Chelsea H
Sat 29 Birmingham A

October
Sat 06 Wigan

Thursday 14 June 2007

Poleni Brother George na Shemeji Georgia

Nimepokea habari za msiba wa mama yetu mpendwa kwa masikitiko makubwa. Kwa kweli mama ameacha pengo lisilozibika.
Poleni sana Nyakaho, Adam & family, Maula, Nuru na ukoo mzima, ndugu na marafiki.
Mimi pamoja na familia yangu tuko pamoja nayi ktk kipindi hiki cha majonzi. Na nawaombea faraja na moyo wa ustahimilivu katika kipindi hiki kigumu.
Mungu Awabariki sana.
Amen.

...nyumba jirani ...

Jaji mmoja mwandamizi amenusurika mvua (jela) baada ya kutuhumiwa kwa kosa la kum-flash mwana mama mmoja Oktoba 2006. Hakimu amesema kuwa mlalamikaji hakutoa ushahidi wa kutosha kutia hatiani mlalamikiwa.
Jaji mtuhumiwa huyo mkazi wa west London maeneo ya Wimbloden alituhumiwa kuwa ktk kipindi hicho Oktoba mara 2 alimvulia nguo za ndani dada huyo ndani ya treni. Ilibidi jaji atoe ushahidi kwa kutumia nguo yake ya ndani aina ya ck na kuonyesha ni jinsi gani ilivyo vigumu kumfunulia mtu maungo yake ya siri, tena ndani ya treni iliyojaa watu. Kwa hiyo huyo jaji alidai kuwa mlalamikaji alikosea kumtambua mtuhumiwa halisi (mistaken identity).
Baada ya hukumu Jaji na mkewe walifurahi na kusema sasa ataendelea na kazi yake kama kawaida maana jina lake limesafishwa.

Wednesday 13 June 2007

Nukuu Za Mwalimu J K Nyerere

'Hakuna umaskini mbaya kama umaskini wa mawazo, ni umaskini mbaya sana'
Mwalimu J. K. Nyerere, 01/5/1995.

'Njia ya kwenda jehanam imejaa tele nia njema'
Mwalimu Nyerere, 1994

'Mtu mwenye akili akikuambia neno la kipumbavu -ukalikubali, anakudharau!'
Mwalimu Nyerere 01/5/1995

Tuesday 12 June 2007

Jicho kwa Nyumba Jirani!

UK wana mpango wa kuanzisha 'compulsory volunteering' kwa vijana. Watu wanasema hii ni 'morden version' ya JKT tuliyokuwa nayo kwetu!
Kwa sasa wanao utaratibu wa Community Service Voluteering (CSV) ambao unafanya kazi.


There is a call to scrap Tests for all children at 7, 11 & 14.
The General Teaching Council (UK) study say that exams are failing to improve standards and put children off school. Also teachers are being forced to 'drill' children to pass tests (for the sake of schools' good positions on the league tables) rather than giving a broader education.
According to the study, exams leave pupils in a state of panic.


UK wameandaa utaratibu wa madaktari (GPs) kupewa nafasi ktk maduka makubwa ili watu waweze kuwaona madaktari bila kukatiza ratiba zao za kila siku! Kwa maana hiyo mtu akienda shopping anamwona daktari dukani huku shopping ikiendelea. Watu wako 'busy' kiasi cha kusahau au kuchoka kwenda hospitalini!


England goes smokefree on July, 01, 2007. It will be against the law to smoke in virtually all enclosed public places and work places. If someone does smoke in public he/she could be fined or end up in court.

Let's Share This

Diane Abbott, MP, has urged black Labour Party members to vote Jon Cruddas for the Deputy Labour Party Leadership post.
She said that he (Jon) will help ordinary black people and he's the change the Party needs. Other areas he will help include immigration and equal rights in employment especially on minimum wages and agency staffs to get equal treatment as permanent ones.

'Nukuu'

'Mimi sina kigugumizi katika kutoa uamuzi wa haki kwa sababu si wakala wa mtu yeyote. Serikali lazima isimame upande wa wanyonge, ikisimama upande mwingine wanyonge hao hawana pa kukimbilia'.
-Rais Jakaya Kikwete, 23/11/2006.

'Kasi ya serikali kushughulikia kero za wanachi ikiwemo rushwa ni ndogo ikilinganishwa na maneno yanayotolewa na viongozi wa serikali'
-Sheikh Suleiman Gologosi, Mkurugenzi, Idara ya Dini Bakwata, 05/12/2006.

'Siri ya Ndoa ... imarisha upendo, utulivu, kuheshimiana (achana na tamaa za kimwili)'.
-Flora Wingia, Maisha Ndivyo Yalivyo, 17/9/2006.

'Defeat at Southend (1-0, Carling Cup) was a timely reminder of the importance of hardwork'.
-Sir Alex Ferguson, Manager Manchester United, 10/11/2006.

'Tensions between migrants and local residents of flashpoints include noise from migrants, accommodation, parking, street drinking, and driving standards'.
-Spending Watchdog (UK), 31/01/2007.

'Politicians are masters at promising and not delivering'.
-Wooly word, Daily Star, 11/6/2007

'You have to fight a lot in life but you come out of it stronger and better'.
-Justine Henin, French Open Champion (Women), 11/6/2007

'Something that doesn't kill you makes you stronger'
-Jordan, Crystal Palace FC Chairman 2004/05 (?)

Monday 11 June 2007

Mko wapi?

Tafadhali tuwasiliane popote mlipo, mie hapa ndio maskani.

1. Bosco Kitura - Mazengo na Masange/Luwa JKT
2. Marwa Kenani - MUSS
3. Zephania Mongo (Mosonga) - MUSS
4. Ernest Makale

And who else ... yes, you who reads this!!!!!!!

Let's share this ...

How to take care of your few coins ...
1. budget properly
2. stick to budget
3. don't spend more than you earn
4. stop unnecessary purchase (careless spending)

Happy Birthday/Anniversary

Jengo jipya la Bunge la Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dodoma linatimiza mwaka mmoja hapo kesho 12/6/2007 tangu lilipofunguliwa rasmi mwaka uliopita na Rais Kikwete.

Napendekeza ...

Mabango/vibao, ukubwa wa maandishi, rangi za kuonyesha majina na anuani za shule za msingi na sekondari za serikali Tanzania ziwe na mfumo mmoja (format/standard).

I didn't know this, did you?

1. Everyday we take 21,600 breaths!

2. Eye tests are recommended every 2 years!

3. A human being have 2 sq.m. of skin (area) and that it weighs a total of 5kg!!

4. We shed 19kg. of skin in our life time!

5. Tony Blair's father was a Conservative (Torry) member who, at one time, wanted to contest for a Parliamentary seat through Torry ticket!!

Thursday 7 June 2007

Wise words

'The secret to happyness is accepting some miserable times are inevitable'
June 2007