Friday 15 May 2009

Kaka Miye!

Ijumaa Mei 15, 2009
Miaka ya 1980 nilikuwa napenda kupitia makala za Kaka Miye, ukurasa mmoja maarufu enzi hizo ktk gazeti la Jumapili la Chama Cha Mapinduzi (Mzalendo).

Sijui kama siku hizi makala hizo zinaendelea.

Pia Radio Tanzania (RTD) nao walikuwa na vipindi fulani vya ucheshi - Mahoka, sijui kama navyo viko hewani ktk muundo wa TBC ya sasa. Bahati mbaya hawa TBC hawana tovuti, ningeweza kufuatilia vipindi vyao vyote!

No comments: