Saturday 9 May 2009

BBC Parliament (mpya?)

Sat 09 May, 2009
BBC Parliament TV channel, wamebadili mfumo wa mpangilio (usanifu) na rangi za TV yao tangu April 22, 2009.
Awali walikuwa wanatumia rangi kama ya chungwa ila sasa wanatumia rangi ya udongo mwekundu sawa na ile inayotumiwa na wenzao wa BBC News (zamani BBC News 24).
Maandishi ya utambulisho yalikuwa yanaandikwa kushoto kwa screen na picha kubanwa upande wa pili, lakini sasa maandishi yote huwa chini ya picha kuu. Na kwa kusema kweli hivi sasa wanatumia mfumo na mpangilio wa BBC News.

Zile alama na rangi za 'logo' kuonyesha aina ya kikao kinachoonyeshwa hazipo tena. Kabla ya April 22, 2009 walitumia logo za House of Commons, za House of Lords, Za Wales, Scottish na Northern Ireland Assemblies kuonyesha kikao kinachoonyeshwa (sasa hazipo tena, nadhani hapo wahusika wamechemsha!)

Bajeti ya Uingereza mwaka huu ilitangazwa tarehe 22/April/2009 na waziri wa fedha wa UK, Chancellor of Exchequer mheshimiwa Alistair Darling.

No comments: