Monday 18 May 2009

'Mama' la madai yote!

Ktk sakata la kisiasa linaloendelea ktk visiwa vya Uk kuhusiana na madai 'hewa' au 'feki' ya gharama za matumizi ya wabunge ktk shughuli zao za kikazi, hii ya waziri wa mambo ya ndani ni kali zaidi.

Mume wa waziri huyo wa mambo ya ndani (home office) aliangalia picha za ngono za kulipia ktk luninga na kisha mke wake (ambae ni mbunge/waziri) akaenda kudai bungeni arejeshewe hela yake (paundi 10 za kuangalia picha 2 za ngono)!!!

Waziri anadai kuwa alipitiwa kwa bahati mbaya kuambatanisha risiti ya mambo ya ngono ktk madai.

Hata hivyo sijui kama waziri huyo atapona panga la waziri mkuu, ktk mabadiliko ya baraza la mawaziri yanayotarajiwa kufanyika baada ya uchaguzi wa serikali za mitaa na wabunge wa bunge la ulaya hapo Juni 04 mwaka huu ambapo chama tawala cha Labour kinatabiriwa kuanguka vibaya ktk chaguzi hizo.

Kwa habari zaidi kuhusiana na madai ya wabunge yasiyo na kichwa wala miguu, fuatilia matoleo ya gazeti la 'the daily telegraph'!

No comments: