Thursday 15 November 2007

Bkr zajengwa upya!

Hii habari ni kuhusu 'virginity repair'.

Kutokana na maadili ya ki-afrika ni vigumu kuiandika waziwazi hapa na kwa undani.

Ila kwa kifupi wapo wateja wa umri wa 'teens' na early 20s wa kike wanafanya 'procedure' hii Uingereza. Gharama zake ni Paundi 4,000/=, na hufanyika siku chache kabla ya mhusika kufunga ndoa na mume mtarajiwa. Zoezi hili humpumbaza 'mume' (pamoja na mashemeji/wakwe) siku ya kwanza ktk ndoa na hivyo kuwa na hisia kuwa ameoa mwanamke bikira.

Wasemaji kutoka wizara ya afya wanasema kuwa lengo lao ni kuhakikisha wanashughulika na kutoa huduma kwa ajili ya 'both physical and psychological health' ya wananchi wao.
Wengi wa wanaofika ktk hospitali kupata huduma hii ni kutoka 'ethnic minority' hasa wenye asili ya Asia wanaoishi Uingereza kwa sababu za imani zao kijamii, ambapo ni kashfa binti akipoteza bikira kabla ya kuolewa!

Huduma hii imekuwa ikitolewa kwa miaka 18 sasa. Nchi Asia, nyingine sheria haziruhusu!

No comments: