Thursday 11 September 2008

Tabia ya mtu

Zipo njia nyingi za kuweza kumuelewa au kumfahamu mtu kitabia au mwenendo wa kimaisha ikiwa haumuelewi au hamjafahamiana kwa kipindi kirefu au ndo mnakutana kwa mara ya kwanza.

Njia rahisi ambayo ninadhani inafaa kujua undani wa huyo mtu ni kupitia vyombo vya habari na pia kupitia njia ya maongezi ya kawaida au kwa simu.

Magazeti
Angalia anapenda kusoma magazeti gani (yapo magazeti ya aina na aina siasa, michezo na burudani n.k.). Pia ktk gazeti au magazeti anayopenda jaribu kuangalia anapenda kusoma kurasa gani -ukurasa wa mbele au nyuma (michezo) au za kati au hadithi, tamthiliya, makala n.k.

Redio na Televisheni
Siku hizi zipo stesheni nyingi sana za radio na TV. Je anasikiliza habari, miziki au michezo kwa upande wa radio. Kwenye Tv anapenda kuangalia nini zaidi.

Vitabu
Kama ni mpenzi wa vitabu anapendelea vitabu vya aina gani au fani gani; hadithi, sayansi, siasa, jamii, maisha n.k.

Hobby
Ni vitu gani anapendelea pale anapokuwa hana shughuli muhimu ya kufanya kutoka na kutembelea watu, kwenda kwenye kumbi za starehe au michezo, kufanya mazoezi n.k.

Maongezi ya kawaida
Ukiondoa salaam, kujuliana hali na kutambulishana, sehemu kubwa ya maongezi yanayofuata yanagusia au yanahusiana na nini.

Huwezi kukosa kumuelewa mtu kama utamtazama kwa tochi hii niliyodokeza. Hata busara na hekima za mtu huyo unaweza pia kuzipata kutumia tochi hiyo hiyo!

1 comment:

MOSONGA RAPHAEL said...

Ghorofa jingine la Wamachinga kujengwa Manispaa ya Temeke

2008-09-10 17:22:29
Na Sharon Sauwa, Temeke


Halamashauri ya Manispaa ya Temeke, Jijini Dar es Salaam imetoa notisi ya kutoendelezwa kwa maeneo waliyopewa katika soko la TAZARA Vetenary ili kupisha ujenzi wa Jengo la kisasa la wamachinga.

Meya wa Manispaa ya Temeke, Bw. Jerome Bwanausi, ameliambia Alasiri kuwa wafanyabiashara hao kuwa hivi sasa, tayari Manispaa hiyo imeshaanza kuandaa michoro kwa ajili ya ujenzi wa jengo hilo.

Hata hivyo, akasema bado haijafahamika jengo hilo litakuwa na uwezo wa kuchukua wafanyabiashara wangapi na gharama za ujenzi wake zikoje.

Akasema wawekezaji kutoka China wameonyesha nia ya kuingia ubia katika ujenzi wa jengo hilo.

"Tayari Halmashauri ya Temeke imeshatoa notisi kwa wafanyabiashara kutoendeleza maeneo hayo kwa ajili ya kujenga jengo hilo,"akasema Bw. Bwanausi na kuongeza kuwa wawekezaji hao kutoka China wamefika katika eneo hilo na kuliangalia.

Akasema wafanyabiashara ambao watatoka katika eneo hilo watapata nafasi katika jengo la wamachinga linalojengwa Kariakoo na kwamba wale watakaokosa nafasi watapewa kipaumbele katika jengo hilo la Tazara litakapokamilika.

Akasema utaratibu unaandaliwa kwa ajili ya kuwapatia nafasi katika jengo la Kariakoo, ili waweze kuachia nafasi kwa ajili ya kuanza ujenzi wa jengo hilo.

Hivi karibuni kundi la wafanyabiashara 68 kutoka katika soko hilo walielezea kuhusiana na kusimamishiwa kwa ujenzi wa vibanda vya biashara Tazara Vetenary.

Mwenyekiti wa wafanyabiashara hao Bw. Musa Kitenga, alisema waliiomba manispaa iyo iwapatie nafasi katika soko hilo kwa kipindi kirefu bila kujibiwa na hivyo kulazimika kumuona Diwani wa kata ya Chang'ombe, Bw. Noel Kipangule, ambaye aliuamuru uongozi wa soko kuwapatia nafasi.

Hata hivyo, akasema wakiwa katika ujenzi uongozi wa manispaa ulifika na kuwakataza kuendelea na ujenzi kwasababu diwani hakuwashirikisha katika maamuzi.

Akaiomba Serikali kuwapatia nafasi ya kufanyia biashara ili waweze kufanya shughuli zao na kuweza kujikimu kimaisha.

SOURCE: Alasiri