raffaeli (wimbo wa kizazi kipya)
nilienda moja kwa moja kwa raffaeli,
nikamkuta nyumbani anasikiliza r kelly,
nikamuuliza raffaeli,
unayo cd ya makaveli?
akaniambia ana cd ya makaveli,
r kelly,
na maria carey.
Showing posts with label Tanzania. Show all posts
Showing posts with label Tanzania. Show all posts
Wednesday, 17 June 2009
Friday, 5 June 2009
Jamii na maisha
Mvuto kwa vijana wa jinsia nyingine
Kuwa na hamu ya ngono ni sehemu ya ujinsia. Kufanya ngono ni namna moja ya kuonyesha ujinsia , lakini ia unaweza kuonyesha ujinsia huu kwa kuongea, kushikana mikono, kupigana busu, kushikanashikana na kupapasana.
Mara nyingi madhumuni ya kufanya ngono ni kutaka kuzaa mtoto. Sababu nyingine za kufanya ngono ni kwa kujifurahisha, kuonyesha mapenzi na kuimarisha uhusiano wa kimapenzi. Jambo la msingi ni kuwa hapo utakapoamua wakati umefika wa kujihusisha na ngono umefika zingatia hiyo ngono iwe salama na kuwa wote yaani wewe na mwenzi wako mifurahie hiyo ngono.
Zamani au hata mila na desturi na desturi zetu zimetufanya tufikiri kwamba mwanamke pekee yake ndiye mwenye jukumu la kumfurahisha mume kwenye ngono bila mume kujali kama mpenzi wake naye ametoshelezwa.
Siku hizi angalau mambo yameeanza kubadilika na wanaume wengi wanatambua umuhimu wa kujali kumtosheleza mwenzi wake wakati wa kujamiiana. Tendo la ngono linakuwa nzuri pale wote wahusika watakapokuwa wamefanya kwa hiari, wametoshelezana na ngono hiyo ilikuwa salama ( hakuna mimba kama haikutakiwa, wala magonjwa ya zinaa au maambukizo ya UKIMWI)
chanzo: tovuti ya cheza salama (tanzania)
Kuwa na hamu ya ngono ni sehemu ya ujinsia. Kufanya ngono ni namna moja ya kuonyesha ujinsia , lakini ia unaweza kuonyesha ujinsia huu kwa kuongea, kushikana mikono, kupigana busu, kushikanashikana na kupapasana.
Mara nyingi madhumuni ya kufanya ngono ni kutaka kuzaa mtoto. Sababu nyingine za kufanya ngono ni kwa kujifurahisha, kuonyesha mapenzi na kuimarisha uhusiano wa kimapenzi. Jambo la msingi ni kuwa hapo utakapoamua wakati umefika wa kujihusisha na ngono umefika zingatia hiyo ngono iwe salama na kuwa wote yaani wewe na mwenzi wako mifurahie hiyo ngono.
Zamani au hata mila na desturi na desturi zetu zimetufanya tufikiri kwamba mwanamke pekee yake ndiye mwenye jukumu la kumfurahisha mume kwenye ngono bila mume kujali kama mpenzi wake naye ametoshelezwa.
Siku hizi angalau mambo yameeanza kubadilika na wanaume wengi wanatambua umuhimu wa kujali kumtosheleza mwenzi wake wakati wa kujamiiana. Tendo la ngono linakuwa nzuri pale wote wahusika watakapokuwa wamefanya kwa hiari, wametoshelezana na ngono hiyo ilikuwa salama ( hakuna mimba kama haikutakiwa, wala magonjwa ya zinaa au maambukizo ya UKIMWI)
chanzo: tovuti ya cheza salama (tanzania)
Mwelekeo wa Bajeti ya 2009/10 TZ
Bajeti ya serikali kwa mwaka ujao wa fedha wa 2009/10 inatarajia kupanda kutoka Sh. trilioni 7.2 za mwaka huu hadi Sh. trilioni 9.5 ikiwa ni ongezeko la asilimia 32, ambayo imeainisha maeneo sita ya kipaumbele.
Akifafanua vipaumbele vya bajeti hiyo ambayo inatarajiwa kusomwa Alhamisi ijayo mjini Dodoma, Mkulo alisema:
-kipaumbele cha kwanza ni elimu ambayo imeongezewa fedha kwa asilimia 22 kutoka Sh. trilioni 1.4 ya mwaka 2008/09 hadi Sh. trilioni 1.7 mwaka ujao wa fedha. Lengo la kutenga kiasi hicho cha fedha ni kuimarisha ukaguzi wa elimu kwa ngazi zote nchi nzima.
-kipaumbele cha pili ni miundombinu ambayo bajeti yake imeongezeka kwa asilimia 12.7 ikilinganishwa na mwaka 2008/09. Katika mwaka wa fedha wa 2009/10, Wizara ya Miundombinu imetengewa Sh. trilioni 1.0 ikilinganishwa na bajeti inayomalizika ya Sh. bilioni 973.3. Serikali inatarajia kuboresha barabara, madaraja, bandari, viwanja vya ndege, kuimarisha mashirika ya reli (TAZARA na TRL) na Shirika la Ndege (ATCL).
-kipaumbele cha tatu ni afya ambayo imetengewa Sh. bilioni 963.0 kutoka Sh.bilioni 910.8 mwaka 2008/09. Kwenye Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, bajeti itajikita katika kutekeleza Mpango wa Maendeleo ya Afya ya Msingi (MMAM), kuimarisha ubora na upatikanaji wa huduma za uzazi na mtoto na kuimarisha rasilimali watu katika ngazi zote.
-kipaumbele cha nne ni kilimo ambacho kimeongezewa bajeti kwa asilimia 30 ikilinganishwa na mwaka jana ambapo bajeti ya wizara hiyo imepanda kutoka Sh. bilioni 513 mwaka unaomalizika hadi Sh. bilioni 666.9 mwaka ujao. Fungu kubwa katika sekta hii linaenda katika kuhakikisha upatikanaji wa pembejeo za kutosha kwa wakulima na wafugaji. Waziri Mkulo alisema katika kutekeleza kaulimbiu ya 'Kilimo Kwanza', serikali itaweka msukumo katika uanzishwaji na uendelezaji wa viwanda vya kusindika mazao ya kilimo na mifugo, viwanda vidogo vidogo, vya kati na vikubwa kwa kushirikiana na sekta binafsi.
-kipaumbele cha tano ni Wizara ya Maji ambayo imetengewa Sh. bilioni 347.3 mwaka huu kutoka Sh. bilioni 231.6 mwaka 2008/09. Hii ndiyo Wizara iliyoongezewa bajeti inayokaribia kufikia asilimia 50. Kipaumbele katika sekta ya maji ni kuboresha upatikanaji wa maji kwa ajili ya matumizi ya kawaida na umwagiliaji.
-kipaumbele cha sita ni Wizara ya Nishati na Madini ambayo hata hivyo, bajeti yake imeporomoka kwa asilimia 24.6 kutoka Sh. bilioni 378.8 mwaka huu hadi Sh. bilioni 285.5 mwaka ujao. Akifafanua sababu za bajeti ya Wizara hiyo kushuka, Waziri Mkulo alisema ni kutokana na kumalizika kwa mikataba ya kuzalisha umeme kwa makampuni matatu ya kukodi ambayo ni Dowans, Alstom Power Rental (APR) na Aggreko. Alisema kipaumbele cha Wizara kwa mwaka 2009/10 ni kuhakikisha upatikanaji wa umeme mijini na vijijini. Hata hivyo, alisema theluthi moja ya bajeti hiyo inatarajiwa kutoka kwa wafadhili.
CHANZO: NIPASHE 05-june-2009
Akifafanua vipaumbele vya bajeti hiyo ambayo inatarajiwa kusomwa Alhamisi ijayo mjini Dodoma, Mkulo alisema:
-kipaumbele cha kwanza ni elimu ambayo imeongezewa fedha kwa asilimia 22 kutoka Sh. trilioni 1.4 ya mwaka 2008/09 hadi Sh. trilioni 1.7 mwaka ujao wa fedha. Lengo la kutenga kiasi hicho cha fedha ni kuimarisha ukaguzi wa elimu kwa ngazi zote nchi nzima.
-kipaumbele cha pili ni miundombinu ambayo bajeti yake imeongezeka kwa asilimia 12.7 ikilinganishwa na mwaka 2008/09. Katika mwaka wa fedha wa 2009/10, Wizara ya Miundombinu imetengewa Sh. trilioni 1.0 ikilinganishwa na bajeti inayomalizika ya Sh. bilioni 973.3. Serikali inatarajia kuboresha barabara, madaraja, bandari, viwanja vya ndege, kuimarisha mashirika ya reli (TAZARA na TRL) na Shirika la Ndege (ATCL).
-kipaumbele cha tatu ni afya ambayo imetengewa Sh. bilioni 963.0 kutoka Sh.bilioni 910.8 mwaka 2008/09. Kwenye Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, bajeti itajikita katika kutekeleza Mpango wa Maendeleo ya Afya ya Msingi (MMAM), kuimarisha ubora na upatikanaji wa huduma za uzazi na mtoto na kuimarisha rasilimali watu katika ngazi zote.
-kipaumbele cha nne ni kilimo ambacho kimeongezewa bajeti kwa asilimia 30 ikilinganishwa na mwaka jana ambapo bajeti ya wizara hiyo imepanda kutoka Sh. bilioni 513 mwaka unaomalizika hadi Sh. bilioni 666.9 mwaka ujao. Fungu kubwa katika sekta hii linaenda katika kuhakikisha upatikanaji wa pembejeo za kutosha kwa wakulima na wafugaji. Waziri Mkulo alisema katika kutekeleza kaulimbiu ya 'Kilimo Kwanza', serikali itaweka msukumo katika uanzishwaji na uendelezaji wa viwanda vya kusindika mazao ya kilimo na mifugo, viwanda vidogo vidogo, vya kati na vikubwa kwa kushirikiana na sekta binafsi.
-kipaumbele cha tano ni Wizara ya Maji ambayo imetengewa Sh. bilioni 347.3 mwaka huu kutoka Sh. bilioni 231.6 mwaka 2008/09. Hii ndiyo Wizara iliyoongezewa bajeti inayokaribia kufikia asilimia 50. Kipaumbele katika sekta ya maji ni kuboresha upatikanaji wa maji kwa ajili ya matumizi ya kawaida na umwagiliaji.
-kipaumbele cha sita ni Wizara ya Nishati na Madini ambayo hata hivyo, bajeti yake imeporomoka kwa asilimia 24.6 kutoka Sh. bilioni 378.8 mwaka huu hadi Sh. bilioni 285.5 mwaka ujao. Akifafanua sababu za bajeti ya Wizara hiyo kushuka, Waziri Mkulo alisema ni kutokana na kumalizika kwa mikataba ya kuzalisha umeme kwa makampuni matatu ya kukodi ambayo ni Dowans, Alstom Power Rental (APR) na Aggreko. Alisema kipaumbele cha Wizara kwa mwaka 2009/10 ni kuhakikisha upatikanaji wa umeme mijini na vijijini. Hata hivyo, alisema theluthi moja ya bajeti hiyo inatarajiwa kutoka kwa wafadhili.
CHANZO: NIPASHE 05-june-2009
Friday, 22 May 2009
"Jengeni kwenu kwanza ..." - Kikwete
Friday, 22/05/2009
Rais Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa wajibu mkubwa wa Watanzania wanaoishi nchi za nje ni kufanya jitihada za kujenga na kuendeleza kwao, ili kuthibitisha ubora wa kuishi kwao nje.
Rais amesema kuwa na wala Watanzania hao wasihangaike na kutafuta jinsi ya kusaidia kuendeleza miradi mikubwa ya maendeleo kwa sababu shughuli hiyo ni wajibu wa Serikali na wanaweza wasiwe na uwezo wa kushiriki katika kuendeleza miradi hiyo mikubwa ya maendeleo.
“Mkiweza kupata mwekezaji mzuri, leteni tu. Mkipata mtu mwenye fedha za kusaidia ujenzi wa miradi mikubwa kama mabarabara na shule leteni, lakini ushauri wangu mkubwa kwenu ni huu… jengeni na endelezeni kwenu kwanza, ili mthibitishe kwa nini ni bora kuishi nje,” Rais Kikwete amewaambia Watanzania wanaoishi katika eneo la Kusini mwa Jimbo la California.
Akizungumza na Watanzania hao leo, Jumanne, Mei 19, 2009, kwenye Hoteli ya Beverly Hills Hilton mjini Los Angeles, Rais Kikwete amesema:
“Ujumbe wangu kwenu ni kwamba msisahau kwenu. Wathibitishie mliowaacha nyumbani kuwa ni bora zaidi kuishi huku mliko kuliko nyumbani. Jengeni kwenu, endelezeni kwenu. Msije kufikia mahali mnarudi nyumbani mkakosa hata mahali pa kufikia,” amewaambia Watanzania hao wanachama wa Chama cha Watanzania Wanaoishi Kusini mwa California.
Rais amewasisitizia Watanzania hao wakati akijibu maswali yao: “Tengenezeni kwenu. Haya makubwa ya ujenzi wa mabarabara, tuachie sisi wa Serikali, ndio maana tupo. Hatutaki kuwasumbua kwa masuala ya ujenzi wa barabara na shule. Hii ndiyo kazi na wajibu wetu. Nyie jengeni kwenu, ili ndugu zenu wajue kuwa kuishi kwenu nje kuna maana.”
Rais Kikwete ambaye amekutana na kuzungumza na Watanzania hao baada ya kuwa amewasili mjini Los Angeles akitokea mjini San Francisco ambako alianzia ziara yake ya Marekani pia ametumia muda mwingi kuelezea mambo makubwa yaliyofanywa na Serikali yake ikiwa ni pamoja na ujenzi wa shule 2,700 za sekondari katika miaka mitatu iliyopita.
Rais amezungumzia mafanikio makubwa yaliyopatikana katika sekta za elimu, afya, ujenzi wa barabara, akisisitiza kuwa, kwa mfano, kiwango cha malaria nchini kimepungua kwa kiasi cha asilimia 38 katika miaka mitatu kutokana na maamuzi ya Serikali tokea iingie madarakani.
“Ni kweli kuwa malaria inabakia ugonjwa unaoua watu wengi zaidi nchini, lakini hatua tulizozichukua katika miaka mitatu, minne iliyopita, zimepunguza kiwango cha malaria kwa asilimia 38. Katika Zanzibar ni kama tumemaliza ungonjwa huo kabisa.”
Rais pia amewaeleza Watanzania hao kuhusu mpango mkubwa wa Serikali kujenga zahanati kila kijiji na kituo cha afya kila kata nchini akiongeza:
“Hata kwa yale magonjwa ambayo tumekuwa tunalazimika kuwapeleka watu nje, tunachukua hatua. Kwa mfano, Wachina wamekubali kutujengea hospitali kubwa ya kutibu magonjwa ya moyo.”
(Source: Ikulu Mawasiliano (Blog). Tuesday, May 19, 2009)
Rais Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa wajibu mkubwa wa Watanzania wanaoishi nchi za nje ni kufanya jitihada za kujenga na kuendeleza kwao, ili kuthibitisha ubora wa kuishi kwao nje.
Rais amesema kuwa na wala Watanzania hao wasihangaike na kutafuta jinsi ya kusaidia kuendeleza miradi mikubwa ya maendeleo kwa sababu shughuli hiyo ni wajibu wa Serikali na wanaweza wasiwe na uwezo wa kushiriki katika kuendeleza miradi hiyo mikubwa ya maendeleo.
“Mkiweza kupata mwekezaji mzuri, leteni tu. Mkipata mtu mwenye fedha za kusaidia ujenzi wa miradi mikubwa kama mabarabara na shule leteni, lakini ushauri wangu mkubwa kwenu ni huu… jengeni na endelezeni kwenu kwanza, ili mthibitishe kwa nini ni bora kuishi nje,” Rais Kikwete amewaambia Watanzania wanaoishi katika eneo la Kusini mwa Jimbo la California.
Akizungumza na Watanzania hao leo, Jumanne, Mei 19, 2009, kwenye Hoteli ya Beverly Hills Hilton mjini Los Angeles, Rais Kikwete amesema:
“Ujumbe wangu kwenu ni kwamba msisahau kwenu. Wathibitishie mliowaacha nyumbani kuwa ni bora zaidi kuishi huku mliko kuliko nyumbani. Jengeni kwenu, endelezeni kwenu. Msije kufikia mahali mnarudi nyumbani mkakosa hata mahali pa kufikia,” amewaambia Watanzania hao wanachama wa Chama cha Watanzania Wanaoishi Kusini mwa California.
Rais amewasisitizia Watanzania hao wakati akijibu maswali yao: “Tengenezeni kwenu. Haya makubwa ya ujenzi wa mabarabara, tuachie sisi wa Serikali, ndio maana tupo. Hatutaki kuwasumbua kwa masuala ya ujenzi wa barabara na shule. Hii ndiyo kazi na wajibu wetu. Nyie jengeni kwenu, ili ndugu zenu wajue kuwa kuishi kwenu nje kuna maana.”
Rais Kikwete ambaye amekutana na kuzungumza na Watanzania hao baada ya kuwa amewasili mjini Los Angeles akitokea mjini San Francisco ambako alianzia ziara yake ya Marekani pia ametumia muda mwingi kuelezea mambo makubwa yaliyofanywa na Serikali yake ikiwa ni pamoja na ujenzi wa shule 2,700 za sekondari katika miaka mitatu iliyopita.
Rais amezungumzia mafanikio makubwa yaliyopatikana katika sekta za elimu, afya, ujenzi wa barabara, akisisitiza kuwa, kwa mfano, kiwango cha malaria nchini kimepungua kwa kiasi cha asilimia 38 katika miaka mitatu kutokana na maamuzi ya Serikali tokea iingie madarakani.
“Ni kweli kuwa malaria inabakia ugonjwa unaoua watu wengi zaidi nchini, lakini hatua tulizozichukua katika miaka mitatu, minne iliyopita, zimepunguza kiwango cha malaria kwa asilimia 38. Katika Zanzibar ni kama tumemaliza ungonjwa huo kabisa.”
Rais pia amewaeleza Watanzania hao kuhusu mpango mkubwa wa Serikali kujenga zahanati kila kijiji na kituo cha afya kila kata nchini akiongeza:
“Hata kwa yale magonjwa ambayo tumekuwa tunalazimika kuwapeleka watu nje, tunachukua hatua. Kwa mfano, Wachina wamekubali kutujengea hospitali kubwa ya kutibu magonjwa ya moyo.”
(Source: Ikulu Mawasiliano (Blog). Tuesday, May 19, 2009)
Friday, 24 April 2009
Enough is enough: Reginald shows the way
IPP Limited Executive Chairman Reginald Mengi:
``Our country is currently facing a huge problem of corruption and is troubled by the fact that the people involved in acts of corruption do not what to be touched.
``The great efforts of His Excellency the President to hasten economic development and better living for every Tanzanian are weakened by the horrendous theft of national resources.
A great majority of Tanzanians still face extreme poverty; they are unable to determine where the one meal a day is going to come from.
``I would like to conclude by saying that all corrupt people and especially those who are being accused of notorious corruption must be dealt with conclusively, otherwise they will rock the stability of our nation. We must realise that we have now reached the stage when we must say enough is enough.``
SOURCE: Guardian, 2009-04-24 12:52:23
By Patrick Kisembo
``Our country is currently facing a huge problem of corruption and is troubled by the fact that the people involved in acts of corruption do not what to be touched.
``The great efforts of His Excellency the President to hasten economic development and better living for every Tanzanian are weakened by the horrendous theft of national resources.
A great majority of Tanzanians still face extreme poverty; they are unable to determine where the one meal a day is going to come from.
``I would like to conclude by saying that all corrupt people and especially those who are being accused of notorious corruption must be dealt with conclusively, otherwise they will rock the stability of our nation. We must realise that we have now reached the stage when we must say enough is enough.``
SOURCE: Guardian, 2009-04-24 12:52:23
By Patrick Kisembo
Tuesday, 21 April 2009
Demokrasia Tanzania
Tue. 21/04/2009
Vyama vya siasa vilivyoshiriki uchaguzi mkuu 2005 na kusimamisha wagombea urais (serikali zote 2) - Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
1. CCM (Chama Cha Mapinduzi) - Jakaya Mrisho Kikwete (Amani Karume, Z'bar)
2. TLP (Tanzania Labour Party) - Augostino Lyatonga Mrema
3. UDP (United Democratic Party) - John Momose Cheyo
4. NLD (National League for Democracy) - Emmanuel Makaidi
5. NCCR-Mageuzi (National Constitution Construction and Reform) - Dk Sengondo Mvungi
6. CUF (Civic United Front) - Prof Ibrahim Lipumba (Seif Shariff Hamadi, Z'bar)
7. DP (Democratic Party) - Mchungaji Christopher Mtikila
8. Demokrasia Makini - Profesa Leonard Shayo*
9. CHAUSTA (Chama cha Haki na Ustawi Tanzania) - James Mapalala
10. TADEA (Tanzania democratic Alliance) - John Lifa Chipaka
11. CHADEMA (Chama Cha Demcrasia na Maendeleo) - Freeman Mbowe
12. SAU (Sauti ya Umma) -
13. NRA (National ... Alliance) -
14. Jahazi Asilia -
15. UMD (Union for Multi-party Democracy) -
16. FORD (...) forum for demcracy?? -
17. UPDP (United People's Demcratic Party) - Omar Awes Dadi, Z'bar
18. PPT Maendeleo (....??) - Bi. Claudia Senkoro
Missing in the List(!?) where are they now?
TPP (Tanzania People's Party) - Dr Alec Che-Mponda (founder and first leader)
Vyama vya siasa vilivyoshiriki uchaguzi mkuu 2005 na kusimamisha wagombea urais (serikali zote 2) - Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
1. CCM (Chama Cha Mapinduzi) - Jakaya Mrisho Kikwete (Amani Karume, Z'bar)
2. TLP (Tanzania Labour Party) - Augostino Lyatonga Mrema
3. UDP (United Democratic Party) - John Momose Cheyo
4. NLD (National League for Democracy) - Emmanuel Makaidi
5. NCCR-Mageuzi (National Constitution Construction and Reform) - Dk Sengondo Mvungi
6. CUF (Civic United Front) - Prof Ibrahim Lipumba (Seif Shariff Hamadi, Z'bar)
7. DP (Democratic Party) - Mchungaji Christopher Mtikila
8. Demokrasia Makini - Profesa Leonard Shayo*
9. CHAUSTA (Chama cha Haki na Ustawi Tanzania) - James Mapalala
10. TADEA (Tanzania democratic Alliance) - John Lifa Chipaka
11. CHADEMA (Chama Cha Demcrasia na Maendeleo) - Freeman Mbowe
12. SAU (Sauti ya Umma) -
13. NRA (National ... Alliance) -
14. Jahazi Asilia -
15. UMD (Union for Multi-party Democracy) -
16. FORD (...) forum for demcracy?? -
17. UPDP (United People's Demcratic Party) - Omar Awes Dadi, Z'bar
18. PPT Maendeleo (....??) - Bi. Claudia Senkoro
Missing in the List(!?) where are they now?
TPP (Tanzania People's Party) - Dr Alec Che-Mponda (founder and first leader)
Wednesday, 8 April 2009
Karume Day
Wednesday, April 08, 2009
Jana Tanzania iliadhimisha siku ambayo Rais wa kwanza wa Zanzibar aliuwawa huko Unguja tarehe 07/April/1972.
Karume Day ni siku ya mapumziko ktk kalenda ya shughuli za serilari nchini Tanzania.
Jana Tanzania iliadhimisha siku ambayo Rais wa kwanza wa Zanzibar aliuwawa huko Unguja tarehe 07/April/1972.
Karume Day ni siku ya mapumziko ktk kalenda ya shughuli za serilari nchini Tanzania.
Thursday, 2 April 2009
Rais Kikwete na sera ya 'Umwagiliaji'*
'Aidha, nawaomba tuendelee kuomba dua Mwenyezi Mungu atujalie mvua itakayonusuru mazao mashambani na kutuepusha na tatizo la upungufu wa chakula mwaka huu.'
-Rais J.Kikwete, 31/03/2009
*Hii ni kauli ya Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete.
Nilitegemea angeongelea mkakati kabambe wa umwagiliaji maji kutoka ktk vyanzo mbalimbali vya maji hapa nchini ili kuepuka utegemezi wa mvua zisizo na uhakika!
Kwa mtaji huu, hata g50 hatuwezi kuwemo karne ijayo!
-Rais J.Kikwete, 31/03/2009
*Hii ni kauli ya Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete.
Nilitegemea angeongelea mkakati kabambe wa umwagiliaji maji kutoka ktk vyanzo mbalimbali vya maji hapa nchini ili kuepuka utegemezi wa mvua zisizo na uhakika!
Kwa mtaji huu, hata g50 hatuwezi kuwemo karne ijayo!
Rais Kikwete na mgao wa umeme Dar
Thu. April 02, 2009
Hali ya Upatikanaji wa Umeme Nchini
Ndugu Wananchi,Kwa takriban miezi mwili sasa umeme umekuwa gumzo kubwa hapa nchini. Mjadala umekuwa wa namna mbili.
Kwanza umehusu nia ya Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) kununua mitambo ya Kampuni ya Dowans pale Ubungo.
Na, pili, umehusu mgao wa umeme unaoendelea tangu tarehe 26 Machi, 2009 mpaka sasa hasa hapa Dar es Salaam na wilaya jirani.
Mgao wa Umeme
Ndugu Wananchi,Kiini cha kuwepo kwa mgao wa umeme ni kuharibika kwa mitambo miwili ya kuzalisha MW 53 za umeme katika kituo cha kuzalisha umeme cha SONGAS. Jumamosi tarehe 28 Machi, 2009 mtambo mmoja wenye uwezo wa kuzalisha MW 20 ulitengemaa hivyo upungufu umebaki MW 33 kutoka kwenye mashine ya pili.
Taarifa niliyopewa leo ni kuwa hitilafu yake ni kubwa hivyo huenda ikachukua mpaka wiki mbili au tatu au zaidi kutengemaa. Maana yake ni kwamba mgao utaendelea kuwepo kwa kipindi hicho.
Hivyo, Ndugu zangu, mgao huu hauna uhusiano na ile hadhari aliyoitoa Dkt. Idris Rashid, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO alipokuwa akizungumzia suala la Dowans kuwa nchi inaweza kuingia kwenye giza siku za usoni.
Ndugu Wananchi;
Kwa mujibu wa wataalamu wa TANESCO, mfumo wetu wa umeme nchini, kwa sasa, hauna ziada ya umeme unaosubiri kutumika kama akiba. Kutokana na hali hiyo, kunapotokea upungufu wowote wa uzalishaji wa umeme kwa sababu yoyote ile, kama huu uliotokea tarehe 26 Machi, 2009, husababisha kuwepo kwa mgao wa umeme kwa watumiaji.
Umeme wote unaozalishwa hapa nchini hutumika na wala mahitaji halisi hayajatoshelezwa. Kimsingi umeme unaopatikana na kutumika ni chini ya mahitaji (supressed demand). Ni asilimia 14 tu ya Watanzania ndiyo wanaopata na kutumia umeme wakati watu wengi sana wanaohitaji umeme bado hawajapata.
Ndugu Wananchi;
Wakati wote Serikali kwa kushirikiana na TANESCO imekuwa na mipango ya kuongeza uzalishaji na usambazaji wa umeme nchini. Kwa upande wa uzalishaji kumekuwepo hata na ratiba ya lini, kituo kipi na cha ukubwa gani kinaratajiwa kuwepo. Utekelezaji wa mipango hiyo ndiyo iliyotufikisha hapa tulipo sasa.
Mwaka 2007, kufuatia matatizo makubwa ya umeme unaozalishwa kwa nguvu ya maji, mpango huo ukaboreshwa na kuongezwa ujenzi wa vituo vya kutumia gesi asilia na makaa ya mawe. Utekelezaji wa mpango wa uzalishaji wa umeme kwa mujibu wa uboreshaji uliofanywa mwaka 2007 uko nyuma ya wakati. Mradi wa kuzalisha umeme wa megawati 200 kwa kutumia makaa ya mawe Kiwira umechelewa kwa sababu ya ugumu wa kupata mikopo kutoka kwenye vyombo vya fedha. Kiini cha tatizo ni hofu inayotokana na taarifa hasi kuhusu mradi huo. Mradi wa kuzalisha megawati 300 kutokana na gesi asilimia ya Mnazi Bay unacheleweshwa na matatizo ya sasa ya kudorora kwa uchumi wa dunia ambapo nimeambiwa kwamba wabia muhimu wamejitoa kwa sasa.
Ndugu Wananchi,
Kuchelewa kutekelezwa kwa miradi hiyo ni dalili kuwa baada ya muda si mrefu hali ya upatikanaji wa umeme itakuwa mbaya hata kama mitambo yote ya sasa itakuwa inafanya kazi kwa ukamilifu. Kwa sasa mahitaji yanaongezeka kwa asilimia 10 – 15 kwa mwaka. Hili ni ongezeko kubwa sana ambalo linahitaji kusiwepo kukwama kokote. Kwa nia ya kutaka kupunguza makali ya tatizo hilo, ndipo uongozi wa TANESCO ukaona waombe kununua mitambo ya Dowans ambayo wakati huo ilikuwa inatangazwa kuuzwa. Uamuzi huo ukazua mtafaruku mkubwa ambao sina haja ya kuelezea kwa kirefu kwani wengi wetu tunaufahamu vizuri. Baada ya kuona ugumu wa kuendelea na nia hiyo, uongozi wa TANESCO umechukua uamuzi wa kuachana na nia yao hiyo.
Ndugu Wananchi;
Katika taarifa yake ya kutamka uamuzi wa kuachana na nia ya kununua mitambo ya Dowans, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO alielezea hofu yake kwamba uamuzi huo unaweza kusababisha nchi kuwa gizani hapo baadaye. Taarifa hiyo imeleta hofu kubwa katika jamii. Nataka kuwatoa hofu na kuwahakikishia Watanzania wenzangu wote kuwa Serikali itafanya kila iwezalo kuhakikisha kuwa nchi yetu haifikii hatua hiyo. Tutahakikisha kuwa nchi haiwi gizani na kwamba umeme wa ziada unaotakiwa utapatikana na shughuli za uzalishaji mali na utoaji huduma zitaendelea kama kawaida.
Ndugu Wananchi;
Tayari Wizara ya Nishati na Madini imeshaanza kuchukua hatua ambazo zinaonesha kuwa na mwelekeo wa kutia matumaini. Naamini tutafanikiwa. Tukiwa tayari, taarifa itatolewa. Penye nia pana njia.
Napenda kutumia nafasi hii kusema mambo mawili.
Kwanza, kwamba, nawapongeza viongozi wa TANESCO kwa uamuzi wao wa busara wa kuachana na nia yao ya kununua mitambo ya Dowans. Wameyasoma vizuri mazingira na nyakati na kufanya uamuzi muafaka.
Pili, niwaombe wanasiasa wenzangu kuwa, maadam waliokuwa na nia ya kununua mitambo hiyo hawanayo tena, suala hili limemalizika.
Sioni sababu ya kuendelea kulumbana, kutiana vidole machoni na kutoleana maneno makali na mengine hata hayastahili kusemwa. Tumekuwa tunawatia hofu wananchi kwa jambo lisilokuwepo tena. Nawaomba muzihifadhi nguvu zenu na bongo zenu ili muwafanyie wananchi mambo yenye tija kwao. Wanalo jukumu kubwa la kujiletea maendeleo kwa lengo la kujiondoa kwenye umaskini na kuwa na hali bora ya maisha yao.
Uongozi wetu wanasiasa unahitajika sana katika juhudi zao hizo. Tuelekeze nguvu zetu na maarifa yetu huko. Wapeni pumzi wananchi kutokana na malumbano haya.
(hotuba ya Rais, 31/march/2009)
Hali ya Upatikanaji wa Umeme Nchini
Ndugu Wananchi,Kwa takriban miezi mwili sasa umeme umekuwa gumzo kubwa hapa nchini. Mjadala umekuwa wa namna mbili.
Kwanza umehusu nia ya Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) kununua mitambo ya Kampuni ya Dowans pale Ubungo.
Na, pili, umehusu mgao wa umeme unaoendelea tangu tarehe 26 Machi, 2009 mpaka sasa hasa hapa Dar es Salaam na wilaya jirani.
Mgao wa Umeme
Ndugu Wananchi,Kiini cha kuwepo kwa mgao wa umeme ni kuharibika kwa mitambo miwili ya kuzalisha MW 53 za umeme katika kituo cha kuzalisha umeme cha SONGAS. Jumamosi tarehe 28 Machi, 2009 mtambo mmoja wenye uwezo wa kuzalisha MW 20 ulitengemaa hivyo upungufu umebaki MW 33 kutoka kwenye mashine ya pili.
Taarifa niliyopewa leo ni kuwa hitilafu yake ni kubwa hivyo huenda ikachukua mpaka wiki mbili au tatu au zaidi kutengemaa. Maana yake ni kwamba mgao utaendelea kuwepo kwa kipindi hicho.
Hivyo, Ndugu zangu, mgao huu hauna uhusiano na ile hadhari aliyoitoa Dkt. Idris Rashid, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO alipokuwa akizungumzia suala la Dowans kuwa nchi inaweza kuingia kwenye giza siku za usoni.
Ndugu Wananchi;
Kwa mujibu wa wataalamu wa TANESCO, mfumo wetu wa umeme nchini, kwa sasa, hauna ziada ya umeme unaosubiri kutumika kama akiba. Kutokana na hali hiyo, kunapotokea upungufu wowote wa uzalishaji wa umeme kwa sababu yoyote ile, kama huu uliotokea tarehe 26 Machi, 2009, husababisha kuwepo kwa mgao wa umeme kwa watumiaji.
Umeme wote unaozalishwa hapa nchini hutumika na wala mahitaji halisi hayajatoshelezwa. Kimsingi umeme unaopatikana na kutumika ni chini ya mahitaji (supressed demand). Ni asilimia 14 tu ya Watanzania ndiyo wanaopata na kutumia umeme wakati watu wengi sana wanaohitaji umeme bado hawajapata.
Ndugu Wananchi;
Wakati wote Serikali kwa kushirikiana na TANESCO imekuwa na mipango ya kuongeza uzalishaji na usambazaji wa umeme nchini. Kwa upande wa uzalishaji kumekuwepo hata na ratiba ya lini, kituo kipi na cha ukubwa gani kinaratajiwa kuwepo. Utekelezaji wa mipango hiyo ndiyo iliyotufikisha hapa tulipo sasa.
Mwaka 2007, kufuatia matatizo makubwa ya umeme unaozalishwa kwa nguvu ya maji, mpango huo ukaboreshwa na kuongezwa ujenzi wa vituo vya kutumia gesi asilia na makaa ya mawe. Utekelezaji wa mpango wa uzalishaji wa umeme kwa mujibu wa uboreshaji uliofanywa mwaka 2007 uko nyuma ya wakati. Mradi wa kuzalisha umeme wa megawati 200 kwa kutumia makaa ya mawe Kiwira umechelewa kwa sababu ya ugumu wa kupata mikopo kutoka kwenye vyombo vya fedha. Kiini cha tatizo ni hofu inayotokana na taarifa hasi kuhusu mradi huo. Mradi wa kuzalisha megawati 300 kutokana na gesi asilimia ya Mnazi Bay unacheleweshwa na matatizo ya sasa ya kudorora kwa uchumi wa dunia ambapo nimeambiwa kwamba wabia muhimu wamejitoa kwa sasa.
Ndugu Wananchi,
Kuchelewa kutekelezwa kwa miradi hiyo ni dalili kuwa baada ya muda si mrefu hali ya upatikanaji wa umeme itakuwa mbaya hata kama mitambo yote ya sasa itakuwa inafanya kazi kwa ukamilifu. Kwa sasa mahitaji yanaongezeka kwa asilimia 10 – 15 kwa mwaka. Hili ni ongezeko kubwa sana ambalo linahitaji kusiwepo kukwama kokote. Kwa nia ya kutaka kupunguza makali ya tatizo hilo, ndipo uongozi wa TANESCO ukaona waombe kununua mitambo ya Dowans ambayo wakati huo ilikuwa inatangazwa kuuzwa. Uamuzi huo ukazua mtafaruku mkubwa ambao sina haja ya kuelezea kwa kirefu kwani wengi wetu tunaufahamu vizuri. Baada ya kuona ugumu wa kuendelea na nia hiyo, uongozi wa TANESCO umechukua uamuzi wa kuachana na nia yao hiyo.
Ndugu Wananchi;
Katika taarifa yake ya kutamka uamuzi wa kuachana na nia ya kununua mitambo ya Dowans, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO alielezea hofu yake kwamba uamuzi huo unaweza kusababisha nchi kuwa gizani hapo baadaye. Taarifa hiyo imeleta hofu kubwa katika jamii. Nataka kuwatoa hofu na kuwahakikishia Watanzania wenzangu wote kuwa Serikali itafanya kila iwezalo kuhakikisha kuwa nchi yetu haifikii hatua hiyo. Tutahakikisha kuwa nchi haiwi gizani na kwamba umeme wa ziada unaotakiwa utapatikana na shughuli za uzalishaji mali na utoaji huduma zitaendelea kama kawaida.
Ndugu Wananchi;
Tayari Wizara ya Nishati na Madini imeshaanza kuchukua hatua ambazo zinaonesha kuwa na mwelekeo wa kutia matumaini. Naamini tutafanikiwa. Tukiwa tayari, taarifa itatolewa. Penye nia pana njia.
Napenda kutumia nafasi hii kusema mambo mawili.
Kwanza, kwamba, nawapongeza viongozi wa TANESCO kwa uamuzi wao wa busara wa kuachana na nia yao ya kununua mitambo ya Dowans. Wameyasoma vizuri mazingira na nyakati na kufanya uamuzi muafaka.
Pili, niwaombe wanasiasa wenzangu kuwa, maadam waliokuwa na nia ya kununua mitambo hiyo hawanayo tena, suala hili limemalizika.
Sioni sababu ya kuendelea kulumbana, kutiana vidole machoni na kutoleana maneno makali na mengine hata hayastahili kusemwa. Tumekuwa tunawatia hofu wananchi kwa jambo lisilokuwepo tena. Nawaomba muzihifadhi nguvu zenu na bongo zenu ili muwafanyie wananchi mambo yenye tija kwao. Wanalo jukumu kubwa la kujiletea maendeleo kwa lengo la kujiondoa kwenye umaskini na kuwa na hali bora ya maisha yao.
Uongozi wetu wanasiasa unahitajika sana katika juhudi zao hizo. Tuelekeze nguvu zetu na maarifa yetu huko. Wapeni pumzi wananchi kutokana na malumbano haya.
(hotuba ya Rais, 31/march/2009)
Rais Kikwete na g20
Thursday, April 02, 2009
Mkutano wa G-20
Ndugu Wananchi;
Jambo la mwisho ambalo ningependa kuliongelea leo hii ni kuhusu msukusuko wa uchumi wa dunia na hasa mkutano wa Kundi la Nchi Ishirini Tajiri Duniani (G-20) ambao unategemewa kufanyika kesho tarehe 2 Aprili na kumazika tarehe 3 Aprili, 2009 mjini London, Uingereza. Mkutano huu umeitishwa kutafuta njia za pamoja za kukabili kudorora kwa uchumi duniani.
Mataifa haya tajiri ishirini, ambayo yanamiliki asilimia 85 ya uchumi wa dunia ni pamoja na Marekani, Uingereza, China, Japan, Ujerumani, Ufaransa, Afrika ya Kusini, Australia, Uturuki, Brazil, Canada, Argentina, Mexico, Indonesia, India, Italy, Urusi, Korea Kusini, Umoja wa Nchi za Ulaya na Saudi Arabia.
Kwa muhtasari, matarajio ya Afrika katika mkutano wa G-20 ni kwa Afrika kusaidiwa kujikinga na kukabili madhara ya kudorora kwa uchumi wa dunia.
Miongoni mwa mambo ambayo tuliyasisitiza ni;
1. haja ya kuanzishwa mfuko maalum ambapo fedha zake zitatumika kuzisaidia nchi za Afrika kuchukua hatua za kunusuru uchumi wao kama wafanyavyo mataifa tajiri.Kwa maneno mengine tuliunga mkono pendekezo la Benki ya Dunia na kutaka Mkutano wa G-20 ukubali kwamba asilimia 0.7 ya fedha walizotumia kugharamia mipango yao ya kuchochea uchumi wao (stimulus packages) zitengwe kwa ajili ya kusaidia kuchochea kukua kwa uchumi kwa nchi za Afrika.
2. tulisitiza kuwa nchi tajiri zisipunguze misaada ya maendeleo kwa nchi maskini. Badala yake misaada hiyo iongezwe kama walivyoahidi kwenye mikutano ya Monterrey, Gleneagles na kwingineko.
3. tulisema kwamba tunatarajia pia misaada kwa Afrika, na uwekezaji kutoka nje vitaelekezwa katika kujenga na kuboresha miundombinu, kuleta mapinduzi katika kilimo, kukuza biashara miongoni mwa nchi za Kiafrika na baina yake na nchi nyingine za dunia na kusaidia zaidi makundi katika jamii ambayo yanahitaji msaada zaidi (vulnerable groups).
4. kwamba nchi tajiri duniani pamoja na Taasisi za Kimataifa za Fedha Duniani zilegeze masharti na kupunguza urasimu wa kupata fedha za misaada na mikopo kwa kutambua kwamba hiki ni kipindi kugumu na cha dharura.
Aidha, masharti ya kukopa kutoka vyombo vingine vya fedha yalegezwe pia.
5. kwamba nchi tajiri zisaidie nchi za Afrika kujenga mitaji ya vyombo vya fedha vya kikanda kama vile Benki ya Maendeleo ya Afrika.
6. kwamba, nchi tajiri zitakubaliana kuruhusu uwazi katika mabenki yao na taasisi zao za fedha ili kuwezesha nchi za Kiafrika kufuatilia na kurudishiwa fedha, majumba na rasilimali zilizoporwa kutoka katika bara letu na kuhifadhiwa kisirisiri katika mabenki ya nchi tajiri.
Ndugu Wananchi, Tunamshukuru Mheshimiwa Waziri Mkuu Gordon Brown kwa kuyapokea mapendekezo haya ya Afrika kwa moyo mkunjufu na kuahidi kuyafikisha na kusaidia kuyatetea katika kikao hicho. Pia tunamshukuru amepokea rai ya Afrika ya kuwakilishwa kwenye mkutano huo kwa kumwalika Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mhe. Meles Zenawi, ambaye atatuwakilisha kwa kofia yake ya Uenyekiti wa NEPAD.
(hotuba ya Mhe Rais, 31/March/2009)
Mkutano wa G-20
Ndugu Wananchi;
Jambo la mwisho ambalo ningependa kuliongelea leo hii ni kuhusu msukusuko wa uchumi wa dunia na hasa mkutano wa Kundi la Nchi Ishirini Tajiri Duniani (G-20) ambao unategemewa kufanyika kesho tarehe 2 Aprili na kumazika tarehe 3 Aprili, 2009 mjini London, Uingereza. Mkutano huu umeitishwa kutafuta njia za pamoja za kukabili kudorora kwa uchumi duniani.
Mataifa haya tajiri ishirini, ambayo yanamiliki asilimia 85 ya uchumi wa dunia ni pamoja na Marekani, Uingereza, China, Japan, Ujerumani, Ufaransa, Afrika ya Kusini, Australia, Uturuki, Brazil, Canada, Argentina, Mexico, Indonesia, India, Italy, Urusi, Korea Kusini, Umoja wa Nchi za Ulaya na Saudi Arabia.
Kwa muhtasari, matarajio ya Afrika katika mkutano wa G-20 ni kwa Afrika kusaidiwa kujikinga na kukabili madhara ya kudorora kwa uchumi wa dunia.
Miongoni mwa mambo ambayo tuliyasisitiza ni;
1. haja ya kuanzishwa mfuko maalum ambapo fedha zake zitatumika kuzisaidia nchi za Afrika kuchukua hatua za kunusuru uchumi wao kama wafanyavyo mataifa tajiri.Kwa maneno mengine tuliunga mkono pendekezo la Benki ya Dunia na kutaka Mkutano wa G-20 ukubali kwamba asilimia 0.7 ya fedha walizotumia kugharamia mipango yao ya kuchochea uchumi wao (stimulus packages) zitengwe kwa ajili ya kusaidia kuchochea kukua kwa uchumi kwa nchi za Afrika.
2. tulisitiza kuwa nchi tajiri zisipunguze misaada ya maendeleo kwa nchi maskini. Badala yake misaada hiyo iongezwe kama walivyoahidi kwenye mikutano ya Monterrey, Gleneagles na kwingineko.
3. tulisema kwamba tunatarajia pia misaada kwa Afrika, na uwekezaji kutoka nje vitaelekezwa katika kujenga na kuboresha miundombinu, kuleta mapinduzi katika kilimo, kukuza biashara miongoni mwa nchi za Kiafrika na baina yake na nchi nyingine za dunia na kusaidia zaidi makundi katika jamii ambayo yanahitaji msaada zaidi (vulnerable groups).
4. kwamba nchi tajiri duniani pamoja na Taasisi za Kimataifa za Fedha Duniani zilegeze masharti na kupunguza urasimu wa kupata fedha za misaada na mikopo kwa kutambua kwamba hiki ni kipindi kugumu na cha dharura.
Aidha, masharti ya kukopa kutoka vyombo vingine vya fedha yalegezwe pia.
5. kwamba nchi tajiri zisaidie nchi za Afrika kujenga mitaji ya vyombo vya fedha vya kikanda kama vile Benki ya Maendeleo ya Afrika.
6. kwamba, nchi tajiri zitakubaliana kuruhusu uwazi katika mabenki yao na taasisi zao za fedha ili kuwezesha nchi za Kiafrika kufuatilia na kurudishiwa fedha, majumba na rasilimali zilizoporwa kutoka katika bara letu na kuhifadhiwa kisirisiri katika mabenki ya nchi tajiri.
Ndugu Wananchi, Tunamshukuru Mheshimiwa Waziri Mkuu Gordon Brown kwa kuyapokea mapendekezo haya ya Afrika kwa moyo mkunjufu na kuahidi kuyafikisha na kusaidia kuyatetea katika kikao hicho. Pia tunamshukuru amepokea rai ya Afrika ya kuwakilishwa kwenye mkutano huo kwa kumwalika Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mhe. Meles Zenawi, ambaye atatuwakilisha kwa kofia yake ya Uenyekiti wa NEPAD.
(hotuba ya Mhe Rais, 31/March/2009)
Friday, 6 March 2009
Ubunifu na mawazo mapya
Rais wa Jamhuri yetu ya Muungano ameongelea umuhimu wa ubunifu na michango ya mawazo mapya ktk kukabiliana na changamoto za kimazingira na maendeleo duniani.
Naunga mkono kauli hii ya Mhe Rais.
...................................................
soma zaidi hapo chini. (nimeifupisha hotuba)
....................................................
Napenda kuanza kwa kutoa shukrani zangu za dhati kwa heshima mliyonipa ya kunishirikisha kwenye sherehe hii adhimu ya uzinduzi wa Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.
Siku ya leo ni siku muhimu sana katika historia ya jeshi letu. Ni siku ambayo tunashuhudia mabadiliko ya muundo wa kiutawala na kiutendaji wa Jeshi letu ukizinduliwa rasmi kwa uzinduzi wa Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu.
Nakupongeza sana CDF kwa uamuzi wako wa busara wa kufanya mabadiliko katika muundo wa Jeshi letu. Ni mabadiliko yanayoenda na wakati. Ndiyo maana sikusita kiyaunga mkono na kuyakubali. Nafarijika sana ninapoona Jeshi letu likijitahidi kuendeleza msukumo wa historia yake ya kubadilika kuendana na mabadiliko ya nyakati. Hiyo ndiyo siri kubwa ya uimara na mafanikio ya Jeshi letu.
Tangu Jeshi letu lianzishwe mwaka 1964, limeshafanya mabadiliko mengi, ya kimuundo na kiutendaji kama matakwa ya kimazingira, kiutendaji na kiteknolojia yalivyojitokeza. Uzinduzi wa Kamandi hii unadhihirisha dhamira ya Jeshi letu ya kwenda na wakati. Mimi naamini ni mabadiliko yenye maslahi kwa Jeshi letu. Yatakaleta ufanisi na kuliimarisha Jeshi letu kwa utendaji kivita na kiutawala. Nawashukuru sana viongozi wa Jeshi na Wizara. Naomba muendelee kuwa wabunifu ili muendelee kufanya mabadiliko stahiki zaidi kwa nia ya kupata ufanisi mkubwa zaidi. Nasema tena hongereni sana.
Wakati tunazindua Kamandi hii na kupongezana napenda kuwaomba muendelee kuwa wabunifu, mfikirie na kufanya mabadiliko zaidi yanayostahili ili muendelee kujiimarisha na kwenda na wakati.
Ni muhimu kwa ajili hiyo mkaangalia miundo ya utumishi wa Jeshi, ikama, mitaala ya ufundishaji, zana na vifaa mbalimbali vya kijeshi ili navyo viendane na wakati. Napenda kuwahakikisheni kuwa Serikali itaendelea kuwaunga mkono katika jitihada zenu kadiri uwezo wa bajeti yetu utakavyoruhusu. Kwa moyo huo huo wa kuendelea kuwaunga mkono ndiyo maana nimekubali kuongeza umri wa kustaafu wa wanajeshi nchini kuwa miaka 60 badala ya 57 ya sasa. Mabadiliko hayo yatakayoanza Julai Mosi mwaka huu tunayafanya ili yaendane na wakati. Siku hizi watu wanachelewa kuzeeka tofauti na ilivyokuwa zamani.
Nitakuwa mwizi wa fadhila kama sitaitumia nafasi hii, kwa mara nyingine kuwapongeza Wanajeshi wetu wote kwa kazi nzuri mnayoifanya ya kulinda uhuru na mipaka ya nchi yetu. Septemba Mosi, mwaka huu JWTZ litatimiza miaka 45 tangu kuasisiwa kwake. Imekuwa ni miaka 45 ya utumishi uliotukuka na mafanikio makubwa. Jeshi letu limetekeleza majukumu yake kwa ushujaa, umahiri, utii na uaminifu wa hali ya juu. Jeshi letu limezingatia kwa dhati misingi ya uweledi na uzalendo. Matokeo yake ni usalama na utulivu endelevu wa nchi yetu na watu wake. Tumefanikiwa kulinda mipaka ya nchi yetu wakati wote hata pale palipotokea tishio la wazi la nchi kuvamiwa na sehemu kutekwa na majeshi ya fashisti Idd Amin wa Uganda mwaka 1978. Nakumbuka Operesheni CHAKAZA mwaka 1978 – 1979. Nawapongeza sana.
Naomba nimalize kwa kuwashukuru tena, kwa kazi nzuri mnayoendelea kuifanya ya kulinda nchi yetu. Napenda kuwahakikishia kwamba Serikali inawajali na inathamini kazi yenu. Nawaomba msisahau kuwa siri kubwa ya mafaniko yetu Jeshini ni: Umoja, Ujasiri, Nidhamu na Uweledi. Yazingatieni. Nawatakia kila kheri katika majukumu yenu.
Asanteni sana.
Naunga mkono kauli hii ya Mhe Rais.
...................................................
soma zaidi hapo chini. (nimeifupisha hotuba)
....................................................
Napenda kuanza kwa kutoa shukrani zangu za dhati kwa heshima mliyonipa ya kunishirikisha kwenye sherehe hii adhimu ya uzinduzi wa Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.
Siku ya leo ni siku muhimu sana katika historia ya jeshi letu. Ni siku ambayo tunashuhudia mabadiliko ya muundo wa kiutawala na kiutendaji wa Jeshi letu ukizinduliwa rasmi kwa uzinduzi wa Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu.
Nakupongeza sana CDF kwa uamuzi wako wa busara wa kufanya mabadiliko katika muundo wa Jeshi letu. Ni mabadiliko yanayoenda na wakati. Ndiyo maana sikusita kiyaunga mkono na kuyakubali. Nafarijika sana ninapoona Jeshi letu likijitahidi kuendeleza msukumo wa historia yake ya kubadilika kuendana na mabadiliko ya nyakati. Hiyo ndiyo siri kubwa ya uimara na mafanikio ya Jeshi letu.
Tangu Jeshi letu lianzishwe mwaka 1964, limeshafanya mabadiliko mengi, ya kimuundo na kiutendaji kama matakwa ya kimazingira, kiutendaji na kiteknolojia yalivyojitokeza. Uzinduzi wa Kamandi hii unadhihirisha dhamira ya Jeshi letu ya kwenda na wakati. Mimi naamini ni mabadiliko yenye maslahi kwa Jeshi letu. Yatakaleta ufanisi na kuliimarisha Jeshi letu kwa utendaji kivita na kiutawala. Nawashukuru sana viongozi wa Jeshi na Wizara. Naomba muendelee kuwa wabunifu ili muendelee kufanya mabadiliko stahiki zaidi kwa nia ya kupata ufanisi mkubwa zaidi. Nasema tena hongereni sana.
Wakati tunazindua Kamandi hii na kupongezana napenda kuwaomba muendelee kuwa wabunifu, mfikirie na kufanya mabadiliko zaidi yanayostahili ili muendelee kujiimarisha na kwenda na wakati.
Ni muhimu kwa ajili hiyo mkaangalia miundo ya utumishi wa Jeshi, ikama, mitaala ya ufundishaji, zana na vifaa mbalimbali vya kijeshi ili navyo viendane na wakati. Napenda kuwahakikisheni kuwa Serikali itaendelea kuwaunga mkono katika jitihada zenu kadiri uwezo wa bajeti yetu utakavyoruhusu. Kwa moyo huo huo wa kuendelea kuwaunga mkono ndiyo maana nimekubali kuongeza umri wa kustaafu wa wanajeshi nchini kuwa miaka 60 badala ya 57 ya sasa. Mabadiliko hayo yatakayoanza Julai Mosi mwaka huu tunayafanya ili yaendane na wakati. Siku hizi watu wanachelewa kuzeeka tofauti na ilivyokuwa zamani.
Nitakuwa mwizi wa fadhila kama sitaitumia nafasi hii, kwa mara nyingine kuwapongeza Wanajeshi wetu wote kwa kazi nzuri mnayoifanya ya kulinda uhuru na mipaka ya nchi yetu. Septemba Mosi, mwaka huu JWTZ litatimiza miaka 45 tangu kuasisiwa kwake. Imekuwa ni miaka 45 ya utumishi uliotukuka na mafanikio makubwa. Jeshi letu limetekeleza majukumu yake kwa ushujaa, umahiri, utii na uaminifu wa hali ya juu. Jeshi letu limezingatia kwa dhati misingi ya uweledi na uzalendo. Matokeo yake ni usalama na utulivu endelevu wa nchi yetu na watu wake. Tumefanikiwa kulinda mipaka ya nchi yetu wakati wote hata pale palipotokea tishio la wazi la nchi kuvamiwa na sehemu kutekwa na majeshi ya fashisti Idd Amin wa Uganda mwaka 1978. Nakumbuka Operesheni CHAKAZA mwaka 1978 – 1979. Nawapongeza sana.
Naomba nimalize kwa kuwashukuru tena, kwa kazi nzuri mnayoendelea kuifanya ya kulinda nchi yetu. Napenda kuwahakikishia kwamba Serikali inawajali na inathamini kazi yenu. Nawaomba msisahau kuwa siri kubwa ya mafaniko yetu Jeshini ni: Umoja, Ujasiri, Nidhamu na Uweledi. Yazingatieni. Nawatakia kila kheri katika majukumu yenu.
Asanteni sana.
Saturday, 28 February 2009
Nafasi za kazi majeshini
Nyumbani kwetu Tanzania ni vigumu wananchi kujua nafasi za kazi ktk majeshi yetu zinapotokea (Jeshi la Wananchi (JWTZ), Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Polisi, Magereza n.k.)
Inatakiwa nafasi ziwe zinatangazwa hadharani kupitia vyombo vyote vya habari (magazetini, tv, na internet kupitia tovuti za serikali) ili wananchi wote wenye sifa wapate nafasi sawa ktk usaili na hatimaye ajira majeshini.
Inatakiwa nafasi ziwe zinatangazwa hadharani kupitia vyombo vyote vya habari (magazetini, tv, na internet kupitia tovuti za serikali) ili wananchi wote wenye sifa wapate nafasi sawa ktk usaili na hatimaye ajira majeshini.
Friday, 27 February 2009
Swali
Nimekuwa najiuliza mara kwa mara swali hili.
Ktk miaka ya 1950 hadi 1960 wanafunzi kutoka barani Afrika walioenda ng'ambo kusoma walipokutana nje ya masomo walikuwa wanajadili mambo ya ukombozi wa bara letu la Afrika. Viongozi kama Mwalimu JK Nyerere, Kwame Nkrumah, Patrice Lumumba, Robert Mugabe n.k. walidhamiria kupigania uhuru mara waliporudi nyumbani kwao. Na kweli miaka ya 1960 ilikuwa ni ya vuguvugu la ukombozi wa Afrika.
Miaka mingi imepita baada ya nchi za kiafrika kujipatia uhuru wao na bado kuna wanafunzi kutoka Afrika wanaendelea kwenda ng'ambo tena kwa kiwango kikubwa kuliko enzi zile za Mwalimu.
Je wanafunzi walioko ng'ambo kwa sasa wana ajenda angalao moja inayowaunganisha kuhusu bara la Afrika? Suala kubwa sasa Afrika linalotawala anga ni umaskini (uchumi), mazingira, magonjwa na utandawazi. Je kwa staili ya kina Mwalimu waafrika waliopata nafasi kufika nje ya nchi na kujionea maendeleo kwingineko duniani wanalo jukwaa la kuratibu uzoefu wao na kujipanga namna ya kusaidia nyumbani Afrika.
Kina Mwalimu, Lumumba, Kenyatta, Sekou Toure kama wangekuwepo tungewaonyesha nini kulinganisha na juhudi zao?
Wito wangu ni kuwa walioko nje waungane na kuwa kitu kimoja, kuwa na sauti moja, kuandaa ajenda ya pamoja ili kuibadilisha Afrika. Vizazi vijavyo vitashukuru endapo uzoefu uliopatikana ng'ambo utairudishwa nyumbani ili kusaidia kuleta mabadiliko ya kiuchumi na kijamii.
Wale wenye taaluma zao (mfano waliosoma uchumi, biashara, sayansi, uhandisi, udaktari n.k.) onyesheni cheche zenu kwa maendeleo ya Taifa mojamoja na bara zima kwa ujumla! Wimbi la mchango wenu litaonekana ikiwa kutakuwa na jukwaa la pamoja ktk kutoa sauti au nasaha zenu kwa manufaa ya nchi zenu na Afrika. Au mnasemaje?
Ktk miaka ya 1950 hadi 1960 wanafunzi kutoka barani Afrika walioenda ng'ambo kusoma walipokutana nje ya masomo walikuwa wanajadili mambo ya ukombozi wa bara letu la Afrika. Viongozi kama Mwalimu JK Nyerere, Kwame Nkrumah, Patrice Lumumba, Robert Mugabe n.k. walidhamiria kupigania uhuru mara waliporudi nyumbani kwao. Na kweli miaka ya 1960 ilikuwa ni ya vuguvugu la ukombozi wa Afrika.
Miaka mingi imepita baada ya nchi za kiafrika kujipatia uhuru wao na bado kuna wanafunzi kutoka Afrika wanaendelea kwenda ng'ambo tena kwa kiwango kikubwa kuliko enzi zile za Mwalimu.
Je wanafunzi walioko ng'ambo kwa sasa wana ajenda angalao moja inayowaunganisha kuhusu bara la Afrika? Suala kubwa sasa Afrika linalotawala anga ni umaskini (uchumi), mazingira, magonjwa na utandawazi. Je kwa staili ya kina Mwalimu waafrika waliopata nafasi kufika nje ya nchi na kujionea maendeleo kwingineko duniani wanalo jukwaa la kuratibu uzoefu wao na kujipanga namna ya kusaidia nyumbani Afrika.
Kina Mwalimu, Lumumba, Kenyatta, Sekou Toure kama wangekuwepo tungewaonyesha nini kulinganisha na juhudi zao?
Wito wangu ni kuwa walioko nje waungane na kuwa kitu kimoja, kuwa na sauti moja, kuandaa ajenda ya pamoja ili kuibadilisha Afrika. Vizazi vijavyo vitashukuru endapo uzoefu uliopatikana ng'ambo utairudishwa nyumbani ili kusaidia kuleta mabadiliko ya kiuchumi na kijamii.
Wale wenye taaluma zao (mfano waliosoma uchumi, biashara, sayansi, uhandisi, udaktari n.k.) onyesheni cheche zenu kwa maendeleo ya Taifa mojamoja na bara zima kwa ujumla! Wimbi la mchango wenu litaonekana ikiwa kutakuwa na jukwaa la pamoja ktk kutoa sauti au nasaha zenu kwa manufaa ya nchi zenu na Afrika. Au mnasemaje?
Wednesday, 25 February 2009
EWW
Miaka ya 1970-80 nchi yetu ilifanikiwa sana ktk kampeni ya kupambana na adui ujinga (kutojua kusoma na kuandika). Kutokana na mafanikio hayo Tanzania ilikuwa ya kwanza ktk bara la Afrika kwa kuwa na asilimia 90 ya watu wanaojua kusoma na kuandika.
Miaka ya 1990 rekodi yetu imeshuka sana hadi kufikia kwenye asilimia 60. Sina uhakika kipindi hiki tunachoanza karne mpya ya 21 kiwango hicho kiko ktk hali gani.
Mwalimu J.K. Nyerere alisema 'jifunze kusoma, wakati ni huu!'
Wakati ambapo serikali inatilia mkazo uanzishwaji na uimarishwaji wa elimu ya shule za msingi, sekondari na vyuo, Elimu ya Watu Wazima (EWW) nayo ipewe kipaumbele stahili ili isizimike kienyeji kwani wapo wanaoihitaji na serikali isiwanyime haki yao!
Miaka ya 1990 rekodi yetu imeshuka sana hadi kufikia kwenye asilimia 60. Sina uhakika kipindi hiki tunachoanza karne mpya ya 21 kiwango hicho kiko ktk hali gani.
Mwalimu J.K. Nyerere alisema 'jifunze kusoma, wakati ni huu!'
Wakati ambapo serikali inatilia mkazo uanzishwaji na uimarishwaji wa elimu ya shule za msingi, sekondari na vyuo, Elimu ya Watu Wazima (EWW) nayo ipewe kipaumbele stahili ili isizimike kienyeji kwani wapo wanaoihitaji na serikali isiwanyime haki yao!
Tuesday, 24 February 2009
'Georgina' - Marijani Rajabu
Pata Miziki ya Dansi (Tanzania) ya kina Marijani Rajabu, Hemedi Maneti n.k.
Ingia link hii
http://home.arcor.de/tizedboy/
Ebu jikumbushe wimbo huu:
GEORGINA - Safari Trippers (Marijani)
[Wote]
Ooo Georginaaaa....
Siku uliyoondoka, uliniacha nalia na machozi.
Umekwenda kuishi mbali nami, Georgina wa mamaaaa.
Sipati usingizi, nikikumbuka tulivyoishi mimi nawe Georginaaaaa.
Ooo Georgina.
(repeat Wote)
(Chorus)
[Wote]:
Umeondoka Georgina, umeniachia masikitiko
Georgina, Georgina oooo (repeat)
[Marijani]
Nauliza Georgina oooo
Ni lini utarudi? oooooo
Uniondoe wasiwasi oooooooo
Georgina wa mama aaa
Georgina Georgina oooo
(Repeat Chorus)
source: Michuzi Blog. Tuesday, February 24, 2009
Ingia link hii
http://home.arcor.de/tizedboy/
Ebu jikumbushe wimbo huu:
GEORGINA - Safari Trippers (Marijani)
[Wote]
Ooo Georginaaaa....
Siku uliyoondoka, uliniacha nalia na machozi.
Umekwenda kuishi mbali nami, Georgina wa mamaaaa.
Sipati usingizi, nikikumbuka tulivyoishi mimi nawe Georginaaaaa.
Ooo Georgina.
(repeat Wote)
(Chorus)
[Wote]:
Umeondoka Georgina, umeniachia masikitiko
Georgina, Georgina oooo (repeat)
[Marijani]
Nauliza Georgina oooo
Ni lini utarudi? oooooo
Uniondoe wasiwasi oooooooo
Georgina wa mama aaa
Georgina Georgina oooo
(Repeat Chorus)
source: Michuzi Blog. Tuesday, February 24, 2009
Tuesday, 17 February 2009
TZ: Upinzani wa kisiasa uwe 24/7
Huwa naona viongozi wetu wa upinzani nchini wakati mwingine wanajisahau na kuwa wananchi wa kawaida tu. Ninamaanisha kuwa hawana kitu au sera mbadala ili kupambanisha na serikali ya CCM ktk maisha ya kila siku.
Mfano kila mwisho wa mwezi Rais wa Jamhuri ya Muungano hutoa hotuba kwa wananchi. Viongozi wa vyama vya upinzani hugeuka wananchi vijiweni kuijadili na wakati mwingine kuipiga 'madongo', wakati hawana kitu mbadala kuonyesha kuwa wao wangefanyaje au wangetoa ujumbe gani tofauti kwa wananchi ktk hali kama ile. Kwa uelewa wangu ningetegemea viongozi wakuu wa vyama vikubwa vya upinzani nao wangetoa salaam zao za kila mwezi na za kufunga mwaka ili wananchi, ambao ni wapiga kura, waone kitu ambacho wanaweza kukipata ikiwa watachagua upinzani.
Viongozi wa upinzani kuweni macho kila wakati kuwapa wananchi kitu ambacho wangekipata endapo wangewachagueni mwaka 2005 au kuwaonyesha wananchi uwezo wenu ikiwa watawachagua mwaka 2010.
Kila hatua ambayo CCM inaipiga navyi pigeni sambamba au zaidi. Pekueni ahadi zote za muda mrefu ambazo CCM imezitoa lakini haijatekeleza au imetekeleza kwa rasha rasha. Mfano wananchi tuliahidiwa maji safi na salama yatapatikana umbali wa mita 400 kwa kila mtanzania ifikapo 1992. Lakini leo hii hata wale waishio mjini maji ni ya shida achilia mbali wa vijijini.
Je wapinzani mna cha kuwahakikishia wananchi endapo watakupigieni kura? Mnasemanje kuhusu hilo la maji. Vipi kuhusu umeme, barabara, uchangiaji elimu toka shule ya msingi hadi elimu ya juu, makazi bora kwa wananchi, matibabu n.k. Wekeni pamoja sera zenu na zijulikane kwa wananchi wakati wote, hakuna haja kusubiri wakati wa uchaguzi. Ziwekeni wazi sera wa kupitia vipeperushi (kwa ajili ya kuwasambazia wananchi), wekeni matangazo ktk vyombo vya habari, internet (mambo ya utandawazi) n.k.
Ni muhimu wapiga kura waelewe ni kitu gani CUF, CHADEMA, TLP, NCCR-Mageuzi n.k. wanaamini na wanasimamia (what is your selling point). Je mnauzika? Wateja watapenda bidhaa zenu (sera)? Mfano mteja akitaka kununua kitu au bidhaa fulani anajua duka au mahala pa kununua. Kwa maana hiyo hiyo ninaamini kuwa wapiga kura wangependa kujua kuwa endapo watahitaji mabadiliko kwa namna moja au nyingine ni chama kipi kiko tayari kuleta tofauti au mabadiliko wanayoyategemea. Kila siku kwenu iwe ni ya mapambano dhidi ya CCM. Wakati mwingine mnajisahau na mnakuwa wana-CCM bila kujijua!!
Pia nawashauri muandae orodha ya wagombea udiwani na ubunge ktk kata na majimbo ambayo yako mikononi mwa CCM ili wanolewe mapema na kuwa tayari kwa wakati wowote (kwa maana chaguzi ndogo huwa hazujulikani ziko lini). Orodha hii iwe kwa ajili ya matumizi ndani ya Chama sio kwa ajili ya Tume ya Uchaguzi. Chadema watakumbuka kilichowapata ktk uchaguzi mdogo kule Mbeya Vijijini hivi karibuni. Sababu yake ni ndogo tu, maandalizi ya zimamoto. Ndio maana nasema vyama vya upinzani jiandaeni sasa kwa kuteua orodha 'ghafi' ya wanaoweza kugombea endapo itatokea uchaguzi mdogo. Hili linawezekana endapo mtawashirikisha wanachama wenu. Mnaelewa ni majimbo gani yako kwa CCM kwa hiyo andaeni orodha ya wagombea (ndani ya chama) ktk majimbo hayo na kata zote kisha muyapitie na kuchuja halafu mnatunza hiyo orodha. Pia mtawapa mafunzo wahusika (candidates) mapema ili nao wawe tayari.
Anzeni sasa, msingoje 2010 MTACHELEWA!
NB: Sikumaanisha muanze kampeni za uchaguzi.
Mfano kila mwisho wa mwezi Rais wa Jamhuri ya Muungano hutoa hotuba kwa wananchi. Viongozi wa vyama vya upinzani hugeuka wananchi vijiweni kuijadili na wakati mwingine kuipiga 'madongo', wakati hawana kitu mbadala kuonyesha kuwa wao wangefanyaje au wangetoa ujumbe gani tofauti kwa wananchi ktk hali kama ile. Kwa uelewa wangu ningetegemea viongozi wakuu wa vyama vikubwa vya upinzani nao wangetoa salaam zao za kila mwezi na za kufunga mwaka ili wananchi, ambao ni wapiga kura, waone kitu ambacho wanaweza kukipata ikiwa watachagua upinzani.
Viongozi wa upinzani kuweni macho kila wakati kuwapa wananchi kitu ambacho wangekipata endapo wangewachagueni mwaka 2005 au kuwaonyesha wananchi uwezo wenu ikiwa watawachagua mwaka 2010.
Kila hatua ambayo CCM inaipiga navyi pigeni sambamba au zaidi. Pekueni ahadi zote za muda mrefu ambazo CCM imezitoa lakini haijatekeleza au imetekeleza kwa rasha rasha. Mfano wananchi tuliahidiwa maji safi na salama yatapatikana umbali wa mita 400 kwa kila mtanzania ifikapo 1992. Lakini leo hii hata wale waishio mjini maji ni ya shida achilia mbali wa vijijini.
Je wapinzani mna cha kuwahakikishia wananchi endapo watakupigieni kura? Mnasemanje kuhusu hilo la maji. Vipi kuhusu umeme, barabara, uchangiaji elimu toka shule ya msingi hadi elimu ya juu, makazi bora kwa wananchi, matibabu n.k. Wekeni pamoja sera zenu na zijulikane kwa wananchi wakati wote, hakuna haja kusubiri wakati wa uchaguzi. Ziwekeni wazi sera wa kupitia vipeperushi (kwa ajili ya kuwasambazia wananchi), wekeni matangazo ktk vyombo vya habari, internet (mambo ya utandawazi) n.k.
Ni muhimu wapiga kura waelewe ni kitu gani CUF, CHADEMA, TLP, NCCR-Mageuzi n.k. wanaamini na wanasimamia (what is your selling point). Je mnauzika? Wateja watapenda bidhaa zenu (sera)? Mfano mteja akitaka kununua kitu au bidhaa fulani anajua duka au mahala pa kununua. Kwa maana hiyo hiyo ninaamini kuwa wapiga kura wangependa kujua kuwa endapo watahitaji mabadiliko kwa namna moja au nyingine ni chama kipi kiko tayari kuleta tofauti au mabadiliko wanayoyategemea. Kila siku kwenu iwe ni ya mapambano dhidi ya CCM. Wakati mwingine mnajisahau na mnakuwa wana-CCM bila kujijua!!
Pia nawashauri muandae orodha ya wagombea udiwani na ubunge ktk kata na majimbo ambayo yako mikononi mwa CCM ili wanolewe mapema na kuwa tayari kwa wakati wowote (kwa maana chaguzi ndogo huwa hazujulikani ziko lini). Orodha hii iwe kwa ajili ya matumizi ndani ya Chama sio kwa ajili ya Tume ya Uchaguzi. Chadema watakumbuka kilichowapata ktk uchaguzi mdogo kule Mbeya Vijijini hivi karibuni. Sababu yake ni ndogo tu, maandalizi ya zimamoto. Ndio maana nasema vyama vya upinzani jiandaeni sasa kwa kuteua orodha 'ghafi' ya wanaoweza kugombea endapo itatokea uchaguzi mdogo. Hili linawezekana endapo mtawashirikisha wanachama wenu. Mnaelewa ni majimbo gani yako kwa CCM kwa hiyo andaeni orodha ya wagombea (ndani ya chama) ktk majimbo hayo na kata zote kisha muyapitie na kuchuja halafu mnatunza hiyo orodha. Pia mtawapa mafunzo wahusika (candidates) mapema ili nao wawe tayari.
Anzeni sasa, msingoje 2010 MTACHELEWA!
NB: Sikumaanisha muanze kampeni za uchaguzi.
Monday, 16 February 2009
Ushauri: Mliodhalilishwa mna haki kudai fidia
Pamoja na serikali kumvua madaraka aliyekuwa Mkuu wa Wilaya fulani (kule Kagera) kwa sababu za kuamrisha walimu wachapwe viboko na polisi, bado mimi naamini kuwa hiyo hatua haitoshi.
Ushauri wangu kwa walimu waliodhalilishwa na Mkuu wa Wilaya:
1. Wafungue kesi ya madai dhidi ya serikali kudai fidia ya fedha kutokana na udhalilishwaji hadharani uliofanywa na serikali. (walimu hao hawana hata kazi ya kutafuta ushahidi, kesi yao iko wazi). Hapa serikali ina kesi ya kujibu na inatakiwa kulipa fidia kwa kiwango abacho mahakama itaona kinafaa.
Pia asasi za kutetea haki za binadamu nchini ziwasaidie hao walimu ili kesi yao iandikishwe mahakamani -na walimu wapate haki yao. Hili litakuwa funzo kwa serikali na wawakilishi wake ili wakati wote wazingatie miiko, maadili ya kazi na kuheshimu katiba ya Jamhuri ya Muungano.
2. Walimu wahamishwe vituo vyao vya kazi kwenda vituo watakavyopenda wenyewe kwenda kufanyakazi.
Ushauri wangu kwa walimu waliodhalilishwa na Mkuu wa Wilaya:
1. Wafungue kesi ya madai dhidi ya serikali kudai fidia ya fedha kutokana na udhalilishwaji hadharani uliofanywa na serikali. (walimu hao hawana hata kazi ya kutafuta ushahidi, kesi yao iko wazi). Hapa serikali ina kesi ya kujibu na inatakiwa kulipa fidia kwa kiwango abacho mahakama itaona kinafaa.
Pia asasi za kutetea haki za binadamu nchini ziwasaidie hao walimu ili kesi yao iandikishwe mahakamani -na walimu wapate haki yao. Hili litakuwa funzo kwa serikali na wawakilishi wake ili wakati wote wazingatie miiko, maadili ya kazi na kuheshimu katiba ya Jamhuri ya Muungano.
2. Walimu wahamishwe vituo vyao vya kazi kwenda vituo watakavyopenda wenyewe kwenda kufanyakazi.
Thursday, 12 February 2009
... hata hivyo ameonyesha uungwana!
hivi karibuni niliandika kuwa mheshimiwa waziri mkuu wetu alikosea mara 2.
pamoja na makosa hayo aliyoyafanya bado anastahili pongezi kwa kuonyesha ukomavu wa kiuongozi pale alipoomba msamaha hadharani (ndani ya bunge). ni ustaarabu unaostahili kuigwa. nategemea yaliyotokea yatakuwa funzo na hayatatokea tena huko mbeleni.
nakupa 5 mhe mizengo p. k. pinda!
pamoja na makosa hayo aliyoyafanya bado anastahili pongezi kwa kuonyesha ukomavu wa kiuongozi pale alipoomba msamaha hadharani (ndani ya bunge). ni ustaarabu unaostahili kuigwa. nategemea yaliyotokea yatakuwa funzo na hayatatokea tena huko mbeleni.
nakupa 5 mhe mizengo p. k. pinda!
Friday, 6 February 2009
Waziri Mkuu alikosea mara 2
Sakata la mauaji ya maalbino, waziri mkuu Mhe Kayanza Mizengo Peter Pinda alikosea.
1. Kutamka kuwa wauaji wa maalbino nao wauwawe. Matamshi yake yalikiuka katiba ya Jamhuri ya Muungano ambayo yeye ameapa kuilinda.
2. Aliomba msamaha kwa masharti, kwa kutumia neno 'kama'.
'Kama' kuna mtu nimemkosea naomba msamaha. Alitakiwa aombe msamaha wa jumla kwani alikosea kwa asilimia 100.
1. Kutamka kuwa wauaji wa maalbino nao wauwawe. Matamshi yake yalikiuka katiba ya Jamhuri ya Muungano ambayo yeye ameapa kuilinda.
2. Aliomba msamaha kwa masharti, kwa kutumia neno 'kama'.
'Kama' kuna mtu nimemkosea naomba msamaha. Alitakiwa aombe msamaha wa jumla kwani alikosea kwa asilimia 100.
Chama Cha Mapinduzi
Hongera kwa CCM kutimiza miaka 32 hapo jana.
Endelezeni yale mazuri yaliyoanzishwa na waasisi wa Chama na kamwe msijisahau au kulewa madaraka ya muda mrefu! Namsiwadharau wananchi, hasa wa kipato cha kawaida maana hao ndio waajiri wenu!
Endelezeni yale mazuri yaliyoanzishwa na waasisi wa Chama na kamwe msijisahau au kulewa madaraka ya muda mrefu! Namsiwadharau wananchi, hasa wa kipato cha kawaida maana hao ndio waajiri wenu!
Subscribe to:
Posts (Atom)