Monday, 2 June 2008

Shirikisho A/Mashariki: ulikuwa ni utabiri au ukweli?

Tarehe 04/12/2006 niliwahi kuisema Kenya juu ya maendeleo yao kidemokrasia kwamba ni kikwazo tosha kutoruhusiwa kuwa mwanachama wa shirikisho (wakati nikijenga hoja kuwa huu sio wakati muafaka kuanzisha shirikisho la Afrika Mashariki).

Na kweli wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka jana (2007) maoni yangu yalipata nguvu zaidi, maana wakenya wenyewe walithibitisha dukuduku langu la wakati huo lilikuwa na ukweli! Ziliibuka vurugu na mapigano ambayo yaligeuka kuwa mauaji ya raia mithili ya vita vya wenyewe kwa wenyewe tulivyosikia au kuona ktk vyombo vya habari huko Somalia, Burundi na Rwanda!

Nilisema hivi: "Kenya demokrasia ni finyu sana na juzijuzi wameshindwa kutuletea wabunge 9 tu wa bunge la A. Mashariki na hadi sasa kesi iko mahakamani. Sasa wana ubavu wa kutoa wabunge wa bunge hilo la shirikisho? Tumeona hawana ubavu huo!! Uongozi wao si wa uwazi, tumeona mawaziri/manaibu waziri wanaachia ngazi" -04/12/2006

Na kweli Kenya hamna ubavu huo wa kutuchagulia wabunge au mnasemaje?

Shirikisho A/Mashariki: Nionavyo IV

Tarehe 11/12/2006 nilihitimisha maoni yangu kwa kubashiri kuwa watanzania walio wengi hawalitaki shirikisho na kweli ndivyo ilivyotokea kuwa. Nikagusia matatizo ya Muungano wetu Bara na Zanzibar; na sasa imebainika ni kweli una mapungufu -angalia maendeleo ya mwafaka ...(soma zaidi hapo chini)!
.............
.............

(at 05:41AM Monday on December 11, 2006):
Wachangiaji wamekuwa wakitoa mapendekezo yao juu ya nini kifanyike. Ukipitia michango kadhaa utapata mapendekezo ya wachangiaji, tena wamependekeza mengi sana. Baadhi ya michango au mapendekezo ni kama ifuatavyo:
1. Jumuiya ya Afrika mashariki iendelezwe na kusaidiwa kikamilifu na nchi wanachama. Mchangiaji mmoja alisema yale mashirika ya jumuiya yarudi, bandari, reli, ndege n.k.
2. Fursa za SADC na COMESA zitumiwe kikamilifu.
3. Kero za muungano wa Tanzani Bara na Zanzibar zitafutiwe ufumbuzi haraka na kwa uwazi. Wazanzibari hawawezi kukubali kuingizwa katika muungano mwingine wakati huu tulio nao hawaufurahii hasa kutokana na mpasuko uliopo pamoja na kero zingine zilizopo ktk muungano wetu.

Tunaweza kuwa competitive ndani ya jumuiya yetu, au ktk SADC/COMESA. Pamoja na hayo, nchi zote za jumuiya ya Afrika Mashariki ziko ktk SADC/COMESA, je hilo shirikisho lina nini kipya?
Mwisho, sio kweli kwamba wakubwa wameshakubali au kupitisha shirikisho. Wananchi ndio tutakaoamua.
Nina imani kubwa watanzania walio wengi watakataa uundwaji wa shirikisho.
Jumuiya-YES, shirikisho-NO.

Shirikisho A/Mashariki: Nionavyo III

Wakati nikitoa maoni yangu kipindi hicho, niliweza kuungwa mkono na watanzania wenzangu ktk nyakati tofauti. Kwa mfano ....
.....................
.....................
(at 06:25AM Tuesday on December 05, 2006, Dr.Khamis said):
Naunga mkono maneno ya Edison na wengineo wanaopinga “FEDERATION”. Sasa hivi kwenye Jumuiya YA Afrika ya Mashariki tuna,Tanzania,Kenya,Uganda,Rwanda na Burundi.
1. Tuwe na ushirikiano kwenye uchumi kama ule wa zamani, Bandari,Reli na Ndege.
2. Tushirikiane kuunda tena East African Airways na tuone kwamba tunafanikiwa sio kama sasa hivi kila nchi ina kampuni yake ya ndege.
3. Tujenge reli mpya na tuziimarishe reli za zamani ili usafiri wa mizigo na abiria uwe wa nafuu.Tukifanya hivi tutapunguza ajali za barabarani.

Nchi ambayo ni ya “amani” katika nchi hizi tano ni Tanzania pekee na kidogo Kenya. Historia ya Uganda ni vita, ya Rwanda ni vita na Burundi ni vita tu. Mpaka dakika hii hakuna Amani Rwanda,Burundi wala Uganda.
Hakuna “democracy” huko Uganda, Burundi wala Rwanda. Wengine wanataka kuwa Rais wa Maisha na kubadilisha katiba zao.
Federation itataka iwe na aina moja ya fedha(Monetary System) kama vile tunavyoona Euro currency katika EU –countries. Fedha ya Tanzania ni dhaifu sana.
Federation itataka iwe na jeshi moja,Bunge moja, serikali moja, rais mmoja tu.

Watanzania bado hatuko tayari na FEDERATION bali tuko tayari na muundo wa ushirikiano kama ule wa zamani wa JUMUAI YA AFRIKA YA MASHARIKI. Ni jukumu la serikali ya Tanzania kuwandaa watanzania kwa Federation. Mapaka muda huu Serikali ya Tanzania haijafanya matayarisho yoyote ya kuwaandaa wananchi wake katika hatua kubwa sana hii ya Federation.

Shirikisho A/Mashariki: Nionavyo II

Nilichosema na mwanachi mmoja kanisaidia kwa kufafanua kuhusu kauli yangu!
................
...............
(at 03:04AM Tuesday on December 12, 2006):
Kitu ambacho mwanakijiji na wengine wanaounga mkono shirikisho wanashindwa kuweka wazi ni kuwa hilo shirikisho lina kitu gani kipya?
Tunayo jumuia ya Afrika Mashariki;
Tuna SADC na COMESA
Huko nyuma ilikuwepo PAFMECSA.
So come out and tell us what difference or addition (if any) will this federation bring to the majority of Tanzanians.
It is clear that we Tanzanians are not ready so why should we rush? I understand there are some Tanzanians abroad who have somehow achieved something and would like to take advantage of the federation system. These are people whom I call greedy and self-centered*. They don't think about the majority of youth in our country who can not compete! We need time to prepare our selves as a NATION, not as individuals who are not even living in the country!
.................

*(at 12:54AM Wednesday on December 13, 2006, Dr.Khamis said):
We “Tanzanians living abroad are not GREEDY AND SELF-CENTERED “.Some of us have given you examples like that of EU just to show how a federation works and how to come around various obstacles. EU for example has one monetary system with EURO as the currency. But not all EU countries have EURO as a day-to-day currency in their monetary system. We are living aboard as well as in Tanzania since we donate money in the form of US$ to our relatives living in Tanzania in this way are helping Tanzania economically.
We are not poor (Thanks GOD) like our brothers and sisters living in Tanzania and have accumulated experience(s) that is highly required in the country.
My advice to you all Tanzanians DON’T JOIN THE FEDERATION UNTIL YOU KNOW WHAT YOU WANT TO ACHIEVE IN THAT FEDERATION.

WHY DO WE WANT A POLITICAL FEDERATION? WHAT ARE THE ADVANTAGES AND DISADVANTAGES OF THIS FEDERATION?
CAN WE SERVIVE AS A NATION OUTSIDE THIS FEDERATION?

Shirikisho A/Mashariki: Nionavyo I

Serikali yetu ilipounda tume ya kukusanya maoni kuhusu mpango wa kuharakisha uanzishwaji wa Shirikisho la Afrika Mashariki, sikubaki nyuma ktk kuchangia maoni yangu. Mimi nilikuwa mmoja wa wananchi waliopinga uanzishwaji wa Shirikisho hilo.
Nilipata fursa kutoa maoni yangu ktk majukwaa mbalimbali.
Baadhi ya maoni niliyoyatoa ni kama ifuatavyo (yako ktk sehemu nne, na niliyatoa kupitia m/kijiji blog):

..............................
..............................

(at 10:34AM Monday on December 04, 2006, edison said):
Naunga mkono dhana ya ushirikiano kibiashara na kiuchumi kama ilivyo sasa na huko nyuma.
Hakuna haja kwa wakati huu kuanzisha shirikisho la kisiasa (rais mmoja na bunge moja).
Kwa kifupi siungi mkono "federation".
Kwanza sijui kuna vigezo gani vimewekwa na wahusika (au viongozi wa A. Mashariki) kwa kila nchi mwanachama wa Jumuiya, ili kujiunga na 'shirikisho!!!".
Haiwezekani eti kwa sababu za kijiografia tu ziwe kigezo cha kila nchi kujiunga.
Mimi nina vigezo vyangu binafsi, labda leo niongelee hivi vitatu kwa pamoja:
Utulivu, Amani na Demokrasia
Nchi pekee inayoweza ku'tick' all the boxes ni TZ tu.
Kenya demokrasia ni finyu sana na juzijuzi wameshindwa kutuletea wabunge 9 tu wa bunge la A. Mashariki na hadi sasa kesi iko mahakamani. Sasa wana ubavu wa kutoa wabunge wa bunge hilo la shirikisho? Tumeona hawana ubavu huo!! Uongozi wao si wa uwazi, tumeona mawaziri/manaibu waziri wanaachia ngazi. Hizo si dalili njema! Sera zao za ARDHI na Tanzania sio haziendani kabisa. WaTZ hatutaweza ku-access ARDHI yao kama watakavyoweza ku-access ARDHI yetu TZ!!!
VERDICT: Kenya haiwezi kujiunga ktk shirikisho.
Uganda: MUSEVENI AMEBADILI KATIBA YA NCHI ILI ATAWALE KWA VIPINDI KADRI ANAVYOJISIKIA (maisha?). Huu si mfano mzuri wa kukumbatia. Uganda kuna vita vya siku nyingi na Lord's Resistance Army na hatujui mustakabali wake! Hili tulifumbie macho na kumkaribisha Konyi na LRA ktk shirikisho, tutambebea mbeleko gani? Mgogoro Uganda na DRC umeishia wapi?
VERDICT: Uganda haistahili kujiunga.
Rwanda: Rekodi ya nchi hii kidemokrasia sio nzuri pia. Sina hakika Kagame ni mwanademokrasia halisi au ni mtu anayetabilika. Wamekuwa ktk vita kwa muda mrefu na tuhitaji muda kuona amani ya kweli ipo Rwanda.
VERDICT: TUNAHITAJI MUDA KUONA MAENDELEO YA AMANI NA DEMOKRASIA YA KWELI. It's a NO, for now!
Burundi: Ndio juzi juzi tu wametia saini makubaliano ya amani na PELIPEHUTU. Tunahitaji muda wa kutosha ku-assess maendeleo ya amani, usalama wa raia na ya demokrasia, pamoja na utekelezaji wa makubaliano yao. Pia tutahitaji ushahidi wa kututhibitishia kuwa silaha zote za kijeshi/kivita zimekabidhiwa kwa vyombo halali vya dola. Wapigaji wote wa msituni wakabidhi miundombinu ya kijeshi/kivita yote waliyo nayo ktk vyombo vya dola ili tuwe na imani juu ya usalama wa raia kwa sasa na siku zijazo na kudhibiti vitendo vya unyang'anyi, ujambazi wa silaha na ujangiri katika eneo la Jumuiya.
VERDICT: NI MAPEMA MNO kuiamini Burundi kama nchi iliyo na amani na demokrasia ya kweli. Hatujui kama hii amani ya sasa ni sawa 'volcano' hai, iliyolala au iliyokufa! I am afraid, it's a NO to Burundi.
Hizi ndio sababu zangu za kulikataa SHIRIKISHO kwa nguvu zangu zote. Ninazo sababu nyingi ila hizi ni za msingi kwangu. Athari zake (shikisho)zinaweza zisitupate sisi, ila vizazi vijavyo vinaweza kutulilia kama hatujali maslahi ya utaifa kwanza!!
NB:
Tusidanganyike kwa kiini macho cha Ajira, kwa hata kwa mazingira ya sasa (bila shikirikisho) ajira ni ngumu na sisi ndio nchi kubwa, mipaka ikiwa wazi wageni wataingia kwetu na kuua kabisa hii ajira iliyopo. Sera ya elimu na ardhi ya TZ ni nzuri kuliko nchi jirani, i.e. zinawajali wanyonge. Rwanda na Burundi kuna 'population density' kubwa sana, kwa hiyo watamiminikia TZ.
Shikisho litawanufaisha zaidi Kenya, Uganda, Burundi na Rwanda, kuliko waTZ tutakavyofaidika nalo. Tuta-loose wala hatuta-benefit a lot!
WAPO WACHACHE KTK TANZANIA WATAKAONUFAIKA SANA NA MUUNDO WA SHIRIKISHO. ILA WATANZANIA WALIO WENGI WATAPATA SHIDA SANA! Sasa lipi bora, wachache wapete na tuwaache wengi ktk shida?
Tusione haya wala aibu kusema 'NO' kwa muungano wa shirikisho! Muundo wa sasa WA JUMUIYA unatosha hasa ktk masuala ya kibiashara na kiuchumi!
Asante sana.

Cristiano Ronaldo v. Man United

Cristiano ronaldo is a great player as he has proved that over time by winning several trophies and honours since he joined Manchester United from Sporting Lisbon.

But unfortunately, since the end of the season, I think he has been given wrong advice from those close to him (like professional advisors or even family members and friends). His comments are not consistent, always giving contradictory remarks about himself on his future football career with Man United!

It would be wise now to focus or concentrate with his national team duty as the Euro 2008 finals are only five days away! Also, if he is a true professional, should remember that he has got a contract to honour at Manchester United.

On the other hand if he feels he can no longer pursue his career at Old Trafford, thats is well and good. I think the club will bless your wish. There is no reason to block his move.

Manchester United is the greatest football club in the world, and without question it will always move forward with or without Cristiano Ronaldo.

Remember, there are still plenty of talented players around who can wear no.7 jersey and perform wonders. It is time now to give them a chance and I am sure they won't let Man United down. The club is always bigger than any individual(s) at the club!!

Bendera ya Taifa letu

Haya hapo chini ni maoni yangu mahala fulani kuhusu tafsiri ya rangi za bendera yetu ya Taifa hasa rangi 'nyeusi'.
Nikiangalia mfano wa wenzetu wa Afrika Kusini*, wao wamebainisha kabisa rangi; -nyeusi na nyeupe- kwa maana kuwa wapo weusi na wasiokuwa weusi ambao wanawakilishwa na rangi nyeupe*!

Ktk maoni yangu haya sina maana ya kuwabagua weupe ila ningependa kujua kama tafsiri ya rangi 'nyeusi' ktk bendera yetu inawawakilisha pia wenzetu wasiokuwa weusi. Ningependa nao wajisikie/waone kuwa wanawakilishwa ktk alama muhimu ya Taifa letu.

Wangwana, kama nimetoka nje ya mstari napenda kuomba radhi 'in advance', lakini nadhani sio vibaya/mwiko kuuliza -eti jamani!
Kuuliza si ujinga!
...........................
...........................
(Na Mosonga. Tarehe October 30, 2007 9:00 PM)
Jamani naomba tuandae mjadala wenye Kichwa cha habari:
Bendera yetu ya Taifa inakidhi matakwa ktk mazingira ya sasa?
Wakati wa kupigania uhuru, kujikomboa na kupata uhuru Tanganyika na mapinduzi ya Zanzibar, rangi za bendera yetu zilikuwa na tafsiri yake ktk mazingira ya wakati huo. Lakini sasa mazingira yamebadilika.
Rangi hizo ni:
Kijani- uoto wa asili
Njano-madini na utajiri
nyeusi-wananchi (kwa maana ni weusi??)
bluu-maji bahari, maziwa na mito

Swali langu liko ktk rangi nyeusi ktk mazingira ya leo inawakilisha nini?
Je ni wakati muafaka kubadili au kuongeza rangi ktk bendera ya taifa ili iwakilishe watanzania wa asili (race) tofauti na weusi??
Naomba nieleweke kuwa sina ugomvi na huyu miss TZ ila (je) bendera yetu inamjumuisha au inambagua? au tuna-assume au kufumba macho na kudhani iko sawa!!
..............................
..............................
*Sahihisho:
Serikali ya A. kusini inasema kuwa rangi ktk bendera yao ya Taifa hazina tafsiri yoyote (www.info.gov.za/aboutgovt/symbols/flag.htm).
"The national flag was designed by a former South African State Herald, Mr Fred Brownell, and was first used on 27 April 1994. The design and colours are a synopsis of principal elements of the country's flag history. Individual colours, or colour combinations represent different meanings for different people and therefore no universal symbolism should be attached to any of the colours."