Tuesday, 4 November 2008

Piga kura yako sasa hivi ili Obama ashinde!

Kwa wale wapiga kura wa Marekani leo ndio siku ya kufanya kweli.

Muda wa kampeni na longolongo umekwisha kabisa. Sasa ni saa ya hukumu.

Tumia kura yako kumpa Seneta Obama ushindi. Seneta Obama hawezi kuwa Rais kwa maneno matupu bali kwa kura yako!

Enyi wapiga kura wa Marekani, mashabiki na wapenzi wa Seneta Obama, amkeni sasa hivi, bila kupoteza wakati, nendeni moja kwa moja kituo cha kupigia kura mkampigie kura Seneta Obama.

Najua wengi wenu mtakuwa mmketi kwenye sofa huku macho yenu yameganda kwenye luninga (TV), mkifuatilia 'exit polls' za wenzenu wakati hata nyie mnatakiwa mkapige kura!

Usitegemee Seneta Obama atashinda kwa kura za wapiga kura wengine. Ukweli ni kwamba Seneta Obama atashinda kwa kura YAKO WEWE, yule na wale! Timizeni wajibu wenu kwa umoja.

If you don't vote now, NO victory for him.

Every vote counts.

So, get up and vote for Sen. Obama, NOW!!!

Mipango miji Lushoto: Vijiji kuwa vitongoji

Vijiji 14 vyafutwa Lushoto...

Serikali imevifuta vijiji 14 vilivyokuwa vinaunda Kata za Ubiri na Lushoto mjini na kuvipa hadhi ya kuwa vitongoji baada ya Ofisi ya Waziri Mkuu,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) kutoa kibali cha kuanzishwa kwa Mamlaka ya Mji mdogo wa Lushoto.

Ofisa Mtendaji Mkuu wa mamlaka hiyo, Gwatako Nyakoki, alisema amri ya kuvifuta vijiji hivyo na kupewa hadhi ya kuwa vitongoji, inatokana na sheria ya serikali za mitaa namba 7 ya mwaka 1982.

Alisema sheria hiyo inatoa mamlaka kwa vijiji kujifuta na kuwa vitongoji ambavyo vitawaruhusu wenyeviti wanaoviongoza kuwa wajumbe wa baraza la mamlaka hiyo.

Nyakoki aliyasema hayo mwishoni mwa wiki wakati akizungumza kwenye uzinduzi wa Mamlaka hiyo uliofanyika mjini hapa mara baada ya kuapishwa kushika wadhifa huo na kukabidhiwa rasmi hati ya kuiongoza.

``Nimekabidhiwa rasmi mikoba ya kuiongoza mamlaka hii ambayo sasa inaanza kazi kwa mujibu wa sheria, ninachokiomba kwa sasa ni ushirikiano kati yangu na wananchi wa mji wa Lushoto…kwa kweli kazi ya kuongoza Mamlaka hii ni ngumu kwa sababu tunatakiwa kukazana ili tupewe hadhi nyingine ya kuwa Halmashauri ya Mji,`` alisema Ofisa huyo aliyeteuliwa akitokea Idara ya Maendeleo ya Jamii.

Awali akifungua rasmi shughuli za mamlaka hiyo, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto, Lucas Shemndolwa alisema Halmashauri yake inakusudia kutoa ushirikiano mkubwa kwa mamlaka hiyo ya mji ili kuisaidia iweze kujitegemea kama zilivyo mamlaka nyingine za miji ya Korogwe, Njombe na Kibaha.

Akizungumzia utendaji wa mamlaka hiyo, Shemndolwa aliitaka kutumia fursa zilizopo wilayani hapa zikiwemo rasilimali mbalimbali za asili kujiimarisha kiuchumi na kuufanya mji huo kuwa sehemu ya mfano nchini.

(SOURCE: Nipashe, 2008-11-04 12:06:21. Na Godfrey Mushi, Lushoto)

Monday, 3 November 2008

EPA: A-Z (3)

Dondoo nyingine muhimu kuhusu EPA ni kama ifuatavyo:-

Benki zilikopitishwa fedha

Bank of Baroda (T) LTD,Barclays, CRDB, Diamond Trust, Eurafrica, Exim Bank, Kenya Commercial Bank, NBC, Standard Chartered na United Bank of Afrca.

Vigogo BoT walioidhinisha

Vigogo hawa walioshika nyadhifa hizi au kuzikaimu katika kipindi cha kuchotwa fedha hizo, ni miongoni mwa watuhumiwa: Gavana wa Benki Kuu (hayati Dkt. Daud Ballali), Mkurugenzi wa Fedha, Katibu wa Benki Kuu (wako wawili) na Mkurugenzi wa Sera za Uchumi (wako wawili).

Wengine ni Naibu Mkurugenzi Idara ya Madeni (wako wawili), Mkuu wa Kitengo cha Madeni ya Biashara, Kaimu Mkurugenzi wa Ukaguzi wa Ndani, Mkurugenzi wa Usimamizi wa Benki na Bodi ya Wakurugenzi iliyokuwepo mwaka 2005/2006.

Kampuni 'zilithibitika' kughushi

Kampuni hizi zilithibitika kuwa ziliwasilisha nyaraka feki katika kuchota fedha kwenye EPA nazo ni Bencon International of Tanzania, VB and Associates of Tanzania, Bima Resorts, Venus Hotel, Njake Hotels and Tours, Mahan Mining company of Tanzania na Money Planners and Consultants.

Nyingine ni Bora Hotels and Apartments, B.V Holdings LTD, Ndovu Soaps, Navy Cut Tobacco LTD, Changanyikeni Residential Complex na Kagoda Agriculture LTD.

Utata kampuni 9

Kampuni tisa zifuatazo ziliwasilisha nyaraka ambazo badohaijathibitika kama ni feki au halali kutokana na kampuni za nje zinazodaiwa kuwaruhusu kupokea malipo kwa niaba yao kila wanapoulizwa kukaa kimya mpaka sasa.

Kampuni hizo ni G&T International, Excellent Servies LTD, Mbale Farm, Liquidity Serives LTD, Clayton Marketing LTD, M/S Lashlas (T) Limited, Malegesi Law Chambers Advocates, Kiloloma and Brothers na KERNEL LTD.

Mapendekezo ya wakaguzi

*Ufanyike uchunguzi kamili wa kijinani dhidi ya makampuni hayo na maofisa wa BoT kisha zichukuliwe hatua kali.

*Uanzishwe utaratibu wa kisheria wa kuhakikisha fedha zinarejeshwa.

*Hatua za kinidhamu dhidi ya maofisa wa BoT waliosaidia kuchotwa fedha hizo.

*Yafanyike mawasiliano na kampuni za nje zinazodaiwa kutoa idhini ili ijulikane ukweli kuhusu zile kampuni tisa ambazo malipo yao yanayofikia sh. bilioni 42.

*Uanzishwe mkataba wa muongozo kati ya Wizara ya Fedha na BoT juu ya uendeshaji wa akaunti ya EPA ili kuwe na:-utaratibu wa kutoa taarifa za mara kwa mara kuhusu maendeleo ya akaunti, hali ya madeni na dhamana zote ziwe zinaidhinishwa na Wizara.

*Ili kupambana na usanii, BoT na Serikali ziangalie ushauri wa kisheria ili siku nyingine zikatae kujihusisha na 'watu wa tatu,' katika ulipaji wa madeni, badala yake kampuni zinazodai zije zenyewe.

*Chanzo:Ripoti ya ukaguzi ya Ernst and Young iliyotolewa Januari, 2008. (kutoka: gazeti majira, 03/11/2008)

A friend who doesn't know me!

I received an electronic mail from a 'friend'.
Suprisingly, this 'friend' of mine doesn't even know me by name, have no my phone number and knows nothing about me!
If you get such mails or messages please do not attempt to reply them. It is good to ignore them!
Just see (below) the message from somebody who claims to be my friend, he looks a 'thief' to me!
..........................................................

Dear Friend.

This Message Might Meet You In Utmost Surprise. However, It's Just My
Urgent Need For Foreign Partner That Made Me To Contact You For This
Transaction. I Am A Banker By Profession From Burkina Faso In West
Africa And Currently Holding The Post Of Head Of Department Accounts
And Auditing In My Bank (BANK OF AFRICA.) Burkinafaso.

I Have The Opportunity Of Transferring The Left Over Funds
($10.5Million) Of One Of My Bank Clients Who Died Along With His Entire
Family In Kenya Plane Crash 1998.

Hence, I Am Inviting You For A Business Deal Where This Money Can Be
Shared Between Us In The Ratio Of 50/40 / 10% For Any income
expenses that will come During the transfer, If You Agree To My
Business Proposal.

Further Details Of The Transfer Will Be Forwarded To You As Soon As I
Receive Your Return Mail.

N/B : I will need your telephone and fax numbers for us to discuss
more about the transaction.

Have A Great Day.

Yours,

GODWIN PAORE.

Friday, 31 October 2008

Man United Goals, so far!

GOALS, as of 29/10/2009!
Darren Fletcher: Prem: (1+1+1) =3
Wayne Rooney:Prem: (1sep+1oct+1) Champ/League:1+1 =5
Dimitar Berbatov: Prem:1 Champ/Lge:2+2 =5
Cristiano Ronaldo: Prem:1+1+2 Lge Cup:1 =5
Ji Sung Park: Prem 1 =1
Luís Carlos Almeida da Cunha ("Nani"): Prem:1 Lge Cup:1 =2
Ryan Giggs:Lge Cup:1 =1
Wes Brown: Prem:1oct =1

Tulikotoka: RTD

Nimeambiwa kuwa siku hizi RTD inaitwa TBC 1. Zamani nilipokuwa mdogo nilipenda sana Vipindi vya Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD) (miaka ya 1980).

Kwanza ni anuani yao:
Pugu Road (Nyerere RD siku hizi), SLP (POBox) 9191 Dar es Salaam.

Vipindi:
Taarifa ya Habari; ngoma za Moris Nyunyusa zilianza kutukaribisha na kutusogeza karibu na redio, kisha ti, ti, ti, ... (mara 6) Kisha; ...
'Hivi sasa ni saa ... kamili', (Mwanadada alisikika akisema)
(kisha akafuatia msoma habari)
Na hii ni taarifa ya habari kutoka Redio Tanzania Dar es Salaam,
Msomaji ni Charles Hilary, au Betty Mkwasa n.k
kwanza ni mkhutasari wake ....
habari kamili. Mwanza. Waziri Mkuu na Makamu wa kwanza wa Rais ....
baada ya dakika tano ...
'mnaendelea kusikiliza taarifa ya habari kutoka redio tanzania dar es salaam'
Tokyo ......
baada ya dk 9 hivi,
'kwa kumaliza taarifa ya habari, sikilizeni tena muhtasari wale'
waziri mkuu na .....
baada ya dk 10,
na huo ndio mwisho wa taarifa ya habari kutoka redio tanzania daresalaam.

Tunawaletea mazumzo baada ya habari (saa 2 usiku, saa 10 alasiri au saa 1 asubuhi).
baada ya dk 5
mazungumzo baada ya habari yamewajia kutoka redio tanzania daresalaam.

au badala ya mazungumzo baada ya habari kuna matangazo ya vifo.

Enzi hizo hakuna redio za watu binafsi. RTD ilikuwa na idhaa 2, ya Taifa (nchi nzima) na ya biashara ikisikika zaidi Dar na maeneo jirani au maeneo ya mijini zaidi.

Vipindi zaidi nilivyovipenda
Misakato
Michezo (michezooo) saa 2 kasorobo usiku
Mama na Mwana (hasa mtangazaji wake mama Debora Mwenda)
Kumekucha (miziki)
Asubuhi Njema (baadae kikaitwa Jambooo) (miziki ya dansi)
Mchana Mwema (miziki ya dansi)
Ombi Lako (baadae kikaitwa 'chaguo lako' (miziki)
Hotuba za Baba wa Taifa saa 2:15 - 2:30 usiku (Jumatatu - Ijumaa)
Mahoka (vichekesho)

Tulikotoka: Majina ya dawa

Nakumbuka madawa tuliyokuwa tunatumia miongo kadhaa iliyopita:

Dawa za kichwa:
-Asprini, ASA
-Aspro
-Cafenol
-Haraka

Dawa za maleria:
-Malaraquin
-Quinin
-Chloroquin, CQ