Friday, 19 December 2008

Usanii Majengo ya Benki Kuu?

UKAGUZI WA MAJENGO BENKI KUU NI USANII MWINGINE

Jamani usanii umetuzidi watanzania. Nahisi magazeti pia hutumiwa kuwajenga hoja zenye kiini macho na kuwazuga wananchi tu – propaganda za kuficha ukweli. Ni kitu cha kufarahisha sana jinsi gazeti la Nipashe la Jumapili 30 Novemba 2008 lilivyoandika kichwa cha habari kikubwa kuwa kampuni ya kimataifa ya wakaguzi wa hesabu wa katika masuala ya majengo M/S Mekon Arc Consult Limited ikishirikiana na kampuni mbili za kimataifa AQE Associates and Bureau for Industries Ltd wameshaanza kazi na wameanza kuuliza maswali kuhusu gharama. Ukweli ni kwamba tenda ya ukaguzi huo – Value for Money, ilikuwa ya ushindani wa kimataifa na makampuni makubwa ya ukaguzi huo wa kitaalamu kutoka nje ya nchi – Africa Kusini, Uingereza, Marekani, Kenya, Uganda walilita tenda zao lakini wote walipigwa chini kwa kuogopa mambo yasiwe kama yale ya wakaguzi wa EPA. Viongozi wenye hekima serikalini waliopendekeza Ernest & Young wachaguliwe kufanya uchunguzi wa EPA wamelaumiwa vibaya sana na vigogo mbalimbali mafisadi serikarini kwani Ernest & Young waliwashikia bango serikari pamoja ni kupigwa mikwara kibao na kuahidiwa tenda kibao za consulting iwapo wangeisaidia serikali kuficha ukweli. Sasa Governor mpya Ndulu alikuja na moto mkali na nia ya kusafisha Benki lakini mambo yanakuwa magumu na naye kashaonywa asaidie kuzima moto na kufukia mashimo, aibu inatosha.

Kampuniya Mekon Arch Consult Limited inamilikiwa na Mtu anaita Moses Mkony yeye hapo zamani alishakuwa Engineer wa serikalini akipafanyakazi National Housing Corporation. Kwa sasa amestaafu na kufungua kampuni yake hiyo ya Mekon Arch Consult Limited iliyokuwa na ofisi zake sehemu ya Kijitonjama kichochoro cha karibu na shule ya msingi kijitonyama.

Kampuni hiyo imeshirikiana na kitengo cha Bureau for Industrial Cooperation (BICO) ni kitengo cha chuo kikuu cha Dar es Salaam chenye kutoa ushauri/consultancy kwa mambo mbali mbali ya ufundi kwa ujumla. Ni mradi wa Chuo Kikuu na sio kampuni binafsi lakini kiongozi wa BICO ni Dr. B.B. Nyichomba. Angalia web page ya BICO katika web site ya chuo kikuu Dar es Salaam

Aqe Associates Ltd pia ni kampuni local ya Quantity Surveyors wako pale Samora Avenue Dar es Salaam,. Tel 255 22 2118225; Tel 255 754 261482 na inamilikiwa na maofisa wa chuo cha Ardhi Institute pale Chuo kikuu, Mmoja wa associates ni Dr. Aldo Lupala mhadhiri pale Ardhi. Hawa ni kuku wa kienyeji mtupu, hakuna hata mzungu wala “ya kimataifa”

Sasa hapo jameni kuna ukweli kuhusu stori ya mwandishi wa Nipashe ya jumapili. Hizi ni kampuni za kimataifa za kukagua mahesabu ya ujenzi kweli? Makao makuu ya MEKON yako uchochoroni kijitonyama nyumba ya kupanga hii kampuni na bwana Mkony wanababe wa kukagua Benki kuu kweli. Kipato chao kidogo kabisa, wanawezaje kuwa independent wakati total income yao ni kiduchu na wanataka kukagua benki kuu yenye mabilioni, je code of ethics za Engineers zinakubali hali kama hiyo?
Watakuwa prone for intimidation kani consulting fee toka Benki kuu kwa kazi hiyo ni kubwa mno.

Benki kuu/Gavana kaamua kuchagua kijikampuni kilicho very local, wenyekukimiliki wako hoi kwa poverty wakikimbiza vijitenda vya ujenzi hapa na pale. Kwa makusudi Gavana anataka aweze kuwa–control. Kwani wamejifunza baada ya kuajiri makampuni ya kimataifa yanakuwa ngangari na kuwashikia bango.

Nafikiri ni suala la muandishi wa nipashe kupotosha ukweli aidha makusudi baada ka kula rushwa ya watuhumiwa ili kuanza kuweka kiini macho, au mwandishi kutoku-fanya utafiti wa kina.

Mkitaka kufuatilia ofisi za Mekon ziko wapi, nitawapa picha ya ofisi hizo, ni kujumba kiko Kijitonyama, ukiwa unatokea makumbusho kuelekea mwenge, unakata kona ya kushoto ya lami pale science kuelekew tandale. Ukiwa barabara hiyo ya Tandale hesabu kona ya tatu kushoto, oposite na car show room moja kata kona hiyo ya kushoto kama uanenda kanisa la KKKT Kijitonyama utaona bango mkono wa kushoto, wanauza makuti ya kusuka, Ukipotea ulizia wanakouza makuti ya kusuka na mafuta ya taa. Ofisi ya Mekon iko hapo. Mekon, Plot 602, Kijitonyama, P O Box 31924 Dar es Salaam, Tel. +255 22 2700784, Fax. +255 22 2647552, Mobile. +255 744 262 249 email
moses_mkony@hotmail.com
. This e-mail address is being protected from spam bots, you need JavaScript enabled to view it au mekon@africaonline.co.tz. This e-mail address is being protected from spam bots, you need JavaScript enabled to view it

Kiini macho hicho cha Gavana Ndulu tumekishutukia. Je kampuni hizo zina utaaalamu wa wa uchunguzi wa kina wa kimahesabu na uwezo wa kugundua wizi wa kalamu?

WANANCHI PASI HIYO, TUENDELEE KUPINGA RUSHWA NA UBADHILIFU WA FEDHA ZA UMMA.

NAOMBA WASOMAJI MUINDELEZE HOJA HII, WANA-NCHI WAPATE UPEO WA SIRI NA VIINI MACHO VYA SERIKARI.

-na Mtanzania No1 - 2.12.08 @ 14:50 | #1438
(source: www.freemedia.co.tz/daima/habari.php?id=299)

Soma maoni yangu ktk 'comments'

Tuesday, 16 December 2008

Watchout, 'brandshop68' web is a con!

Dear all,
Today I have received an e-mail from my friend suggesting to me to use an online shopping service -brandshop68.com- as a cheap alternative to purchase elctronic products like games consoles, laptops etc.
But later on I came to realise that the mail is not from the sender whom I know but from 'strangerss' somewhere in the Far East!

My advice to you; don't use this website at all.

Further warnings had been given via www.forums.macrumors in July this year
(see below).
...................................................................

operator207Jul 28, 2008, 11:07 AM
My email account has been used to send spam email... by an ip address that seems to be in China. The emails are being sent to my entire address book- not to strangers- but my internal yahoo address book. What can I do in this case? Is it a virus?

I notice that most forums/websites about this issue suggest that it just "looks" like the emails are being sent by my email account because the spam tool fakes the sender's email address. It seems like a different issue if the emails are being sent to my entire address book...

Please help. I am not sure where to start or what I can do about it.

You say "internal Yahoo Address Book". Does this Address Book reside on Yahoo's servers too? If so, maybe someone has hacked your Yahoo Address Book, or maybe you opened an email that grabbed it all somehow.

Regardless, they have your Address Book contents, even if you change passwords at Yahoo, they would still have them. This happens with Viruses on Windows where the virus grabs your Outlook Address Book.

It almost sounds more personal than what a virus would normally do. Which is grab your AB, then send emails from the AB email addresses to the AB email addresses. Yours sounds like its spamming using your email address to those AB email addresses.

Not to sound rude, but have you angered anyone using your Yahoo email address, or angered someone who knows your Yahoo address, or could gain access to your Yahoo Address Book? I ask because this sounds a bit more personal than most.

The worst case is your going to need to change your Yahoo email address, and definitely change your password. Then tell all your contacts that you have changed your email address.

--------------------------------------------------------------------------------

angelasbJul 29, 2008, 04:45 AM
You say "internal Yahoo Address Book". Does this Address Book reside on Yahoo's servers too? If so, maybe someone has hacked your Yahoo Address Book, or maybe you opened an email that grabbed it all somehow.

Regardless, they have your Address Book contents, even if you change passwords at Yahoo, they would still have them. This happens with Viruses on Windows where the virus grabs your Outlook Address Book.

It almost sounds more personal than what a virus would normally do. Which is grab your AB, then send emails from the AB email addresses to the AB email addresses. Yours sounds like its spamming using your email address to those AB email addresses.

Not to sound rude, but have you angered anyone using your Yahoo email address, or angered someone who knows your Yahoo address, or could gain access to your Yahoo Address Book? I ask because this sounds a bit more personal than most.

The worst case is your going to need to change your Yahoo email address, and definitely change your password. Then tell all your contacts that you have changed your email address.

My address book is on the yahoo server. I don't know who could have gained access to my email account. I checked the IP address and it seems to be coming from China. It has been sent out multiple times to the thousand+ addresses in my address book. The email is some kind of advertisement jpg.

I ran a virus check on my computer and it did not find anything. If it is a virus infecting my account on the yahoo server, could it be located and disinfected on my local drives?

I am going to keep trying a bit before I switch email accounts...

Thank you.

--------------------------------------------------------------------------------

operator207Jul 29, 2008, 09:10 AM
My address book is on the yahoo server. I don't know who could have gained access to my email account. I checked the IP address and it seems to be coming from China. It has been sent out multiple times to the thousand+ addresses in my address book. The email is some kind of advertisement jpg.

I ran a virus check on my computer and it did not find anything. If it is a virus infecting my account on the yahoo server, could it be located and disinfected on my local drives?

I am going to keep trying a bit before I switch email accounts...

Thank you.

I am trying to say, your Yahoo account's username and password are most likely compromised. They are most likely not in China, but bouncing off a proxy in China. They got into your account, got a copy of your addressbook, and took off with it. You will not find a virus (especially on OS X) that could do this. And if the Yahoo servers had a virus, I would imagine there would be thousands of people complaining about exactly what your going through.

I would suggest, at minimum, change your password. If this was me, I would dump that email address, its going to get into spam blocks, and get a new one.

--------------------------------------------------------------------------------

AbstractJul 29, 2008, 09:30 AM
Change your password, foo!

--------------------------------------------------------------------------------

kyutihAug 6, 2008, 01:49 AM
it happened to me too few days back. i really have no idea how i got that. i just checked my sent items and found that spam email which was sent to my contacts that i have in my yahoo address book. fortunately i only have 3 contacts since my email is just 2-month old. what i did was changed my password and deleted all my contacts.

i just want to know why it happened and how to prevent it. please help!

here is the spam email...

Subject: Apple iPod touch Digital Media Player

Hi, dear friend
how are you ?
My friend told me an electronics online shopping mall. He bought some Iphones , game consoles and laptops.
They could offer original stuff with very low price.More details,Please Browse the following website.
http://www.brandshop68.com
MSN :brandshop998@hotmail.com
E-mail : brandshop68@yahoo.cn

:apple:

--------------------------------------------------------------------------------

comeonglosOct 20, 2008, 04:30 PM
I can't help you with the hijacking but I would like to warn you and other not to use brandshop68. I unfortunately fell for the CON because I had an email from a friend so I sent 190 euros. After lots of chasing and emailing I got nothing. They didn't reply and stopped me using MSN messenger to them.

DO NOT use brandshop68 it is a CON - that is why they are hijacking email addresses.

Ukistaajabu ya Musa utaona ya 'SIRIKALI'!

Richmond bado yaitesa Serikali
Serikali imefungua uwanja mpya wa mapambano dhidi ya wabunge baada ya kutangaza wazi kwamba ina mpango wa kununua mitambo ya kufua umeme ya kampuni ya Dowans, uamuzi ambao unapingwa vikali na wawakilishi hao wa wananchi.

Dalili za kuibuka kwa mapambano kati ya watunga sheria na watawala, zilijidhihirisha jana baada tu ya kubainika kwamba zile tetesi za muda mrefu kuwa serikali ilikuwa na mpango wa kununua mitambo hiyo zilikuwa za kweli, baada ya Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, kuwathibitisha wabunge kuwa mpango huo ni wa kweli.

Mipango ya serikali iliwekwa hadharani jana na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, William Shelukindo, wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, kuhusu msimamo wa kamati yake kuhusiana na suala hilo.

Mara kadhaa gazeti hili limewahi kuandika kuwa kuna mpango wa siri wa serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini kutaka kununua mitambo ya Dowans, lakini habari hizo zimekuwa zikikanushwa na wahusika au kutotolewa ufafanuzi wa kutosha.

Shelukindo aliweka mambo yote hadharani mbele ya waandishi wa habari kuwa serikali imefikia uamuzi wa kununua mitambo hiyo kwa gharama ya Sh. bilioni 70.

Alieleza kuwa kamati yake juzi iliitwa na Waziri Ngeleja, na kuelezwa uamuzi huo wa serikali na kutakiwa kutoa maoni yake.

Hata hivyo, Shelukindo alisema kamati yake imeieleza wazi serikali kuwa haikubaliani na uamuzi huo kwa kile alichoeleza kuwa unakwenda kinyume cha Azimio la Bunge ambalo linataka mapendekezo yote yaliyotolewa na Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza mkataba wa kampuni ya Richmond ambayo iliiuzia mitambo hiyo Dowans kwanza yatekelezwe kabla ya kufikiwa uamuzi wowote wa kuinunua mitambo hiyo.

``Jana (juzi) kamati iliitwa kwenye kikao cha dharura na Waziri wa Nishati na Madini kuelezwa uamuzi wa serikali kutaka kununua mitambo ya Dowans na tukatakiwa kutoa maoni yetu.

Sisi kama wabunge tumekataa kushirikishwa katika uamuzi huo kwa sababu kwanza kanuni za Bunge haziruhusu jambo lililokwisha pitishwa na Bunge kujadiliwa upya na pili, Sheria ya Manunuzi ya Umma hairuhusu serikali kununua vifaa au mitambo chakavu,`` alisema Shelukindo.

Shelukindo ambaye katika mkutano huo na waandishi wa habari alikuwa amefuatana na mjumbe mmoja wa kamati yake, Christopher Ole Sendeka, alionyesha wazi kukerwa na uamuzi huo wa serikali, ambao alisema ni dharau kwa Bunge.

Alifafanua kuwa moja ya mapendekezo yaliyotolewa na Kamati Teule ya Bunge iliyokuwa ikichunguza mkataba wa Richmond ni kutaka watu wote waliohusika kupitisha mkataba huo wachukuliwe hatua za kisheria, lakini kamati yake ikashangazwa kuona kuwa kabla ya hatua hizo kuchukuliwa, serikali imechukua uamuzi wa kutaka kununua mitambo hiyo iliyoleta matatizo makubwa.

``Tulitegemea tumeitwa ili tuelezwe utekelezaji wa maazimio ya Kamati Teule ya Bunge iliyokuwa ikichunguza mkataba wa Richmond na si kuibua tena suala la Dowans, kuihusisha Kamati ya Bunge katika maamuzi haya ni kinyume cha taratibu kwa sababu ilishaamuliwa na Bunge kwa hiyo kuridhia itakuwa ni kuleta mgogoro kati ya Bunge na Serikali,`` alisema Shelukindo, ambaye ni Mbunge wa Bumbuli (CCM).

``Hii ni sawa umemkamata mwizi wa mali yako na baada ya kumkamata mnakaa kuzungumza ili akuuzie mali aliyokuibia,`` alisema.

Alieleza kuwa kama Serikali iliona kuna umuhimu wa kuchukua uamuzi huo, kwanza ilitakiwa kujenga hoja ya msingi badala ya kulifanya jambo hilo kuwa siri na kisha kuwashtukiza wabunge kutaka ushauri wao.

``Tumeambiwa kuwa mitambo ipo minne lakini yote imekwisha tumika isipokuwa mmoja ambao ni mpya kidogo, lakini pia umetumika, sheria ya manunuzi ya umma inakataza serikali kununua mitambo chakavu,`` aliongeza.

Kwa upande wake, Ole Sendeka alisema kisheria serikali hairuhusiwi kununua vitu chakavu, lakini inashangaza Wizara ya Nishati na Madini inataka kununua mitambo chakavu.

Alisema ni heri hizo Sh. bilioni 70 zikatumika kuimarisha miundombinu ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) na kutafuta vyanzo vingine vya uzalishaji umeme kuliko kununua mitambo hiyo.

Sendeka alisema wabunge wameshangaa kuarifiwa uamuzi huo wa serikali siku mbili kabla haijapeleka zabuni ya kununua mitambo hiyo.

``Tumekataa kushiriki kubariki kutumia Sh. bilioni 70 kununua mitambo chakavu, serikali ikiamua kufanya hivyo tutajuana mbele, lakini hatutaki kuwa sehemu ya manunuzi hayo,`` alisema Ole Sendeka.

Akizungumza na Nipashe hivi karibuni, Ngeleja alisema hawezi kulizungumzia suala la endapo serikali ina mpango wa kununua mitambo ya kuzalisha umeme ya kampuni ya Dowans, kwa kile kile alichoeleza kuwa suala hilo kwanza ni lazima lipitie ngazi mbalimbali za maamuzi za serikali pamoja na kufuata taratibu za kisheria.

``Siwezi kuzungumzia suala hili, unajua serikali ina ngazi zake mbalimbali za maamuzi na kama lipo ni lazima lipitie kwanza ngazi hizo pamoja na kufuata taratibu za kisheria,`` alisema.

Hata hivyo, Ngeleja alisema serikali katika mipango yake ya kushughulia tatizo la uhaba wa umeme nchini, imejiwekea mikakati ya muda mfupi na ya muda mrefu ya kulitafutia ufumbuzi wa kudumu tatizo hilo na moja ya mikakati hiyo ni kununua mitambo mipya ya kuzalisha umeme.

Alipoulizwa na Nipashe, endapo katika mipango hiyo ya serikali ya kununua mitambo mipya inafikiria kununua mitambo ya kampuni ya Dowans, alisema hawezi kuzungumza lolote kwani serikali ina taratibu zake za kushughulikia suala kama hilo.

``Unajua kama nchi tuna tatizo kubwa la uhaba wa umeme na katika kulitafutia ufumbuzi suala hili na ni lazima tutanunua mitambo mipya kwa sababu ni jambo muhimu,`` alisisitiza waziri huyo.

Kutokana na hatua hiyo, Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, katika wiki ya mwisho ya mkutano wa 13 wa Bunge mjini Dodoma, ilimuita Ngeleja na kumuonya dhidi ya uamuzi huo kwani ni ukiukaji na dharau dhidi ya agizo la Bunge na ni mwendelezo wa maslahi binafsi ya watendaji waandamizi wa Tanesco kwenye Dowans iliyonunua mitambo hiyo kutoka kampuni ya Richmond.

Baada ya Shelukindo kutangaza uamuzi wa kamati yake jana, Ngeleja alitafutwa na Nipashe kutoa maoni yale, lakini simu yake ya kiganjani wakati wote ilikuwa haipatikani.
(SOURCE: Nipashe, 2008-12-16 11:52:35 Na Abdallah Bawazir na Joseph Mwendapole)

Saturday, 13 December 2008

.....................................
'if you can meet triumph and disaster, treat these two the same way'
.....................................

Jengo la Maliasili Samora Ave. lawaka moto

Ofisi ya Waziri nusra iungue


Ofisi ya Waziri wa Maliasili na Utalii iliyopo katika Mtaa wa Samora Jijini imenusurika kuungua wakati sehemu ya jengo la wizara yake liliposhika moto usiku wa kuamkia leo.

Kaimu Kamanda wa Polisi katika Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Evarist Mangala, amesema moto huo ulianza jana kuanzia mishale ya saa 5:30 usiku na kuendelea kwa saa kadhaa kabla ya kuzimwa.

Akasema moto huo ulianzia katika ofisi ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo katika ghorofa ya tatu na kisha kusambaa kwenye ofisi nyingine zilizopo kwenye jengo hilo.

Kamanda Mangala amesema sehemu kubwa ya ofisi ya Katibu Mkuu huyo wa Wizara inayoongozwa na Waziri Shamsa Mwangunga, imeteketea kwa moto na kusababisha hasara kubwa.

Amevitaja baadhi ya vitu vilivyoteketea kwa moto kuwa ni kompyuta, simu, kabati, seti ya televisheni na mafaili kibao muhimu yaliyokuwa ndani ya ofisi hiyo.

Hata hivyo, Kamanda Mangala amesema moto huo ulidhibitiwa na watu mbalimbali walioshirikiana na askari wa zimamoto ambao waliwahi kufika eneo hilo na kutekeleza wajibu wao.

Aidha, amesema chanzo cha moto huo kinadhaniwa kuwa ni hitilafu ya umeme, ingawa akadai kuwa uchunguzi zaidi wa kitaalam kuhusiana na tukio hilo bado haujafanyika ili kubaini chanzo cha kuwepo na hitilafu hiyo ya umeme.

Kamanda Mangala ameongeza kuwa moto huo haukuwa na madhara yoyote kwa binadamu na kwamba hadi sasa, hasara halisi iliyotokana na tukio hilo bado haijafahamika.

(SOURCE: Alasiri, 2008-12-12 21:48:36 Na Emmanuel Lengwa na Kiyao Hoza, Jijini)

Clandestine "Dollarisation" is a problem!

13/12/2008
Dollarisation now a chronic problem
The Governor of the Bank of Tanzania (BoT), Professor Benno Ndulu, has admitted that dollarisation of the domestic economy is a growing problem which requires serious institutional reforms for it to be redressed.
In an exclusive interview in Dar es Salaam on Wednesday, the BoT boss said existing financial laws were not competent enough in dealing with the problem effectively, much as focused inter-institutional cooperation was equally lacking to arrest the currency mess.
Presently, he said, financial laws of the land did not specifically restrict the use of the US dollar as a medium of exchange in conducting domestic transactions.
However, Ndulu was categorical that ``BoT will never encourage use of foreign currency, especially the US dollar, in carrying out home-based transactions``.
``We are so much concerned about the matter. We therefore plead with the public to leak to us any information that will lead to unveiling networks oiling and fueling the dirty game,`` he said.
What is happening in Tanzania, according to analysts, is a process of unofficial or partial dollarisation, whereby individuals substitute domestic money with foreign cash in order to conduct transactions and protect their purchasing power.
While dollarisation is an observable process, it can only be measured accurately if financial transactions using foreign currency are permitted, which is not the case in Tanzania for the time being.
Our survey shows that landlords in Dar es Salaam\'s high-ended Mbezi Beach, notoriously charge rentals in US dollars.
Even rentals for office and school spaces in some parts of Tegeta, Mikocheni and Masaki in the city are charged in hard currencies.
Ndulu confirmed to have heard about rumours related to such rental transactions in US dollars, yet he insisted that tenants should refrain from settling their bills in foreign currencies.
``We will stage serious investigations across suspected areas, as well as raising more public awareness about the economic maladies of dollarisation``, he said.
At a later stage, he hinted, the issuance of national identity cards would make it easier to trace agents running this disgraceful underground financial system.
As for Bureax de Change, he said there were elaborate rules and regulations guiding their businesses, including requirement that every transaction must be furnished with receipt.
Likewise, all tourist hotels are supposed to have an in house bureau de change outfit to facilitate foreign exchange transactions for incoming and outgoing visitors.
``Tanzanians seeking accommodation in tourist hotels are not supposed to pay their bills in US dollars``, he said.
When reached for comments, Finance and Economy Minister Mustapha Mkulo said dollarisation was truly an embarrassing issue, taking into account the endless complaints made by various individuals, including MPs, business people and individuals.
However, he disclosed that plans were underway for a joint meeting with the BoT with the aim of investigating the relevance of the existing financial laws that govern currency, in the upshot, proposing permanent solutions.
``Rampant dollarisation of the economy is dangerous for the wellbeing of the nation.
We will come up with a statement after having discussions with BoT over the matter``, he said.
Michael James, a Mbezi Beach resident, complained to this reporter about the kind of hassles he undergoes when it comes to paying rent in US dollars.
``I am obliged to travel all the way downtown to change local currency in bureau de change for the US dollar, otherwise my landlord will not accept local currency``, he said.
(SOURCE: Guardian, 2008-12-13 11:51:44. By Joyce Kisaka)

Friday, 12 December 2008

.....................................
'we have to fight aids; not people with aids'
-man united/unicef campaign
.....................................
'don't shoot the messenger'
.....................................