tag:blogger.com,1999:blog-1405840685412848847.post6842046446732493495..comments2023-12-17T20:07:35.752+00:00Comments on OPEN HEART, OPEN MIND: Mbunge Richard Nyaulawa afariki duniaMOSONGA RAPHAELhttp://www.blogger.com/profile/11344559339311484137noreply@blogger.comBlogger1125tag:blogger.com,1999:blog-1405840685412848847.post-25059432724995356042008-11-14T13:08:00.000+00:002008-11-14T13:08:00.000+00:00Richard Nyaulawa Pumziko la mileleMAISHA siku na n...Richard Nyaulawa Pumziko la milele<BR/><BR/>MAISHA siku na nyakati katika dunia hii ya aliyekuwa Mbunge wa Mbeya Vijijini (CCM), Bw. Richard Nyaulawa vimefikia kikomo rasmi baada ya kuzikwa kijijini kwake Inyala, Mbeya Vijijini, umbali wa kilometa 20 kutoka Mbeya Mjini. <BR/><BR/>Maziko hayo yaliyofanyika jana alasiri, pia yalihitimisha siku takribani tano za marehemu Nyaulawa kuliliwa na wengi, kuhuzunisha wengi na kuwaachia wengi simanzi na kutoamini kilichotokea tangu alipofariki dunia alfajiri ya Jumapili iliyopita kwa ugonjwa wa saratani ya ini. <BR/><BR/>Ni maziko yaliyowaachiwa wanafamilia yake, ndugu zake, wafanyakazi wake katika kampuni ya magazeti ya Business Times aliyoiasisi na kuiongoza vyema, tafakuri nzito, tafakuri ya maisha mapya na ukurasa mpya bila yeye. <BR/><BR/>Maziko hayo ambayo yaliongozwa na Rais Jakaya Kikwete na mkewe, Mama Salma, Naibu Spika wa Bunge, Bibi Anne Makinda, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Bw. John Mwakipesile, wabunge wenzake na viongozi waandamizi wa vyama mbalimbali vya siasa na wananchi, yalivuta hisia za wengi na kutoa tafsiri pana juu ya Nyaulawa kuwa mwanadamu wa aina gani katika Dunia hii wakati wa uhai wake. <BR/><BR/>Huzuni aliyokuwa nayo Rais Kikwete inaweza isieleweke kirahisi kwa wengi-si kwa sababu alimfahamu Nyaulawa kama mmoja wa wabunge makini kiasi cha kumpa nyadhifa za kumsaidia ukiwamo ujumbe wa Bodi ya Mamlaka za Bandari na uenyekiti wa Bodi ya Pareto, bali pia tafsiri moja ya huzuni ya Rais inarudi miaka ya 1970 walipokuwa katika siku ngumu za uanafunzi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. <BR/><BR/>Ni katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambapo wakati Rais Kikwete akiwa mbele kwa darasa moja katika darasa la Uchumi, Bw. Nyaulawa alikuwa nyuma yake na waliokuwa nao nyakati hizo, akiwamo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Abbas Kandoro aliyekuwa darasa moja na marehemu, wanamkumbuka jinsi alivyokuwa mmoja wa wanafunzi waliokuwa wakisifika kwa umahiri darasani, kiasi cha kufahamika hata kwa wanafunzi wa madarasa ya juu. <BR/><BR/>Maziko ya marehemu Nyaulawa, huzuni ya Rais Kikwete na historia hii adhimu ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, inalikumbusha Taifa kuwa Rais Kikwete binafsi aliwahi kukumbwa na mshituko mwingine kutokana na kifo cha kiongozi mwingine mwandamizi wa nyakati hizo za UDSM-marehemu Juma Akukweti ambaye alisoma mwaka mmoja na Rais. <BR/><BR/>Mwili wa marehemu Nyaulawa ulisafirishwa jana alfajiri kwa ndege ya Zan Air iliyoongozwa na rubani Kanali Hamisi kutoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius K. Nyerere na kuwasili uwanja wa Ndege wa Mbeya saa 4.15 asubuhi na kusafirishwa kwenda kijijini Inyala kwa gari. <BR/><BR/>Kukusanyika kwa wananchi wengi barabarani kila mwili huo ulikokuwa ukipitishwa, kulizidi kuonesha jinsi hayati Nyaulawa alivyoishi katika Dunia hii kwa miaka yake 57 aliyojaaliwa na Mola wake. <BR/><BR/>Si wananchi wote kati ya wengi waliokuwa wakilipungia jeneza hilo, waliweza kupata fursa ya kuwasilisha uchungu uliokuwa nyoyoni mwao, lakini hotuba ya Padri Tresfoni Tweve wa Kanisa Katoliki Parokia ya Bakita, Inyala, ilionekana kuwakilisha huzuni ya wengi. <BR/><BR/>Katika hotuba yake hiyo katika misa ya wafu kwa marehemu Nyaulawa, kiongozi huyo wa dini alimsifu marehemu kwa mambo matatu ambayo ni adhimu na adimu-aliipenda jamii yake; aliipenda nchi yake na alimpenda Mungu wake. <BR/><BR/>Akifafanua mtazamo wa marehemu ulioakisi mapenzi yake hayo matatu, Padri huyo alisema akiwa hai, marehemu Nyaulawa alimweleza kuwa aliingia katika siasa si kutafuta chochote kingine, bali kuitumikia nchi yake huku pia mkewe, Bibi Getrude Nyaulawa naye akistaafu kazi, ili akaishi kijijini Inyala akasaidie kuinua vikundi vya akina mama. <BR/><BR/>Pamoja na kuwa jana ilikuwa siku ngumu kwa wengi, hasa wanafamilia lakini mtu mmoja maalumu, mwenye sababu maalumu na zenye umaalumu wa pekee, Bw. Rashid Mbuguni, kipenzi cha siku nyingi na mtu ambaye walishibana na marehemu na kushirikiana sana katika biashara zao, baada ya siku tano za kuamua kutosema chochote, akihuzunika tu moyoni, jana aliamua kusema, akimuaga kwa uchungu mshirika wake. <BR/><BR/>Unapozungumzia kampuni ya Business Times inayochapisha pamoja na gazeti hili magazeti ya Business Times, Dar Leo na Spoti, kituo cha Radio Times FM 100.5, Kiwanda cha Uchapishaji cha Business Printers na kampuni ya ushauri wa biashara na uwekezaji ya Business Care Group, unazungumzia pacha wawili-Nyaulawa na Mbuguni. <BR/><BR/>Ni mawazo yao ya muda mrefu ya kuhakikisha kuwa Tanzania inaendelea kwa kuwa na sekta ya habari iliyo huru yaliyokuwa kweli, rasmi Novemba 5 mwaka 1988 walipoanza kuchapisha nakala ya kwanza ya gazeti huru na la kwanza binafsi nchini la Business Times lililofuatiwa na Majira miaka kadhaa baadaye. <BR/><BR/>Katika miaka yote 20 ya kuwapo kampuni hiyo, Nyaulawa na Mbuguni ndivyo 'vichwa' viwili adhimu vilivyokuwa nyuma ya mafanikio ambayo kampuni hizo zimeyafikia kwa sasa. <BR/><BR/>Akimuaga mpendwa wake, mwenza wake na mshirika wake, Bw. Mbuguni alitoa ahadi iliyoonekana kuwa si ya wanafamilia na wafanyakazi wa Business Times pekee, bali ahadi yake kwa Watanzania wote, kuwa wale ambao marehemu amewaainisha kuendeleza biashara zake, atafanya nao kazi na kuwachukulia kuwa ni familia moja. <BR/><BR/>Maisha ya hayati Nyaulawa kwa miaka 57 duniani pamoja na kuhitimika kwa sifa zote zilizowaachia wengi huzuni, kwa upande mwingine yanaipa furaha familia, wafanyakazi na wabunge wenzake na wote waliomjua au kufaidika na kazi za mikono yake-kwa sababu ni mmoja wa wanadamu wachache ambao katika kipindi chote cha maisha yao, alitenda wema na hakutazama nyuma, amekwenda zake, kwa Mola wake, ni pumziko la milele. <BR/><BR/>(source: majira, Na Masoud Sanani, Mbeya)MOSONGA RAPHAELhttps://www.blogger.com/profile/11344559339311484137noreply@blogger.com